Rais Magufuli afanya uteuzi wa Fhika, Nzuki, Chogelo na kutengua uteuzi wa Kafulila, na Sophia Mjema Ole Sendeka na Katambi

mwanamwana

JF-Expert Member
Aug 1, 2011
1,076
4,113
Rais Magufuli amemteua Dkt. Jumanne Fhika kuwa RC wa Njombe akichukua nafasi ya Christopher ole Sendeka. Kabla ya kuteuliwa Dkt. Fhika alikuwa Ofisi ya Rais.

Dkt. Aloyce Nzuki ameteuliwa kuwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Maliasili. Kabla ya uteuzi huo, alikuwa Naibu Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, anachukua nafasi ya Prof. Adolf Mkenda.

Rais Magufuli amemteua Dkt. Allan Kijazi kuwa Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Maliasili. Dk. Kijazi pia ataendelea kuwa Kamishna wa Uhifadhi wa Shirika la Hifadhi za Taifa (TANAPA).

Mhandisi Anthony Sanga ameteuliwa na Rais kama Katibu Mkuu Wizara ya Maji, nafasi ambayo ilikuwa inashikiliwa na Prof. Kitila Mkumbo. Rais Magufuli amemteua Mhandisi Nadhifa Kemikimba kuwa Naibu Katibu Mkuu wa Wizara hiyo.

Aidha, Fadhili Mohamed Juma ameteuliwa kuwa Mkuu wa Wilaya ya Geita akichukua nafasi ya josephat Paulo Maganga ambaye amehamishwa kituo. Kabla ya uteuzi huo, alikuwa Mwenyekiti wa CCM Mkoani Lindi.

Josephat Paulo amekuwa Mkuu wa Wilaya ya Dodoma, nafasi ambayo hapo awali ilikuwa chini ya Patrobas Katambi
1.jpg
2.jpg
 
Ubunge mtamu. Asikwambie mtu... Yule jamaa alivyo, hawa majina yao hayarudi kwenye Ubunge. Watafute biashara za kufanya. Tuliwaambia baada ya sisi ni wao, wakapinga. Sasa zamu yao imefika. Hakuna kugombea Ubunge, japo Katiba ya Jamhuri ya Muungano inaruhusu.
 
Demokrasia inawapofusha watu na kudhani ndio njia sahihi ya kutokea.
Tatizo watu hawapendi kutumwa na kutumika under pressure,wanapenda kurelax na kuwatuma wengine majukumu ili wanaposhindwa wapate pa kuponea kwa kuwasakizia walio chini.
Tutegemee hotuba kali ya Mh. Rais July 20.
 
Nafurahi Kwa kuwa WATANZANIA wengine wapate fursa hizo.
Hao nahisi barua zao zilishatumwa muda mrefu kabla ya kauli ya Rais ila zilikuwa bado kumfikia mkuu.

Na naamini bado zipo zingine njiani hazijamfikia zipo masijala na wahusika wapo hoi wakitamani kuzifuta lakini haiwezekani tena.

2020
 
Demokrasia inawapofusha watu na kudhani ndio njia sahihi ya kutokea.
Tatizo watu hawapendi kutumwa na kutumika under pressure,wanapenda kurelax na kuwatuma wengine majukumu ili wanaposhindwa wapate pa kuponea kwa kuwasakizia walio chini.
Tutegemee hotuba kali ya Mh. Rais July 20.
Labda yy mwenyewe mkuu ndio amesababisha haya...wateuliwa wanajifeel insecure,..kasi yake ya kutumbua ukifanya mistake kidogo imewafanya wateule watafute pa kutokea ,wanajua kwenye ubunge hakuna stress za kutumbuliwa kwa at least miaka 5,..maisha ya kila mkuu akiwa na press na media ,ww roho juu labda ndio yanawakimbiza....unafanya kaz kila ukitoka ofisin hauna uhakika kama kesho utarud tena humo kupiga kazi au utarud kukabidhi ofisi ...
 
Back
Top Bottom