Rais Magufuli akutana na mawaziri wa Elimu na TAMISEMI, apiga marufuku michango ya aina yoyote shuleni

Jembekillo,
Mkuu,

Neno Elimu bure kwa kiswahili nilichosoma darasani miaka mimgi sana ni sentensi zenye maana zaidi ya mbili ila moja chanya ya pili ni hasi.

Hata Elimu bila malipo nayo ni yale yale.

Yaani, zinatoa maana zaidi ya mbili ambapo moja inakinzana moja kwa moja na ile iliyokusudiwa.

Mfano,
Rais, anasema "Elimu Bure"

Kwanza: Elimu pasi kutoa michango.

Pili: Elimu bure ni aina ya Elimu isiyo kuwa na tija au faida kwa mpokeaji.

Waziri. Anasema, Elimu bila malipo,
Kwanza : Hautoi hela kuipata hiyo Elimu.

Pili: Haitakusaidia maana, haina mrejesho chanya kwa anayesoma.

Kwa hiyo, wote wanapambana kutumia neno lenye muonekano na tafsiri chanya tu ila kwa bahati mbaya kiswahili kinawatupa mkono wote wawili katika kuchagua sentence au kauli mbiu sahihi.

Wangeweza kusema "Serikali itagharimia mahitaji yote ya wanafunzi kuanzia ngazi ya darasa la 1 hadi kidato cha 4".
Prof ndalichako,ninakushauri,jitafakari Sana, wizara ya elimu imekushinda, au umuombe mh Rais aigawanye uwe wizara mbili. Kwa hali ilivyo , na kwa Kasi ya Rais wetu na serikali yake unashikwa pabaya. Wazazi walianza kuchangishwa fedha tango December 2017, hadi Rais anakuja kukuambia Jana Ina maana ulikuwa huna habari? Mungy nisamee tulikutarajia utafanya makubwa baada ya kuchaguliwa ILA tumekata tamaa kabisa na utendaji Wako.vyuo vya ualimu vimechoka,idara za elimu kwenye halimashauri zimechoka,walimu wamekata tamaa, majengo ya sule na vyou yamechoka,vyuo vikuu navyo hivyo hivyo.
 
Kuna shule mtoto analipa ada milioni tatu (Private ) lkn kuna shule za serikali zinapata hela isiyozidi milioni kumi Kwa mwaka (Ada ya wanafunzi watatu wa private).Hivi hii shule itakuja kufanya vizuri kweli? Wazazi tukazane kutafuta hela watoto wetu wasome shule Bora hizi za bure naona ni mbinu ya kutufanya tuendelee kuwa wajinga
 
Elimu bure ni wazo zuri lkn utekelezaji wake umekuwa ni mzigo.
Ila inasaidia kuleta ajira Kwa wengine maana huenda vijiwe vya tuition vikawa na soko kuliko wakati wowote.
Halafu na Mwenge nao ungekuwa unakimbizwa bure siyo kuhangaisha watanzania kuchangia Mwenge,bora kuchangia Elimu lkn siyo Mwenge
 
hiyo kauli iliyo tolewa na Mzee mkubwa ni nzuri lkn itafuatiliwa kuhakikisha haki inatendeka kwa wananchi na wakuu wa wilaya au itaishia ewani
 
Waziri wa elimu anapwaya mnoo mh. Raisi ,michango ilirudi kwa kazi sana. Halafu waziri anakaa tu ofisini . Nakushauri fukuza Huyo waziri . huwezi kuwa na waziri wewe unaagiza maagizo hakuna mzazi kuchangishwa halafu yeye muda huo huo anasema michango wazazi wasilazimishwe watoe kwa hiari yao. Hata anachokiongea hakijui. Hiyo wizara apewe MTU mfuatiliaji sio mkaaji wa ofisini . apewe kigwangala.

Hapana, Waziri anachoshindwa ni uwezo wa kumshauri tu Rais kuhusu gharama halisi za kuendesha shule hizi. Mimi ni mjumbe wa kamati moja ya shule wa fulani kule mkoani. Ukweli ni kwamba gharama za kuendesha shule ziko juu by far kuliko hela inayotumwa shuleni pale. Mwalimu Mkuu anachanganyikiwa nini afanye, badala yake inamlazimu abuni njia zake za kupata fedha kama vile michango ya chakula, masomo ya ziada, safari za kimasomo, ulinzi, nk.

Bahati mbaya mwalimu na Waziri hawaruhusiwi kusema hela haitoshi. Jamani msioongeeongee tu humu bila kufahamu ukweli wa mambo. Unaweza kufurahia maagizo kwakuwa yanakufurahaisha lakini maagizo hayo yakatafuna hatima ya mwanao kielimu.

Achilia mbali kuendesha shule lakini hata kipato cha mwl kiko chini saana kuweza kuimudu kazi yake, hasa kwa yule mwl ambae amenunua kigari cha mkopo au cha kupewa na "mtu" na kukiendesha barabarani kila siku kufika kazini.

Hii ni kawaida kama mama nyumbani akipewa hela kidogo za matumizi atatumia mbinu hata chafu kupata hela.
 
Mkuu una mtoto au ndugu anayesoma shule ya serikali ya kutwa? Kule hakuna bajeti ya serikali ya chakula inayoenda huko. Je, Wazazi wakukubaliana kuchanga pesa ya uji na ugali mchana ni kosa? Ni vizuri ukafanya utafiti ili ujiridhishe kuliko kulaumu upande mmoja na kusifia kauli unazofikiri ni sahihi hata kama zimetoka kwa nani
Pesa ikusanywe na Mkurugenzi sio Mwl, mkurugenzi ndiye atakayenunua chakula cha wanafunzi, c/o Rais. Hawa walimu hawaaminiki kabisa. Jamani tunakwenda wapi kwanini mwalimu siku hizi haaminiki? tumemfanya nini?
 
tunakoelekea ni kubaya bora hiyo michango ilikuwa inafanya mambo yanaenda..,poleni wadogo zangu mnaosoma hiki kipindi nasikia wengine sekondari wanakaa mpaka chini
 
Nafurah sana kuona jf inawatu wanaojali utu na heshima ya wenzao.
Pongezi kwa kila mwana jf àliye ona kuna haja ya kumkemea @jembekilio na maneno ya fedheha kwa waziri mama ndalichako
 
Pesa ikusanywe na Mkurugenzi sio Mwl, mkurugenzi ndiye atakayenunua chakula cha wanafunzi, c/o Rais. Hawa walimu hawaaminiki kabisa. Jamani tunakwenda wapi kwanini mwalimu siku hizi haaminiki? tumemfanya nini?
swala hapa sio mwl kutoaminika. Ishu ni siasa ili kuwa be mbele za wananchi huku tukiusahsu ukweli.

Shule zote hakuna bajet ya chakula so wanafunzi wale home shule wajinunulie Mandaz na kigogo. Hebu niambie huyu mtt toka saa 12 yuko shule bila menu kitasomeka?

Serikal ipeleke bajeti ya msosi wa wanafunzi mashulen
Hapo tutawaelewa
 
mimi nadhani kunawatendaji wa serikali hawaielewi vizuri kauli ya mkuu wa kaya, nafikiri mkuu angewaainishia kabisa michango ya aina ipi haiihitajiki maana sasa mkuu anasema no michango halafu watendaji wanaibuka na tumichango fulani fulani mara hela ya mlinzi mara hela ya karatasi za kufanyia mtihani bongo bana kazi ipo understanding yetu sijui inakuaje
 
Taarifa haijakamilika ila kwa maoni yangu binafsi Kuna kutokuelewana Kati ya rais Na watendaji wake. Rais anasema marufuku michango ya aina yoyote shuleni wakati huo watendaji Na wawakilishi wake wanachangisha michango kila Leo Na baadhi ya maDC wanahamasisha michango.

Na niliwahi kumsikia waziri wa tamisemi aliyepita bwana simbachawene anasema kilichoondolewa Ni ada Na Kama michango imekubaliwa na wazazi basi ichangwe na mzazi asiyechanga achukuliwe hatua.

naona Kuna watumishi wanataka kumchonganisha rais magufuli na wananchi wake au hawamwelewi rais au rais nae ndo walewale.

nilicheka siku moja rais kasema elimu bure waziri anasema sio elimu bure Ni elimu bila malipo sasa sijui tofauti Ni nini.
Kuna tatizo linalonyemelea taifa. Bahati mbaya kauli ya Rais ni amri..
Sijaona sababu ya kuwaita mawaziri wale wawili Ikulu kuwapa maagizo. Mmoja ni Waziri ndani ya ofisi yake na mwingine wa Elimu. Ningekuwa yeye (lakini siitamani kazi yake hata kwa mabilioni) lingekuwa ni suala la baraza zima la mawaziri, baada ya kupokea ushauri kutoka Wizara zote au Kurugenzi za Elimu. Sio kweli kwamba walimu wanachangisha hela wanafunzi kwa manufaa yao. Hali ni mbaya sana mashuleni, na kile wanachoweza hukitumia mara na wapo wazazi wanaweza kushuhudia hili.

Kinachofanyika sasa ni kufanya zile shule ambazo changamoto yao kubwa ilikuwa ni gharama za kujiendesha- maana ya vitabu na madaftari, na sasa walikuwa wanaelekeza jitihada kwenye kuboresha, kukata tamaa. Wakurugenzi wengi ni wageni- wana majukumu makubwa ya kisekta. Ujuzi wangu mdogo unaashiria katazo jipya hasa kwenye maeneo ambayo shule hazifikiki kiraisi. Ni vigumu kuona mzazi akienda kutoa mchango wa hiari kupitia MKURUGENZI- kwani mwishoni Mwl Mkuu ndiye mtekelezaji.

Naona taifa linanyemelewa na mfumo wa papo kwa papo bila kujali tunakopaswa kuendelea.
 
yaan sisi huku kwetu ndo yaleyale kuandiksha watoto tuna ambiwa mtoto anatakiwa aende na dawati au ela ya kuchongeshea dawati tena hiyo ela ya dawati apewe mwl mkuu
:confused::confused:
 
Back
Top Bottom