Rais Magufuli aidha amedanganywa kuhusu Barakoa au kuna tatizo sehemu (kwa alichoongea leo Feb 21, 2021)

n00b

JF-Expert Member
Apr 10, 2008
1,006
2,667
Wakuu,

Nimemsikiliza Rais Magufuli akiwa anaongea leo kanisani. Nimeshtuka, Rais anaongea kama layman kabisa. Hii ni hatari kwa Usalama wa Taifa kwa mtu ambaye amepewa dhamana ya juu kabisa hapa nchini.

Rais ni Comforter-in-Chief hivyo kama mfariji mkuu wa Taifa ana mamlaka makubwa aliyobebeshwa na hili inaelekea Magufuli analisahau sana. Huwezi toka huko na kuanza kuwambia watanzania eti “Kufa tutakufa tu”.

Rais ni kama BABA katika familia, na kwa Taifa yeye anasimama kama kichwa cha familia. Huwezi kuwa baba bora ukawa unatishia watu wako (wanao, mkeo, ndugu n.k). Kama baba, unaweza kulaumiwa, unaweza kuliliwa, unaweza kupongezwa, unaweza kuumizwa na hatutarajii kuwa utaitangazia familia kuwa wakome kufanya hivyo! Utakuwa umeshindwa kutekeleza majukumu yako.

Rais ni KIUNGO katika Taifa. Unapotokea mgawanyiko, ana wajibu wa kuhakikisha Watanzania wanakuwa wamoja. Hili limekuwa likionekana kuwa tofauti kwa Rais wetu huyu.

Rais anapotoa kauli, ni kauli ya Taifa si yake. Mambo mengi anayoongea Magufuli watanzania walio wengi (wanaojielewa) watakubaliana nami kuwa si yale ambayo kimataifa tungependa kiongozi wetu ayaongee kwa niaba yetu!

Msikilize:



Sasa:

1) Magufuli leo kaongea UONGO mwingi kuhusu barakoa. Alichokiongea ni matusi kwa serikali yake mwenyewe!

- Kama barakoa zilizoingizwa nchini zina virusi au hazifai; kwanini watendaji wake wameziacha ziingizwe sokoni? Anataka kutuambia kuwa TBS na TFDA hawajui kazi yao? Kwanini watendaji wakuu wa taasisi hizi bado wapo kazini?

- Tukubali kuwa tumeingiziwa barakoa zenye kuwa na virusi ambazo zitawaua watanzania: Kwanini Mkurugenzi wa Idara ya Usalama wa Taifa, IGP na CDF bado wapo kazini? Taifa letu manake usalama wake upo hatarini. Kwa mantiki hiyo, maduka ya madawa yavamiwe mara moja na barakoa zote ziondolewe sokoni

2) Magufuli amekuwa Rais wa kwanza mimi kumuona akiwa anahubiri katika Ibada za Kanisa Katoliki. Huu ni utaratibu wa kawaida kwa wakatoliki? Halafu anawachamba viongozi wa kanisa kwa kuhimiza waumini kujilinda?

3) Rais ametangaza dawa kadhaa kama Bupiji, COVIDOL etc, anataka kuwaaminisha watanzania kuwa Sayansi nyingine haifanyi kazi tena? Kuwa watanzania wasiziamini dawa nyingine zinazotolewa hospitali tena? Haya matangazo ya dawa za asili imekuwaje hadi wasaidizi wake wamwacha hadi ataje baadhi ya dawa moja kwa moja (kwa kutaja baadhi tu)? Ana maslahi nazo? Nasikia mtu aliwahi kuwa RC wa Dar ana mkono kwenye pharmacy chain flani, na kuna tetesi kuwa yupo kwa niaba ya ‘mzee’; hii haoni inazidi kujenga hisia zisizo sahihi?

Nitarejea
 
Anasema watu wanakufa kwa mipango ya Mungu. Anajivua lawama kwamba hata watu wafe wangapi yeye hahusiki, hana uwezo wala jukumu la kuzuia hilo.

Ana uwezo mdogo sana wa kufikiri na anawapa kazi sana wasaidizi wake. Nahisi wameamua wamuache tu!
 
- Kama barakoa zilizoingizwa nchini zina virusi au hazifai; kwanini watendaji wake wameziacha ziingizwe sokoni? Anataka kutuambia kuwa TBS na TFDA hawajui kazi yao? Kwanini watendaj
Leta ushahidi wa barakoa zilizoingizwa nchini bila uhakiki wa taasisi husika!
 
Ndugu n00b, nimefurahi kukuona tena jukwaani.

Wewe ukiwa mkongwe mwenzangu wa JamiiForums, tafadhali sana nakuomba utuwekee video ya Mh. JPM aliyaongea hayo ili tuweze kujadili tukiwa na uhakika wa alichotamka.

Wengine tulipo hatuna access ya Youtube, mainstream media na social media zaidi ya JamiiForums.

Akhsante.
 
Leta ushahidi wa barakoa zilizoingizwa nchini bila uhakiki wa taasisi husika!
Mkuu,

Umenisoma vema? Msikilize Magufuli wewe mwenyewe umsikie anachoongea.

Inauma sana kuwa Kiongozi wetu anaongea mambo juu juu bila ninyi wasaidizi wake kumwambia yanamaanisha nini.

Sijasema zimeingizwa barakoa bila uhakiki bali kauli zake zinaleta tafsiri hiyo.

Kimsingi, anatuambia sisi raia wa kawaida kwamba we are vulnerable as a nation.

Msiweke propaganda mbele badala ya Utaifa kwanza. Tunaaibika pamoja kama Taifa!
 
Ndugu n00b, nimefurahi kukuona tena jukwaani.

Wewe ukiwa mkongwe mwenzangu wa JamiiForums, tafadhali sana nakuomba utuwekee video ya Mh. JPM aliyaongea hayo ili tuweze kujadili tukiwa na uhakika wa alichotamka.

Wengine tulipo hatuna access ya Youtube, mainstream media na social media zaidi ya JamiiForums.

Akhsante.
Mkuu,

Nimewaomba Mods wanisaidie kuiweka video. Nipo, nilikuwa nachungulia zaidi hapa maana maisha ya sasa ni mchakamchaka sana.

Magufuli kasababisha nishindwe kuvumilia kwani najua baadhi ya wasaidizi wake ni wana JF wenzetu humu ambao tumekuwa pamoja katika mambo mengi ila kwa sasa ndo wanaendesha serikali.

Inasikitisha kuwa Rais anaweza kuteleza hivi na wasaidizi wake waone sawa.

Nimependa approach ya wasaidizi wake kutoa tamko ambalo kalirusha Msigwa likiwa limeandikwa kwa weledi na baadae la Wizara ya Afya ingawa bado kuna ukakasi mwingi.

Public Health si sehemu ya kufanyia siasa za mizaha, unakuwa unacheza na Usalama wa Taifa lako! Wananchi kufa au kuugua si jambo la mzaha hata kidogo
 
Barakoa zina corona,chanjo ina madhara makubwa ikiwemo kuwafanya wanawake wagumba na wanaume mazezeta, social distance ni njia ya kutuletea hofu na kufanya tusizaliane hakuna corona ni magonjwa ya kawaida ya changamoto ya kupumua(serikali).

Wataam wa afya na vyombo vya dini 'corona ipo tuchukue tahadhari za kuvaa barakoa,social distance na kufwata ushauri wa wataalam wa afya'.

Hivi hii chanjo aliyo chanjwa biden,Obama,prince Philip,Queen Elizabeth, Putin na viongozi wengine wakubwa ndiyo iyo tunaambiwa si salama?. Tujaribu kuwaza tu hyprocratic politicians kama yule anaye vaa tai ya taifa,yule prof wa jalalani ni kweli hawajapigwa chanjo hadi muda huu?
 
Hujawahi kutumia dawa yoyote ya asili ikakusaidia?
Did I dispute matumizi ya dawa za asili? Hapana, nataa narrative ya kuwa barakoa wanazotumia watanzania si salama.

BCE7F206-F948-4F80-85F6-F265FADCEC0A.jpeg
 
Ana mkono kwenye barakoa za msd, barakoa za nje ni salama kabisa ndio mana zipo nchini ila hataki tuzinunue.

Vita yake ya kiuchumi anaileta kwenye uhai wetu.

Hata chanjo hazitaki sababu mwanzo zitauzwa kwa bei ndogo kuchangia gharama kwa watengenezaji , baadae zitauzwa kwa bei ya soko, hataki kutengeneza soko la chanjo za covid.
.
Anataka tutumie mikorogo yake na nyungu ili apige hela za wafadhili na za covidol.
 
Kama alivyotuasa wazir mkuu pamoja na Mhe Rais, tutumie barakoa zinazozalishwa ndani kwani barakoa zinazoingizwa nchini zinaweza zisiwe salama.

Kwa mukatadha huu najaribu kujiuliza watu wanaoangalia viwango vya bidhaa wanasubiri Nini Hadi bidhaa zenye madhara zinaingia nchini bila wao kudhibiti?

Lakini pia Taifa halijashindwa kushona barakao, naamini likitolewa Tangazo la kila mtu atumie barakoa za ndani tutakuza soko lakini pia tutapunguza hatari ya wananchi kutumia barakoa zisizo na ubora au zenye madhara kwa wananchi.

Hii Ni Vita lazima viongozi wenye dhamana mjipange kuipigana. Chukue hatua mapema kuwaepusha Watanzania na madhara ya corona
 
Back
Top Bottom