Rais Magufuli akutana na Balozi wa Umoja wa Ulaya (EU) Jijini Dar es Salaam

Battery

JF-Expert Member
Jul 25, 2019
263
263
Rais Magufuli leo tarehe 05 Feb2020 amekutana na Balozi wa Umoja wa Ulaya Mr. Manfred Fanti Ikulu jijini Dar es salaam. Mr. Fanti amesema mazungumzo yake na JPM yamekuwa ya manufaa makubwa ambayo yalijikita katika maendeleo ya Tanzania na kuimarisha ushirikiano mzuri uliopo kati ya Tanazania na EU.

Fanti katika mazungumzo yake amesema hivi karibuni EU wamekamilisha mazungumzo yao juu ya mpango wao wa kuendelea kuchangia katika budget ya maendeleo ya Tanzania ambapo 132 billion zilizokuwa zimezuiliwa sasa zitatolewa kwa ajili ya kuchangia katika budget ya maendeleo ya Tanzania, kwani wamefurahishwa na maendeleo makubwa yanayoendelea hapa nchini.

Wakati huo huo wanaandaa mpango mwingine wa miaka 7 ambao unaanza mwaka huu wa 2020.

Wakati huo Rais Dk. Magufuli amemshukuru Mh. Balozi Fanti kwa kazi nzuri anayofanya ya kudumisha ushirikiano mzuri kati ya Tanzania na Umoja wa Ulaya (EU).

Sent from my iPhone using JamiiForums
 
Kwa maendeleo yetu ya kisiasa, kiuchumi ,kielimu na kisayansi na kijamii Rais Magufuli hana mpinzani katika kizazi hiki
bila kumsahau BAS
Kwa maendeleo yetu ya kisiasa, kiuchumi ,kielimu na kisayansi na kijamii Rais Magufuli hana mpinzani katika kizazi hiki
BASHITE alikuwepoo
 
Balozi hakukumbuka chochote kuhusu "uchaguzi utakaokuwa huru na wa wazi" ili waTanzania waweze kuwachagua viongozi wao bila ya kuwekewa mizengwe?

Inaelekea yaliyoletwa hapa JF ni kama 'propaganda' ya upande mmoja.

Mbinu hizi zinaeleweka kwa watu wanaotumia akili kuzielewa.
 
Balozi hakukumbuka chochote kuhusu "uchaguzi utakaokuwa huru na wa wazi" ili waTanzania waweze kuwachagua viongozi wao bila ya kuwekewa mizengwe?

Inaelekea yaliyoletwa hapa JF ni kama 'propaganda' ya upande mmoja.

Mbinu hizi zinaeleweka kwa watu wanaotumia akili kuzielewa.
Unataka balozi ndio akufanyie uchaguzi uwe huru na haki?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom