Rais Magufuli aliposema tuna akiba ya fedha za kigeni kuendesha Nchi kwa miezi sita bila kuzalisha hawakuamini, sasa tunaenda mwezi wa tatu

Bia yetu

JF-Expert Member
Apr 14, 2020
6,923
8,314
Mimi huwa namwamini sana Rais Magufuli katika hotuba si mtu wa porojo wala kupindisha maneno, anaongea ukweli

Unaweza kumwita Magufuli ni Mussa anayetupeleka katika Nchi ya ahadi, alinusa kuwa dunia itakumbwa na msuko suko wakajipanga mapem.

Kipindi cha nyuma kidogo Rais Magufuli aliwahi kuwaambia Wananchi wake kuwa Serkali ina akiba ya fedha za kigeni kuendesha Nchi kwa miezi sita bila kuzalisha,kuna baadhi ya wanasiasa walitilia mashaka maneno yake

Lakini ukweli Sasa umedhihirika ,tunaingia mwezi wa watatu toka korona iingie Africa mashariki Hivyo kupelekea shughuli nyingi za uchumi kusimama Mfano sector ya utalii imesimama kabisa ambayo inachangia kwa kiasi kikubwa katika pato la Taifa ,na shughuli nyingine nyingi za kiuchumi zimesimama Kwasasa

Lakini Ukiangalia Mambo yanaenda barabara husikii ukosefu wa petrol, husikii wabunge wamekosa posho tofauti na Rwanda ambapo Viongozi wanakatwa mishahara ili kufidia mapungufu ya Serkali yaani kwa ufupi Mambo ni swadakta

Hii Ndio faida ya kiongozi anayewaza mambo ya kesho

Tunazidi kukuombea Rais wetu, Mungu aendelee kukupa busara na upendo ili uendelee kututumikia vyema sisi Watanzania.

Corona upite mbali uiache Tanzania ,Ndani ya May shughuli za kiuchumi zirejelee



Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ifike mahali Watanzania wajiamini,tuna kiongozi bora sana wa Nchi ,

Sisi Tanzania tumebahatika kupata kiongozi anayechukia rushwa sana

Ni aghalabu kwa Nchi za kiafrica kumpata kiongozi Mzalendo kama Magufuli, viongozi Wengi wa Africa ni wapenda rushwa, Wengi wanashirikiana na Mabeberu kuwaibia Wananchi

Lakini Rais Magufuli amejitenga na ubadhirifu huo anawatumikia Wananchi wake kwa moyo mmoja, hana muda wa kwenda kwa Mabeberu kula kodi za Wananchi

Awamu ya tano awamu iliyojaa uzalendo

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Bado kivipi Mkuu tayari tupo mwezi wa tatu Nchi haizalishi na mambo yanaenda

Naamini Ndani ya May corona itafutika mambo yarudi kama inavyotakiwa
Mbona bado mapema..??
Unalijua joto la jiwe..?
Sio jiwe lile lililolala juu ya jiwe!,Bali jiwe lile lililokuja kuvunja jiwe

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hoja ni kwamba tunaingia mwezi wa watatu toka korona iingie Africa mashariki Mkuu, hivyo shughuli nyingi za kiuchumi zimesimama hapo tayari ni kama tupo lockdown kiuchumi

Hili hulioni Mkuu au unanishambulia tu
Ukisikia Mantid brain a.k.a ubongo wa panzi ndo huu, usiombe itokee total lockdown ya lazima kwa uchumi huu ni wiki Mbili tu, mabeberu wataitwa wahisani, wadau wa maendeleo yaani "all weather friends"

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mimi huwa namwamini sana Rais Magufuli katika hotuba si mtu wa porojo wala kupindisha maneno, anaongea ukweli

Unaweza kumwita Magufuli ni Mussa anayetupeleka katika Nchi ya ahadi, alinusa kuwa dunia itakumbwa na msuko suko wakajipanga mapem.

Kipindi cha nyuma kidogo Rais Magufuli aliwahi kuwaambia Wananchi wake kuwa Serkali ina akiba ya fedha za kigeni kuendesha Nchi kwa miezi sita bila kuzalisha,kuna baadhi ya wanasiasa walitilia mashaka maneno yake

Lakini ukweli Sasa umedhihirika ,tunaingia mwezi wa watatu toka korona iingie Africa mashariki Hivyo kupelekea shughuli nyingi za uchumi kusimama Mfano sector ya utalii imesimama kabisa ambayo inachangia kwa kiasi kikubwa katika pato la Taifa ,na shughuli nyingine nyingi za kiuchumi zimesimama Kwasasa

Lakini Ukiangalia Mambo yanaenda barabara husikii ukosefu wa petrol, husikii wabunge wamekosa posho tofauti na Rwanda ambapo Viongozi wanakatwa mishahara ili kufidia mapungufu ya Serkali yaani kwa ufupi Mambo ni swadakta

Hii Ndio faida ya kiongozi anayewaza mambo ya kesho

Tunazidi kukuombea Rais wetu, Mungu aendelee kukupa busara na upendo ili uendelee kututumikia vyema sisi Watanzania.

Corona upite mbali uiache Tanzania ,Ndani ya May shughuli za kiuchumi zirejelee



Sent using Jamii Forums mobile app
Unapoandika hizi thread zako pata ushauri na kibali toka kwa mabosi wako sio unajiandikia tuu.
Unakoelekea unataka kumuaibisha kwa kuandika mada ambazo ziko juu sana ya uwezo wako na huwezi kuzitetea zaidi ya kumuacha utupu unayempigia chapuo.
Nikufundishe kitu kijana, ukipewa kazi ya kumnyoa Mfalme sehemu za siri sio kuwa umeruhusiwa kuchezea korodani!
Shauri yako! Hiyo ajira yenyewe haina hata wiki mbili.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mkuu soma vizuri na uelewe,

Usisome ukiwa na hasira, Naamini uzi unaeleweka
Unapoandika hizi thread zako pata ushauri na kibali toka kwa mabosi wako sio unajiandikia tuu.
Unakoelekea unataka kumuaibisha kwa kuandika mada ambazo ziko juu sana ya uwezo wako na huwezi kuzitetea zaidi ya kumuacha utupu unayempigia chapuo.
Nikufundishe kitu kijana, ukipewa kazi ya kumnyoa Mfalme sehemu za siri sio kuwa umeruhusiwa kuchezea korodani!
Shauri yako! Hiyo ajira yenyewe haina hata wiki mbili.

Sent using Jamii Forums mobile app

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom