figganigga
JF-Expert Member
- Oct 17, 2010
- 25,491
- 54,884
Leo Watanzania kutoka nchi mbili za Zanzibar na Tanzania Bara wanaungano kusherehekea miaka 54 ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ulioasisiwa April 26, 1964
-
Lakini Muungano huu bado una kero ambazo hazijatafutiwa ufumbuzi licha ya kuwepo mijadala mbalimbali iliyolenga kuinua na kuimarisha Muungano
-
Changamoto(kero) mojawapo ni Hati ya Muungano ambayo inasimama kama Katiba ya Muungano ambayo bado inaleta changamoto katika uimarishaji wa Jamhuri.
-
Prof. Sherrif anaeleza kuwa, katika Hati ya Muungano, kitu kilichofanyika ni kwamba, jina la Serikali ya Tanganyika likabadilishwa na kupewa jina la Muungano wa Jamhuri ya Tanganyika na Jamhuri ya Watu wa Zanzibar
-
Anaeleza kuwa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar ipo lakini madaraka 11 ya serikali hiyo yalihamishwa na kupelekwa kwenye Serikali ya Muungano
-
Akahoji kuwa kwasasa tukiweka serikali 2 hizi katika mizani, zitakuwa hazina usawa tena, kwa sababu Serikali ya Muungano sasa imekusanya madaraka yote ya Tanganyika na mambo 11 ya Zanzibar
======
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli ameupandisha hadhi Mji wa Dodoma kutoka Halmashauri ya Manispaa na kuwa Halmashauri ya Jiji, na amemteua aliyekuwa Mkurugenzi wa Manispaa ya Dodoma Bw. Godwin Kunambi kuwa Mkurugenzi wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma.
Mhe. Rais Magufuli ametangaza uamuzi huo tarehe 26 Aprili, 2018 wakati akihutubia katika sherehe za kuadhimisha miaka 54 ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar zilizofanyika katika uwanja wa Jamhuri Jijini Dodoma.
Pamoja na kuupandisha hadhi Mji wa Dodoma Mhe. Rais Magufuli ameagiza taratibu za kisheria zifanyike kukamilisha mchakato huo, na amesisitiza kuwa azma ya Serikali kuhamia Dodoma inaendelea kutekelezwa na kwamba yeye mwenyewe atahamia Dodoma mwaka huu.
Sherehe hizo zimehudhuriwa na viongozi mbalimbali wakiwemo Makamu wa Rais Mhe. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dkt. Ali Mohamed Shein, Mke wa Rais Mhe. Mama Janeth Magufuli, Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mhe. Seif Ali Idd na Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa Majaliwa.
Viongozi wengine ni Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Job Yustino Ndugai, Jaji Mkuu wa Tanzania Mhe. Ibrahim Hamis Juma, Spika wa Baraza la Wawakilishi Zanzibar Mhe. Zubeir Ali Maulid, Jaji Mkuu wa Zanzibar Mhe. Omar Othman Makungu na Rais Mstaafu wa Awamu ya Tatu Mhe. Benjamin William Mkapa.
Katika sherehe hizo zilizohudhuriwa na Rais wa Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB) Dkt. Akinumwi Adesina, Mhe. Rais Magufuli ameishukuru AfDB kwa ufadhili wa miradi ya maendeleo yenye thamani ya Dola za Marekani Bilioni 3.457 sawa na Shilingi Trilioni 7 na Bilioni 778 za Tanzania zikiwemo fedha za miradi 25 zilizotolewa kuanzia mwezi Novemba, 2017 yenye thamani ya Dola za Marekani Bilioni 1.986 sawa na Shilingi Trilioni 4 na Bilioni 467 za Kitanzania.
Mhe. Rais Magufuli amewapongeza Watanzania wote kwa kutimiza miaka 54 ya muungano na amesisitiza kuwa yeye na Rais wa Zanzibar Dkt. Ali Mohamed Shein wapo imara na wataendelea kuwa imara kuulinda na kuudumisha muungano, kuilinda amani na kupigania maendeleo ya Tanzania.
“Taifa letu linakwenda vizuri, uchumi wetu unakua vizuri, mwaka jana umekuwa kwa wastani wa asilimia 7 na mwaka huu tunatarajia utakua kwa wastani wa asilimia 7.1, mfumuko wa bei umeendelea kuwa chini kwa wastani wa asilimia 4” amesema Mhe. Rais Magufuli.
Kabla ya kuhutubia wananchi Mhe. Rais Magufuli amekagua gwaride rasmi lililoandaliwa na majeshi ya ulinzi na usalama na amewaongoza viongozi mbalimbali na wananchi kushuhudia maonesho ya gwaride, mazoezi ya kujihami, halaiki, muziki wa dansi na ngoma za makabila mbalimbali zilizotumbuiza uwanjani hapo.
Aidha, Mhe. Rais Magufuli amefanya mazungumzo rasmi na Rais wa AfDB Dkt. Adesina yaliyofanyika katika Ikulu ndogo ya Jijini Dodoma na kuhudhuriwa na Rais wa Zanzibar Mhe. Dkt. Shein.
Baada ya Mazungumzo hayo Dkt. Adesina amempongeza Mhe. Rais Magufuli kwa kazi kubwa anayoifanya kuimarisha uchumi wa Tanzania na amesema wamejadiliana mambo kadhaa yakiwemo namna benki hiyo ilivyosaidia juhudi za maendeleo za Tanzania tangu mwaka 1971 na inavyoendelea kusaidia katika ufadhili wa miradi mbalimbali ya maendeleo.
Ametaja baadhi ya maeneo ambayo AfDB itatoa ufadhili kuwa ni uzalishaji na usambazaji wa nishati, uboreshaji wa miundombinu ikiwemo ujenzi wa miundombinu ya Jiji la Dodoma hasa barabara.
“Yote kwa yote nimemhakikishia Mhe. Rais Magufuli kuwa AfDB itamuunga mkono katika mipango yake na maono yake ili tuweze kuisaidia Tanzania kukua zaidi, nimefurahi kuzungumza na Mhe. Rais na naona Tanzania ipo katika njia sahihi” amesema Dkt. Adesina.
Gerson Msigwa
Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, IKULU
Dodoma
26 Aprili, 2018
-
Lakini Muungano huu bado una kero ambazo hazijatafutiwa ufumbuzi licha ya kuwepo mijadala mbalimbali iliyolenga kuinua na kuimarisha Muungano
-
Changamoto(kero) mojawapo ni Hati ya Muungano ambayo inasimama kama Katiba ya Muungano ambayo bado inaleta changamoto katika uimarishaji wa Jamhuri.
-
Prof. Sherrif anaeleza kuwa, katika Hati ya Muungano, kitu kilichofanyika ni kwamba, jina la Serikali ya Tanganyika likabadilishwa na kupewa jina la Muungano wa Jamhuri ya Tanganyika na Jamhuri ya Watu wa Zanzibar
-
Anaeleza kuwa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar ipo lakini madaraka 11 ya serikali hiyo yalihamishwa na kupelekwa kwenye Serikali ya Muungano
-
Akahoji kuwa kwasasa tukiweka serikali 2 hizi katika mizani, zitakuwa hazina usawa tena, kwa sababu Serikali ya Muungano sasa imekusanya madaraka yote ya Tanganyika na mambo 11 ya Zanzibar
======
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli ameupandisha hadhi Mji wa Dodoma kutoka Halmashauri ya Manispaa na kuwa Halmashauri ya Jiji, na amemteua aliyekuwa Mkurugenzi wa Manispaa ya Dodoma Bw. Godwin Kunambi kuwa Mkurugenzi wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma.
Mhe. Rais Magufuli ametangaza uamuzi huo tarehe 26 Aprili, 2018 wakati akihutubia katika sherehe za kuadhimisha miaka 54 ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar zilizofanyika katika uwanja wa Jamhuri Jijini Dodoma.
Pamoja na kuupandisha hadhi Mji wa Dodoma Mhe. Rais Magufuli ameagiza taratibu za kisheria zifanyike kukamilisha mchakato huo, na amesisitiza kuwa azma ya Serikali kuhamia Dodoma inaendelea kutekelezwa na kwamba yeye mwenyewe atahamia Dodoma mwaka huu.
Sherehe hizo zimehudhuriwa na viongozi mbalimbali wakiwemo Makamu wa Rais Mhe. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dkt. Ali Mohamed Shein, Mke wa Rais Mhe. Mama Janeth Magufuli, Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mhe. Seif Ali Idd na Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa Majaliwa.
Viongozi wengine ni Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Job Yustino Ndugai, Jaji Mkuu wa Tanzania Mhe. Ibrahim Hamis Juma, Spika wa Baraza la Wawakilishi Zanzibar Mhe. Zubeir Ali Maulid, Jaji Mkuu wa Zanzibar Mhe. Omar Othman Makungu na Rais Mstaafu wa Awamu ya Tatu Mhe. Benjamin William Mkapa.
Katika sherehe hizo zilizohudhuriwa na Rais wa Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB) Dkt. Akinumwi Adesina, Mhe. Rais Magufuli ameishukuru AfDB kwa ufadhili wa miradi ya maendeleo yenye thamani ya Dola za Marekani Bilioni 3.457 sawa na Shilingi Trilioni 7 na Bilioni 778 za Tanzania zikiwemo fedha za miradi 25 zilizotolewa kuanzia mwezi Novemba, 2017 yenye thamani ya Dola za Marekani Bilioni 1.986 sawa na Shilingi Trilioni 4 na Bilioni 467 za Kitanzania.
Mhe. Rais Magufuli amewapongeza Watanzania wote kwa kutimiza miaka 54 ya muungano na amesisitiza kuwa yeye na Rais wa Zanzibar Dkt. Ali Mohamed Shein wapo imara na wataendelea kuwa imara kuulinda na kuudumisha muungano, kuilinda amani na kupigania maendeleo ya Tanzania.
“Taifa letu linakwenda vizuri, uchumi wetu unakua vizuri, mwaka jana umekuwa kwa wastani wa asilimia 7 na mwaka huu tunatarajia utakua kwa wastani wa asilimia 7.1, mfumuko wa bei umeendelea kuwa chini kwa wastani wa asilimia 4” amesema Mhe. Rais Magufuli.
Kabla ya kuhutubia wananchi Mhe. Rais Magufuli amekagua gwaride rasmi lililoandaliwa na majeshi ya ulinzi na usalama na amewaongoza viongozi mbalimbali na wananchi kushuhudia maonesho ya gwaride, mazoezi ya kujihami, halaiki, muziki wa dansi na ngoma za makabila mbalimbali zilizotumbuiza uwanjani hapo.
Aidha, Mhe. Rais Magufuli amefanya mazungumzo rasmi na Rais wa AfDB Dkt. Adesina yaliyofanyika katika Ikulu ndogo ya Jijini Dodoma na kuhudhuriwa na Rais wa Zanzibar Mhe. Dkt. Shein.
Baada ya Mazungumzo hayo Dkt. Adesina amempongeza Mhe. Rais Magufuli kwa kazi kubwa anayoifanya kuimarisha uchumi wa Tanzania na amesema wamejadiliana mambo kadhaa yakiwemo namna benki hiyo ilivyosaidia juhudi za maendeleo za Tanzania tangu mwaka 1971 na inavyoendelea kusaidia katika ufadhili wa miradi mbalimbali ya maendeleo.
Ametaja baadhi ya maeneo ambayo AfDB itatoa ufadhili kuwa ni uzalishaji na usambazaji wa nishati, uboreshaji wa miundombinu ikiwemo ujenzi wa miundombinu ya Jiji la Dodoma hasa barabara.
“Yote kwa yote nimemhakikishia Mhe. Rais Magufuli kuwa AfDB itamuunga mkono katika mipango yake na maono yake ili tuweze kuisaidia Tanzania kukua zaidi, nimefurahi kuzungumza na Mhe. Rais na naona Tanzania ipo katika njia sahihi” amesema Dkt. Adesina.
Gerson Msigwa
Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, IKULU
Dodoma
26 Aprili, 2018