Rais Magufuli akutana na mawaziri wa Elimu na TAMISEMI, apiga marufuku michango ya aina yoyote shuleni

Kuna tatizo linalonyemelea taifa. Bahati mbaya kauli ya Rais ni amri..
Sijaona sababu ya kuwaita mawaziri wale wawili Ikulu kuwapa maagizo. Mmoja ni Waziri ndani ya ofisi yake na mwingine wa Elimu. Ningekuwa yeye (lakini siitamani kazi yake hata kwa mabilioni) lingekuwa ni suala la baraza zima la mawaziri, baada ya kupokea ushauri kutoka Wizara zote au Kurugenzi za Elimu. Sio kweli kwamba walimu wanachangisha hela wanafunzi kwa manufaa yao. Hali ni mbaya sana mashuleni, na kile wanachoweza hukitumia mara na wapo wazazi wanaweza kushuhudia hili.

Kinachofanyika sasa ni kufanya zile shule ambazo changamoto yao kubwa ilikuwa ni gharama za kujiendesha- maana ya vitabu na madaftari, na sasa walikuwa wanaelekeza jitihada kwenye kuboresha, kukata tamaa. Wakurugenzi wengi ni wageni- wana majukumu makubwa ya kisekta. Ujuzi wangu mdogo unaashiria katazo jipya hasa kwenye maeneo ambayo shule hazifikiki kiraisi. Ni vigumu kuona mzazi akienda kutoa mchango wa hiari kupitia MKURUGENZI- kwani mwishoni Mwl Mkuu ndiye mtekelezaji.

Naona taifa linanyemelewa na mfumo wa papo kwa papo bila kujali tunakopaswa kuendelea.
nzuri hiyo ndugu njirembela wew n mwl eti
 
Ndalichako na Jafo kuna ka shule kenye usajili wa s4048 kaangazieni michango.
Halafu Ndalichako ulitoa zawadi ya fedha hapo ta kupanda ufaulu kaulize zipo wapi, na kama kuna mgao je walimu wote wamepata?
Elimu bure!!!
Pole mwalimu kwa kukosa mgao wa fedha kutoka kwa Ndalichako.
 
Hapana, Waziri anachoshindwa ni uwezo wa kumshauri tu Rais kuhusu gharama halisi za kuendesha shule hizi. Mimi ni mjumbe wa kamati moja ya shule wa fulani kule mkoani. Ukweli ni kwamba gharama za kuendesha shule ziko juu by far kuliko hela inayotumwa shuleni pale. Mwalimu Mkuu anachanganyikiwa nini afanye, badala yake inamlazimu abuni njia zake za kupata fedha kama vile michango ya chakula, masomo ya ziada, safari za kimasomo, ulinzi, nk.

Bahati mbaya mwalimu na Waziri hawaruhusiwi kusema hela haitoshi. Jamani msioongeeongee tu humu bila kufahamu ukweli wa mambo. Unaweza kufurahia maagizo kwakuwa yanakufurahaisha lakini maagizo hayo yakatafuna hatima ya mwanao kielimu.

Achilia mbali kuendesha shule lakini hata kipato cha mwl kiko chini saana kuweza kuimudu kazi yake, hasa kwa yule mwl ambae amenunua kigari cha mkopo au cha kupewa na "mtu" na kukiendesha barabarani kila siku kufika kazini.

Hii ni kawaida kama mama nyumbani akipewa hela kidogo za matumizi atatumia mbinu hata chafu kupata hela.
Motisha hata wanafunzi hawapewi ,watapewa itatoka fungu lipi.Walimu pia hawawezi Toa hela zao kisa wampe motisha mtoto ambaye katelekezwa na mzazi wake.
 
mimi nadhani kunawatendaji wa serikali hawaielewi vizuri kauli ya mkuu wa kaya, nafikiri mkuu angewaainishia kabisa michango ya aina ipi haiihitajiki maana sasa mkuu anasema no michango halafu watendaji wanaibuka na tumichango fulani fulani mara hela ya mlinzi mara hela ya karatasi za kufanyia mtihani bongo bana kazi ipo understanding yetu sijui inakuaje
Sera ya Elimu bure walidandia tu mwaka wa tatu huu lkn Bado ufanisi wake haueleweki.Form four ya kwanza ya Magu itakuwa ni balaa.Hata form two ya kwanza ya Mzee mmejionea Elimu bure ilivyopigwa
 
Niko huku kwetu walimu wakuu wameingia mitini na hela huku wakurugenzi na maDC wakihaha kuweka mambo sawa, wazazi wanataka pesa zao.

Kuna shule zilifungia madawati store mtoto anatoa elfu 70 wanaenda kumfungulia store anachukua dawati mzazi akigoma mtoto anaambiwa akae chini.

Zipo shule zimedahili watoto zaidi ya uwezo wao na kuanzisha michango ya ujenzi wa madarasa huku shule zenye miundo mbinu zikigawiwa wanafunzi kiduchu,

kwa kweli leo vijijini ni nderemo kwa kwenda mbele, hapa chadema msahau kupata kura vijijini,
 
Hili swala la Elimu bure kwenye shule za msingi na Secondary naona haijakaa sawa... NIMETOKA KULIPA ADA YA MWANANGU WA FORM ONE SHULE MOJA HAPA ARUSHA.. 225,000/= SASA NIMEIBIWA AU? Naomba kujua hii thana ya Elimu bure..
 
Rais Dkt.John Pombe Magufuli amekutana na Waziri wa TAMISEMI Mhe. Selemani Jafo na Waziri wa Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi Profesa Joyce Ndalichako Ikulu Dar es salaam Mhe.Rais amepiga marufuku aina yoyote ya michango katika shule za serikali za msingi na sekondari.

Rais Magufuli: Tumesema elimu bure, elimu bure haiwezi kaja tena kwa mgongo mwingine ikawa elimu pesa. Tumeweka utaratibu kuanzia shule ya msingi mpaka sekondari form four hakuna kulipa ada yoyote. Nimewapa maelekezo kwamba kuanzia leo iwe ni marufuku na wakalisimamie hili. Mzazi sitaki kusikia akilalamika mwanae amerudishwa shule kwa sababu ya michango.

Rais Magufuli: Na walimu wote wasishike mchango wowote toka kwa mwanafunzi, mchango kama kuna mwananchi anataka kuchangia apeleke kwa mkurugenzi, mkurugenzi kama anataka kutengeneza madawati atatengeneza na kupeleka kwenye shule inayohusika. Siyo mwanafunzi ameenda shuleni akarudishwa kwasababu hajatoa michango.

Rais Magufuli: Kwahiyo nimemweleza waziri na waziri mwenzake kwasababu ndio wanaoshughulikia elimu. Lakini kwa taarifa hii mkawaeleze wakuu wa mikoa, wakuu wa mikoa na wakurugenzi.

Rais Magufuli: Nikisikia kuna shule katika wilaya fulani ambayo mtoto anarudishwa kwasababu hajachangia michango huyo mkurugenzi hana kazi. Na hii waanze kutekeleza kuanzia leo. Maafisa elimu wote wakasimamie hili, wanalipwa kwa ajili ya kusimamia. Tunajua enrolment ya wanafunzi imeongezeka hizi ni challenge ambazo lazima tuzibebe sisi kama serikali lakini hii isiwe sasa ni demotivation nyingine ya kuwazuia watoto, sasa hivi watoto wameacha kwenda shule kutokana na michango hii inayotolewatolewa sasa waziri mkalisimamie hili.

Maagizo haya yanakuja ikiwa ni siku moja baada ya malalamiko ya mwanaJF kuhusu kutozwa sh 70,000 huko Butiama mkoani Mara, zaidi soma=> Mkanganyiko elimu bure: Huko Butiama wananchi walazimishwa kuchanga elfu 70, la sivyo unanyang'anywa kuku, sufuria, n.k.




View attachment 677768
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli ameagiza kuchukuliwa hatua dhidi ya viongozi na watendaji ambao shule za msingi na sekondari zilizopo katika maeneo yao zinawatoza wanafunzi michango mbalimbali kinyume na muongozo uliotolewa na Serikali wa utoaji wa elimu bila malipo.

Mhe. Rais Magufuli ametoa maagizo hayo leo asubuhi tarehe 17 Januari, 2018 Ikulu Jijini Dar es Salaam alipokutana na kufanya mazungumzo na Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Joyce Lazaro Ndalichako na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) Mhe. Selemani Said Jafo.

Mhe. Rais Magufuli amesema Serikali inatoa Shilingi Bilioni 23.875 kila mwezi kwa ajili ya kuwezesha utoaji wa elimu bila malipo lakini inashangaza kuona bado kuna walimu wanaendelea kuwatoza michango ama kuwarudisha nyumbani wanafunzi ambao wanashindwa kutoa michango hiyo.

“Nawaagiza Mawaziri, sitaki kusikia mwanafunzi anarudishwa nyumbani kwa kushindwa kutoa michango, na fikisheni maagizo haya kwa Wakuu wa Mikoa, Wakuu wa Wilaya, Wakurugenzi na wote wanaohusika, nikisikia tena mahali jambo hili linaendelea hawa niliowateua mimi wataondoka.

“Haiwezekani tumefuta ada, halafu walimu wanaamua kuanzisha michango tena mikubwa ambayo watu masikini wanashindwa kusomesha watoto wao, na kama wazazi wanataka kuchangia kitu shuleni wapeleke michango yao kwa Mkurugenzi, lakini sitaki kusikia mwanafunzi anapewa sharti la kutoa mchango ndipo apokelewe shule” amesema Mhe. Rais Magufuli.

Mhe. Rais Magufuli ametoa maagizo hayo baada ya kupata taarifa kuwa zipo baadhi ya shule ambazo wanafunzi wanadaiwa michango mbalimbali tena kwa kiwango kikubwa ikiwemo chakula, maabara, madawati na ziara za kujifunza, hali iliyosababisha wazazi kushindwa kumudu.

Waziri Prof. Joyce Lazaro Ndalichako ameagiza walimu na viongozi wa halmashauri kuwarudisha shule mara moja wanafunzi wote waliorudishwa nyumbani kwa kutotoa michango na pia kurejesha mara moja michango iliyokusanywa kinyume na mwongozo wa Serikali.

Waziri Mhe. Selemani Said Jafo amewaagiza Wakuu wa Mikoa na Wakuu wa Wilaya kuwasilisha taarifa ya shule ambazo zimetoza michango kinyume na mwongozo wa Serikali ifikapo Ijumaa wiki hii (tarehe 19 Januari, 2018) ili hatua zichuliwe dhidi ya walimu na maafisa elimu ambao kwa makusudi wamekiuka mwongozo huo.

Gerson Msigwa

Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, IKULU

Dar es Salaam

17 Januari, 2018

viwanda vimegoma

manunuzi ya wapinzani bado hayajabadili upepo

SGR imebuma

Bombardier ndo hivyo tena

uchumi ndo kwishney

makinikia holaaa!

kwahiyo kilichobaki ni kumpa kiki ni elimu bure lakini bado miaka 2 tu.
 
Rais Dkt.John Pombe Magufuli amekutana na Waziri wa TAMISEMI Mhe. Selemani Jafo na Waziri wa Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi Profesa Joyce Ndalichako Ikulu Dar es salaam Mhe.Rais amepiga marufuku aina yoyote ya michango katika shule za serikali za msingi na sekondari.

Rais Magufuli: Tumesema elimu bure, elimu bure haiwezi kaja tena kwa mgongo mwingine ikawa elimu pesa. Tumeweka utaratibu kuanzia shule ya msingi mpaka sekondari form four hakuna kulipa ada yoyote. Nimewapa maelekezo kwamba kuanzia leo iwe ni marufuku na wakalisimamie hili. Mzazi sitaki kusikia akilalamika mwanae amerudishwa shule kwa sababu ya michango.

Rais Magufuli: Na walimu wote wasishike mchango wowote toka kwa mwanafunzi, mchango kama kuna mwananchi anataka kuchangia apeleke kwa mkurugenzi, mkurugenzi kama anataka kutengeneza madawati atatengeneza na kupeleka kwenye shule inayohusika. Siyo mwanafunzi ameenda shuleni akarudishwa kwasababu hajatoa michango.

Rais Magufuli: Kwahiyo nimemweleza waziri na waziri mwenzake kwasababu ndio wanaoshughulikia elimu. Lakini kwa taarifa hii mkawaeleze wakuu wa mikoa, wakuu wa mikoa na wakurugenzi.

Rais Magufuli: Nikisikia kuna shule katika wilaya fulani ambayo mtoto anarudishwa kwasababu hajachangia michango huyo mkurugenzi hana kazi. Na hii waanze kutekeleza kuanzia leo. Maafisa elimu wote wakasimamie hili, wanalipwa kwa ajili ya kusimamia. Tunajua enrolment ya wanafunzi imeongezeka hizi ni challenge ambazo lazima tuzibebe sisi kama serikali lakini hii isiwe sasa ni demotivation nyingine ya kuwazuia watoto, sasa hivi watoto wameacha kwenda shule kutokana na michango hii inayotolewatolewa sasa waziri mkalisimamie hili.

Maagizo haya yanakuja ikiwa ni siku moja baada ya malalamiko ya mwanaJF kuhusu kutozwa sh 70,000 huko Butiama mkoani Mara, zaidi soma=> Mkanganyiko elimu bure: Huko Butiama wananchi walazimishwa kuchanga elfu 70, la sivyo unanyang'anywa kuku, sufuria, n.k.




View attachment 677768
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli ameagiza kuchukuliwa hatua dhidi ya viongozi na watendaji ambao shule za msingi na sekondari zilizopo katika maeneo yao zinawatoza wanafunzi michango mbalimbali kinyume na muongozo uliotolewa na Serikali wa utoaji wa elimu bila malipo.

Mhe. Rais Magufuli ametoa maagizo hayo leo asubuhi tarehe 17 Januari, 2018 Ikulu Jijini Dar es Salaam alipokutana na kufanya mazungumzo na Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Joyce Lazaro Ndalichako na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) Mhe. Selemani Said Jafo.

Mhe. Rais Magufuli amesema Serikali inatoa Shilingi Bilioni 23.875 kila mwezi kwa ajili ya kuwezesha utoaji wa elimu bila malipo lakini inashangaza kuona bado kuna walimu wanaendelea kuwatoza michango ama kuwarudisha nyumbani wanafunzi ambao wanashindwa kutoa michango hiyo.

“Nawaagiza Mawaziri, sitaki kusikia mwanafunzi anarudishwa nyumbani kwa kushindwa kutoa michango, na fikisheni maagizo haya kwa Wakuu wa Mikoa, Wakuu wa Wilaya, Wakurugenzi na wote wanaohusika, nikisikia tena mahali jambo hili linaendelea hawa niliowateua mimi wataondoka.

“Haiwezekani tumefuta ada, halafu walimu wanaamua kuanzisha michango tena mikubwa ambayo watu masikini wanashindwa kusomesha watoto wao, na kama wazazi wanataka kuchangia kitu shuleni wapeleke michango yao kwa Mkurugenzi, lakini sitaki kusikia mwanafunzi anapewa sharti la kutoa mchango ndipo apokelewe shule” amesema Mhe. Rais Magufuli.

Mhe. Rais Magufuli ametoa maagizo hayo baada ya kupata taarifa kuwa zipo baadhi ya shule ambazo wanafunzi wanadaiwa michango mbalimbali tena kwa kiwango kikubwa ikiwemo chakula, maabara, madawati na ziara za kujifunza, hali iliyosababisha wazazi kushindwa kumudu.

Waziri Prof. Joyce Lazaro Ndalichako ameagiza walimu na viongozi wa halmashauri kuwarudisha shule mara moja wanafunzi wote waliorudishwa nyumbani kwa kutotoa michango na pia kurejesha mara moja michango iliyokusanywa kinyume na mwongozo wa Serikali.

Waziri Mhe. Selemani Said Jafo amewaagiza Wakuu wa Mikoa na Wakuu wa Wilaya kuwasilisha taarifa ya shule ambazo zimetoza michango kinyume na mwongozo wa Serikali ifikapo Ijumaa wiki hii (tarehe 19 Januari, 2018) ili hatua zichuliwe dhidi ya walimu na maafisa elimu ambao kwa makusudi wamekiuka mwongozo huo.

Gerson Msigwa

Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, IKULU

Dar es Salaam

17 Januari, 2018

viwanda vimegoma

manunuzi ya wapinzani bado hayajabadili upepo

SGR imebuma

Bombardier ndo hivyo tena

uchumi ndo kwishney

makinikia holaaa!

kwahiyo kilichobaki ni kumpa kiki ni elimu bure lakini bado miaka 2 tu.
 
Na utakuta kuna watanzania wenye akili zilizotimia wanaoshangilia uamuzi huu wa Magufuli wakati watoto wao hawapati elimu inayofaa. Shule ya msingi ya kijiji chetu mwaka huu imesajili jumla ya wanafunzi 733 na kuna darasa moja tu lenye uwezo wa kubeba wanafunzi 25. Sasa hawa wanafunzi 726 wanaobaki watakaa wapi? Kuna mwalimu mmoja tu wa darasa la kwanza. Mwalimu huyu atamuduje kuwafundisha watoto hawa wote ndani ya darasa moja? Hii nchi aliyeiroga kafa.
 
Binafsi yangu sioni taabu kutoa michango kwa shule ili mwanangu asome kwa raha
Inapendeza kama watoto watakula mchana shule
Wafanye test na mitihani iliyochapishwa
Hivi hao watoto watakulaje shuleni bila michango wakati serikali haitoi fedha ya chakula? Hii ni nchi ya kiqumer sana.
 
Ile habari iliyoletwa hapa jana JF huenda ndio chanzo.

Hata hivyo,marufuku hii inaweza kuwa ni ya kisiasa tu ili iripotiwe na vyombo vya habari na mkulu aonekane amechukua hatua lakini mambo yakawa ni yale yale tu.

CCM sio watu wa kuwaamini hata kidogo.
Marfuku hii wala sio ya kwanza...marufuku iliwahi kutolewa mara ya kwanza na haikuleta tofauti yeyote...bado mambo yalibaki vilevile. CCM ni mijitu yenye akili za kiqumer sana.
 
Ipo siku ukweli utafahamika tu! Je mzazi upo tayari mwanao ashinde njaa toka asubuhi hadi saa tisa na nusu? Shule nyingi za kata hazina hosteli na hazina ruzuku ya chakula! Leo tunashangilia marufuku ya mchango wwote kutozwa kwa mwanafunzi. Bilashaka inajumuisha kuhusu masuala ya vyakula na malazi. Tutegemee utoro utaongezeka mashuleni ,

Na pia tutegemee kizazi cha watu wavivu kuongezeka!Elimu ndio sehemu muhimu kwa nchi yyte ili iweze kustawi,miradi mingi tu ya elimu hasa ktk shule za kata imesimama, kwa mfano maabara nyingi zimebaki pale alipoziacha Jk, hatuwezi kuwa na uchumi imara kama misingi ya kuzalisha nguvu kazi inachezewa, ni heri basi ibaki kuwa elimu bure idhamini ruzuku ya ada lakini miundo mbinu ya kuifanya elimu iwe bora ni lazima mwananchi ashiriki, kwa mfano kujenga hosteli bora za wanafunzi, madarasa safi, uhakika wa vifaa vya kujifunzia, uhakika wa chakula kwa watoto wao hasa shule za kata sabu hazina ruzuku ya chakula
 
Ikatokea watu wenye akili za kishitholes, madiwani wa ccm wakaona gere dhidi ya Mwl Yule nakumtilia vikwazo na kashfa mbaya sana wakidai eti anaiba pesa anajikusanyia mfukoni.

Wakti huo tulikuwa tunalipa fedha elfu 12 kwa mlo wa miezi mitatu.

Baada ya kuona mwl anahangaishwa kwa vitu vya kipumbavu na wakati anatengeneza maisha ya watoto wao aliamua kuitisha kikao kikubwa sana akahudhuria mkurugenzi wa wilaya na mkuu wa wilaya, kutokana na maneno ya hivyo waliyolishwa wazazi( samahani) wa hovyo walikubaliana kusitisha zoezi la kula.

Mwl alihamishwa kituo na akafariki ndani ya miaka miwili. Shule ilianza kudidmia sana mpaka.mwaka juzi ilipata division zero 100.

Kwenye kijiji chetu karibu kila familia au jirani au rafimi yako kwao kuna mtoto mwenye divisio ZERO.

R.I.P Mwl Claudio Kaseha shule ya sekondari Munanila.

NATIONAL EXAMINATIONS COUNCIL OF TANZANIA

CSEE 2015 EXAMINATION RESULTS

S0585 MUNANILA SECONDARY SCHOOL

DIV-I = 0; DIV-II = 1; DIV-III = 9; DIV-IV = 59; DIV-0 = 78

NATIONAL EXAMINATIONS COUNCIL OF TANZANIA

CSEE 2016 EXAMINATION RESULTS

S0585 MUNANILA SECONDARY SCHOOL

DIV-I = 1; DIV-II = 4; DIV-III = 7; DIV-IV = 58; DIV-0 = 37
 
Back
Top Bottom