Rais Magufuli aamuru Kikokotoo kilichokuwa kinatumiwa awali kiendelee hadi 2023 (kulingana na mfuko husika)

Watupatie chetu kwa asilimia miamoja. Sijawa mzalendo kiasi hicho pesa yangu ikajenge reli.

Sent using Jamii Forums mobile app
Wasioelewa wanachoomba husema hivyo. Lakini ungejaliwa kufikia umri wa kustaafu haungesema hivyo. Ukitaka kuelewa ukweli watazame wale wastaafu wa Afrika Mashariki wanavyohangaika kila mwaka kuiomba serikali iwaingize kwenye daftari la wastaafu ili wao nao wapate pensheni kila mwezi kama wenzao waliokuwa kwenye mifuko. Kawaulize wastaafu wa PPF waliolipwa 100% kila siku nasikia wapo ofisini wakiomba na wao warudishwe kwenye daftari la wastaafu ili wawe wanalipwa kila mwezi. Kuchukua chako chote kwa sasa hivi ni kutoona mbali. Ni kujifanya wewe ni mjanja wa kupanga matumizi na kwamba unayaweza. Ni kusahau kwamba binadam huwa anabadilika akiwa na pesa mkononi na anaweza kutumia pesa vibaya akabaki hana mbele wa nyuma. Hiyo ndiyo sifa ya binadamu duniani kote. Ndiyo maana ukiajiriwa kwa mkataba wa Mwaka au miaka 5 hawakulipi mishahara yako yote ya miaka 5 ili ukajijue mwenyewe. Utazimaliza pesa zote kabla ya hiyo miaka 5 na utaanza kusumbua mwajiri wako.
 
Nimpongeze Mh. Rais kwa maamuzi yake ya kipindi cha mpito ili kupisha utafiti zaidi na kuwa na maamuzi yatakayokuwa na Tina kwa pande zote. Ni kweli wafanyakazi awmelia sana na kikokotoo kipya na ili una sana moyo. Ila kwa maamuzi haya inatia moyo.
Ni kweli sheria inaweza kupitishwa na Mh. akaisaini lakini pale anapogundua kuwa in Aleta shida katika utekelezaji wake bado nafasi yake ameitumia vizuri kubadilisha / kusitisha ili uchunguzi zaidi ufanyike. HONGERA MH. RAIS KWA MAAMUZI YA KIUME ULIYOYAFANYA. CHAPA KAZI KUINUA WANYONYE WATANZANIA NA TAIFA KWA UJUMLA.
BWANA AZIDI KUKUBARIKI NA KUKUTUMIA. HIZI KELELE ZA CHURA ZISIKUTISHE. HAPA KAZI TU.

Mimi nadhani ni mapema sana. Ukweli ukiujua hali ilivyo kwenye Mifuko hiyo utawaza upya. Kwa kikokotoo hicho alichopendekeza kitumike kuwalipa mafao wastaafu, napenda kukueleza kwamba Mfuko mpya wa PSSSF hautaweza kuwalipa wastaafu wake hata kwa miaka 3 tu. Fomula hiyo inafyooooonza sana fedha za Mfuko. Fomula hiyo haina tofauti na DECI system au UPATU au PONZI Scheme. Hiyo fomula iliyopendekezwa inatumiwa na makundi ya UPATU duniani kulipana pesa kuuubwa kutoka kwenye kuchangiana wao kwa wao na hatimaye wanakuwepo watu wengine chini wanaokosa malipo au mafao wakija kudai kwa sababu ya kanuni au fomula inayotumika kulipana.

Ni vyema kushauriana na kuambiana ukweli. Hiyo fomula haipo duniani kote. Ipo tu kwenye vyama vya UPATU. Kama hukubaliani nami nenda kote duniani ukaulize fomula inayotumika kulipa mfao kwenye mifuko ya Hifadhi ya Jamii duniani.
 
Kwanza nimpongeza Mhesh.Raisi kwa maamuzi ya kizalendo na busara ya kusimamisha kikokotozi kipya cha ssra.
Ili kuondoa dhana ya ubaguzi wakati mifuko yote ni kwaajili ya watanzania,, tunapoenda kama taifa kutengeneza kikokotozi kimpya ni vema na haki mifuko yote miwili,NSSF na PSSSF ikawa na kikokotozi KIMOJA TUU kinachofanana kwa mifuko yote.
Hii itaondoa unyonyaji wa mfuko wa NSSF ambao mkupuo ni 25% tu.

Hii siyo HAKI na haikubaliki hata kidogo. Na ni kinyume cha matakwa ya katiba ya nchi inayozuia kutunga sheria za jamuhuri zenye ubaguzi wa aina yoyote ile.
SSRA ilishindwa kutekeleza majukumu yake ya kuhakikisha mifuko inawanufaisha wenye mifuko, SIYO uwekezaji wa hovyo.
 
UPDATES:



Viongozi wa Vyama vya wafanyakazi wametoa historia ya walikotoka hadi walikofika. Aidha, wamedokeza kuwa wapo waliozimia kwenye ofisi za Mifuko ya Hifadhi ya Jamii.

Rais Magufuli anawasikiliza na anataka kila mtu aongee na kutoa dukuduku ili aweze kuongea.

Viongozi wa vyama vya wafanyakazi (upande wa walimu) wanadai kikokotoo kimekuwa ni suala kubwa na Rais Magufuli kama mwalimu anatambua changamoto za walimu. Wanamwomba Rais aliangalie suala la kikokotoo kwa jinsi atakavyoweza kwakuwa wanajua anaweza na kwa wanavyomsaidia Mungu atamsaidia alitatue hili.

TUGHE: Tunakupongeza Mhe. Rais, lakini tunapenda ufahamu kuwa wastaafu wengi hawakuwa wameandaliwa na mabadiliko haya yametokea ghafla na kusababisha negative impact. Morali ya kazi imeshuka!

Waziri Mhagama
Hoja na kuunganisha mifuko ilikuwa ni hoja ya wafanyakazi.

Hapa tunazungumza tu kikokotoo, ili tupate kikokotoo lazima turudi kwenye contribution rate, tukitaka tuendelee na kikokotoo cha 50% contribution itabidi itoke kwenye 20% hadi 25%.

TUCTA: Tunafahamu kwa moyo wako na unavyowasaida wanyonge. Tunaamini utasaidia kutatua

Mwanzo Wastaafu walikuwa wanapata 50% kwa mkupuo na 50% kidogo kidogo kila mwaka

Tulipendekeza mkupuo uwe 40% na si 25%


CHAMA CHA WALIMU: Suala la kikokotoo ni shida, hakuna asiyejua shida za waalimu. Uzuri ni kwamba hata wewe Rais ni Mwalimu

Kwasasa hata mishahara ya mwisho wa mwezi haitoshi. Kwa namna unavyofanya mambo makubwa najua hata hili unaliweza


TUGHE: Wastaafu wengi hatukuwaandaa kisaikolojia. Mabadiliko haya ya kikokotoo cha mafao yametokea kwa ghafla sana.

Wafanyakazi wa umma waliowengi wanalalamika nakuomba mheshimiwa Rais uongee chochote ili Wafanyakazi warudi kwenye morali ya kazi

TUICO: Watu wa sekta binafsi kima chao cha chini ni 100,000. Ili kwenda vizuri kamati itakayoundwa ikachunguze hii mishahara

Pia kuna fao la kupoteza ajira hawalipwi na makampuni mengi yanaondoka bila ya kuwalipa


WAFANYAKAZI WA RELI: Tumepitia misukosuko sana ikiwemo mishahara kuwa kidogo na ulipwaji wake ni wa kusuasua sana

Tulitegemea mafao ya kustaafu yatusaidie kujenga nyumba ili hata tukifa tufe vizuri.

Ile 50% ya awali kama haiwezekani basi tunakubali iwe 40%


TAMICO: Kwenye suala la kikokotoo kuna shida hasa kwenye fao la kujitoa ambalo mbadala wake ni fao la kukosa ajira

Sekta binafsi tunapata shida kwasababu kazi zetu si za muendelezo. Tunaomba iwepo tofauti kwa watu wa sekta ya migodi na ujenzi kwenye fao la kukosa ajira


SERIKALI ZA MITAA: Tunapenda mifuko iwe imara lakini kwa mishahara yetu hii midogo kwa kweli inaumiza

Rais kelele ni nyingi sana, na kwa kikokotoo hiki mfanyakazi akistaafu atashindwa hata kujenga


CHAMA CHA WAAJIRI: Sheria hii ya mifuko ya jamii, ililenga kuiweka mifuko hii kuwa katika hali ya usawa

Baada ya mifuko kuunganishwa uchangiaji umekuwa ukitofautiana kutoka mfanyakazi mmoja hadi mwingine.

Kila mfuko una tafsiri yake ya mchango wa mwanachama


HOTUBA YA RAIS MAGUFULI

Nimeamua niwaite wote ili niwe referee na inawezekana nikawa refaree mbaya

Nisingeweza kuwaita Wafanyakazi wote na tatizo hili naona litafikia mwisho.

Rais Magufuli: Kwenye baraza la Mawaziri tulikubaliana kuinganisha mifuko ya jamii

Hatua hii ilitokana na maombi ya muda mrefu ya vyama vya Wafanyakazi kutaka mifuko iiunganishwe

Watu walijua inaelekea kufa na kweli ilikuwa inaelekea huko

Nimewasikiliza, hapa tunaweza kuongea ikafika jioni. Tunaweza kunaliza yakaletwa mengine na ndio maana nataka tu concentrate sehemu moja. Ndio maana nimeleta regulator ili watoe mawazo yaliyo academic.

Nilipokuwa mwalimu nilianza na mshahara wa 1045, ninapofanya kazi nikataka kustaafu nianze kupata usumbufu naomba sio vizuri ndio maana nimewaita hapa tuzungumze.

Mtakumbuka tarehe 20 Oktoba 2017 baraza la mawaziri tulipitisha kuunganisha mifuko ya kijamii iwe mmoja kwabajili ya watumishi wa umma na NSSF ifanyiwe marekebisho ili iwe kwa ajili ya wafanyakazi wa sekta binafsi.

Sababu ya kuunganisha mifuko hii ni kwamba watu walijua inakwenda kufa na kweli ilikuwa inakwenda kufa.

Kabla ya mifuko kuunganishwa kila mfuko ulikuwa na wanachama wake. Jumla ya wanachama wote ilikuwa milioni 1.2.

Awamu ya tano mifuko ilikuwa hali mbaya na walikuwa wanapigana vita na kugombania wanachama.

Hii mifuko pengine ilikuwa inaendesha kiajabu ajabu. Miradi mingi ikawa inaanzishwa hasa ya majengo. Nenda Dege Eco Village, Kigamboni uangalie majengo yale sasa mwekezaji alikuwa anategemea return gani?

Tulipoingia madarakan tulikuwa deni kubwa la trilioni 1.2, ikabidi tutafuta pesa Serikalini tukaanza kulipa madeni haya na tumelipa yote mpaka March 2017.

Rais Magufuli: Sheria inawataka wapewe kidogokidogo si bora unipe zote nikafe vizuri

Mtu anafanyakazi yake kwa muda wote, halafu anamaliza unamwambia apewe asilimia 25, haiingii akilini. utanipa kidogokidogo? hata Waziri akimaliza Ubunge wake ukimwambia utampa 25% kisha nyingine kidogo kidogo hawezi kukubali

Kuna challanges ambazo hatuwezi kuzikwepa kwenye mifuko hii na ninyi wenyewe mmesema kuwa matatizo yapo

Ni lazima kuzitatua changamoto hizi, mmesema watu wanapenda #Kikokotoo kitoe angalau 50% ya mafao kama ilivyokuwa hapo awali

Wakati wa kuunganisha mifuko wastaafu walikuwa wanadai bilioni 700 na zaidi ya bilioni 500 zimelipwa.

Hii fomula iliyotumiwa na PSPF na NSSF haipo duniani.

Walioiweka ni makatibu wakuu wa wakati ule, sio wakati wangu

Rais Magufuli: Niombe kwenye mifuko waboreshe daftari la wastaafu ili kuondoa wastaafu hewa

Kama tulikuwa na wanafunzi hewa, watumishi hewa, pembejeo hewa hatuwezi kukosa wastaafu hewa

Rais Magufuli: Hifadhi za Jamii zipunguze matumizi ya hovyo, zikiwa fedha za Wastaafu zinatakiwa kulipwa kwa mkupuo hata wa 60% haitawezekana kwasababu hakutakuwa na hizo fedha

Yawezekana tatizo halianzi kwenye kikokotoo bali hata uendeshwaji wa mashirika haya

Nafahamu shirika moja linalotumia bilioni 1.3 kuchapisha kaenda na matangazo. Wanachama hamuwezi kujua kama fedha zenu zinatumika hovyo

Limeajiri walinzi na kuwalipa bilioni 2 kwa mwaka, kama wangeajiri SUMA JKT wangelipa bilioni 1

Nitoe wito kwa watendaji wakuu, tupunguze gharama za uendeshaji wa mifuko. Sasa imebaki mifuko 2 hakuna sababu za kushindana

Wafanyakazi wa Serikali ambao ni wanachama wa NSSF wahamishiwe PSSSF na wale wa sekta binafsi vivyo hivyo

Mashirika yaanze kuangalia namna ya kuongeza wanachama sioni sababu ya NSSF kuwa na wanachama laki nne nchi nzima wakati sekta binafsi inakuwa kila siku

Wale wafanyakazi wa migodi na ujenzi kuna sababu gani ya wao kusubiri hadi miaka 60 wakati kazi zao ni za kipindi kifupi.

Tuongeze option za wanachama. Kustaafu sio dhambi, kustaafu ni heshima lazima mstaafu awe respected

Mwalimu aliyefundisha kwa uaminifu miaka 40 hadi chaki zimemharibia macho na aliowafundisha wamekuwa na mishahara mikubwa na wengine ndio wakurugenzi wa NSSF

Ukitaka kuchukua mafao yake unamwambia nitakupa kidogo ili ukaishi, aliyekwambia nani ataishi?

Nimeamua tuwe na kipindi cha mpito, nimeamua kikokotoo kilichokuwa kinatumika kabla ya mifuko kuunganishwa kiendelee katika kipindi cha miaka yote ya mpito

Kipindi cha mpito ni hadi mwaka 2023 ambapo wanachama wa mfuko 58,000 ndio watastaafu kipindi hicho.

Wanachama watakaokuwa wanastaafu wataendelea na kikokotoo cha 50%

Rais Magufuli: Mimi nitaichungulia hiyo mifuko na nina uhakika Waziri na Katibu Mkuu wa wizara zinazohusika wafuatilie mifuko isitumike hovyo

Katika kipindi hicho watawalipa watu mafao vizuri na kwasababu hali itakuwa imeimarika tutafanya mazungumzo ya mfumo bora

Niakubaliana kuwa si kweli lengo langu mifuko, ndani ya Serikali na vyama vya wafanyakazi mkae mjadili njia bora ya kukokotoa mafao

Mifuko itakuwa imeimarika na itaweza kulipa, hata mkikubaliana kupeana 70% mimi sina neno

Si kweli kwamba lengo langu mifuko ife, ndani ya Serikali na vyama vya wafanyakazi mkae pamoja mjadili njia bora ya kukokotoa mafao

Mifuko itakuwa imeimarika na itaweza kulipa, hata mkikubaliana kupeana 70% mimi sina neno

Viongozi wa wafanyakazi muache kutumiwa na wanasiasa, watakaotumiwa na wanasiasa wataondoka

Mafao yakiwa bora hata wizi na ufisadi utapungua, kwasababu kila mmoja atakuwa anajua kuwa akistaafu atapata fungu lake

sie wengine tulishamuelewa mapema! Wali wa kushiba unaonekana siniani! Mungu azidi kumuongoza rais wetu mpendwa Magu na serikali yetu kwa ujumla! Mungu azidi ibariki Tz!
 
UPDATES:



Viongozi wa Vyama vya wafanyakazi wametoa historia ya walikotoka hadi walikofika. Aidha, wamedokeza kuwa wapo waliozimia kwenye ofisi za Mifuko ya Hifadhi ya Jamii.

Rais Magufuli anawasikiliza na anataka kila mtu aongee na kutoa dukuduku ili aweze kuongea.

Viongozi wa vyama vya wafanyakazi (upande wa walimu) wanadai kikokotoo kimekuwa ni suala kubwa na Rais Magufuli kama mwalimu anatambua changamoto za walimu. Wanamwomba Rais aliangalie suala la kikokotoo kwa jinsi atakavyoweza kwakuwa wanajua anaweza na kwa wanavyomsaidia Mungu atamsaidia alitatue hili.

TUGHE: Tunakupongeza Mhe. Rais, lakini tunapenda ufahamu kuwa wastaafu wengi hawakuwa wameandaliwa na mabadiliko haya yametokea ghafla na kusababisha negative impact. Morali ya kazi imeshuka!

Waziri Mhagama
Hoja na kuunganisha mifuko ilikuwa ni hoja ya wafanyakazi.

Hapa tunazungumza tu kikokotoo, ili tupate kikokotoo lazima turudi kwenye contribution rate, tukitaka tuendelee na kikokotoo cha 50% contribution itabidi itoke kwenye 20% hadi 25%.

TUCTA: Tunafahamu kwa moyo wako na unavyowasaida wanyonge. Tunaamini utasaidia kutatua

Mwanzo Wastaafu walikuwa wanapata 50% kwa mkupuo na 50% kidogo kidogo kila mwaka

Tulipendekeza mkupuo uwe 40% na si 25%


CHAMA CHA WALIMU: Suala la kikokotoo ni shida, hakuna asiyejua shida za waalimu. Uzuri ni kwamba hata wewe Rais ni Mwalimu

Kwasasa hata mishahara ya mwisho wa mwezi haitoshi. Kwa namna unavyofanya mambo makubwa najua hata hili unaliweza


TUGHE: Wastaafu wengi hatukuwaandaa kisaikolojia. Mabadiliko haya ya kikokotoo cha mafao yametokea kwa ghafla sana.

Wafanyakazi wa umma waliowengi wanalalamika nakuomba mheshimiwa Rais uongee chochote ili Wafanyakazi warudi kwenye morali ya kazi

TUICO: Watu wa sekta binafsi kima chao cha chini ni 100,000. Ili kwenda vizuri kamati itakayoundwa ikachunguze hii mishahara

Pia kuna fao la kupoteza ajira hawalipwi na makampuni mengi yanaondoka bila ya kuwalipa


WAFANYAKAZI WA RELI: Tumepitia misukosuko sana ikiwemo mishahara kuwa kidogo na ulipwaji wake ni wa kusuasua sana

Tulitegemea mafao ya kustaafu yatusaidie kujenga nyumba ili hata tukifa tufe vizuri.

Ile 50% ya awali kama haiwezekani basi tunakubali iwe 40%


TAMICO: Kwenye suala la kikokotoo kuna shida hasa kwenye fao la kujitoa ambalo mbadala wake ni fao la kukosa ajira

Sekta binafsi tunapata shida kwasababu kazi zetu si za muendelezo. Tunaomba iwepo tofauti kwa watu wa sekta ya migodi na ujenzi kwenye fao la kukosa ajira


SERIKALI ZA MITAA: Tunapenda mifuko iwe imara lakini kwa mishahara yetu hii midogo kwa kweli inaumiza

Rais kelele ni nyingi sana, na kwa kikokotoo hiki mfanyakazi akistaafu atashindwa hata kujenga


CHAMA CHA WAAJIRI: Sheria hii ya mifuko ya jamii, ililenga kuiweka mifuko hii kuwa katika hali ya usawa

Baada ya mifuko kuunganishwa uchangiaji umekuwa ukitofautiana kutoka mfanyakazi mmoja hadi mwingine.

Kila mfuko una tafsiri yake ya mchango wa mwanachama


HOTUBA YA RAIS MAGUFULI

Nimeamua niwaite wote ili niwe referee na inawezekana nikawa refaree mbaya

Nisingeweza kuwaita Wafanyakazi wote na tatizo hili naona litafikia mwisho.

Rais Magufuli: Kwenye baraza la Mawaziri tulikubaliana kuinganisha mifuko ya jamii

Hatua hii ilitokana na maombi ya muda mrefu ya vyama vya Wafanyakazi kutaka mifuko iiunganishwe

Watu walijua inaelekea kufa na kweli ilikuwa inaelekea huko

Nimewasikiliza, hapa tunaweza kuongea ikafika jioni. Tunaweza kunaliza yakaletwa mengine na ndio maana nataka tu concentrate sehemu moja. Ndio maana nimeleta regulator ili watoe mawazo yaliyo academic.

Nilipokuwa mwalimu nilianza na mshahara wa 1045, ninapofanya kazi nikataka kustaafu nianze kupata usumbufu naomba sio vizuri ndio maana nimewaita hapa tuzungumze.

Mtakumbuka tarehe 20 Oktoba 2017 baraza la mawaziri tulipitisha kuunganisha mifuko ya kijamii iwe mmoja kwabajili ya watumishi wa umma na NSSF ifanyiwe marekebisho ili iwe kwa ajili ya wafanyakazi wa sekta binafsi.

Sababu ya kuunganisha mifuko hii ni kwamba watu walijua inakwenda kufa na kweli ilikuwa inakwenda kufa.

Kabla ya mifuko kuunganishwa kila mfuko ulikuwa na wanachama wake. Jumla ya wanachama wote ilikuwa milioni 1.2.

Awamu ya tano mifuko ilikuwa hali mbaya na walikuwa wanapigana vita na kugombania wanachama.

Hii mifuko pengine ilikuwa inaendesha kiajabu ajabu. Miradi mingi ikawa inaanzishwa hasa ya majengo. Nenda Dege Eco Village, Kigamboni uangalie majengo yale sasa mwekezaji alikuwa anategemea return gani?

Tulipoingia madarakan tulikuwa deni kubwa la trilioni 1.2, ikabidi tutafuta pesa Serikalini tukaanza kulipa madeni haya na tumelipa yote mpaka March 2017.

Rais Magufuli: Sheria inawataka wapewe kidogokidogo si bora unipe zote nikafe vizuri

Mtu anafanyakazi yake kwa muda wote, halafu anamaliza unamwambia apewe asilimia 25, haiingii akilini. utanipa kidogokidogo? hata Waziri akimaliza Ubunge wake ukimwambia utampa 25% kisha nyingine kidogo kidogo hawezi kukubali

Kuna challanges ambazo hatuwezi kuzikwepa kwenye mifuko hii na ninyi wenyewe mmesema kuwa matatizo yapo

Ni lazima kuzitatua changamoto hizi, mmesema watu wanapenda #Kikokotoo kitoe angalau 50% ya mafao kama ilivyokuwa hapo awali

Wakati wa kuunganisha mifuko wastaafu walikuwa wanadai bilioni 700 na zaidi ya bilioni 500 zimelipwa.

Hii fomula iliyotumiwa na PSPF na NSSF haipo duniani.

Walioiweka ni makatibu wakuu wa wakati ule, sio wakati wangu

Rais Magufuli: Niombe kwenye mifuko waboreshe daftari la wastaafu ili kuondoa wastaafu hewa

Kama tulikuwa na wanafunzi hewa, watumishi hewa, pembejeo hewa hatuwezi kukosa wastaafu hewa

Rais Magufuli: Hifadhi za Jamii zipunguze matumizi ya hovyo, zikiwa fedha za Wastaafu zinatakiwa kulipwa kwa mkupuo hata wa 60% haitawezekana kwasababu hakutakuwa na hizo fedha

Yawezekana tatizo halianzi kwenye kikokotoo bali hata uendeshwaji wa mashirika haya

Nafahamu shirika moja linalotumia bilioni 1.3 kuchapisha kaenda na matangazo. Wanachama hamuwezi kujua kama fedha zenu zinatumika hovyo

Limeajiri walinzi na kuwalipa bilioni 2 kwa mwaka, kama wangeajiri SUMA JKT wangelipa bilioni 1

Nitoe wito kwa watendaji wakuu, tupunguze gharama za uendeshaji wa mifuko. Sasa imebaki mifuko 2 hakuna sababu za kushindana

Wafanyakazi wa Serikali ambao ni wanachama wa NSSF wahamishiwe PSSSF na wale wa sekta binafsi vivyo hivyo

Mashirika yaanze kuangalia namna ya kuongeza wanachama sioni sababu ya NSSF kuwa na wanachama laki nne nchi nzima wakati sekta binafsi inakuwa kila siku

Wale wafanyakazi wa migodi na ujenzi kuna sababu gani ya wao kusubiri hadi miaka 60 wakati kazi zao ni za kipindi kifupi.

Tuongeze option za wanachama. Kustaafu sio dhambi, kustaafu ni heshima lazima mstaafu awe respected

Mwalimu aliyefundisha kwa uaminifu miaka 40 hadi chaki zimemharibia macho na aliowafundisha wamekuwa na mishahara mikubwa na wengine ndio wakurugenzi wa NSSF

Ukitaka kuchukua mafao yake unamwambia nitakupa kidogo ili ukaishi, aliyekwambia nani ataishi?

Nimeamua tuwe na kipindi cha mpito, nimeamua kikokotoo kilichokuwa kinatumika kabla ya mifuko kuunganishwa kiendelee katika kipindi cha miaka yote ya mpito

Kipindi cha mpito ni hadi mwaka 2023 ambapo wanachama wa mfuko 58,000 ndio watastaafu kipindi hicho.

Wanachama watakaokuwa wanastaafu wataendelea na kikokotoo cha 50%

Rais Magufuli: Mimi nitaichungulia hiyo mifuko na nina uhakika Waziri na Katibu Mkuu wa wizara zinazohusika wafuatilie mifuko isitumike hovyo

Katika kipindi hicho watawalipa watu mafao vizuri na kwasababu hali itakuwa imeimarika tutafanya mazungumzo ya mfumo bora

Niakubaliana kuwa si kweli lengo langu mifuko, ndani ya Serikali na vyama vya wafanyakazi mkae mjadili njia bora ya kukokotoa mafao

Mifuko itakuwa imeimarika na itaweza kulipa, hata mkikubaliana kupeana 70% mimi sina neno

Si kweli kwamba lengo langu mifuko ife, ndani ya Serikali na vyama vya wafanyakazi mkae pamoja mjadili njia bora ya kukokotoa mafao

Mifuko itakuwa imeimarika na itaweza kulipa, hata mkikubaliana kupeana 70% mimi sina neno

Viongozi wa wafanyakazi muache kutumiwa na wanasiasa, watakaotumiwa na wanasiasa wataondoka

Mafao yakiwa bora hata wizi na ufisadi utapungua, kwasababu kila mmoja atakuwa anajua kuwa akistaafu atapata fungu lake


hicho kikokoto wali nunua duka gani.maana kilipata mpaka mzabuni itakuwa na fisim wakipitisha na dk asiye kuwa hospital
 
mpaka sasa bado wastaafu hawajalipwa mafao yao na shule zimefunguliwa sasa hapo sijui hawakumuelewa Raisi au amedanganya mbele ya vyama vya wafanyakazi,ukienda kwenye mifuko ya jamii wanakuambia wanasubiri kanuni zipitiwe na bunge huku Raisi alisema watumi kanuni zao za zamani. Tanzania matatizo makubwa
 
mpaka sasa bado wastaafu hawajalipwa mafao yao na shule zimefunguliwa sasa hapo sijui hawakumuelewa Raisi au amedanganya mbele ya vyama vya wafanyakazi,ukienda kwenye mifuko ya jamii wanakuambia wanasubiri kanuni zipitiwe na bunge huku Raisi alisema watumi kanuni zao za zamani. Tanzania matatizo makubwa
Shida kubwa ni je_hayo mafao yatalipwa kwa wakati ama usumbufu wa nssf wa njoo kesho njoo week ijayo utaendelea...hata hizo 33.3 % zilizopokelewa tangu November 2018 bado hawajawalipa
...nenda nssf hapo Ilala/Temeke utawaonea watu huruma

Sent using Jamii Forums mobile app
 
mpaka sasa bado wastaafu hawajalipwa mafao yao na shule zimefunguliwa sasa hapo sijui hawakumuelewa Raisi au amedanganya mbele ya vyama vya wafanyakazi,ukienda kwenye mifuko ya jamii wanakuambia wanasubiri kanuni zipitiwe na bunge huku Raisi alisema watumi kanuni zao za zamani. Tanzania matatizo makubwa

Hatari Sana... Yupo mwanasiasa anasema hiyo mifuko imefilisika... Pesa nyingi imeliwa ktk miradi na mikopo kwa watu maalum...
 
Hivi mbona mambo mengine yanashughulikiwa kwa haraka hivyo, iweje mafao ya uzeeni na mafao mengine yanasuasua utafikiri tunazikopa, kuna ndugu zangu wengi tu wanasubiria pension yao mpaka leo mwaka umepita sasa, hela ni zetu nyambafu sio za mkopo,
 
Maamuzi ya Rais hayakuwasaidia watumishi Wa umma waliokuwa wanachangia NSSF na PPF. Wameendelea kulipwa Kwa kikokotoo chao cha asilimia 25 hata kama wote walihamishiwaPSSSF! Ukistaafu kikokotoo cha asilimia 25 kinakuhusu!! Ni maumivu mpaka basi!
 
Chonde chonde wafanyakakazi , muda wenu ndio huu
Hahahaha
Mtafukua makaburi ambayo tayari wafu walishafufuka kitambo.

Rais alishatoa maelekezo ya kusimamisha hicho kikokotoo.

Hii hoja ya 2018 unaiibua leo ili kuitumia kwenye kampeni...
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom