Rais Magufuli; Achana na mambo ya Football

Patriot

JF-Expert Member
Feb 11, 2008
5,698
4,693
Mwanasiasa yeyote angependa asifiwe na kila kundi la wapiga kura. Juhudi za hivi karibuni ktk awamu hii, naweza kusema ni juhudi za kutaka wapenda michezo wamwage sifa zao kwa serikali. Matokeo yetu ya jana yameonekana, pesa iliyokwisha tumika ktk mchezo huu tunaikumbuka tangu awamu ya 4 na sasa awamu ya 5. Nioancho tunapoteza pesa nyingi kwa matokeo hafifu kabisa.

Ubora wa wachezaji wetu uko chini sana! Hata kama utawaahidi kuwapiga kwata, hawana akili hiyo. Sababu kubwa ni nidhamu duni. Yawezekana ni kwa sababu ya ulevi, bagi, na anasa kibao wanazoziona ni muhimu kwao. Hakuna nchi inayotumia wachezaji wa ubora huo na kufanikiwa. Wanachohangaika nacho ni kunyoa nywele, basi! Kwa nini serikali itoe pesa kwa watu ambao ubora wao haupangwi na serikali? Walio juu kimichezo hukataa hata anayevuta sigara!

Mh. Rais, ni vizuri pesa hizo zikatumika kujengea madarasa, au vyoo ktk shule zetu kuliko kuhangaika na kizazi kinachotafuta sifa mitaani badala ya uwanjani. Siyo kila nchi duniani inacheza mpira.
 
Hakika!
Alikuja mBrazil akapita, wakaja wengine akina nani sijui na sasa huyu mNigeria, naye atapita. Yaani iishe miaka 20, awamu mbili bila mafanikio sisi tunaendelea tu! NOO!

Wekezeni kwenye riadha, tuachane na mambo ya ya kutuma walevi kuleta sifa. Eti Konki. Konki! Hopeless!
 
Jamaa anatafuta means za kushinda uchaguzi kwa uhalali, ila kila mkakati unabuma mapema sana, na option iliyobaki ya kuchakachua matokeo inampa hofu maana chochote kinaweza kutokea sababu kesha gombana na wakubwa, hivyo wanaweza tia mguu ikala kwake, na mbaya zaidi amejilimbikizia maadui wa kufa mtu.
 
Mh. Rais, ni vizuri pesa hizo zikatumika kujengea madarasa, au vyoo ktk shule zetu kuliko kuhangaika na kizazi kinachotafuta sifa mitaani badala ya uwanjani. Siyo kila nchi duniani inacheza mpira.
Maneno mzito Sana haya!
 
Unajua hadi Ulaya kwenye mabar wanaonyesha AFCON. .Kuna watu duniani wamesikia nchi inayoitwa Tanzania kwa mara ya kwanza kupitia mashindano haya. .Kushiriki faida ni nyingi kuliko hasara..Tukutane AFCON 2021 Cameron
 
Hivi kwa nini wameendelea na mechi hii ya kuaibisha? The best walichonancho ni nywele za ajabu eti nao wameiga!
 
Kuna wakati unashangaa kukuta mtu anahangaika na mambo yanayostahili kuitwa ya mitaani. Football industry yetu iko mitaani na wale wazee wa Simba na Yanga. HAwa hawataweza kuijenga footbal labda biashara ya kuuza wachezaji. Ndowanaotuingizia wavuta bangi.
 
Back
Top Bottom