johnthebaptist
JF-Expert Member
- May 27, 2014
- 82,754
- 139,560
Rais Magufuli anafungua kiwanda cha ngozi kinachomilikiwa na tajiri maarufu nchini Dr Rostam Aziz Kihonda mkoani Morogoro.
Tukio liko mubashara TBC Channel ten na ITV
Up dates;
Rais Magufuli amemtaja Mbunge wa Mororogo Mjini, Aziz ABood kuwa alipewa kiwanda cha Canvas na Moproco tangu mwaka 1996 ambavyo alivishindwa hadi aliponyang'anywa mwaka 2020. Ambapo kwa sasa wamepewa watu wengine
Aidha ametaka atafutwe muwekezaji kupewa kiwanda cha mafuta cha Moproco ili kutoa mafuta kwa ajili ya watanzania.
Magufuli amwambia Rostam Aziz aende kugombea ubunge Morogoro ili amtoe Aziz Abood.
----
Magufuli amsema Abood kuwa alimilikishwa viwanda ambavyo alitumia kuchukua mikopo ambayo alitumia kununua magari na sio kuendeleza viwanda vya Moproco na Canvas
Kiwanda cha Rostam Aziz kinatarajia kuajiri watu 1000
=====
Rais wa Tanzania, Dkt. John Magufuli ameagiza Serikali kuchukua viwanda kutoka kwa wawekezaji ambao wamepewa na kushindwa kuviendeleza
Amesema, "Waziri wa Viwanda usichelewe wala usiulize, inawezekana hata wapo viongozi wengine wa CCM walijimilikisha kwa chini chini, nyang'anya"
Ameagiza hayo Mkoani Morogoro wakati wa uzinduzi wa Kiwanda cha Ngozi cha Ace Leather Tanzania Limited akisema Serikali inataka Watanzania wapate Ajira. Vilevile amesisitiza Tanzania ni sehemu bora zaidi kufanya uwekezaji
Rais John Magufuli amesema Mbunge wa Morogoro Mjini, Abdul - Aziz Aboud amekaa na viwanda, akakopea fedha na kununua mabasi huku viwanda vikifa. Ameongeza kuwa, hata Wafanyakazi wakawa wanakufa na yeye anawabeba kwenye mabasi kwenda kuwazika
Ameeleza hayo mapema leo wakati akizindua Kiwanda cha Ngozi ambapo amesema "Ninampenda sana Aboud lakini kwenye Viwanda hapana. Kwa Morogoro aliviua Mbunge wetu"
Amesema Mbunge huyo ameshindwa kuendesha Viwanda viwili vikubwa ambavyo amekaa navyo kwa zaidi ya miaka 25.
Tukio liko mubashara TBC Channel ten na ITV
Up dates;
Rais Magufuli amemtaja Mbunge wa Mororogo Mjini, Aziz ABood kuwa alipewa kiwanda cha Canvas na Moproco tangu mwaka 1996 ambavyo alivishindwa hadi aliponyang'anywa mwaka 2020. Ambapo kwa sasa wamepewa watu wengine
Aidha ametaka atafutwe muwekezaji kupewa kiwanda cha mafuta cha Moproco ili kutoa mafuta kwa ajili ya watanzania.
Magufuli amwambia Rostam Aziz aende kugombea ubunge Morogoro ili amtoe Aziz Abood.
----
Magufuli amsema Abood kuwa alimilikishwa viwanda ambavyo alitumia kuchukua mikopo ambayo alitumia kununua magari na sio kuendeleza viwanda vya Moproco na Canvas
Kiwanda cha Rostam Aziz kinatarajia kuajiri watu 1000
=====
Rais wa Tanzania, Dkt. John Magufuli ameagiza Serikali kuchukua viwanda kutoka kwa wawekezaji ambao wamepewa na kushindwa kuviendeleza
Amesema, "Waziri wa Viwanda usichelewe wala usiulize, inawezekana hata wapo viongozi wengine wa CCM walijimilikisha kwa chini chini, nyang'anya"
Ameagiza hayo Mkoani Morogoro wakati wa uzinduzi wa Kiwanda cha Ngozi cha Ace Leather Tanzania Limited akisema Serikali inataka Watanzania wapate Ajira. Vilevile amesisitiza Tanzania ni sehemu bora zaidi kufanya uwekezaji
Rais John Magufuli amesema Mbunge wa Morogoro Mjini, Abdul - Aziz Aboud amekaa na viwanda, akakopea fedha na kununua mabasi huku viwanda vikifa. Ameongeza kuwa, hata Wafanyakazi wakawa wanakufa na yeye anawabeba kwenye mabasi kwenda kuwazika
Ameeleza hayo mapema leo wakati akizindua Kiwanda cha Ngozi ambapo amesema "Ninampenda sana Aboud lakini kwenye Viwanda hapana. Kwa Morogoro aliviua Mbunge wetu"
Amesema Mbunge huyo ameshindwa kuendesha Viwanda viwili vikubwa ambavyo amekaa navyo kwa zaidi ya miaka 25.