My Son drink water
JF-Expert Member
- Nov 30, 2016
- 4,932
- 13,283
Dunia nzima inajua kuwa Tanzania mikononi mwako haina Demokrasia ,umefanya kila unaloweza kuua Demokrasia na Uhuru wa Habari.
Mimi hapa nakuandikia nikiwa natumia ID fake ili kulinda usalama wangu.
Lakini jukwaa hili la Jamiiforums nalotumia linaandamwa na serikali ili litoe siri au majina halisi ya wakosoaji wa serikali humu, na hadi sasa Kesi ipo mahakamani.
Wewe ni mkuu wa nchi, mfalme wa taifa la Tanzania, kutamka kwako hadharani kwamba eti Tanzania ina Demokrasia kubwa, ni kuwadhihaki watu wako uliowanyima haki yao ya kikatiba ya kuchagua viongozi wanaowataka.
Nikueleze wazi kwamba tangu umeingia madarakani umesahau kabisa kuwa maisha yana kesho, leo hii wewe ni Rais ila siku zijazo hutakuwa Rais tena, na hawa wanaokupa sifa kila siku hata ambako hustahili watakugeuka wote na kuanza kumsifia Rais atakayekuwa madarakani.
Mh Rais, hofu yako iko wapi hasa? mbona kuna sehemu unafanya vizuri kiasi cha kukubalika na watu automatically? Kwanini umekubali kuchoreshwa kiasi hicho?
Yaani wewe ni Binadamu, una mapungufu mengi tu sasa iweje ukubali kusifiwa kiasi hicho na wanaokukosoa waonekane wabaya?
Mwl Nyerere aliulizwa swali na mwandishi wa BBC enzi za uhai wake akiwa Rais mwaka 1983.
"Why are you getting ready to retire? "
Mwl Nyerere alijibu.
"Because I need to create a fresh legacy of mine and my country as well ".
Leo hii watanzania tunajivunia Mwl Nyerere, hata mabeberu walimpenda na kumwogopa Mwl.
Nyerere aliwahi kumshauri Kaunda na kumwambia.
"Mzee mwenzangu, achia madaraka kabla watu hawajakuchoka ".
Kaunda alikuwa Kiburi, hakuwa na hekima, hakusikiliza ushauri wa Mwl, matokeo yake alikuja kuondoka madarakani kwa aibu kubwa mno.
Wazambia hawana Rais wa kujivunia Kama sisi watanzania tunavyojivunia kwa Nyerere.
Ni kwa sababu Kaunda hakuacha Legacy nzuri.
Kikwete ameondoka madarakani na kuacha Legacy ya kuheshimu mfumo wa vyama vingi na Demokrasia.
Miaka ya nyuma Kati ya 1980 au 1984 Tanzania ilikumbwa na balaa la njaa, Nyerere hakuwaambia watanza nia kwamba ni wavivu na hawalimi watakufa njaa...
Alikimbilia Marekani kuomba msaada wa Chakula kwa ajili ya watu wake, msaada ulikuja haraka na malori yakaanza kusambaza Chakula nchi nzima, kila kaya iligawiwa Chakula cha kutosha, Mahindi ya njano, Burga (American meal) Maziwa ya unga pamoja na mafuta ya kupikia.
Wananchi walikula na kusaza hadi balaa la njaa lilipoisha .
Je wewe utaacha Legacy gani kwa taifa lako?
Rejea ya Tetemeko la Bukoba, MV Nyerere, Wafanyakazi, Demokrasia na Uhuru wa Habari, Uchumi wa nchi na anguko kuu la Mihimili ya Serikali.
=====
Maoni ya Wadau
Mimi hapa nakuandikia nikiwa natumia ID fake ili kulinda usalama wangu.
Lakini jukwaa hili la Jamiiforums nalotumia linaandamwa na serikali ili litoe siri au majina halisi ya wakosoaji wa serikali humu, na hadi sasa Kesi ipo mahakamani.
Wewe ni mkuu wa nchi, mfalme wa taifa la Tanzania, kutamka kwako hadharani kwamba eti Tanzania ina Demokrasia kubwa, ni kuwadhihaki watu wako uliowanyima haki yao ya kikatiba ya kuchagua viongozi wanaowataka.
Nikueleze wazi kwamba tangu umeingia madarakani umesahau kabisa kuwa maisha yana kesho, leo hii wewe ni Rais ila siku zijazo hutakuwa Rais tena, na hawa wanaokupa sifa kila siku hata ambako hustahili watakugeuka wote na kuanza kumsifia Rais atakayekuwa madarakani.
Mh Rais, hofu yako iko wapi hasa? mbona kuna sehemu unafanya vizuri kiasi cha kukubalika na watu automatically? Kwanini umekubali kuchoreshwa kiasi hicho?
Yaani wewe ni Binadamu, una mapungufu mengi tu sasa iweje ukubali kusifiwa kiasi hicho na wanaokukosoa waonekane wabaya?
Mwl Nyerere aliulizwa swali na mwandishi wa BBC enzi za uhai wake akiwa Rais mwaka 1983.
"Why are you getting ready to retire? "
Mwl Nyerere alijibu.
"Because I need to create a fresh legacy of mine and my country as well ".
Leo hii watanzania tunajivunia Mwl Nyerere, hata mabeberu walimpenda na kumwogopa Mwl.
Nyerere aliwahi kumshauri Kaunda na kumwambia.
"Mzee mwenzangu, achia madaraka kabla watu hawajakuchoka ".
Kaunda alikuwa Kiburi, hakuwa na hekima, hakusikiliza ushauri wa Mwl, matokeo yake alikuja kuondoka madarakani kwa aibu kubwa mno.
Wazambia hawana Rais wa kujivunia Kama sisi watanzania tunavyojivunia kwa Nyerere.
Ni kwa sababu Kaunda hakuacha Legacy nzuri.
Kikwete ameondoka madarakani na kuacha Legacy ya kuheshimu mfumo wa vyama vingi na Demokrasia.
Miaka ya nyuma Kati ya 1980 au 1984 Tanzania ilikumbwa na balaa la njaa, Nyerere hakuwaambia watanza nia kwamba ni wavivu na hawalimi watakufa njaa...
Alikimbilia Marekani kuomba msaada wa Chakula kwa ajili ya watu wake, msaada ulikuja haraka na malori yakaanza kusambaza Chakula nchi nzima, kila kaya iligawiwa Chakula cha kutosha, Mahindi ya njano, Burga (American meal) Maziwa ya unga pamoja na mafuta ya kupikia.
Wananchi walikula na kusaza hadi balaa la njaa lilipoisha .
Je wewe utaacha Legacy gani kwa taifa lako?
Rejea ya Tetemeko la Bukoba, MV Nyerere, Wafanyakazi, Demokrasia na Uhuru wa Habari, Uchumi wa nchi na anguko kuu la Mihimili ya Serikali.
=====
Maoni ya Wadau
My son Drink Water naweza kukubaliana nawe kwenye kiini na dhamira ya uzi wako lakini napenda nitofautiane nawe kwenye baadhi ya facts ulizozileta ku support argument yako hasa kumhusu marehemu Mwalimu Nyerere
Tofauti na ulivosema kwamba Nyerere alimshauri Kaunda aachie ngazi ukweli ni kwamba Mwalimu alimshauri Kaunda asifanye uchaguzi kwa sababu taarifa za ki intelijensia alizokua nazo(na Mwalimu was good at that) zilionyesha Kaunda asingeshinda uchaguzi huo. Hayo ni maneno yake mwenyewe Nyerere na aliyatoa hadharani na kumbukumbu zipo
Kwa maneno mengine(hii ni tafsiri yangu) ni kama alikua anamwambia Kaunda awafanyie ubabe raia wake asifanye uchaguzi!!! Kama ikiwezekana aibe uchaguzi abakie kua Rais wa Zambia ushauri ambao Mzee Kaunda aliukataa, akaingia kwenye uchaguzi akiwa na tume huru kabisa kabisa kabisaaaa ya uchaguzi na matokeo yalipotangazwa aliyakubali bila kinyongo wala hila!
Hii ni legacy aliyoicha Mzee Kaunda ya ku set precedence ya kuheshimu demokrasia na kukubali matakwa ya raia na sauti yao kupitia sanduku la kura na kwa hilo Zambia wametushinda sana.
Kwa taarifa yako tu marehemu Mwalimu Nyerere ndiye alikua championi wa siasa za hila na ubabe wa kichama na ndio muasisi wa katiba tunayoilalamikia sasa na hata yeye mwenyewe baada ya kuachia ngazi kama rais lakini pia ndie fundi mkuu na injinia wa supremacy ya kibabe na ujanja ya Chama Cha Mapinduzi akidaiwa ndie aliyesimamia na ku set precedence ya kupindua matokeo ya chaguzi za Zanzibar (mbinu inayoigwa na Tanzania Bara pia) kwani hakutaka wala hakuamini chama au mtu asiyekua CCM aongoze Tanzania
Aliwahi tu wakati mmoja kumsifia Mandela kwamba ni bora kaondoka mapema madarakani kwani akisubiri azeeke akili inaweza kukataa kuondoka madaralani. Hapa kweli alikua anampiga vijembe Mugabe aliyekua amegoma kuachia wengine wagombee urais wa Zimbabwe
Tofauti yake na waliokuja kumrithi ni uwezo wake mkubwa wa kujenga hoja, akili angavu ya kuona mbali na hata uadilifu(hakuiibia nchi wala kua na double standards kwa wasaidizi wake). Kiasi kwamba mkono wake wa chuma haukuonekana wala hila zake hazikung'amuliwa mapema!
Pili ni suala la hali ngumu ya kiuchumi iliyoikumba nchi miaka ya mwanzoni ya 1980s hasa baada vita ya Kagera. Ni kweli yaliagizwa mahindi ya Yanga kutoka Marekani lakini si kweli kwamba yalitosheza na kwamba eti watu walikula na kusaza!!!
Kulikua na uhaba wa kila kitu ikiwemo bidhaa zote muhimu kama sukari, sabuni, mafuta ya kula na ya nishati n.k, ambapo zilipatikana kwa foleni na wakati mwingine kwa rushwa na hii ni kutokana na rigidity ya Mwalimu Nyerere kukataa kukubaliana na sera za mashrika ya fedha ya kimataifa na nchi wafadhili/wahisani