Rais kukaa Chato ni gharama kwa Taifa

singojr

JF-Expert Member
Oct 28, 2014
5,307
6,883
Toka Rais Magufuli ameingia madarakani amekuwa na desturi ya kurudi nyumbani kwao Chato kila kipindi cha likizo yake kinapowadia.

Ni jambo zuri sana, ukilinganisha na wale waliokuwa kila kukicha wanasafiri kwenda nje.

Lakini swali kubwa lipo hapa, Ikulu ipo Dodoma, wafanyakazi wote wa ofisi ya Rais kwa sasa wanamakazi Dodoma, je anapoenda Chato gharama za malazi, chakula na fedha ya kujikimu nani analipia?

Gharama za kusafirisha polisi, wanajeshi na wafanyakazi wote wanaoambatana nae kwenda Chato nani analipia?

Tunakazana sana kulipa kodi kizalendo basi matumizi ya kodi zetu nayo yawe ya kizalendo. La sivyo tutatafutana ubaya.
 
Huwezi kuwa perfect leader hata siku moja na ili ufikie viwango hivyo na useme ww ni kiongozi wa wanyonge lzm ujinyime sana la sivyo utajikuta unanyonga wanyonge kwa kulewa madaraka tu na ukafika pahala ambapo ww hujali gharama ila kinachokusukuma ni ile kusema mm ndio Rais bwana.
 
Kooo kukaa Chato tatizo sio mbona mnakua na mawazo finyu huwa anapanda ndeg au.si gari na huwez kulijua asa hap ghrama zikoo wap www MBN mnabalaa ww kama ww orodhesha gharam unazo zion sio unapost tu kam kupost
 
Kooo kukaa chato tatizo sio MBN mnakua na mawazo finyu huwa anapanda ndeg au.si gari na huwez kulijua asa hap ghrama zikoo wap www MBN mnabalaa ww kama ww orodhesha gharam unazo zion sio unapost tu kam kupost
Gharama za gari ni kubwa kuliko ndege
 
Kwa upande wa gharama sidhan Kama ni issue, Kama ni polisi hata chato wapo. Jamaa hajawahi kusafiri hivyo ameokoa billions. It's a minor issue guys

Minor issue unajua per diem wanazolipana. Nchi ni masikini lazima kila kinachopatikana kitumike kwa usahihi usipotumia vizuri hela ndogo hata kubwa itakuwa vivyo hivyo
 
Kwahiyo asiende likizo kwao kama mkataba wa kazi unavyotoa siku 30 za likizo kwa mwaka!?
Kama anatekeleza majukumu yake ya Urais hiyo haiwezi kuwa likizo kwa kuwa alichokifanya hata makamu wa Rais angeweza kukifanya, hapo amekwenda Chato kusalimia na wakati huo huo anatekeleza majukumu yake ili mambo yaendelee kama kawaida vinginevyo angemwachia makamu wa Rais na Waziri mkuu kama kweli ni likizo kwa mujibu wa kazi.
 
Kooo kukaa chato tatizo sio MBN mnakua na mawazo finyu huwa anapanda ndeg au.si gari na huwez kulijua asa hap ghrama zikoo wap www MBN mnabalaa ww kama ww orodhesha gharam unazo zion sio unapost tu kam kupost

Unajua malipo ya kukaa nje ya kituo cha kazi? Watu wote walioongozana nae wamejenga nyumba au kupanga Chato? Unadhani nani analipia gharama zao za malazi?
 
Back
Top Bottom