Rais Magufuli afanya uteuzi wa wenyeviti watatu wa Bodi za Taasisi za Serikali na Ubia

The Sheriff

JF-Expert Member
Oct 10, 2019
613
1,776
Rais Magufuli amefanya uteuzi wa wenyeviti 3 watakaoongoza bodi za taasisi mbili za serikali na moja ya ubia wa serikali na sekta binafsi, ambapo kwa mujibu wa taarifa ya Katibu Mkuu Kiongozi Mh. Balozi John Kijazi, uteuzi huo umeanza jana tarehe 30 Januari,2020

Rais amemteua Bwana Gabriel Pascal Malata ambaye ni Naibu Wakili Mkuu wa Serikali kuwa Mwenyekiti Mjumbe wa kuiwakilisha serikali katika Bodi ya Kampuni ya Airtel Tanzania Ltd.

Aidha, Amemteua Prof. Martha Qorro, ambaye ni Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam kuwa Mwenyekiti wa Baraza la Uongozi wa Chuo cha Mipango na Maendeleo Vijijini (Institute of Rural Development Plan – IRDP)

Uteuzi wa tatu ni wa Prof Joseph Rwegasira Buchweshaija kuwa Mwenyekiti wa Baraza la Sayansi na Teknolojia ya Nelson Mandela (NM-AIST)

1580476660719.png
 
Loooo my no 1 ana mamlaka ya kuteua viongozi wote wa nchi,maana hizi teuzi zingine ndio kwanza nazisikia awamu hii,awamu ya kwanza hizi teuzi sikuzisikia mara kwa mara,ndio maana serikali yetu ni kubwa mno,gharama za uendeshaji ni kubwa mno,ebu futa huu utitiri wa mikoa,bakisha mikoa 8 hadi 10,wilaya 30 hivi,cabinet 15 ministers,tutaokoa fedha nyingi mno,wananchi wanahitaji service deliveries sio utitiri huu tuliokua nao.Driving ya kutoka Tunduma hadi Dar es Salaam unavuka mikoa kama 7!!!!.
 
Back
Top Bottom