Rais Magufuli achana na mbeleko ya CCM utatuletea tena matatizo

SANCTUS ANACLETUS

JF-Expert Member
Mar 5, 2016
3,337
4,664
Ulituomba tukuamini wewe hata kama hatukuiamini tena CCM.Ulitusihi tukuamini na usingetuangusha kama vile CCM ilivyokuwa imetuangusha.

Tulikuelewa na tumekuamini sana.Tunaelekea kukuamini upeo.Tunaomba nawe utuamini.Ni zamu yako nawe kutusikiliza.Maisha ni kutoa na kisha kupokea.Tulitoa masikio na mioyo yetu.Ni wakati wako nawe kutoa.Miongoni mwa tunayokuomba kutoa ni kutoendelea kubebeka katika mbeleko ya CCM.Utatuletea tena matatizo makubwa baada ya kuondoka.

Hivi umemuelewa vizuri jana Mzee Butiku juu ya alichokueleza? Ni hivi CCM iliyopewa uweza wa kufanya kazi kama Jua ilishaishiwa nuru na nguvu ya kuangaza nchi yetu.CCM yenye wasomi waliokabidhiwa dhima ya kutoa dira walishakuwa Mbwa vibogoyo.CCM ilishakuwa Tarumbeta lisilotoa sauti zilizopangilika.CCM ilishakuwa Gitaa linalotoa midundiko ambayo wachezaji(wananchi) badala ya kucheza wamevaa nguo wachezaji wakicheza wanavua nguo.Ndio watanzania wakicheza midundiko inayocharazwa na CCM wanasanua nguo zote na kuzitundika kichwani na kisha kuanza kukimbia hovyo hovyo.Matokeo yake ndo hayo mambo yanayokuliza mtu mzima.Watu wanauza nchi.Unalilia peke yako.Unanibisha? Nionyeshe machozi ya Kinana.Nionyeshe machozi ya Bulembo. Nionyeshe machozi ya Ndugai hapo jana.Ndugai jana maneno yake yalikuwa ya muombolezaji tu na si ya mfiwa! Upo hapo?

CCM,Mzee Butiku amesema sio majasiri kitambo! Kwa nini unaendelea kung'ang'ana na CCM? Kwa nini unataka tukikuamini basi tuiamini na CCM wakati huo huo? Sisi tumekuamini wewe peke yako.Kwa nini unalazimisha tuiamini na CCM pia?

Hivi una maana gani kumpa Ndugai kazi ya kuangazia uchunguzi mikataba iliyosalia ya Rasilimali zetu zingine za Asili kama Gesi, Almasi na Mafuta? Hivi Ndugai amezaliwa Leo? Hivi unafikiria Ndugai anao uwezo wa Kijasiri na wa Kiakili wa kutokuwa "compromised" na wezi kama wale waliojaribu kuwa-compromise wateule wa Kamati zako?

Hivi Ndugai angekuwa msomi jasiri alishindwaje kutengeneza "miundombinu" ili Chenge asiwe Mwenyekiti wa Bunge? Ndugai angekuwa Msomi Jasiri alishindwa nini kumpiga "Kafumu" "Magongo" ya Kimkakati ili asiweze kuwa Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Nishati na Madini?Hivi aliwezaje kumpiga mwenzie magongo kichwani hadi akashindwa kuwa Mbunge na akashindwa kwa hao niliowatolea mifano na wengineo?

Hivi Wabunge wa CCM wangekuwa Wasomi Jasiri kama wewe kama alivyokuchora Mzee Butiku walishindwa nini kuyaona mambo haya ya kuibiwa watanzania na kufanywa mazuzu kwa rasilimali zetu?

Orodha ya mambo yanayowafanya CCM wasiwe na sifa ya Ujasiri ni ndefu sana.Itoshe wewe kuona kuwa nje ya wewe CCM hawatufai.Achana nao.Acha kuendelea kubebeka nao.CCM ni fisi.Wako wanaongozana na wewe wakinyatia "mnofu" ulioubeba(rasilimali zetu).Nakuambia ukiutua tu wanao.Ukiondoka madarakani watatushambulia haijapata kutokea!

Ndiposa tunakuomba utuamini.Achana na CCM kabisa.Anza kuasisi "Jua" lingine la kuangazia nchi yetu iwapo utang'ang'ania kuondoka 2025.Tengeneza Chama kingine chenye watu jasiri.Tuachie Chama kisichotuchezesha Makhirikhiri na hivi watanzania kuvalia nguo zetu vichwani.Acha Kabisa.
 
Kabisa Yani
ili mzee afanikishe harakati zake kweli ambazo amejipambanua kuzifanya kwa ajili ya watanzania
AACHE KUTUMIA KIVULI CHA CCM
[HASHTAG]#HappyAnniversaryToMeInJF[/HASHTAG]
 
Ulituomba tukuamini wewe hata kama hatukuiamini tena CCM.Ulitusihi tukuamini na usingetuangusha kama vile CCM ilivyokuwa imetuangusha.

Tulikuelewa na tumekuamini sana.Tunaelekea kukuamini upeo.Tunaomba nawe utuamini.Ni zamu yako nawe kutusikiliza.Maisha ni kutoa na kisha kupokea.Tulitoa masikio na mioyo yetu.Ni wakati wako nawe kutoa.Miongoni mwa tunayokuomba kutoa ni kutoendelea kubebeka katika mbeleko ya CCM.Utatuletea tena matatizo makubwa baada ya kuondoka.

Hivi umemuelewa vizuri jana Mzee Butiku juu ya alichokueleza? Ni hivi CCM iliyopewa uweza wa kufanya kazi kama Jua ilishaishiwa nuru na nguvu ya kuangaza nchi yetu.CCM yenye wasomi waliokabidhiwa dhima ya kutoa dira walishakuwa Mbwa vibogoyo.CCM ilishakuwa Tarumbeta lisilotoa sauti zilizopangilika.CCM ilishakuwa Gitaa linalotoa midundiko ambayo wachezaji(wananchi) badala ya kucheza wamevaa nguo wachezaji wakicheza wanavua nguo.Ndio watanzania wakicheza midundiko inayocharazwa na CCM wanasanua nguo zote na kuzitundika kichwani na kisha kuanza kukimbia hovyo hovyo.Matokeo yake ndo hayo mambo yanayokuliza mtu mzima.Watu wanauza nchi.Unalilia yako peke yako.Unanibisha? Nionyeshe machozi ya Kinana.Nionyeshe machozi ya Bulembo. Nionyeshe machozi ya Ndugai jana.Ndugai jana maneno yake yalikuwa ya muombolezaji tu na si mfiwa! Upo hapo?

CCM,Mzee Butiku amesema sio majasiri kitambo! Kwa nini unaendelea kung'ang'ana na CCM? Kwa nini unataka tukikuamini basi tuiamini na CCM wakati huo huo? Sisi tumekuamini wewe peke yako.Kwa nini unalazimisha tuiamini na CCM pia?

Hivi una maana gani kumpa Ndugai kazi ya kuangazia uchunguzi mikataba iliyosalia ya Rasilimali zetu zingine za Asili kama Gesi, Almasi na Mafuta? Hivi Ndugai amezaliwa Leo? Hivi unafikiria Ndugai anao uwezo wa Kijasiri na wa Kiakili wa kutokuwa "compromised" na wezi kama wale waliojaribu kuwa-compromise wateule wa Kamati zako?

Hivi Ndugai angekuwa msomi jasiri alishindwaje kutengeneza "miundombinu" ili Chenge asiwe Mwenyekiti wa Bunge? Ndugai angekuwa Msomi Jasiri alishindwa nini kumpiga "Kafumu" "Magongo" ya Kimkakati ili asiweze kuwa Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Nishati na Madini?Hivi aliwezaje kumpiga mwenzie magongo kichwani hadi akashindwa kuwa Mbunge na akashindwa kwa hao niliowatolea mifano na wengineo?

Hivi Wabunge wa CCM wangekuwa Wasomi Jasiri kama wewe kama alivyokuchora Mzee Butiku walishindwa nini kuyaona mambo haya ya kuibiwa watanzania na kufanywa mazuzu kwa rasilimali zetu?

Orodha ya mambo yanayowafanya CCM wasiwe na sifa ya Ujasiri ni ndefu sana.Itoshe wewe kuona kuwa nje ya wewe CCM hawatufai.Achana nao.Acha kuendelea kubebeka nao.CCM ni fisi.Wako wanaongozana na wewe wakinyatia "mnofu" ulioubeba(rasilimali zetu).Nakuambia ukiutua tu wanao.Ukiondoka madarakani watatushambulia haijapata kutokea!

Ndiposa tunakuomba utuamini.Achana na CCM kabisa.Anza kuasisi "Jua" lingine la kuangazia nchi yetu iwapo utang'ang'ania kuondoka 2025.Tengeneza Chama kingine chenye watu jasiri.Tuachie Chama kisichotuchezesha Makhirikhiri na hivi watanzania kuvalia nguo zetu vichwani.Acha Kabisa.
Dah! Kuna watu jf mnawaza kwa utulivu sana hadi raha.
Mkiangazia matendo yote yafanywayo na vigogo mbalimbali wanaojifanya makada watiifu kwa utulivu mkubwa. Post nimeipenda.
Ivi tukijiuliza sote, Chenge na kashifa zote alizokuwa nazo, alipenyapenyaje hadi kuchukua fomu hatimaye kushinda uenyekiti? Matusi hayo aelekezwe nani?
Na hiyo alifanya janja yake kupata madaraka na uwezo wa kuzima hoja zinazomhusu za mafisadi bungeni.
Unaonaje hoja ya Makonda alivyoishadadia!
Na huyo Ngeleja alichukuaje fomu ya ubunge na kushinda, wakati alishafukuzwa uwaziri sababu ya matusi ya uporaji?
Ukifuatilia ubunge wa Kafumu naye ni utata mtupu. Picha hiyo peke yake inahalalisha tafakuri yako.
Uliyoeleza yana mashiko sana. Magufuli ni rais kipenzi cha watanzania kwa sasa, lakini mbeleko iliyombeba inamatobo, yafaa abadilishiwe, maana yaweza kumuangusha.
Leo Magufuli akianzisha chama kipya, wallah ccm kitakufa kama kilivyokufa kanu.
Sababu zitakazosababisha kife ni kutokujitathimini wale wanaojiita makada mumiani wachumia tumbo.
Na walishang'ang'ania ofisi, wanazaliana humo hadi wanakuza na kukabidhi watoto zao funguo. Jina moja linatawala hata miongo mi5, yaani utemi system!
Pia kutofukuza wanachama majizi wanaofahamika kwa uhalifu wao miaka nenda rudi ni tatizo la mauti ya chama.
Hili la makinikia likisomba watuhumiwa wake wakaenda na maji bila ya kuangalia makunyanzi ya mtu, hakika Magufuli atakuwa amemaanisha anayoyanadi kila uchao na vyama vya kwenye briefcase, vitafute maneno ya akili kuweza kushindana na huyu 'Tiger'katika nyanja za siasa nchini.
 
Kuna hatari kubwa sana huko mbeleni lazima CCM izalishwe upya vinginevyo taifa litavurugika sana huko mbele tena Nina CCM inabidi ife kabisa ukizunguka kwenye kampeni utajua ni kiasi gani watu wanachukia CCM huwezi amini watu wamekichoka chama me CCM ila hali sio nzuri upinzani unapotoka kwenye chama na kuamia kwa wananchi ni hatari.Hata rais haaminiki maana yupo kwa kivuli cha CCM.Razima tujue no gain without pain
 
Watanzania tumuungeni mkono raisi wetu ndugu JOHN POMBE MAGUFULI .kwenye vitahii ngumu ya maslahi yanchi. Tuache tofauti zetu kando tupambane kwa maslahi ya Taifa letu.
Tukumbuke hata gadafi alianza mapambano ya kuondoa unyonyaji kwa taabu sana lakini matokeo yake yalikuwa mazuri kwa maslahi ya nchi yake ya Libya so sasa nizamu yetu sisi watanzania.
wahenga walisema ukiona kiza kimezidi ujue kuwa karibu kutapambazuka (jua linakaribia kutoka) it means freedom is coming tomorrow. Thanks .
 
Dah! Kuna watu jf mnawaza kwa utulivu sana hadi raha.
Mkiangazia matendo yote yafanywayo na vigogo mbalimbali wanaojifanya makada watiifu kwa utulivu mkubwa. Post nimeipenda.
Ivi tukijiuliza sote, Chenge na kashifa zote alizokuwa nazo, alipenyapenyaje hadi kuchukua fomu hatimaye kushinda uenyekiti? Matusi hayo aelekezwe nani?
Na hiyo alifanya janja yake kupata madaraka na uwezo wa kuzima hoja zinazomhusu za mafisadi bungeni.
Unaonaje hoja ya Makonda alivyoishadadia!
Na huyo Ngeleja alichukuaje fomu ya ubunge na kushinda, wakati alishafukuzwa uwaziri sababu ya matusi ya uporaji?
Ukifuatilia ubunge wa Kafumu naye ni utata mtupu. Picha hiyo peke yake inahalalisha tafakuri yako.
Uliyoeleza yana mashiko sana. Magufuli ni rais kipenzi cha watanzania kwa sasa, lakini mbeleko iliyombeba inamatobo, yafaa abadilishiwe, maana yaweza kumuangusha.
Leo Magufuli akianzisha chama kipya, wallah ccm kitakufa kama kilivyokufa kanu.
Sababu zitakazosababisha kife ni kutokujitathimini wale wanaojiita makada mumiani wachumia tumbo.
Na walishang'ang'ania ofisi, wanazaliana humo hadi wanakuza na kukabidhi watoto zao funguo. Jina moja linatawala hata miongo mi5, yaani utemi system!
Pia kutofukuza wanachama majizi wanaofahamika kwa uhalifu wao miaka nenda rudi ni tatizo la mauti ya chama.
Hili la makinikia likisomba watuhumiwa wake wakaenda na maji bila ya kuangalia makunyanzi ya mtu, hakika Magufuli atakuwa amemaanisha anayoyanadi kila uchao na vyama vya kwenye briefcase, vitafute maneno ya akili kuweza kushindana na huyu 'Tiger'katika nyanja za siasa nchini.

nashukuru umeelezea vyema, na hapo ndio makada wengi wanashindwa kutuelewa,.. chini ya mwamvuli wa CCM huwezi kuendeleza hili Taifa. Kama una nia njema na ujasiri ni vizuri ukaachana na CCM.. Wenyewe wana wimbo wao, wanasema CCM inawenyewe, Mh Magufuri huwezi kuikarabati CCM imeshakuwa beyond repair, inahitaji kwenda scap yard..
 
Watanzania tumuungeni mkono raisi wetu ndugu JOHN POMBE MAGUFULI .kwenye vitahii ngumu ya maslahi yanchi. Tuache tofauti zetu kando tupambane kwa maslahi ya Taifa letu.
Tukumbuke hata gadafi alianza mapambano ya kuondoa unyonyaji kwa taabu sana lakini matokeo yake yalikuwa mazuri kwa maslahi ya nchi yake ya Libya so sasa nizamu yetu sisi watanzania.
wahenga walisema ukiona kiza kimezidi ujue kuwa karibu kutapambazuka (jua linakaribia kutoka) it means freedom is coming tomorrow. Thanks .

sio kupitia mwamvuli wa CCM, ukiwa na nia nzuri na ujasiri huwezi kuijenga hii nchi kupitia CCM hapo ilishakataa,,
 
Tunaposema watanganyika ni AJABU LA 8 la DUNIA tunamaanisha mambo kama haya
Mtawala asieamini mabadiliko ya KATIBA
...ambayo inasema mtu hawezi kuwa RAIS mpaka apitiee kwenye Chama cha SIASA....na Mh..anajua anachofanya anailinda CCM kwa Mkono wa Chuma
Then watu wanamwaga eti
Aiache CCM Kwanini tusionekane wapuuzi
 
Watanzania tumuungeni mkono raisi wetu ndugu JOHN POMBE MAGUFULI .kwenye vitahii ngumu ya maslahi yanchi. Tuache tofauti zetu kando tupambane kwa maslahi ya Taifa letu.
Tukumbuke hata gadafi alianza mapambano ya kuondoa unyonyaji kwa taabu sana lakini matokeo yake yalikuwa mazuri kwa maslahi ya nchi yake ya Libya so sasa nizamu yetu sisi watanzania.
wahenga walisema ukiona kiza kimezidi ujue kuwa karibu kutapambazuka (jua linakaribia kutoka) it means freedom is coming tomorrow. Thanks .
Mbona yeye hakuwaunga Mkono wapinzani walipokuwa wanalalamikia hii Mikataba
 
Watanzania tumuungeni mkono raisi wetu ndugu JOHN POMBE MAGUFULI .kwenye vitahii ngumu ya maslahi yanchi. Tuache tofauti zetu kando tupambane kwa maslahi ya Taifa letu.
Tukumbuke hata gadafi alianza mapambano ya kuondoa unyonyaji kwa taabu sana lakini matokeo yake yalikuwa mazuri kwa maslahi ya nchi yake ya Libya so sasa nizamu yetu sisi watanzania.
wahenga walisema ukiona kiza kimezidi ujue kuwa karibu kutapambazuka (jua linakaribia kutoka) it means freedom is coming tomorrow. Thanks .
Mbona yeye hakuwaunga Mkono wapinzani walipokuwa wanalalamikia hii Mikataba
 
Ulituomba tukuamini wewe hata kama hatukuiamini tena CCM.Ulitusihi tukuamini na usingetuangusha kama vile CCM ilivyokuwa imetuangusha.

Tulikuelewa na tumekuamini sana.Tunaelekea kukuamini upeo.Tunaomba nawe utuamini.Ni zamu yako nawe kutusikiliza.Maisha ni kutoa na kisha kupokea.Tulitoa masikio na mioyo yetu.Ni wakati wako nawe kutoa.Miongoni mwa tunayokuomba kutoa ni kutoendelea kubebeka katika mbeleko ya CCM.Utatuletea tena matatizo makubwa baada ya kuondoka.

Hivi umemuelewa vizuri jana Mzee Butiku juu ya alichokueleza? Ni hivi CCM iliyopewa uweza wa kufanya kazi kama Jua ilishaishiwa nuru na nguvu ya kuangaza nchi yetu.CCM yenye wasomi waliokabidhiwa dhima ya kutoa dira walishakuwa Mbwa vibogoyo.CCM ilishakuwa Tarumbeta lisilotoa sauti zilizopangilika.CCM ilishakuwa Gitaa linalotoa midundiko ambayo wachezaji(wananchi) badala ya kucheza wamevaa nguo wachezaji wakicheza wanavua nguo.Ndio watanzania wakicheza midundiko inayocharazwa na CCM wanasanua nguo zote na kuzitundika kichwani na kisha kuanza kukimbia hovyo hovyo.Matokeo yake ndo hayo mambo yanayokuliza mtu mzima.Watu wanauza nchi.Unalilia peke yako.Unanibisha? Nionyeshe machozi ya Kinana.Nionyeshe machozi ya Bulembo. Nionyeshe machozi ya Ndugai hapo jana.Ndugai jana maneno yake yalikuwa ya muombolezaji tu na si ya mfiwa! Upo hapo?

CCM,Mzee Butiku amesema sio majasiri kitambo! Kwa nini unaendelea kung'ang'ana na CCM? Kwa nini unataka tukikuamini basi tuiamini na CCM wakati huo huo? Sisi tumekuamini wewe peke yako.Kwa nini unalazimisha tuiamini na CCM pia?

Hivi una maana gani kumpa Ndugai kazi ya kuangazia uchunguzi mikataba iliyosalia ya Rasilimali zetu zingine za Asili kama Gesi, Almasi na Mafuta? Hivi Ndugai amezaliwa Leo? Hivi unafikiria Ndugai anao uwezo wa Kijasiri na wa Kiakili wa kutokuwa "compromised" na wezi kama wale waliojaribu kuwa-compromise wateule wa Kamati zako?

Hivi Ndugai angekuwa msomi jasiri alishindwaje kutengeneza "miundombinu" ili Chenge asiwe Mwenyekiti wa Bunge? Ndugai angekuwa Msomi Jasiri alishindwa nini kumpiga "Kafumu" "Magongo" ya Kimkakati ili asiweze kuwa Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Nishati na Madini?Hivi aliwezaje kumpiga mwenzie magongo kichwani hadi akashindwa kuwa Mbunge na akashindwa kwa hao niliowatolea mifano na wengineo?

Hivi Wabunge wa CCM wangekuwa Wasomi Jasiri kama wewe kama alivyokuchora Mzee Butiku walishindwa nini kuyaona mambo haya ya kuibiwa watanzania na kufanywa mazuzu kwa rasilimali zetu?

Orodha ya mambo yanayowafanya CCM wasiwe na sifa ya Ujasiri ni ndefu sana.Itoshe wewe kuona kuwa nje ya wewe CCM hawatufai.Achana nao.Acha kuendelea kubebeka nao.CCM ni fisi.Wako wanaongozana na wewe wakinyatia "mnofu" ulioubeba(rasilimali zetu).Nakuambia ukiutua tu wanao.Ukiondoka madarakani watatushambulia haijapata kutokea!

Ndiposa tunakuomba utuamini.Achana na CCM kabisa.Anza kuasisi "Jua" lingine la kuangazia nchi yetu iwapo utang'ang'ania kuondoka 2025.Tengeneza Chama kingine chenye watu jasiri.Tuachie Chama kisichotuchezesha Makhirikhiri na hivi watanzania kuvalia nguo zetu vichwani.Acha Kabisa.
Umemtahadharisha vizuri kabisa. Mimi binafsi ninamuamini Magufuli, na kumuunga mkono lakini siyo CCM hii kokoro. Hebu aturudishie CCM-proletariat tuliyokuwa nayo zamani.
 
Dawa ni magufuli apitishe katiba ya warioba/wananchi halafu awe mgömbea BINAFSI asiwe ccm wala upinzani, tutamuunga mköno asilîmia mia môja!
 
Kuna hatari kubwa sana huko mbeleni lazima CCM izalishwe upya vinginevyo taifa litavurugika sana huko mbele tena Nina CCM inabidi ife kabisa ukizunguka kwenye kampeni utajua ni kiasi gani watu wanachukia CCM huwezi amini watu wamekichoka chama me CCM ila hali sio nzuri upinzani unapotoka kwenye chama na kuamia kwa wananchi ni hatari.Hata rais haaminiki maana yupo kwa kivuli cha CCM.Razima tujue no gain without pain
Mku ulichomanisha kiko sawa Mimi ni mwanaccm tena ambaye anapiga mpaka zile kura za ndani ya chama lakini ukiangalia yanayoendelea nashindwa kuelewa nini lengo la hiki chama kwa hii tabia ya kuhubiri chuki baina ya upinzani ambayo haiwezi kutuacha ccm wanaccm salama kwa ndo wanzilishi wa hizi chuki
 
6 Reactions
Reply
Back
Top Bottom