Patriot
JF-Expert Member
- Feb 11, 2008
- 5,698
- 4,693
Mwanasiasa yeyote angependa asifiwe na kila kundi la wapiga kura. Juhudi za hivi karibuni ktk awamu hii, naweza kusema ni juhudi za kutaka wapenda michezo wamwage sifa zao kwa serikali. Matokeo yetu ya jana yameonekana, pesa iliyokwisha tumika ktk mchezo huu tunaikumbuka tangu awamu ya 4 na sasa awamu ya 5. Nioancho tunapoteza pesa nyingi kwa matokeo hafifu kabisa.
Ubora wa wachezaji wetu uko chini sana! Hata kama utawaahidi kuwapiga kwata, hawana akili hiyo. Sababu kubwa ni nidhamu duni. Yawezekana ni kwa sababu ya ulevi, bagi, na anasa kibao wanazoziona ni muhimu kwao. Hakuna nchi inayotumia wachezaji wa ubora huo na kufanikiwa. Wanachohangaika nacho ni kunyoa nywele, basi! Kwa nini serikali itoe pesa kwa watu ambao ubora wao haupangwi na serikali? Walio juu kimichezo hukataa hata anayevuta sigara!
Mh. Rais, ni vizuri pesa hizo zikatumika kujengea madarasa, au vyoo ktk shule zetu kuliko kuhangaika na kizazi kinachotafuta sifa mitaani badala ya uwanjani. Siyo kila nchi duniani inacheza mpira.
Ubora wa wachezaji wetu uko chini sana! Hata kama utawaahidi kuwapiga kwata, hawana akili hiyo. Sababu kubwa ni nidhamu duni. Yawezekana ni kwa sababu ya ulevi, bagi, na anasa kibao wanazoziona ni muhimu kwao. Hakuna nchi inayotumia wachezaji wa ubora huo na kufanikiwa. Wanachohangaika nacho ni kunyoa nywele, basi! Kwa nini serikali itoe pesa kwa watu ambao ubora wao haupangwi na serikali? Walio juu kimichezo hukataa hata anayevuta sigara!
Mh. Rais, ni vizuri pesa hizo zikatumika kujengea madarasa, au vyoo ktk shule zetu kuliko kuhangaika na kizazi kinachotafuta sifa mitaani badala ya uwanjani. Siyo kila nchi duniani inacheza mpira.