Rais Magufuli aidha amedanganywa kuhusu Barakoa au kuna tatizo sehemu (kwa alichoongea leo Feb 21, 2021)

Walivyo sema serikali haina dini, ilikuwa kuwa tofauti na kidogo na nchi za Mataifa ya nje ambayo yalitutawala. Kwani yote yaliongozwa kwa mfumo wa dini, si tu dini bali dhehebu. Mfano Sweden, Ujerumani wao walikuwa Waromani baada ya Mageuzi ya Martin Luther watawala wa nchi hizo waliamua nchi zao ziwe za Kirutheri. Nyerere aliposhika madaraka akasema serikali haina dini. Hii ilimaanisha zaidi kutokuwa na kanisa au kutokuwa na imani ya Uislamu itakayo ongoza Taifa. Hii ndo maana ya serikali haina dini. Ila serikali inaamini Mungu yupo na watu wake wanadini.
Rais hajaongelea dini. Ameongelea mambo ya kitaifa kwa ujumla yanayowagusa wananchi wake. Ndo maana hata kanisa au uslamu wanaongelea mambo ya jamii. Mfano makanisa kadhaa yametoa waraka juu ya tahadhari za Covid 19. Uwezi tenganisha policy na kanisa. Serikali inakataza kutenda maovu, pia dini inakataza kutenda maovu. Ndini ipo kuboresha au kujenga imani ya mtu kwa Mungu wake lakini ipo pia kujenga maisha ya kijamii na huduma mbalimbali. Ndo maana dini au madhehebu yanatoa huduma za kijamii ambazo utolewa na serikali. Nenda kokote duniani uwezi tenganisha. Dini uwafunza watu maisha ya ujasiriamali, afya, elimu, na mazingira haya yote ufanywa chini ya sera za serikali.
Rais alichoongelea ni tahadhari ya kiafya kwa ujumla, hakubagua wala kuonesha maswala ya kidini. Rais ni wa wote, anapo pata nafasi ataongelea maswala ya kitaifa. Si rais wa kwanza kuhudhuria ibada. Marais wengi ufanya hivyo na ndiyo maana wakati wa sherehe za Idd kwa waislamu ualika viongozi wa kitaifa awe Rais, Makamu, hata Waziri Mkuu kuhutubia. Ili limekuwepo toka uhuru na uwa haijarishi Rais ni Mwislamu au lah! Kipindi hicho Rais uweza kutoa sadaka kwa vituo mbalimbali vya watoto yatima mfano Mbuzi, mafuta ya kula, sukari na kadharika. Kwa wakristo pia wakati wa Krismas au Pasaka ualika viongozi wa kitaifa. Limekuwepo miaka yote.
Tuache chuki, hata kama tutaweka chuki yeye tayari ni Rais haito saidia. Kikubwa ni nchi yetu sote tusikae kufatilia vitu vidogovidogo visivyo jenga jamii. Tuwe wabunifu tujenge Taifa letu. Hapo ulipo jiulize umefanya nini kwa jamii. Siyo kukashifu kupinga. Hivi hata tukifa Mungu akakuuliza nilikuweka duniani nini ulifanya jibu hakuna. Tukosoe kwa kuwa na mawazo mbadala yatakayo leta ufanisi kwa jamii. Je rais kuongea vile kaathiri imani ya mtu?
Umeeongelea Kuhusu issue za kitaifa pale kaongelea issue za Taifa. Unaposema issue ikihusu ulevi ikaongelewa bar unanishitua kidogo. Mfano baba akiwa na mtoto mlevi atamchukua wakaongelee bar. Kama hatahitaji mkanya mtoto juu ya ulevi. Wazazi wengi hata akikosea mtoto mmoja. Mfano ni mlevi mara nyingi mzazi uweka kikao cha familia ili kuweka funzo kwa watoto wote. Corona ni issue ya Taifa na kimataifa, kilichoongelewa pale ilikuwa kwa manufaa ya Taifa.
Ubarikiwe,
Wasalaam Walykum!
Hatukatai anaweza kuzungumza ila hawez kuingilia utaratibu wa kanisa kwasababu kanisa hupokea miongozo kutoka kanisa kuu ambao wanaamini yanatoka mbinguni. Je ni sahihi rais kulipa muongozo kanisa katholic tofauti na papa? Je kwann rais akejeli waumini hadhari kwsababu mamb ya imani kila mtu anaongozwa na Mungu kwa namna yake na hakuna uthibitisho wa macho unaoona nani nd kaongozwa vizuri. Ndyo maan bible inasema usikuhumu usihukumiwe. Yule ajionae mkubwa kuliko wote basi nae ni mdogo kati yao katika ufalme wa mbingu. Je unawezaje kumuambia mtu kuwa huna Imani ndo maan unavaa barakoa wakati huo umeingia na bunduki kanisani? Kumbuka story ya mtoza ushuru na farisayo.
NB: TUENDELEE KUMTEGEMEA MUNGU ATUVUSHE KATIKA HILI PIA TUSISAHAU KOMBEO ZETU WAKATI WA KUPAMBANA NA GOLIATH MAAN TUKIMKABIDHI MUNGU HIZO KOMBEO HUWA HATARI KULIKO PANGA LA GOLIATH. AMEN.

Sent from my SM-J111F using JamiiForums mobile app
 
Rais wa Tunisia anasema Mungu atatulinda wakati yeye anatembea na mamia ya walinzi kwanini asimtegemee Mungu kumlinda..
 
Wakuu,

Nimemsikiliza Rais Magufuli akiwa anaongea leo kanisani. Nimeshtuka, Rais anaongea kama layman kabisa. Hii ni hatari kwa Usalama wa Taifa kwa mtu ambaye amepewa dhamana ya juu kabisa hapa nchini.

Rais ni Comforter-in-Chief hivyo kama mfariji mkuu wa Taifa ana mamlaka makubwa aliyobebeshwa na hili inaelekea Magufuli analisahau sana. Huwezi toka huko na kuanza kuwambia watanzania eti “Kufa tutakufa tu”.

Rais ni kama BABA katika familia, na kwa Taifa yeye anasimama kama kichwa cha familia. Huwezi kuwa baba bora ukawa unatishia watu wako (wanao, mkeo, ndugu n.k). Kama baba, unaweza kulaumiwa, unaweza kuliliwa, unaweza kupongezwa, unaweza kuumizwa na hatutarajii kuwa utaitangazia familia kuwa wakome kufanya hivyo! Utakuwa umeshindwa kutekeleza majukumu yako.

Rais ni KIUNGO katika Taifa. Unapotokea mgawanyiko, ana wajibu wa kuhakikisha Watanzania wanakuwa wamoja. Hili limekuwa likionekana kuwa tofauti kwa Rais wetu huyu.

Rais anapotoa kauli, ni kauli ya Taifa si yake. Mambo mengi anayoongea Magufuli watanzania walio wengi (wanaojielewa) watakubaliana nami kuwa si yale ambayo kimataifa tungependa kiongozi wetu ayaongee kwa niaba yetu!

Msikilize:



Sasa:

1) Magufuli leo kaongea UONGO mwingi kuhusu barakoa. Alichokiongea ni matusi kwa serikali yake mwenyewe!

- Kama barakoa zilizoingizwa nchini zina virusi au hazifai; kwanini watendaji wake wameziacha ziingizwe sokoni? Anataka kutuambia kuwa TBS na TFDA hawajui kazi yao? Kwanini watendaji wakuu wa taasisi hizi bado wapo kazini?

- Tukubali kuwa tumeingiziwa barakoa zenye kuwa na virusi ambazo zitawaua watanzania: Kwanini Mkurugenzi wa Idara ya Usalama wa Taifa, IGP na CDF bado wapo kazini? Taifa letu manake usalama wake upo hatarini. Kwa mantiki hiyo, maduka ya madawa yavamiwe mara moja na barakoa zote ziondolewe sokoni

2) Magufuli amekuwa Rais wa kwanza mimi kumuona akiwa anahubiri katika Ibada za Kanisa Katoliki. Huu ni utaratibu wa kawaida kwa wakatoliki? Halafu anawachamba viongozi wa kanisa kwa kuhimiza waumini kujilinda?

3) Rais ametangaza dawa kadhaa kama Bupiji, COVIDOL etc, anataka kuwaaminisha watanzania kuwa Sayansi nyingine haifanyi kazi tena? Kuwa watanzania wasiziamini dawa nyingine zinazotolewa hospitali tena? Haya matangazo ya dawa za asili imekuwaje hadi wasaidizi wake wamwacha hadi ataje baadhi ya dawa moja kwa moja (kwa kutaja baadhi tu)? Ana maslahi nazo? Nasikia mtu aliwahi kuwa RC wa Dar ana mkono kwenye pharmacy chain flani, na kuna tetesi kuwa yupo kwa niaba ya ‘mzee’; hii haoni inazidi kujenga hisia zisizo sahihi?

Nitarejea

Jamaa Jinga sana yan; eti linasimama hadharani kabisa linatangazia dunia kuwa kuna dawa ya Corona inaitwa "Bubej"....Jinga kabisa, hovyo kabisa!
 
Wakuu,

Nimemsikiliza Rais Magufuli akiwa anaongea leo kanisani. Nimeshtuka, Rais anaongea kama layman kabisa. Hii ni hatari kwa Usalama wa Taifa kwa mtu ambaye amepewa dhamana ya juu kabisa hapa nchini.

Rais ni Comforter-in-Chief hivyo kama mfariji mkuu wa Taifa ana mamlaka makubwa aliyobebeshwa na hili inaelekea Magufuli analisahau sana. Huwezi toka huko na kuanza kuwambia watanzania eti “Kufa tutakufa tu”.

Rais ni kama BABA katika familia, na kwa Taifa yeye anasimama kama kichwa cha familia. Huwezi kuwa baba bora ukawa unatishia watu wako (wanao, mkeo, ndugu n.k). Kama baba, unaweza kulaumiwa, unaweza kuliliwa, unaweza kupongezwa, unaweza kuumizwa na hatutarajii kuwa utaitangazia familia kuwa wakome kufanya hivyo! Utakuwa umeshindwa kutekeleza majukumu yako.

Rais ni KIUNGO katika Taifa. Unapotokea mgawanyiko, ana wajibu wa kuhakikisha Watanzania wanakuwa wamoja. Hili limekuwa likionekana kuwa tofauti kwa Rais wetu huyu.

Rais anapotoa kauli, ni kauli ya Taifa si yake. Mambo mengi anayoongea Magufuli watanzania walio wengi (wanaojielewa) watakubaliana nami kuwa si yale ambayo kimataifa tungependa kiongozi wetu ayaongee kwa niaba yetu!

Msikilize:



Sasa:

1) Magufuli leo kaongea UONGO mwingi kuhusu barakoa. Alichokiongea ni matusi kwa serikali yake mwenyewe!

- Kama barakoa zilizoingizwa nchini zina virusi au hazifai; kwanini watendaji wake wameziacha ziingizwe sokoni? Anataka kutuambia kuwa TBS na TFDA hawajui kazi yao? Kwanini watendaji wakuu wa taasisi hizi bado wapo kazini?

- Tukubali kuwa tumeingiziwa barakoa zenye kuwa na virusi ambazo zitawaua watanzania: Kwanini Mkurugenzi wa Idara ya Usalama wa Taifa, IGP na CDF bado wapo kazini? Taifa letu manake usalama wake upo hatarini. Kwa mantiki hiyo, maduka ya madawa yavamiwe mara moja na barakoa zote ziondolewe sokoni

2) Magufuli amekuwa Rais wa kwanza mimi kumuona akiwa anahubiri katika Ibada za Kanisa Katoliki. Huu ni utaratibu wa kawaida kwa wakatoliki? Halafu anawachamba viongozi wa kanisa kwa kuhimiza waumini kujilinda?

3) Rais ametangaza dawa kadhaa kama Bupiji, COVIDOL etc, anataka kuwaaminisha watanzania kuwa Sayansi nyingine haifanyi kazi tena? Kuwa watanzania wasiziamini dawa nyingine zinazotolewa hospitali tena? Haya matangazo ya dawa za asili imekuwaje hadi wasaidizi wake wamwacha hadi ataje baadhi ya dawa moja kwa moja (kwa kutaja baadhi tu)? Ana maslahi nazo? Nasikia mtu aliwahi kuwa RC wa Dar ana mkono kwenye pharmacy chain flani, na kuna tetesi kuwa yupo kwa niaba ya ‘mzee’; hii haoni inazidi kujenga hisia zisizo sahihi?

Nitarejea

Magufuli ni idd amini wa Tanzania, anafanana naye kwa kila kitu
 
Hoja ya vita ya uchumi naifananisha na ile kauli kuwa mkiwachagua wapinzani kutatokea vita
 
Huyu mzee kavu sana
Vitambulisho vya utaifa vina saini ambayo ipo ndani kama security
Na kwa hilo walipewa zawadi

Yeye akaja na ya kuwadanganya Tanzania kuwa kitambulisho hakina saini

Leo hii yy peke yake ndo anaona ana uwezo wa kuzuia uhujumu kuliko hata vyombo vya usalama

Anapokuja na sababu za barakoa naona ni yale yale ya vitambulisho vya taifa ili afanye yake

Kimsingi huyu jamaa hatufai,anatumia ofisi kuu nchini kufanya yake na ni huyu huyu atakayeangamiza watu ikiwa anaona cake yake inanyemelewa

Hana utu

Azory na saa nane wameuliwa na jamaa 1 mlafi sana
 
Utter trash...! Udhihirishwa kwa "uvundo" wake. Tuonyeshe uvundo wa hicho unachokiita trash!!!

Kabla ya kupeleka sampuli za oil, kware, mbuzi nakadhalika...si tulikuwa tunaambiwa vipimo vya korona viko vizuri!? Je. Nini kilitokea baada ya hapo!?
Wewe utakuwa mjinga,do think kipimo kinachopima mtu Kama ana mimba kinaweza kikapima Kama mbuzi pia ana mimba? Unajua maana ya gabage in gabage out? Kupima mapapai na nini sijui was nonsense act from layman individuals.Lakini pia Kama vipimo vilikuwa vibovu na vikaingia nchi kutumika ni hatua gani zilichukuliwa kwa wadhibiti ubora wa bidhaa zinazotumika nchi hii?
 
Wewe utakuwa mjinga,do think kipimo kinachopima mtu Kama ana mimba kinaweza kikapima Kama mbuzi pia ana mimba? Unajua maana ya gabage in gabage out? Kupima mapapai na nini sijui was nonsense act from layman individuals.Lakini pia Kama vipimo vilikuwa vibovu na vikaingia nchi kutumika ni hatua gani zilichukuliwa kwa wadhibiti ubora wa bidhaa zinazotumika nchi hii?
Jioni njema, nikiamini upo nchini Tanzania.
 
Mkuu ukweli ni kwamba, hadi sasa mask hazijaweza kuondolewa zote mtaani. Mfano mimi hapa nina box mbili za mask za kichina ambazo nilizinunua mwaka jana April, nilitumia chache tu kabla serikali haijahimiza matumizi ya mask za kushona wenyewe. Hivyo bado kama Rais ana wajibu wa kuwakumbusha watu kuhusu hilo. Sasa hivi serikali imeweka mazingira magumu ya uingizwaji wa hizo mask, na pia inafanya misako na ukaguzi wa kushtukiza kwenye outlets zote zinazofahamika kwa wakati huu. Na kingine imewapa nguvu MSD kufanya uzalishaji mkubwa ili kuziba pengo la imported masks.
Mkuu sijui kama we ni mwanabailojia?

Virus labda wakiwekwa kwenye barakoa wataishi kwa muda gani?

Una wasi wasi nazo ila hujazichoma moto,ukimaanisha hata ww unatishia usalama ambao raisi anaupigania

Na hujaitaji kabisa kuwashtaki china au kampuni husika?

Yewezekana sisi tunamvesha raisi taji la miba au raisi na wewe mnatuvalisha taji la miba


Beli beli mia 5
 
2) Magufuli amekuwa Rais wa kwanza mimi kumuona akiwa anahubiri katika Ibada za Kanisa Katoliki. Huu ni utaratibu wa kawaida kwa wakatoliki? Halafu anawachamba viongozi wa kanisa kwa kuhimiza waumini kujilinda?
Aaah, inawezekana alikuwa akimjibu Askofu R'uaichi?

Naanza kuona msukumo wa hoja yake potofu.

Huyu jamaa ni mtu wa ajabu sana. Ana matatizo.

Sijui kama anaweza kukubali kupewa msaada; lakini anahitaji msaada.
 
Sisi tuna subiri kuandikwa kitabu chake kusoma kuwa alijutia kama mwenzake.
Hapana.
Kitabu cha huyu kitasomeka kama "Fiction" hivi!

Na movie yake itakuwa 'blockburster'.

Kitabu cha yule mwingine kilikuwa ni serious stuff na boring kukisoma.
 
Wakuu,

Nimemsikiliza Rais Magufuli akiwa anaongea leo kanisani. Nimeshtuka, Rais anaongea kama layman kabisa. Hii ni hatari kwa Usalama wa Taifa kwa mtu ambaye amepewa dhamana ya juu kabisa hapa nchini.

Rais ni Comforter-in-Chief hivyo kama mfariji mkuu wa Taifa ana mamlaka makubwa aliyobebeshwa na hili inaelekea Magufuli analisahau sana. Huwezi toka huko na kuanza kuwambia watanzania eti “Kufa tutakufa tu”.

Rais ni kama BABA katika familia, na kwa Taifa yeye anasimama kama kichwa cha familia. Huwezi kuwa baba bora ukawa unatishia watu wako (wanao, mkeo, ndugu n.k). Kama baba, unaweza kulaumiwa, unaweza kuliliwa, unaweza kupongezwa, unaweza kuumizwa na hatutarajii kuwa utaitangazia familia kuwa wakome kufanya hivyo! Utakuwa umeshindwa kutekeleza majukumu yako.

Rais ni KIUNGO katika Taifa. Unapotokea mgawanyiko, ana wajibu wa kuhakikisha Watanzania wanakuwa wamoja. Hili limekuwa likionekana kuwa tofauti kwa Rais wetu huyu.

Rais anapotoa kauli, ni kauli ya Taifa si yake. Mambo mengi anayoongea Magufuli watanzania walio wengi (wanaojielewa) watakubaliana nami kuwa si yale ambayo kimataifa tungependa kiongozi wetu ayaongee kwa niaba yetu!

Msikilize:



Sasa:

1) Magufuli leo kaongea UONGO mwingi kuhusu barakoa. Alichokiongea ni matusi kwa serikali yake mwenyewe!

- Kama barakoa zilizoingizwa nchini zina virusi au hazifai; kwanini watendaji wake wameziacha ziingizwe sokoni? Anataka kutuambia kuwa TBS na TFDA hawajui kazi yao? Kwanini watendaji wakuu wa taasisi hizi bado wapo kazini?

- Tukubali kuwa tumeingiziwa barakoa zenye kuwa na virusi ambazo zitawaua watanzania: Kwanini Mkurugenzi wa Idara ya Usalama wa Taifa, IGP na CDF bado wapo kazini? Taifa letu manake usalama wake upo hatarini. Kwa mantiki hiyo, maduka ya madawa yavamiwe mara moja na barakoa zote ziondolewe sokoni

2) Magufuli amekuwa Rais wa kwanza mimi kumuona akiwa anahubiri katika Ibada za Kanisa Katoliki. Huu ni utaratibu wa kawaida kwa wakatoliki? Halafu anawachamba viongozi wa kanisa kwa kuhimiza waumini kujilinda?

3) Rais ametangaza dawa kadhaa kama Bupiji, COVIDOL etc, anataka kuwaaminisha watanzania kuwa Sayansi nyingine haifanyi kazi tena? Kuwa watanzania wasiziamini dawa nyingine zinazotolewa hospitali tena? Haya matangazo ya dawa za asili imekuwaje hadi wasaidizi wake wamwacha hadi ataje baadhi ya dawa moja kwa moja (kwa kutaja baadhi tu)? Ana maslahi nazo? Nasikia mtu aliwahi kuwa RC wa Dar ana mkono kwenye pharmacy chain flani, na kuna tetesi kuwa yupo kwa niaba ya ‘mzee’; hii haoni inazidi kujenga hisia zisizo sahihi?

Nitarejea
Hakuna anayemdanganya huyo baba, ni uwezo tu wa ka brain kake. Saa hizi anashtuka siku ina masaa 48 nani atamdanganya?
 
Anaharibu sana separation of church and state.

Nyerere alikuwa anaenda kanisani kila siku. Si kila Jumapili. Kila siku aliyokuwa Dar alikuwa anaanza na sala St. Peters.

Mkapa yeye alienda kanisani Jumapili alivyokuwa rais.

Sikuwahi kuwasikia hawa wakisimama mbele kanisani kutoa hotuba za kisiasa.

Walijua kitu kinaitwa "separation of church and state".

Huyu wa sasa akiambiwa na Waislamu kwamba nchi inaongozwa na Mfumokristo atakataa?
Atakataa sana. Atawaambia yeye amejenga misikiti..., na mengi mengine ya kuwaneemesha wao.

Msukumo wa hiki alichokiongelea kanisani safari hii, ni kujibu moja kwa moja kauli aliyoitoa mkuu wa kanisa hilo Askofu Ru'aichi hivi juzi kuhusu matumizi ya barakoa.

Lakini katika kujibu kauli hiyo, inamfungua zaidi kiongozi huyu na kumwonyesha jinsi alivyo mtu wa matatizo makubwa.
 
Atakataa sana. Atawaambia yeye amejenga misikiti..., na mengi mengine ya kuwaneemesha wao.

Msukumo wa hiki alichokiongelea kanisani safari hii, ni kujibu moja kwa moja kauli aliyoitoa mkuu wa kanisa hilo Askofu Ru'aichi hivi juzi kuhusu matumizi ya barakoa.

Lakini katika kujibu kauli hiyo, inamfungua zaidi kiongozi huyu na kumwonyesha jinsi alivyo mtu wa matatizo makubwa.
Ansbert Ngurumo kachambua kirefu hapa.


Magufuli na “maparoko wake” wana kesi ya kujibu

[http://0]

Ansbert Ngurumo21st February 2021

NIMEMSIKILIZA Rais John Magufuli akihutubia waamini leo katika Kanisa la Mt. Petro, Dar es Salaam, na nimebaini mambo machache ambayo ni muhimu kuyajadili kwa ufupi. Nitadokeza mambo 10 tu.

Kwanza, Magufuli ameonyesha kuwa anakerwa na matamko ya maaskofu na msimamo wa Kanisa juu ya Corona. Sababu zinaeleweka. Hakutaka waseme Corona ipo kwa kuwa yeye alishasema haipo. Na sasa tutarajie kejeli, matusi ya rojorojo, vijembe na hujuma nyingi dhidi ya maaskofu. Atatumia vyombo vyake kuwabana na kuwadhalilisha.

Pili, ingawa ametamka kuwa yeye hakatazi uvaaji wa barakoa, pale pale kanisani ameonyesha kuchukizwa na uvaaji wa barakoa. Ndiyo maana amemsifu “paroko” ambaye hakuvaa, na akajaribu kumchonganisha na askofu aliyeagiza watu wavae barakoa. Ndiyo maana alimsuta sista aliyevaa barakoa na akawasifia masista ambao hawajazivaa.

Ndiyo maana alishukuru wanakwaya kwa kutovaa barakoa; akamshutumu Jaji Mstaafu Thomas Mihayo (na mkewe) kwa kuvaa barakoa; na akasisitiza kuwa wasaidizi wake hawavai barakoa. Si kwamba hawataki, bali hawawezi kuvizaa mbele yake. Yeye hataki! Sijui anapata faida gani.
Tatu, ameendelea kutumia “Jina la Mungu” kushambulia viongozi wa dini – akitaka kuonyesha kuwa kwa vile wao wanasema kuna Corona na wamehamasisha waamini kujikinga, basi viongozi hao wana imani haba! Amekuwa anayasema haya mara kwa mara awapo kanisani au hata kwenye majukwaa ya kisiasa, labda kama njia ya kuwaaminisha wananchi kuwa yeye ni mcha Mungu kuliko viongozi wao wa kiroho.
Hata leo, ametumia njia hiyo kushutumu masista na askofu – ili ionekane kwamba wanaovaa barakoa hawamtegemei Mungu. Ametumia kauli hiyo dhidi ya padri mwongoza ibada, akitaka kuonyesha kwamba kwa vile askofu aliagiza matumizi ya barakoa, na padri hakuitumia, basi amefanya vizuri kumkaidi askofu na “kumfuata Mungu” – kana kwamba Mungu anazuia matumizi ya barakoa!

Nne, rais amejaribu kukatisha tamaa wanaovaa barakoa, akawambia kuwa hizi zitokazo nje ya nchi si salama. Anawataka ama wanunue zinazotengenezwa hapa nchini au watengeneze wao wenyewe kienyeji.
Ajabu! Serikali anayoongoza ndiyo inayodhibiti ubora wa bidhaa zote zinazoingia nchini. Anataka kusema hizo mbovu zimepita wapi kuingia nchini katika mazingira ya sasa ya kujihadhari na Corona? Na kwanini mbovu ziletwe Tanzania? Na hizi anazotaka wajitengenezee, je, hazitarajiwi kuwa na viwango maalumu vinavyohitajika? Kila mmoja ajiokotee kitambaa avae ilimradi tu zimefunika midomo na pua?
Yawezekana yeye, kwa changamoto zake binafsi, akizivaa zinamdhuru kiafya. Si awaache wasio na changamoto kama zake watumie?

Tano, wakati rais anasema hayo yote, yeye anayerubuni watu kwa jina la Mungu ameingia kanisani akiwa na vikosi vya kijeshi vinavyomlinda. Mara kadhaa, walinzi wake wamekuwa wanaingilia liturjia na kusababisha vurugu isiyo ya lazima kanisani. Waamini wanasemea chini chini tu, lakini wanakerwa.
Sasa, kama yeye anamtumaini Mungu ambaye anaona wengine hawamtumaini ipasavyo, kwanini analindwa na majeshi kila aendapo, tena wakati mwingine wakiwa na silaha za kijeshi na helikopta?
Mungu huyu anayetuelekeza ameshindwa kumlinda yeye? Kwanini rais anaona fahari kuongopea Watanzania? Kwanini hapendi wajilinde? Anapata faida au furaha gani wao wakipoteza uhai – tena kizembe? Kwanini anaumia wao wanapojilinda?

Sita, rais ameendelea kudanganya wananchi kuwa mwaka jana Corona iliondoka Tanzania. Hataki kukiri kuwa kati ya Machi na Juni 2020, Tanzania ilikuwa na maambukizi machache mno yaliyokuwa yameingia, na ilikuwa imedhibiti kuenea kwa maambukizi hayo kwa sababu wananchi waliambiwa wachukue hatua, na wageni hawakuingia nchini kiholela.

Baada ya rais kutangaza kuwa hakuna Corona, watu waliacha kuzingatia masharti, waliokuwa na maambukizo wakayaeneza kirahisi, kupitia mijumuiko mingi tu – pamoja na mikutano ya kampeni za uchaguzi – sherehe, starehe, sikukuu, sokoni, kwenye ibada, na kadhalika.

Hapo hapo, wageni (watalii) wameendelea kuingia Tanzania, na baadhi yao wameeneza virusi. Hiki tunachoona sasa ni matokeo ya uamuzi wake wa mwaka jana kusema “hakuna Corona.” Mambukizi yamekuwa yanaendelea, na kirusi kinajibadilisha, na aina nyingine zimeingizwa kwa sababu ya uzembe wetu na ubabe wa rais.

Saba, wakati Magufuli anataja nchi nyingine ambazo raia wake wamekufa kwa wingi, anatumia takwimu ambazo nchi hizo zimeweka wazi kama inavyotakiwa. Anataka kutuhadaa kuwa kwa kuwa sisi hatutangazi takwimu, basi watu wetu hawaugui wala hawafi.
Kimsingi, watu waliokufa ni wengi lakini kwa kuwa hakuna takwimu, wenye kujua misiba hiyo ni hao wanaoguza na wanaofiwa. Familia zimefiwa mno. Sasa imefika mahali wakafa watu wenye vyeo vikubwa kwenye jamii ndipo wakubwa wakaanza kushtuka. Lakini kimsingi tumepoteza wananchi wengi sana. Kuficha takwimu hakuwafufui wala hakumfanyi yeye kuwa kiongozi mungwana. Sana sana rais anaonekana ni mtu asiyejali uhai wa wenzake.
Hata wagekufa wachache, sioni kwanini Magufuli haoni kuwa hawakustahili kujengewa mazingira ya kufa. Tayari amepoteza hata washauri na wasaidizi wake waandamizi – watu wake wa karibu. Yeye bado anasema “tupo salama.” Nani afe ndipo Magufuli ashtuke?

Nane, sasa ameanza kuona ukweli kuwa tunajua kwamba Corona ipo – jambo ambalo amekuwa anaepuka kulikiri. Amekuwa anatumia mimbari za makanisani kutangazia wananchi kuwa hakuna Corona. Huku ni kutumia kanisa kueneza Corona! Wanaomruhusu kufanya hivyo walipaswa wajue kwamba nao wameshiriki kuua watu.
Baada ya hali kuwa mbaya sana na maaskofu wakamruka, wakaamua kutangaza wenyewe kwa waamini wao, sasa serikali nayo inaelekea kukiri ukweli huo huo, lakini bado inasema kwa kuzunguzunguka.
Hata hivyo, hii ni hatua. Tumemtoa kwenye hali ya kukataa katakata hadi kusema “watu wachukue tahadhari.” Si jambo jepesi, hasa kwa kiongozi anayeshupaza shingo. Tuendelee kumkumbusha na kumsukuma. Hata kama hataki, ipo siku atatuelewa.

Tisa, waamini waliokuwa wanamsikiliza leo kanisani wamemnyima makofi na vigelegele kama alivyozoea. Alikuwa anajitahidi kuzungumza kwa msisitizo na kumtaja Mungu kila baada ya maneno machache, halafu anasita kidogo kungoja magofi. Wapi! Wamegoma kuyapiga.
Maana yake ni nini? Waamini nao wamempa ujumbe moja kwa moja, pale pale, kwamba wameshajua sarakasi zake za kutumia mimbari za makanisa na jina la Mungu kufanya siasa na kujitukuza. Atambue tu kuwa hawafurahi anapowakejeli maaskofu wao na kujifanya kiranja wao.

Kumi, bado Magufuli hajatambua kuwa yeye ni muumini kama wengine. Anadhani urais wake una nguvu mbele ya madhabahu.

Anaonyesha dharau ya wazi kwa viongozi wa Kanisa, anathubutu kuwagawa kwa kuwapatia sifa na zawadi baadhi yao – hasa michango na misaada ya fedha. Na kila anapokwenda kusali anawapanga mapema viongozi wa ibada wampe nafasi ya “kusalimia” waamini baada ya misa, na yeye anaitumia kueneza propaganda zake.

Kwa viwango vyovyote, Magufuli si Mkatoliki mwanana kama alivyokuwa Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere. Wala hamkaribii Rais wa awamu ya tatu Benjamin Mkapa (Mungu ampe pumziko jema).
Lakini hatukuwahi kuona marais hawa wakijitangaza na kuhutubia wananchi kila walipokwenda kanisani kusali. Walitambua nafasi yao ya uumini, si urais, mbele ya madhabahu.
Inashangaza sasa kuwa huyu ambaye amekuwa anazurura kwenye makanisa kadhaa ya kilokole kwa miaka kadhaa, aliyerejeshewa ukatoliki kwa sababu za kisiasa, kwa jitihada binafsi za Mwadhama Polycarp Kardinali Pengo miezi michache kabla ya uchaguzi mkuu 2015, ndiye anataka kuwa kiranja wa maaskofu wetu.

Ndiye huyu ambaye maparoko kadhaa wanamruhusu awaswage kama punda? Ndiyo, yeye ana matatizo yake kadhaa, tunayatambua. Lakini nadhani na hawa wanaomruhusu atumie mimbari zao kueneza uwongo unaohatarisha afya za watu, wana kesi ya kujibu. Siku moja watajibu.
 
Hivi malimau, mchaichai, tangawizi asali ni dawa ya asili. Si ni sawa na pishi kama pishi pilau. Kama uvaavyo kondom kupunguza maambukizi ya ngono na ukimwi, chandarua kuzuia Malaria. Chukua hatua kwenye Corona. Jilinde na mlinde mwenzako.
Mlinzi wa kwanza wa maisha ni wewe.
 
Kama taifa tuliishi kabla, kama taifa tutaishi baada. Uchumi tunauona bora sasa, hautokuwa bora kesho. Tuifanye Tanzania salama, tujilinde na tulinde wapendwa wetu
 
Wakuu,

Nimemsikiliza Rais Magufuli akiwa anaongea leo kanisani. Nimeshtuka, Rais anaongea kama layman kabisa. Hii ni hatari kwa Usalama wa Taifa kwa mtu ambaye amepewa dhamana ya juu kabisa hapa nchini.

Rais ni Comforter-in-Chief hivyo kama mfariji mkuu wa Taifa ana mamlaka makubwa aliyobebeshwa na hili inaelekea Magufuli analisahau sana. Huwezi toka huko na kuanza kuwambia watanzania eti “Kufa tutakufa tu”.

Rais ni kama BABA katika familia, na kwa Taifa yeye anasimama kama kichwa cha familia. Huwezi kuwa baba bora ukawa unatishia watu wako (wanao, mkeo, ndugu n.k). Kama baba, unaweza kulaumiwa, unaweza kuliliwa, unaweza kupongezwa, unaweza kuumizwa na hatutarajii kuwa utaitangazia familia kuwa wakome kufanya hivyo! Utakuwa umeshindwa kutekeleza majukumu yako.

Rais ni KIUNGO katika Taifa. Unapotokea mgawanyiko, ana wajibu wa kuhakikisha Watanzania wanakuwa wamoja. Hili limekuwa likionekana kuwa tofauti kwa Rais wetu huyu.

Rais anapotoa kauli, ni kauli ya Taifa si yake. Mambo mengi anayoongea Magufuli watanzania walio wengi (wanaojielewa) watakubaliana nami kuwa si yale ambayo kimataifa tungependa kiongozi wetu ayaongee kwa niaba yetu!

Msikilize:



Sasa:

1) Magufuli leo kaongea UONGO mwingi kuhusu barakoa. Alichokiongea ni matusi kwa serikali yake mwenyewe!

- Kama barakoa zilizoingizwa nchini zina virusi au hazifai; kwanini watendaji wake wameziacha ziingizwe sokoni? Anataka kutuambia kuwa TBS na TFDA hawajui kazi yao? Kwanini watendaji wakuu wa taasisi hizi bado wapo kazini?

- Tukubali kuwa tumeingiziwa barakoa zenye kuwa na virusi ambazo zitawaua watanzania: Kwanini Mkurugenzi wa Idara ya Usalama wa Taifa, IGP na CDF bado wapo kazini? Taifa letu manake usalama wake upo hatarini. Kwa mantiki hiyo, maduka ya madawa yavamiwe mara moja na barakoa zote ziondolewe sokoni

2) Magufuli amekuwa Rais wa kwanza mimi kumuona akiwa anahubiri katika Ibada za Kanisa Katoliki. Huu ni utaratibu wa kawaida kwa wakatoliki? Halafu anawachamba viongozi wa kanisa kwa kuhimiza waumini kujilinda?

3) Rais ametangaza dawa kadhaa kama Bupiji, COVIDOL etc, anataka kuwaaminisha watanzania kuwa Sayansi nyingine haifanyi kazi tena? Kuwa watanzania wasiziamini dawa nyingine zinazotolewa hospitali tena? Haya matangazo ya dawa za asili imekuwaje hadi wasaidizi wake wamwacha hadi ataje baadhi ya dawa moja kwa moja (kwa kutaja baadhi tu)? Ana maslahi nazo? Nasikia mtu aliwahi kuwa RC wa Dar ana mkono kwenye pharmacy chain flani, na kuna tetesi kuwa yupo kwa niaba ya ‘mzee’; hii haoni inazidi kujenga hisia zisizo sahihi?

Nitarejea

uliahidi utarejea mkuu!
 
Back
Top Bottom