Obedi Milinga
Member
- Dec 31, 2018
- 11
- 4
Wasioelewa wanachoomba husema hivyo. Lakini ungejaliwa kufikia umri wa kustaafu haungesema hivyo. Ukitaka kuelewa ukweli watazame wale wastaafu wa Afrika Mashariki wanavyohangaika kila mwaka kuiomba serikali iwaingize kwenye daftari la wastaafu ili wao nao wapate pensheni kila mwezi kama wenzao waliokuwa kwenye mifuko. Kawaulize wastaafu wa PPF waliolipwa 100% kila siku nasikia wapo ofisini wakiomba na wao warudishwe kwenye daftari la wastaafu ili wawe wanalipwa kila mwezi. Kuchukua chako chote kwa sasa hivi ni kutoona mbali. Ni kujifanya wewe ni mjanja wa kupanga matumizi na kwamba unayaweza. Ni kusahau kwamba binadam huwa anabadilika akiwa na pesa mkononi na anaweza kutumia pesa vibaya akabaki hana mbele wa nyuma. Hiyo ndiyo sifa ya binadamu duniani kote. Ndiyo maana ukiajiriwa kwa mkataba wa Mwaka au miaka 5 hawakulipi mishahara yako yote ya miaka 5 ili ukajijue mwenyewe. Utazimaliza pesa zote kabla ya hiyo miaka 5 na utaanza kusumbua mwajiri wako.Watupatie chetu kwa asilimia miamoja. Sijawa mzalendo kiasi hicho pesa yangu ikajenge reli.
Sent using Jamii Forums mobile app