Rais kubadilisha mawazo sio unyonge na sio ushindi wa CHADEMA

Mtaka Haki

JF-Expert Member
Oct 1, 2010
492
149
Nimewaza kuwa ni muhimu na kwa haraka tukaweka bayana kuwa endapo rais Mh. Dr. Jakaya Kikwete ataamua kutokutia saini muswada wa katiba. Basi ijulikane sio unyonge bali ni busara, hekima na heshima kwake. Kwa upande wa CDM ni muhimu nao wakatae kulitumia hilo au watu watakaolitumia hilo kama ushindi. Haya mambo yaonekana kama madogo lakini yasipowekwa sawa yanazuia ufanisi huko mbele.

Chadema wakatae kupokea sifa katika hili na wao waseme kwa nguvu kuwa ni busara ya Rais na utashi wake. Naye rais ni muhimu akasisitiza kuwa ameheshimu mawazo chanya yaliyopelekwa kwake na kama baba ameamua kuwasikiliza watoto wote.

Hongera Mh Dr. Jakaya Kikwete kwa busara zako na usikivu wako. Hongereni viongozi wa CHADEMA.

Hongereni wananchi wa Tanzania kwa umoja na mshikamano wenu.
 
JK yu mtegoni... Ni kweli ni busara kama atabadili mawazo juu ya kilichoamuliwa na wabunge wa CCM, Lakini hivi kwa nini ya busara yaamuliwe kibusara baada ya pressure? Tukumbuke kuna sheria moja alishawahi kuisaini kwa mbwembwe kumbe alichomekewa mengine na akasaini. Kama kuna jambo amekubaliana na CDM halafu asaini bila jambo hilo kujadiliwa na kuwemo kwenye muswada huo, atakuwa amekaribisha vurugu kwa kutaka kuwafurahisha wana CCM wenzie
 
Nimesoma habari ya Ikulu leo na raisi mwenyewe hajiiti Dr hivyo tungeacha kumwita Dr wakati yeye hataki kujiita Dr!. Vilevile swala la katiba si la kisiasa ni la Tanzania nzima na kama unafikiria kisiasa kwenye swala la katiba basi umelewa siasa kwani maamuzi yatakayo fanywa hapa ni ya miaka mingi sana ijayo na miaka hiyo CCM na Chadema wanaweza wasiwepo.
 
photo+3-IMG_1745.jpg


Katiba ndio ubongo unaoongoza nchi, tifua bongo uone control ya mwili inavyoshindikana hadi mtu kupoteza maisha.
 
jk amekuwa msikivu nadhani hakubaliani na ubabe wa bi kiroboto wakati wa mchakato wa katiba bungeni
 
....Chadema wakatae kupokea sifa katika hili na wao waseme kwa nguvu kuwa ni busara ya Rais na utashi wake. Naye rais ni muhimu akasisitiza kuwa ameheshimu mawazo chanya yaliyopelekwa kwake na kama baba ameamua kuwasikiliza watoto wote.......

Binafsi ninakubaliana nawe. Kuna mambo ambayo CDM inatakiwa iwe inawaelimisha vema mashabiki wake na hili la wapi pa kushangilia na jinsi ya kushangilia ushindi ni mojawapo. Amasivyo watakuwa wanajiwekea magogo mbele ya safari ya usuhishi wa kidiplomasia katika mambo ya Kitaifa. Kutaka kujionyesha mwamba au mshindi ndiko kumepelekea baadhi ya nchi au vyama Tawala kugeuka Madikteta.
 
Nimewaza kuwa ni muhimu na kwa haraka tukaweka bayana kuwa endapo rais Mh. Dr. Jakaya Kikwete ataamua kutokutia saini muswada wa katiba. Basi ijulikane sio unyonge bali ni busara, hekima na heshima kwake. Kwa upande wa CDM ni muhimu nao wakatae kulitumia hilo au watu watakaolitumia hilo kama ushindi. Haya mambo yaonekana kama madogo lakini yasipowekwa sawa yanazuia ufanisi huko mbele.
Chadema wakatae kupokea sifa katika hili na wao waseme kwa nguvu kuwa ni busara ya Rais na utashi wake. Naye rais ni muhimu akasisitiza kuwa ameheshimu mawazo chanya yaliyopelekwa kwake na kama baba ameamua kuwasikiliza watoto wote.
Hongera Mh Dr. Jakaya Kikwete kwa busara zako na usikivu wako. Hongereni viongozi wa CHADEMA. Hongereni wananchi wa Tanzania kwa umoja na mshikamano wenu.

Mtaka haki, nakupongeza kwa busara za zilizomo kwenye ujumbe wako huo juu. Kama inawezekana, watumie wajumbe wa CDM kila mmoja ujumbe huu ausome. Ni ujumbe muhimu sana kwa mtu mwenye nia njema. Bahati mbaya sina contacts za wajumbe wa CDM. Huu ni ujumbe muhimu sana kwao kuufahamu na kuufuata kama wanataka kusonga mbele na nia yao nzuri.
 
Nimewaza kuwa ni muhimu na kwa haraka tukaweka bayana kuwa endapo rais Mh. Dr. Jakaya Kikwete ataamua kutokutia saini muswada wa katiba. Basi ijulikane sio unyonge bali ni busara, hekima na heshima kwake. Kwa upande wa CDM ni muhimu nao wakatae kulitumia hilo au watu watakaolitumia hilo kama ushindi. Haya mambo yaonekana kama madogo lakini yasipowekwa sawa yanazuia ufanisi huko mbele.
Chadema wakatae kupokea sifa katika hili na wao waseme kwa nguvu kuwa ni busara ya Rais na utashi wake. Naye rais ni muhimu akasisitiza kuwa ameheshimu mawazo chanya yaliyopelekwa kwake na kama baba ameamua kuwasikiliza watoto wote.
Hongera Mh Dr. Jakaya Kikwete kwa busara zako na usikivu wako. Hongereni viongozi wa CHADEMA. Hongereni wananchi wa Tanzania kwa umoja na mshikamano wenu.
Wewe kweli ni great thinker lakini umesahau kuwapa hongera CCM, CUF, na TLP pia kwa mchango wao kwa namna moja au nyingine kwa kazi yao inayolalamikiwa na CHADEMA.
 
Wewe kweli ni great thinker lakini umesahau kuwapa hongera CCM, CUF, na TLP pia kwa mchango wao kwa namna moja au nyingine kwa kazi yao inayolalamikiwa na CHADEMA.

Mchango wao ulikuwa kupongeza serikali, kupiga makofi na meza wakisikia vijembe bila hata kujua maudhui ya wanachopitisha!
 
[h=2]
icon1.png
Rais kubadilisha mawazo sio unyonge na sio ushindi wa chadema[/h]

ndio ajue alivyo na wabunge vilaza
 
Wana JF

Kuna tetesi kuwa Mh JK ameamua kwa dhati kutafakari upya mustakabali wa nchi yetu kwa kuamua kufikiria upya juu ya mswada wa kusaidia kuundwa kwa katiba mpya mimi nasema kama ni kweli basi Rais unahitaji pongezi kwa kuona mbali. Nasema hivyo kwa kuwa huu tayari ulikuwa ni ufa wa pili baada ya ule wa udini ambao atafanikiwa kuuziba nakupongeza sana kwa hili.

Pili nakupongeza pia kwa ahadi kuwa unadhamira ya kweli ya kuhakikisha kuwa nchi yetu inapata katiba mpya kwa mazingira yatakayopelekea Taifa letu kubakia kuwa wamoja kwa vizazi vijavyo hili ni jambo zuri Mh Rais.

Mimi nikushauri tuu kuwa usikubali matakwa ya watu wa chache ambao wao wanafikiri kuwa nchi hii wameumbiwa wao kuitawala hivyo kulazimisha michakato itakayotupeleka kubaya. Tutengeneze katiba yenye haki kwa wote bila kutazama maslai ya chama. Kwa msingi huo utakuwa umejijengea heshama kubwa kwa watanzania na tanzania itaendelea kuwa na amani.

Wasikudanganye hao kuwa kukiwa na katiba mpya CCM ikishindwa unaweza kushitakiwa mara utakapomaliza urais wako, mimi nitashangaa atakayekushitaki kama utakuwa umefanya jambo kubwa kama hili ambalo linastahili kufuta mazambi yako yote kwani wewe ni binadamu kama binadamu wengine.

MUNGU AKUBARIKI SANA MHE RAIS
 
Wana JF

Kuna tetesi kuwa Mh JK ameamua kwa dhati kutafakari upya mustakabali wa nchi yetu kwa kuamua kufikiria upya juu ya mswada wa kusaidia kuundwa kwa katiba mpya mimi nasema kama ni kweli basi Rais unahitaji pongezi kwa kuona mbali. Nasema hivyo kwa kuwa huu tayari ulikuwa ni ufa wa pili baada ya ule wa udini ambao atafanikiwa kuuziba nakupongeza sana kwa hili.

Pili nakupongeza pia kwa ahadi kuwa unadhamira ya kweli ya kuhakikisha kuwa nchi yetu inapata katiba mpya kwa mazingira yatakayopelekea Taifa letu kubakia kuwa wamoja kwa vizazi vijavyo hili ni jambo zuri Mh Rais.

Mimi nikushauri tuu kuwa usikubali matakwa ya watu wa chache ambao wao wanafikiri kuwa nchi hii wameumbiwa wao kuitawala hivyo kulazimisha michakato itakayotupeleka kubaya. Tutengeneze katiba yenye haki kwa wote bila kutazama maslai ya chama. Kwa msingi huo utakuwa umejijengea heshama kubwa kwa watanzania na tanzania itaendelea kuwa na amani.

Wasikudanganye hao kuwa kukiwa na katiba mpya CCM ikishindwa unaweza kushitakiwa mara utakapomaliza urais wako, mimi nitashangaa atakayekushitaki kama utakuwa umefanya jambo kubwa kama hili ambalo linastahili kufuta mazambi yako yote kwani wewe ni binadamu kama binadamu wengine.

MUNGU AKUBARIKI SANA MHE RAIS

Anaweza kufanya hivyo kwa kujua kuwa itakapoanza yeye atakuwa amemaliza muda wake.
 
Nimewaza kuwa ni muhimu na kwa haraka tukaweka bayana kuwa endapo rais Mh. Dr. Jakaya Kikwete ataamua kutokutia saini muswada wa katiba. Basi ijulikane sio unyonge bali ni busara, hekima na heshima kwake. Kwa upande wa CDM ni muhimu nao wakatae kulitumia hilo au watu watakaolitumia hilo kama ushindi. Haya mambo yaonekana kama madogo lakini yasipowekwa sawa yanazuia ufanisi huko mbele.
Chadema wakatae kupokea sifa katika hili na wao waseme kwa nguvu kuwa ni busara ya Rais na utashi wake. Naye rais ni muhimu akasisitiza kuwa ameheshimu mawazo chanya yaliyopelekwa kwake na kama baba ameamua kuwasikiliza watoto wote.
Hongera Mh Dr. Jakaya Kikwete kwa busara zako na usikivu wako. Hongereni viongozi wa CHADEMA. Hongereni wananchi wa Tanzania kwa umoja na mshikamano wenu.[/QUO

Red Naunga mkono na ni vema sana iwe hivyo

Blue CDM lazima wapewe hizo sifa, ni ukweli na ni haki yao. Nilazima tu watapata na tuwape. Labda isiwe kwa sura ya majigambo

Violet binafsi sioni umuhimu wa kusema kwa nguvu zao, yatosha kusema na kujua ukweli kuwa ni busara na utashi wa raisi kufanya hivyo.

Green ni wajibu wa raisi na wala siyo huruma. Ijulikane pia ni wajibu wa kila mmoja wetu anayeishi kwenye sayari hii kufuata na kuunga mawazo chanya na kupinga kwa namna zote yale yaliyo hasi kama muswada wa makinda (mtu moja humu alimwita bi kiroboto)

Mi nauliza kama raisi hata saini je mama Makinda ataunda tume kuchunguza madharau na udhalilishaji wa bunge? Au atatafakari na kurekebisha udikteta wake!
 
Back
Top Bottom