Cherenganya
JF-Expert Member
- Jan 21, 2018
- 2,309
- 1,775
Wasalaam watu wa Mungu
Miezi 6 tu baada ya uteuzi wa wakuu wa mikoa isiyokua bahati ilimshukia Mama Anne Kilango Malecela. Watu wengi walijua huyu buana anatafuta publicity.
Walichosahau tu ni Kwamba huyu ni mke wa Waziri mkuu wa Tanzania 1990-1994 aidha Makamu mwenyekiti CCM 1995-2007 na mjumbe wa kamati kuu ya CCM. Mtu huyu si wakumbeza yeye wala kizazi chake kwani ni mtu mwenye kuifahamu serikali na chama kindaki ndaki.
Alipomtumbua "mwana" Mh. Charles Kitwanga, kwanini nasema mwana, taarifa zilizopo mtaani ni kwamba Mh. Kitwanga na Mh. Rais ni marafiki wakubwa sana si wa kukutana baa bali wa kuja njumbani na kukaribishwa sebuleni akakabidhiwa rimoti na kubadilisha chaneli.
Alipo kamatwa Mke wa Waziri mmoja na trafiki akajibu shit alafu Mh. Rais akasema hata mke wangu akizingua kamata, mmh hili lilikua fikirishi hasa kwa wenye fikra.
Alipowaambia waandishi wa Habari NOT TO THAT EXTENT, tukalalama tukaingiwa na hofu tasnia pendwa imevamiwa, sisi tunajinasibu kuwa Mhimili wa nne usio rasmi.
TISS hii ni taasisi nyeti kuliko unyeti unaoyamkinika, kiongozi wake si tu kwamba anaongoza watu wenye uwezo mkubwa wa kufikiri, bali wenye mafunzo mahsusi juu ya nyanja mbali mbali za kubashiri yajayo na utambuzi wa viashiria kabla kutendeka kwa tukio.
Hivyo kusikia Mkurugenzi wake kuondolewa chomboni, sio jambo lakufikirisha tu, bali limegongelea msumari wa mwisho kwenye jeneza kwamba kigezo pekee ni UCHAPA KAZI NA WELEDI KATIKA KAZI na si unajua mimi ni nani.
Ni muda muafaka Sasa yeyote mwenye dhamana ya uongozi katika serikali hii kujua kwamba kitu pekee kitakacho linda kibarua chako ni weledi uliotukuka katika nafasi uliyopo na sio vinginevyo.
Nawasilisha
Miezi 6 tu baada ya uteuzi wa wakuu wa mikoa isiyokua bahati ilimshukia Mama Anne Kilango Malecela. Watu wengi walijua huyu buana anatafuta publicity.
Walichosahau tu ni Kwamba huyu ni mke wa Waziri mkuu wa Tanzania 1990-1994 aidha Makamu mwenyekiti CCM 1995-2007 na mjumbe wa kamati kuu ya CCM. Mtu huyu si wakumbeza yeye wala kizazi chake kwani ni mtu mwenye kuifahamu serikali na chama kindaki ndaki.
Alipomtumbua "mwana" Mh. Charles Kitwanga, kwanini nasema mwana, taarifa zilizopo mtaani ni kwamba Mh. Kitwanga na Mh. Rais ni marafiki wakubwa sana si wa kukutana baa bali wa kuja njumbani na kukaribishwa sebuleni akakabidhiwa rimoti na kubadilisha chaneli.
Alipo kamatwa Mke wa Waziri mmoja na trafiki akajibu shit alafu Mh. Rais akasema hata mke wangu akizingua kamata, mmh hili lilikua fikirishi hasa kwa wenye fikra.
Alipowaambia waandishi wa Habari NOT TO THAT EXTENT, tukalalama tukaingiwa na hofu tasnia pendwa imevamiwa, sisi tunajinasibu kuwa Mhimili wa nne usio rasmi.
TISS hii ni taasisi nyeti kuliko unyeti unaoyamkinika, kiongozi wake si tu kwamba anaongoza watu wenye uwezo mkubwa wa kufikiri, bali wenye mafunzo mahsusi juu ya nyanja mbali mbali za kubashiri yajayo na utambuzi wa viashiria kabla kutendeka kwa tukio.
Hivyo kusikia Mkurugenzi wake kuondolewa chomboni, sio jambo lakufikirisha tu, bali limegongelea msumari wa mwisho kwenye jeneza kwamba kigezo pekee ni UCHAPA KAZI NA WELEDI KATIKA KAZI na si unajua mimi ni nani.
Ni muda muafaka Sasa yeyote mwenye dhamana ya uongozi katika serikali hii kujua kwamba kitu pekee kitakacho linda kibarua chako ni weledi uliotukuka katika nafasi uliyopo na sio vinginevyo.
Nawasilisha