Rais Magufuli aagiza Mkuu wa Wilaya Nkasi na RPC Rukwa kumlipa mama aliyeibiwa ng'ombe 25 fidia ya Tsh milioni 15 kwa sababu ya uzembe

johnthebaptist

JF-Expert Member
May 27, 2014
83,777
141,646
Rais Magufuli amemwamuru mkuu wa wilaya ya Nkasi pamoja na mkuu wa polisi wa wilaya hiyo kumlipa mama mjane jumla ya sh milioni 15 ikiwa ni thamani ya ng'ombe zake alizoibiwa.

DC na OCD walizembea na kusababisha mwizi wa ng'ombe kutoroka ilhali alishakamatwa na kufikishwa polisi.

Rais Magufuli amewapa siku 5 kulipa deni hilo.

Chanzo: TBC!
******

Rais Magufuli ameagiza Polisi wakiongozwa na Kamanda wa Polisi Mkoani humo, Mathias Nyange na Mkuu wa Wilaya ya Nkasi, Said Mtanda kumlipa Felista Mkombo Tsh. Milioni 15

Fedha hizo ni kama fidia kutokana na Polisi kutoshughulikia vizuri suala lake la kuibiwa ng’ombe ambapo mama huyo aliibiwa ng’ombe 25 na Polisi walimwachia Mtuhumiwa na baadaye Mtuhumiwa huyo akatoroka

Aidha, amesikitishwa na namna viongozi wa Mkoa huo wanavyoshughulikia kero za Wananchi na mara baada ya hotuba yake aliagiza viongozi hao wakiongozwa na Mkuu wa Mkoa, Joachim Wangabo kubaki mkutanoni na kusikiliza kero za Wananchi waliokuwa wamebeba mabango
 
Rais ampatia DC na RPC kumlipa Mama mmoja Wilaya Nkasi mkoani Rukwa milioni 15,000,000/=(Milioni kumi na tano) ndani ya siku tano kwa sababu ya uzembe wa kusimamia kesi ya uwizi wa ng'ombe. Inaelezwa mshukiwa alitoroka bada ya kupewa dhamana.

Wakati Rais akitoa hotuba kuna Mama alisimama na kusema aliibiwa ng'ombe 25. Mwizi alikamatwa na akalipa ng'ombe wawili. Lakini akiwa bado yupo mahabusu polisi walimtoa kwa dhanana na akapotea. Sasa ni muda mrefu huyo mama mjane anafuatilia wilayani na mkoani bila mafanikio.

Pia Mh Rais ametoa rai kwa viongozi kuwa inapotokea kuna kiongozi amefanya kosa mahali fulani asihamishiwe mahali pengine bali wafukuzwe na sheria zingine kufuata.
 
Saa Nyingine Viongozi Ninaowateua Hawawasiliani Hivi Ulishindwa Kumwagiza OCD Ampige Pingu Huyo Manager Wa Tanesco
 
Huu ni unyanyasaji kutoka kwa mtu anaejinasibu kuwa ni kiongozi wa nyonge na niuingiliaji wa muhimili mwingine wa mahakama, hili jambo ni la kisheria kama sheria inaruhusu dhamana kwa mtuhumiwa OCD na DC wanalipaje? na hiyo fedha wanaitoa wapi kwa muda wa siku 5?.
 
Kuna
Rais ampatia DC na RPC kumlipa Mama mmoja Wilaya Nkasi mkoani Rukwa milioni 15,000,000/=(Milioni kumi na tano) ndani ya siku tano kwa sababu ya uzembe wa kusimamia kesi ya uwizi wa ng'ombe. Inaelezwa mshukiwa alitoroka bada ya kupewa dhamana.

Wakati Rais akitoa hotuba kuna Mama alisimama na kusema aliibiwa ng'ombe 25. Mwizi alikamatwa na akalipa ng'ombe wawili. Lakini akiwa bado yupo mahabusu polisi walimtoa kwa dhanana na akapotea. Sasa ni muda mrefu huyo mama mjane anafuatilia wilayani na mkoani bila mafanikio.

Pia Mh Rais ametoa rai kwa viongozi kuwa inapotokea kuna kiongozi amefanya kosa mahali fulani asihamishiwe mahali pengine bali wafukuzwe na sheria zingine kufuata.
Kuna askari katajwa maarufu kama GADAFI aliehamishiwa mjini si angemshughulikia na huyo....anaonekana anahusika kabisa na kula rushwa.
 
Rais Magufuli amemwamuru mkuu wa wilaya ya Nkasi pamoja na mkuu wa polisi wa wilaya hiyo kumlipa mama mjane jumla ya sh milioni 15 ikiwa ni thamani ya ng'ombe zake alizoibiwa.

DC na OCD walizembea na kusababisha mwizi wa ng'ombe kutoroka ilhali alishakamatwa na kufikishwa polisi.

Rais Magufuli amewapa siku 5 kulipa deni hilo.

Chanzo: TBC!
----

Rais JPM alikumbuka pia Kumuhakikishia Ulinzi madhubuti huyo Mama Mjane ili pengine ndani ya hizo Siku asiambiwe Kafa?
 
Rais ampatia DC na RPC kumlipa Mama mmoja Wilaya Nkasi mkoani Rukwa milioni 15,000,000/=(Milioni kumi na tano) ndani ya siku tano kwa sababu ya uzembe wa kusimamia kesi ya uwizi wa ng'ombe. Inaelezwa mshukiwa alitoroka bada ya kupewa dhamana.

Wakati Rais akitoa hotuba kuna Mama alisimama na kusema aliibiwa ng'ombe 25. Mwizi alikamatwa na akalipa ng'ombe wawili. Lakini akiwa bado yupo mahabusu polisi walimtoa kwa dhanana na akapotea. Sasa ni muda mrefu huyo mama mjane anafuatilia wilayani na mkoani bila mafanikio.

Pia Mh Rais ametoa rai kwa viongozi kuwa inapotokea kuna kiongozi amefanya kosa mahali fulani asihamishiwe mahali pengine bali wafukuzwe na sheria zingine kufuata.
Hiii imekaaa vizuri, maaaana waajiriwa wa serikali walikuwa waonevu sana
 
Back
Top Bottom