Rais kwa teuzi hizi bado katiba ya Warioba inahitajika sana;

stigajemwa

JF-Expert Member
Nov 12, 2016
449
430
Wanabodi;
Nianze kwa kukumbushia msimamo wa Rais wa JMT kuwa katiba mpya si kipaumbele chake. Lakini kwa namna mambo yanavyokwenda bado inambidi aikubali katiba pendekezwa ya Warioba.

Imekuwa ni kawaida sasa kusikia Rais kafanya uteuzi Fulani.Yaani toka ameingia madarakani ni miaka mitatu lakini bado hajamaliza kuunda serikali.

Hii inatokana na ubovu wa katiba tuliyonayo ambayo inampa mamlaka makubwa rais, mojawapo ikiwa ni hiyo ya kuhusika na teuzi zote za watendajia na viongozi wa serikali bila mipaka.

Hasara ya jambo hill ni Rais kuteua viongozi na watendaji wabovU hivyo kujikuta kila Siku anateua na kutumbua kwa sababu ikulu pekee haina uwezo wa kutambua sifa na tabia za kila RAIA anayefaa kuwa kiongozi au mtendaji ndani ya nchi kubwa kijiografia na idadi ya watu kama Tanzania

Katiba pendekezwa ya Warioba ilimwekea mipaka Rais ktk teuzi zake,ambapo ilipendekeza kuwepo kwa kamati zinazohusika na kuandaa orodha ya wenye sifa husika kisha kupitia orodha hiyo ndio Rais anateua.

Katiba ya Warioba ingemsaidia rais kuokoa pesa za walipa kodi kwani hawa wanaotenguliwa kwa kukosea scouting wanarigharimu Taifa pesa nyingi.

Tumechoka hii hali Leo unateua mkurugenzi Takukuru kesho umemtengua,kesho kutwa mkurugenzi halmashauri Fulani siku inayofuata umemtengua.

Hawa wote wanaotenguliwa hulazimika kulipwa kwa kuwa utenguzi wao huwa ni mabadiliko ya kawaida ya kiutendaji. Au hulazimika kubadilishiwa kazi hivyo kuwa mzigo kwa Taifa.

Taifa linahitaji mfumo maalum unaohusika na scouting, mfumo ambao unahusisha kamati ya wataalamu wa fani husika ambao wanafanya kazi ya kuandaa orodha ndefu ya wadau wenye sifa. Kazi ya Rais inakuwa ni kupitia orodha hiyo na kufanya uteuzi.
Hii itaondoa kuwa na wateule wenye sifa zinazotia shaka kimaadili na kiutendaji kama ilivyo sasa kwa teuzi nyingi za wakurugenzi wa mashirika ya umma,wakurugenzi halmashauri mbalimbali, wakuu wa Wilaya na mikoa.

Miaka mitano itakwisha Rais anafikiria kuteua na kutengua badala ya kufikiria kuboresha maisha ya Watanzania.
Nawasilisha.
 
Wanabodi;
Nianze kwa kukumbushia msimamo wa Rais wa JMT kuwa katiba mpya si kipaumbele chake. Lakini kwa namna mambo yanavyokwenda bado inambidi aikubali katiba pendekezwa ya Warioba.

Imekuwa ni kawaida sasa kusikia Rais kafanya uteuzi Fulani.Yaani toka ameingia madarakani ni miaka mitatu lakini bado hajamaliza kuunda serikali.

Hii inatokana na ubovu wa katiba tuliyonayo ambayo inampa mamlaka makubwa rais, mojawapo ikiwa ni hiyo ya kuhusika na teuzi zote za watendajia na viongozi wa serikali bila mipaka.

Hasara ya jambo hill ni Rais kuteua viongozi na watendaji wabovU hivyo kujikuta kila Siku anateua na kutumbua kwa sababu ikulu pekee haina uwezo wa kutambua sifa na tabia za kila RAIA anayefaa kuwa kiongozi au mtendaji ndani ya nchi kubwa kijiografia na idadi ya watu kama Tanzania

Katiba pendekezwa ya Warioba ilimwekea mipaka Rais ktk teuzi zake,ambapo ilipendekeza kuwepo kwa kamati zinazohusika na kuandaa orodha ya wenye sifa husika kisha kupitia orodha hiyo ndio Rais anateua.

Katiba ya Warioba ingemsaidia rais kuokoa pesa za walipa kodi kwani hawa wanaotenguliwa kwa kukosea scouting wanarigharimu Taifa pesa nyingi.

Tumechoka hii hali Leo unateua mkurugenzi Takukuru kesho umemtengua,kesho kutwa mkurugenzi halmashauri Fulani siku inayofuata umemtengua.

Hawa wote wanaotenguliwa hulazimika kulipwa kwa kuwa utenguzi wao huwa ni mabadiliko ya kawaida ya kiutendaji. Au hulazimika kubadilishiwa kazi hivyo kuwa mzigo kwa Taifa.

Taifa linahitaji mfumo maalum unaohusika na scouting, mfumo ambao unahusisha kamati ya wataalamu wa fani husika ambao wanafanya kazi ya kuandaa orodha ndefu ya wadau wenye sifa. Kazi ya Rais inakuwa ni kupitia orodha hiyo na kufanya uteuzi.
Hii itaondoa kuwa na wateule wenye sifa zinazotia shaka kimaadili na kiutendaji kama ilivyo sasa kwa teuzi nyingi za wakurugenzi wa mashirika ya umma,wakurugenzi halmashauri mbalimbali, wakuu wa Wilaya na mikoa.

Miaka mitano itakwisha Rais anafikiria kuteua na kutengua badala ya kufikiria kuboresha maisha ya Watanzania.
Nawasilisha.

Kuna mahala una Hoja ya Msingi ila sehemu nyingi ' umepotosha ' sana na umeweka mno hisia zako za ' Chuki ' kwa Rais Dr. Magufuli na Serikali yake hii ya awamu ya Tano. Jamani siku zingine tunapokua Kulaumu humu basi tuwe na ' Ushahidi ' na tuonyeshe kweli Sisi ni ' Great Thinkers ' kuliko kuja na taarifa za ' Vijwe Kahawa ' na ' Vijiwe Majungu '. Kwa Umri wangu namshukuru Mungu sana kwamba Uongozi wa Mwinyi niliukuta mwishoni mwishoni ila nina Kumbukumbu nao, Uongozi wa Mkapa na Kikwete nimeushuhudia na nakumbuka hata Wao pia walikuwa wakifanya ' teuzi ' hivi hivi hata wakiwa mwaka wa mwisho.

Kinachotakiwa hapa ni ' Ufanisi ' na siyo Kupinga ' Teuzi ' zake. Tujitahidi sana Kumkosoa Mheshimiwa Rais kwa mambo yenye ' Tija ' na siyo kuja na chuki zetu na majungu yetu dhidi yake. Mbona Kikwete alifanya hivi mlinyamaza? Halafu kinachonishangaza kuna mambo ya Kipuuzi sana yalifanyika katika Awamu zilizopita ila hamzisemi na wala hatukuwaona mkijitokeza ' Kukemea ' lakini hakuna jambo ambalo Mzee wa Watu Rais Magufuli atalifanya mtaliona la maana.

Ni kweli Rais Magufuli hawezi kuwa ' Perfect ' na Kumfurahisha kila Mtanzania ila kwa Utafiti wangu mdogo tu nimegundua ya kwamba yawezekana hana nyota ya Kupendwa kama aliyemtangulia ila bado ana nyota njema ya kutuletea Maendeleo Watanzania na bahati nzuri Kazi yake kwa miaka hii mitatu angalau inaonekana na Kitu cha Kipekee ambacho nina uhakika nacho GENTAMYCINE ni kwamba huenda siku ambayo Rais Magufuli ' atang'atuka ' Madarakani akawa ametutoa Watanzania katika 65% na akawa ametufikisha hadi 85% Kimaendeleo na tutakuja Kumkumbuka na pengine hata Kumlilia.

Naheshimu sana Mawazo yenu ya Kumkosoa kwani ndiyo afya yenyewe hiyo ya Kidemokrasia ila kuna muda Watanzania tunazidisha ' Chuki ' dhidi yake. Hebu tumpe ushirikiano, tumshauri pale inapobidi ila na Sisi pia huu muda wetu mwingi ambao tunautumia Kumponda na Kumchukia tuutumie katika Kufikiria miradi ya kufanya na kutumia fursa zilizopo ili basi kwa pamoja nguvu yake Yeye kama Rais wa nchi na Sisi Wananchi wake tuweze Kuipeleka Tanzania yetu katika Kilele cha Mafanikio na Maendeleo.

Mungu ibariki Afrika
Mungu ibariki Tanzania
Mungu ibariki JamiiForums
Mungu mbariki GENTAMYCINE
 
Wanabodi;
Nianze kwa kukumbushia msimamo wa Rais wa JMT kuwa katiba mpya si kipaumbele chake. Lakini kwa namna mambo yanavyokwenda bado inambidi aikubali katiba pendekezwa ya Warioba.

Imekuwa ni kawaida sasa kusikia Rais kafanya uteuzi Fulani.Yaani toka ameingia madarakani ni miaka mitatu lakini bado hajamaliza kuunda serikali.

Miaka mitano itakwisha Rais anafikiria kuteua na kutengua badala ya kufikiria kuboresha maisha ya Watanzania.
Nawasilisha.
Kuna kwa ukweli fulani umekasema hapa, kuna kitu na mimi niliwahi kusema hapa, karibu kifanane na hoja yako
Maamuzi ya Serikali ni Shaghala Baghala! No Coordination! We Need a System, Not a 1-Man Show - JamiiForums
Mnatambua kuwa baadhi ya Maamuzi ya Magufuli yanaligharimu Taifa kiuchumi? - JamiiForums

P.
 
Wanabodi;
Nianze kwa kukumbushia msimamo wa Rais wa JMT kuwa katiba mpya si kipaumbele chake. Lakini kwa namna mambo yanavyokwenda bado inambidi aikubali katiba pendekezwa ya Warioba.

Imekuwa ni kawaida sasa kusikia Rais kafanya uteuzi Fulani.Yaani toka ameingia madarakani ni miaka mitatu lakini bado hajamaliza kuunda serikali.

Hii inatokana na ubovu wa katiba tuliyonayo ambayo inampa mamlaka makubwa rais, mojawapo ikiwa ni hiyo ya kuhusika na teuzi zote za watendajia na viongozi wa serikali bila mipaka.

Hasara ya jambo hill ni Rais kuteua viongozi na watendaji wabovU hivyo kujikuta kila Siku anateua na kutumbua kwa sababu ikulu pekee haina uwezo wa kutambua sifa na tabia za kila RAIA anayefaa kuwa kiongozi au mtendaji ndani ya nchi kubwa kijiografia na idadi ya watu kama Tanzania

Katiba pendekezwa ya Warioba ilimwekea mipaka Rais ktk teuzi zake,ambapo ilipendekeza kuwepo kwa kamati zinazohusika na kuandaa orodha ya wenye sifa husika kisha kupitia orodha hiyo ndio Rais anateua.

Katiba ya Warioba ingemsaidia rais kuokoa pesa za walipa kodi kwani hawa wanaotenguliwa kwa kukosea scouting wanarigharimu Taifa pesa nyingi.

Tumechoka hii hali Leo unateua mkurugenzi Takukuru kesho umemtengua,kesho kutwa mkurugenzi halmashauri Fulani siku inayofuata umemtengua.

Hawa wote wanaotenguliwa hulazimika kulipwa kwa kuwa utenguzi wao huwa ni mabadiliko ya kawaida ya kiutendaji. Au hulazimika kubadilishiwa kazi hivyo kuwa mzigo kwa Taifa.

Taifa linahitaji mfumo maalum unaohusika na scouting, mfumo ambao unahusisha kamati ya wataalamu wa fani husika ambao wanafanya kazi ya kuandaa orodha ndefu ya wadau wenye sifa. Kazi ya Rais inakuwa ni kupitia orodha hiyo na kufanya uteuzi.
Hii itaondoa kuwa na wateule wenye sifa zinazotia shaka kimaadili na kiutendaji kama ilivyo sasa kwa teuzi nyingi za wakurugenzi wa mashirika ya umma,wakurugenzi halmashauri mbalimbali, wakuu wa Wilaya na mikoa.

Miaka mitano itakwisha Rais anafikiria kuteua na kutengua badala ya kufikiria kuboresha maisha ya Watanzania.
Nawasilisha.
sijui kama ataelewa japo ujumbe utamfikia keshasema yeye hapangiwi over
 
Huwa nadhn anapokutna na wenzake wanapokunywa kahawa ndo .... Wanadiscuss teuo hizi

Hili ni tatz kwa kwel

Sema stone hawez kukusikia
 
Back
Top Bottom