Rais Kikwete, Watanzania wana imani na wewe achana na hoja dhaifu za Chadema

asilimia kubwa wanaomchukia rais wa tanzania, ni vijana ambayo ni jobless tena wengi waliokimbia shule,wanafunzi wanaosomea siasa pamoja na vijana waliotekwa kimawazo na wanasiasa!na sio wakulima kama unavyodai!! Tena vijana wavivu wa dar es salaam ndio wanaongoza kumchukia rais wa jamuhuri ya muhungano wa tz.
Tatizo lako unashinda kwenye key bord hutembei huku saiti tuliko wenzako, wenzio tunaoshinda na hawa wakulima tunajua kinachoendelea. Ole wako uje na visuti vyako huku au uwe kwenye gari lenye namba za serikali jaribu kuongea nao au waulize kitu uone hasira zao. Juzi tulikuwa na gari la elimu kutembelea shule moja ya kata tukapotea njia tulipoulizia kwenye kundi la wakulima waliokuwa hapo njiani hatukuamini kama walikuwa ni watanzania wenzetu! walivurumisha mitusi ya nguvu na kutuambia tukamuulize kikwete anayetulipa mishahara. We wacha kabisa.
 
Wanabodi.

Watanzania bado wana imani kubwa na Rais Jakaya Kikwete, kuna baadhi ya watu ambao wanaishambulia serikali ya JK kuwa kuna ufajaji wa fedha za umma, ufajaji wa fedha za umma kwa vigogo wa serikali hayakuanza leo bali tangu serikali zilizopita.

Rais Kikwete amezipa meno na mamlaka za kisheria Takukuru na ofisi ya CAG kuwafungulia mashtaka moja kwa moja mahakamani, Rais ameweza kuvunja hata mtandao mkongwe wa viongozi kulindana na ndio maana hata wabunge sasa wanakamatwa kwa rushwa tofauti na huko nyuma.

Baada ya uchafu wa hesabu fedha za umma kubainika, kwa mara ya kwanza Kikwete kuunda kamati ya ukaguzi inayojumuisha wataalam wa ukaguzi wa hesabu, Takukuru, Polisi, Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP), Maofisa Upelezi, Usalama wa Taifa, kwa kutumia ripoti ya CAG wanaweza kubaini wizi, kiasi kilichoibiwa kwa njia gani na wahuisika wote.. Kuna normal auditing (ukaguzi wa hesabu wa kawida) na forensic auditing (ukaguzi wa hesabu unaobaini wizi na vielelezo vya kumshtaki mahakamani mhusika) kwa miaka yote Ofisi ya CAG imekuwa ikifanya ukaguzi wa normal auditing na kugundua uchafu na serikali kukaa kimya na wizi wa fedha umma ulikithiriri sana.

Utaratibu wa forensic auditing Wakurugenzi wengi katika halmashauri zetu wengi lazima wafikishwe mahakamani.

Rais Kikwete kwa muda wake takribani miaka sita ameweza kuvunja rekodi ya ujenzi wa barabara kakamilisha ujenzi wa barabara zenye urefu wa takriban kilomita 11,000 kwa kiwango cha lami, ikilinganishwa na kilomita takriban 6.000 tu zilizojengwa na serikali zilizomtangulia, za Mwl Julius Nyerere, Ali Hassan Mwinyi, Benjamin Mkapa.
JF Daima
Ritz, mimi nitakujibu kwa kunukuu haya aliyosema Jenerali Ulimwengu katika gazeti la Raia Mwema la tarehe 20/6/2012. Naoma uisome kwa makini halafu tuendelee na majadiliano.
Jenerali Ulimwengu said:
Wananchi si wajinga, si vipofu, lakini hata wajinga na vipofu leo wanatambua na leo wanaona. Chama-tawala kinayajua haya, na kiko tayari kutoka nje na kufanya mikutano mikubwa kama ule wa Jangwani majuzi, na kuyazungumzia haya? Au kitaendelea kutoa taarifa za utendaji kazi wa Serikali, ambalo bila shaka ni jambo jema lakini si jukumu la chama kwenda Jangwani kueleza.

Napenda sana kusikiliza takwimu za idadi ya kilometa zilizojengwa "kwa kiwango cha lami," lakini hizi naweza kuzipata katika mitandao nikitaka. Iwapo tunataka kujadili "viwango vya lami" ni bora tujadili "viwango vya lami" hivyo ni viwango vya lami inayobanduka, kuchimbika au kuumuka kama mabonge makubwa ya ugali mweusi baada ya miezi mitatu ya kukabidhiwa?

Viwangio gani vya lami, ile ya Barabara ya Kilwa au ile ya Mlandizi /Chalinze, yenye mawimbi yanayoyumbisha gari kiasi cha kutishia maisha? Huwa najiuliza, na naamini watu wengine pia hujiuliza, hivi inawezekana barabara kama hizi zikakabidhiwa kwa wakuu wa serikali nao wakazipokea, halafu asiwepo mtu aliyekwenda jela, aliyefukuzwa ukurugenzi, au kufutwa katika orodha ya makandarasi?


Waziri aistuhesabie kilometa za kukariri; ubongo wa waziri unatakiwa ufanye kazi nyingine, ngumu zaidi kuliko kukariri, nayo ni kuongoza sekta ya miundombinu kwa kutekeleza sera za serikali yake zinazotokana na itikadi ya chama chake, iliyojengeka juu ya falsafa inayojulikana, kama nilivyosema hapo juu.

Iwapo ni falsafa ya Usawa wa Binadamu, waziri bila shaka atausumbua ubongo wake kujua iwapo miundombinu inayojengwa inawapa watu wote fursa sawa za usafiri na usafirishaji; kwamba mikoa yote itatendewa haki, wilaya zote zitaangaliwa kwa usawa; kwamba maeneo ya watu wa kipato cha chini hayatatelekezwa; kwamba watemnbea kwa miguu na wapanda baisikeli nao ni raia wenye haki ya kutumia barabara kwa usalama wa maisha yao, na kadhalika.

Kisha, waziri asituambie kwamba idadi ya kilometa za barabara alizojenga zingejengwa Burundi nchi hiyo isingebakiwa na eneo la kulima. Ndiyo maana yeye si waziri wa Burundi, ni waziri wa Tanzania, na napaswa kuiangalia Tanzania. Na wala hakuna sababu ya kuwabeza wapinzani eti watatumia barabara hizo hizo kuandamana kutaka kuking'oa chama-tawala madarakani. Kumbe wangepita wapi?

Udhaifu ni udhaifu tu hata ukipakwa rangi. Kikwete ni Raisi dhaifu kuliko wote waliomtangulia na si ajabu kaipa Tanzania sifa ya pili ulimwenguni baada ya ile ya umasikini, Raisi dhaifu anayeongoza serikali legelege akitokea chama cha kipuuzi.
 
naomba niulize humu kuna watu huwa wanalipwa kuanzisha mada yoyote kwa ajili ya kutetea vitu ambavyo hata mtoto wa std seven anaona si haki??
 
Rais aliyeanzisha hoja ya udini ili kuingia ikulu, na bado ameshindwa kuwakemea na kwachukulia hatua wanaoendeleza ubaguzi alouasisi

Rais aliyelazimishwa kuvunja baraza la mawaziri kwa rekodi, kuteua kwa kuzingatia urafiki na huyu wa kwetu bila kujali uwezo wa mtu.

Rais aliyefanya utalii zaid ughaibuni kuliko wote na kurekodi matumizi mabaya ya fedha za maskini wa tanzania hii.

Rais aliyeweka rekodi ya kuombaomba zaidi ya wote waliomtangulia huko ughaibuni na misaada isioneshe impact yoyote kiuchumi.

Rais aliyeweka record ya kukusanya pesa,serikali haina fedha na haijulikani makusanyo yanaenda wapi

Rais aliyeweka record ya mfumko wa bei usio na kificho wala ulinganifu, hata wasio na elimu sasa wanafahamu maana ya mfumko wa bei

Rais aliyeshindwa kuchukua maamuzi magumu kiasi kwammba serikali yake imekuwa ya kishikaji na wazinzi, morogoro na sasa singida, hakuna anawajibika hatakama tuhuma zikowazi kwa waziri husika.

Rais pekee aliyeruhusu idadi kubwa ya wanyama kuondoka na warabu bila intelijensia yake kujua nani asulubiwe

NISAIDIEN KUOREDHESHA UDHAIFU .................... ORODHA NI NDEFU, imani ya watanzania itatoka wapi????

My God, mama weee!!!, ma weeeeee!!!!! hakika hata wale wanaomsifia ni mdomoni tu mioyo yao lazima iko mbali na JK
 
Wewe Ritz yaani nikiona posts zako najua tu ni kuiongelea vizuri CCM.

Hata kusoma sikusomi maana umeombwa uingie humu JF kufagilia maovu na kutetea. Duh unajitahidi kila kukicha kusafisha udhaifu mlionao.

Inasikitisha kuwa hata wana CCM wengi wanakushangaa why unafagilia hivi hata mida mingine ni kama unalia au unawish ungejua nani ni nani humu uwapige vibao etc

Unalipwa kiasi gani?
 
Tatizo kubwa la Watanzania ni kungoja kufanyiwa kila kitu. Kuna ngazi za kupita na njia za kufanya na matatizo yanaweza kutatuliwa kabla hayajafika kwa Rais, lakini sikusikitikii, bado tuna miaka mingi sana ya kujifunza (wengine wamejaaliwa kujifunza haraka na wengine wamejaaliwa kuchelewa kujifunza).

Chifu hizo ngazi unazozisema ndizo hazifanyi kazi ipaswavyo! Hao mabwana/mabibi shamba na maafisa kilimo wanaohusika katika ugawaji wa pembejeo, wenyewe ndiyo wezi wakubwa wa hizo pembejeo. Mkulima akienda kwa afisa kilimo wa wilaya ni kuzungushwa tu kwa kuwa afisa huyo na maafisa wa kilimo katika ngazi za chini yake, lao ni moja.
Sasa hapo mkulima unataka aende wapi?! Akijichukulia hatua, polisi wenye mabomu na maji ya kuwasha wanatumwa haraka sana "kuwadhibiti" bila kujiuliza kwa nini wakulima hao wameamuwa kufanya hivyo!!

Hiyo yote kutokana na bosi wako mkuu kuwa dhaifu - hasiye weza kuchukua maamuzi magumu ya kurudisha heshima na uwajibikaji katika ngazi zote za serikali.

Na huo ni mfano mmoja tu kutoka sekta ya kilimo - mambo kama hayo sasa yapo karibu katika kila sekta hapa Tanzania. Kila sehemu ni ubabaishaji na "upigaji" tu - watumishi wanawaza "kupiga" tu ili kujinufaisha matumbo yao - hakuna nidhamu kabisa katika ofisi za umma siku hizi. Sasa hapo unataka wananchi waende wapi kama kila sehemu ni uozo??

Suluhisho ondoa rais dhaifu, fumua mfumo wote wa serikali ulio dhaifu sana kwa sasa.
 
Wanabodi.

Watanzania bado wana imani kubwa na Rais Jakaya Kikwete, kuna baadhi ya watu ambao wanaishambulia serikali ya JK kuwa kuna ufajaji wa fedha za umma, ufajaji wa fedha za umma kwa vigogo wa serikali hayakuanza leo bali tangu serikali zilizopita.

Rais Kikwete amezipa meno na mamlaka za kisheria Takukuru na ofisi ya CAG kuwafungulia mashtaka moja kwa moja mahakamani, Rais ameweza kuvunja hata mtandao mkongwe wa viongozi kulindana na ndio maana hata wabunge sasa wanakamatwa kwa rushwa tofauti na huko nyuma.

Baada ya uchafu wa hesabu fedha za umma kubainika, kwa mara ya kwanza Kikwete kuunda kamati ya ukaguzi inayojumuisha wataalam wa ukaguzi wa hesabu, Takukuru, Polisi, Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP), Maofisa Upelezi, Usalama wa Taifa, kwa kutumia ripoti ya CAG wanaweza kubaini wizi, kiasi kilichoibiwa kwa njia gani na wahuisika wote.. Kuna normal auditing (ukaguzi wa hesabu wa kawida) na forensic auditing (ukaguzi wa hesabu unaobaini wizi na vielelezo vya kumshtaki mahakamani mhusika) kwa miaka yote Ofisi ya CAG imekuwa ikifanya ukaguzi wa normal auditing na kugundua uchafu na serikali kukaa kimya na wizi wa fedha umma ulikithiriri sana.

Utaratibu wa forensic auditing Wakurugenzi wengi katika halmashauri zetu wengi lazima wafikishwe mahakamani.

Rais Kikwete kwa muda wake takribani miaka sita ameweza kuvunja rekodi ya ujenzi wa barabara kakamilisha ujenzi wa barabara zenye urefu wa takriban kilomita 11,000 kwa kiwango cha lami, ikilinganishwa na kilomita takriban 6.000 tu zilizojengwa na serikali zilizomtangulia, za Mwl Julius Nyerere, Ali Hassan Mwinyi, Benjamin Mkapa.

JF Daima

Wana imani pia na Mwigulu,Komba,Malima na new entry Simbachawene
 
Mwenye data halisi atoe, JK na serikali yake wanasema wamejenga barabara zenye urefu wa km 11,000. Ninazozifahamu ni Minjingu Babati km 160 Babati Singida km 163, Manyoni Singida Kamalizia km 60 zilizobaki katika barabara ya Dodoma mpaka kanda ya ziwa, Ndundu Somanga km 60 alizoacha Ben bado hazijaisha, Handeni Mkata km 110, hazijakamilika, Babati Kondoa km 5 tu zina lami, Kondoa Dodoma imeanza kujengwa km 3 (kuna jumla ya km 290 za barabara hii), Dodoma Mtera Iringa km 320 zimekamilika km 35. Hizo nilizozitaja zina jumla ya km 1,163. Tuwekeeni mambo hadharani hizo barabara zenye urefu wa km 10,000 nyingine ni zipi? Au ndio zile za Tabora - Nzega, Tabora - Manyoni, Sengerema, Nyakanazi - Kibondo, Kigoma - Kasulu - Mpanda, Tunduma - Sumbawanga na kadhalika. Tuwekeeni data tupate km 11,000 as per magufuli data.

Hadi kufika mwaka 2015 barabara ya kutoka Nyakanazi-Uvinza- Mpanda- Sumbawanga hadi Tunduma itakuwa imekamilika kwa kiwango cha lami, huku barabara ya kutoka Mwandiga jimboni kwa Zitto Kabwe hadi Kidahwe-Nguruka-Urambo hadi Tabora itakuwaimishakamilika baada ya kukamilika ujenzi wa daraja la Mto Malagalasi ambalo lilizishinda serikali zilizotangulia kabla ya JK.

wapendwa Ritz na mwenzako zomba,

nyie ndio mnaosababisha wana-ccm tuonekane ni DHAIFU kwa hoja. mwenzako mundali kaweka mchanganuo wa kila barabara na kilometa zake, wewe unaweka majina ya barabara bila kuainisha ni kilometa ngapi zimejengwa hadi sasa. kama haitoshi unaweka na ndoto zako za kuwa zitakuwa zimekamilika kabla ya 2015.

hebu kuweni "wakubwa" jamani. ujingaujinga kama huu ndio umeiponza ccm hadi sasda inaonekana DHAIFU. tunataka ule umahiri wa siasa za ccm uonekane sasa. kama huwezi siasa kuwa msomaji tu, yatosha.

mbarikiwe sana wapendwa

Glory to God!
 
Ritz,

Kwa hayo hayo ndio Kikwete hapendeki. Ukitazama wengi wa wanaoleta chuki na kejeli utakuta wengi ni wale wale waliozibiwa mianya ya wizi kwa mara ya kwanza toka hii nchi ipate Uhuru katika kipindi hiki cha Kikwete.

Baada ya muda mfupi, Kikwete anaanza kushughulikia fedha zilizowekwa nje ya nchi na hawa wizi wa mali za umma. Ni kazi ngumu sana, lakini ipo njiani inakuja, tutaona chuki zikizidi. Ukitazama kijuu juu tu hata bila ya uchunguzi wa kina utakuta wote wenye chuki ni wale wale 83%. Hao ndio "wasomi" bila kuelimika, hao ndio walioifikisha nchi ilipofika na hao ndio wezi wakubwa.

Tunamtakia kila la heri Kikwete kwa hii kazi ngumu aifanyayo sasa, na matokeo tunayaona. Na hapo ndiyo eti "dhaifu".

Subiri uone majibu sifuri sasa hivi.

dakika za majeruhi hizi, hajanunua meli mpya alizoahidi kila alipoona kidimbwi cha maji wakati wa kampeni, hajajenga bandari, hajaifanya mwanza kuwa california, kigamboni kuwa kama sijui wapi aaagh hata nimeshasahau.
 
Kusema ukweli kabisa mimi simpendi kabisa Rais legelege,umeniudhi sana na kunipa hasira jioni hii kumtetea mtu kama huyu asiyejua kwanini nchi yetu ni masikini
 
Wanabodi.

Watanzania bado wana imani kubwa na Rais Jakaya Kikwete, kuna baadhi ya watu ambao wanaishambulia serikali ya JK kuwa kuna ufajaji wa fedha za umma, ufajaji wa fedha za umma kwa vigogo wa serikali hayakuanza leo bali tangu serikali zilizopita.

Rais Kikwete amezipa meno na mamlaka za kisheria Takukuru na ofisi ya CAG kuwafungulia mashtaka moja kwa moja mahakamani, Rais ameweza kuvunja hata mtandao mkongwe wa viongozi kulindana na ndio maana hata wabunge sasa wanakamatwa kwa rushwa tofauti na huko nyuma.

Baada ya uchafu wa hesabu fedha za umma kubainika, kwa mara ya kwanza Kikwete kuunda kamati ya ukaguzi inayojumuisha wataalam wa ukaguzi wa hesabu, Takukuru, Polisi, Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP), Maofisa Upelezi, Usalama wa Taifa, kwa kutumia ripoti ya CAG wanaweza kubaini wizi, kiasi kilichoibiwa kwa njia gani na wahuisika wote.. Kuna normal auditing (ukaguzi wa hesabu wa kawida) na forensic auditing (ukaguzi wa hesabu unaobaini wizi na vielelezo vya kumshtaki mahakamani mhusika) kwa miaka yote Ofisi ya CAG imekuwa ikifanya ukaguzi wa normal auditing na kugundua uchafu na serikali kukaa kimya na wizi wa fedha umma ulikithiriri sana.

Utaratibu wa forensic auditing Wakurugenzi wengi katika halmashauri zetu wengi lazima wafikishwe mahakamani.

Rais Kikwete kwa muda wake takribani miaka sita ameweza kuvunja rekodi ya ujenzi wa barabara kakamilisha ujenzi wa barabara zenye urefu wa takriban kilomita 11,000 kwa kiwango cha lami, ikilinganishwa na kilomita takriban 6.000 tu zilizojengwa na serikali zilizomtangulia, za Mwl Julius Nyerere, Ali Hassan Mwinyi, Benjamin Mkapa.

JF Daima
Ni vizuri sana uzidi kumfariji ili asishtuke kwamba hali ya chama chake ni mbaya, maana akishtuka tu atachukua hatua za haraka za kurejesha imani ya watanzania kwa chama kitu ambacho kitafanya mabadiliko ya kisiasa yasitokee mwaka 2015
 
JK ni dhaifu sanaaaaaa kwasababu

a. Anajipendekeza kwa watu ambao hata akijipendekeza vipi hawampendi..83/17 kawajaza tele kwenye teuzi zake; wacha wamkomoe

b. Anapeleka pesa za umma kwenye hospitali za kanisa bado wanagoma wacha wamkomoe maana ni kilaza..wa kujipendekeza

c. Ameondoa issue ya mahakama ya kwa shinikizo la maaskofu..na haishi kujipendekeza kwao wacha wamkomoa....

Mwisho wa kujipendekeza ndio hiyo kutukanwa hata mitoto midogo...
 
dakika za majeruhi hizi, hajanunua meli mpya alizoahidi kila alipoona kidimbwi cha maji wakati wa kampeni, hajajenga bandari, hajaifanya mwanza kuwa california, kigamboni kuwa kama sijui wapi aaagh hata nimeshasahau.

Bajeti "0" ndiyo italeta yote hayo?
 
hakuna alipo jipendekeza, isipokuwa kilain aliingia mkenge kumsingizia mungu, mungu amejidhilisha kwamba hakuna wa kumsemea wala kumtabilia.

Aliyesema maisha bora kwa kila mtanzania ninani kama sio Jk sasa imekuwaje ametimiza au ndo kimeahalibika zaid?

Amerusu mahakama bali wakuisimamia bado wanajipanga, nakumbuka alitangaza live redion na kunako tvs

Anatukanwa na watoto kwa kushindwa kutetea, kutekeleza haki za watoto kwa kuwapatia maisha bora kupitia elimu na afya bora

Jamni udhaifu wa rais uko wazi mno........
 
Chifu hizo ngazi unazozisema ndizo hazifanyi kazi ipaswavyo! Hao mabwana/mabibi shamba na maafisa kilimo wanaohusika katika ugawaji wa pembejeo, wenyewe ndiyo wezi wakubwa wa hizo pembejeo. Mkulima akienda kwa afisa kilimo wa wilaya ni kuzungushwa tu kwa kuwa afisa huyo na maafisa wa kilimo katika ngazi za chini yake, lao ni moja.
Sasa hapo mkulima unataka aende wapi?! Akijichukulia hatua, polisi wenye mabomu na maji ya kuwasha wanatumwa haraka sana "kuwadhibiti" bila kujiuliza kwa nini wakulima hao wameamuwa kufanya hivyo!!

Hiyo yote kutokana na bosi wako mkuu kuwa dhaifu - hasiye weza kuchukua maamuzi magumu ya kurudisha heshima na uwajibikaji katika ngazi zote za serikali.

Na huo ni mfano mmoja tu kutoka sekta ya kilimo - mambo kama hayo sasa yapo karibu katika kila sekta hapa Tanzania. Kila sehemu ni ubabaishaji na "upigaji" tu - watumishi wanawaza "kupiga" tu ili kujinufaisha matumbo yao - hakuna nidhamu kabisa katika ofisi za umma siku hizi. Sasa hapo unataka wananchi waende wapi kama kila sehemu ni uozo??

Suluhisho ondoa rais dhaifu, fumua mfumo wote wa serikali ulio dhaifu sana kwa sasa.

Kama una ushahidi wa huo wizi, unangoja nini kuwashtaki? unangoja aje Rais kuwashtaki? Vituo vya Polisi hujui vilipo? amma kweli.
 
Wanabodi.



Rais Kikwete amezipa meno na mamlaka za kisheria Takukuru na ofisi ya CAG kuwafungulia mashtaka moja kwa moja mahakamani, Rais ameweza kuvunja hata mtandao mkongwe wa viongozi kulindana na ndio maana hata wabunge sasa wanakamatwa kwa rushwa tofauti na huko nyuma.

Baada ya uchafu wa hesabu fedha za umma kubainika, kwa mara ya kwanza Kikwete kuunda kamati ya ukaguzi inayojumuisha wataalam wa ukaguzi wa hesabu, Takukuru, Polisi, Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP), Maofisa Upelezi, Usalama wa Taifa, kwa kutumia ripoti ya CAG wanaweza kubaini wizi, kiasi kilichoibiwa kwa njia gani na wahuisika wote.. Kuna normal auditing (ukaguzi wa hesabu wa kawida) na forensic auditing (ukaguzi wa hesabu unaobaini wizi na vielelezo vya kumshtaki mahakamani mhusika) kwa miaka yote Ofisi ya CAG imekuwa ikifanya ukaguzi wa normal auditing na kugundua uchafu na serikali kukaa kimya na wizi wa fedha umma ulikithiriri sana.

Utaratibu wa forensic auditing Wakurugenzi wengi katika halmashauri zetu wengi lazima wafikishwe mahakamani.

Rais Kikwete kwa muda wake takribani miaka sita ameweza kuvunja rekodi ya ujenzi wa barabara kakamilisha ujenzi wa barabara zenye urefu wa takriban kilomita 11,000 kwa kiwango cha lami, ikilinganishwa na kilomita takriban 6.000 tu zilizojengwa na serikali zilizomtangulia, za Mwl Julius Nyerere, Ali Hassan Mwinyi, Benjamin Mkapa.

JF Daima





.................





....


.........................





...
Watanzania bado wana imani kubwa na Rais Jakaya Kikwete, kuna baadhi ya watu ambao wanaishambulia serikali ya JK kuwa kuna ufajaji wa fedha za umma, ufajaji wa fedha za umma kwa vigogo wa serikali hayakuanza leo bali tangu serikali zilizopita.


Umesahau rekodi ya kuwapa UDC mahawara zake!!

Kororoka usiku kwenda mahotelini kulala na mahawara zake!!

Kuchekacheka misibani!!

Mfumuko wa bei!!

DHAIFU!!
 
Wanabodi.

Watanzania bado wana imani kubwa na Rais Jakaya Kikwete, kuna baadhi ya watu ambao wanaishambulia serikali ya JK kuwa kuna ufajaji wa fedha za umma, ufajaji wa fedha za umma kwa vigogo wa serikali hayakuanza leo bali tangu serikali zilizopita.

Rais Kikwete amezipa meno na mamlaka za kisheria Takukuru na ofisi ya CAG kuwafungulia mashtaka moja kwa moja mahakamani, Rais ameweza kuvunja hata mtandao mkongwe wa viongozi kulindana na ndio maana hata wabunge sasa wanakamatwa kwa rushwa tofauti na huko nyuma.

Baada ya uchafu wa hesabu fedha za umma kubainika, kwa mara ya kwanza Kikwete kuunda kamati ya ukaguzi inayojumuisha wataalam wa ukaguzi wa hesabu, Takukuru, Polisi, Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP), Maofisa Upelezi, Usalama wa Taifa, kwa kutumia ripoti ya CAG wanaweza kubaini wizi, kiasi kilichoibiwa kwa njia gani na wahuisika wote.. Kuna normal auditing (ukaguzi wa hesabu wa kawida) na forensic auditing (ukaguzi wa hesabu unaobaini wizi na vielelezo vya kumshtaki mahakamani mhusika) kwa miaka yote Ofisi ya CAG imekuwa ikifanya ukaguzi wa normal auditing na kugundua uchafu na serikali kukaa kimya na wizi wa fedha umma ulikithiriri sana.

Utaratibu wa forensic auditing Wakurugenzi wengi katika halmashauri zetu wengi lazima wafikishwe mahakamani.

Rais Kikwete kwa muda wake takribani miaka sita ameweza kuvunja rekodi ya ujenzi wa barabara kakamilisha ujenzi wa barabara zenye urefu wa takriban kilomita 11,000 kwa kiwango cha lami, ikilinganishwa na kilomita takriban 6.000 tu zilizojengwa na serikali zilizomtangulia, za Mwl Julius Nyerere, Ali Hassan Mwinyi, Benjamin Mkapa.

JF Daima

riz, umejenga hoja yako vizuri lakini umeonyesha udhaifu mkubwa kudhibitisah namna mifumo mifumo hii ilivyoweza kudhibiti ubadhilifu wa mali ya umma. tunachokiona ni kichekesho kwani kama kamati za bunge ndizo zinaofichua uozo na ubadhilifu wa mali za umma wakati tunao taasisi zenye mafunzo ya kutosha na ambazo zimepewa dhamana ya kushughulikia mambo hayo kama usalama wa taifa, PCCB, intelligensia(polisi) na nyininezo zinashindwa kuona na kuintervine kwa wakati hadi tuzisubiri kamati za bunge ujue kazi ipo.
Aidha kuhusu ujenzi wa kilometa za mabarabara ni kweli kuwa miradi hiyo imejengwa lakini tukumbuke kuwa iko chini ya idadi kulingana na ilani ya chama cha mapinduzi (2010- 2015) na wasiwasi ni mkubwa kutokana na deni la taifa kuongezeka kwa kasi ya kutisha ukilinganisha na miradi ya maendeleo ilitekelezwa kwa trilion takribani 16 alizokopa kipindi cha utawala wake.
nadhani tunatakiwa tujielekeze katika kuleta maendeleo ya watu na sio idadi ya kilommeta za lami na majumba ya kifahari yaliyojengwa na serikali. watu waone na washiriki katika kuleta maendeleo yao na si kuletewa kama inavyohubiriwa siku hizi.
 
Hadi kufika mwaka 2015 barabara ya kutoka Nyakanazi-Uvinza- Mpanda- Sumbawanga hadi Tunduma itakuwa imekamilika kwa kiwango cha lami, huku barabara ya kutoka Mwandiga jimboni kwa Zitto Kabwe hadi Kidahwe-Nguruka-Urambo hadi Tabora itakuwaimishakamilika baada ya kukamilika ujenzi wa daraja la Mto Malagalasi ambalo lilizishinda serikali zilizotangulia kabla ya JK.

Mundali ametoa takwimu kuonesha ni Km 1600 tu zimeishajengwa, wewe nawe toa takwimu kuonesha ni Km 11,000! sio hadithi za ikifika lini tutakuwa tumefanya nini? Hoja Dhaifu toka kwa mtu Dhaifu anaemtetea mwenyekiti dhaifu wa chama cha Kipuuzi!
 
JK ni dhaifu sanaaaaaa kwasababu

a. Anajipendekeza kwa watu ambao hata akijipendekeza vipi hawampendi..83/17 kawajaza tele kwenye teuzi zake; wacha wamkomoe

b. Anapeleka pesa za umma kwenye hospitali za kanisa bado wanagoma wacha wamkomoe maana ni kilaza..wa kujipendekeza

c. Ameondoa issue ya mahakama ya kwa shinikizo la maaskofu..na haishi kujipendekeza kwao wacha wamkomoa....

Mwisho wa kujipendekeza ndio hiyo kutukanwa hata mitoto midogo...

ANAJIPENDEKEZA? Kwa maana hiyo unakiri kwamba JJ Alisema ukweli, DHAIFU!
 
Back
Top Bottom