Rais Kikwete ruhusu mjadala wa Muungano kunusuru amani

Candid Scope

JF-Expert Member
Nov 8, 2010
11,886
6,883
kikwete.jpg


Tukio la amani kuvurugia huko kisiwani Zanzibar na kusababisha mali za watu pamoja na baadhi ya makanisa kuchomwa serikali haiwezi kukwepa lawama kutokana na dalili za wazi watu kutaka mjadala wa Katiba mpya uende sambamba na kujadili Muungano wetu. Hakuna wenye kuchukia Muungano, ila kero mbalimbali zilizofumbiwa macho miaka nenda rudi ndizo zinazofanya watu wafikie hatu ya kuona sasa inatosha, tunataka tujadili Muungano wetu.

Kauli ya Rais Kikwete kabla na alipotangaza kamati ya kuratibu mapendekezo ya marekebisho ya Katiba, alisema Suala la Muungano sisiguswe. Kauli hiyo inaweza kujenga maswali mengi na pengine kufikisha kwenye tukio la Zanzibar ukosekanaji wa amani kama ilivyotoke.

Ulimwengu wa leo utandawazi ndio unaofanya amani ipatikane, na pale wananchi wanaposhinikizwa kutogusa au kuongelea jambo linalowahusu hapo wanachukua njia nyingine ya kudai haki yao.

Busara kwa Rais wetu Kikwete kuruhusu Muungano ujadiliwe na wananchi katika mapendekezo ya mabadiliko ya katiba ya nchi, kwani kwa hali inavyoonekana sasa hivi jambo hilo halikwepeki kwa namna ye yote vinginevyo ni kukaribisha maafa zaidi ya yaliyotokea Zanzibar.
 
Candid ni kweli, kama hawa wanaodai kujadili Muungano kama mlango ungekuwa umefunguliwa wasingefikia hapa hadi kusababisha machafuko. Ndio maana kuwazuia wamefikia hatua ya kutaka kupiga kura ya kutokukubaliana na Muungano.
 
Candid ni kweli, kama hawa wanaodai kujadili Muungano kama mlango ungekuwa umefunguliwa wasingefikia hapa hadi kusababisha machafuko. Ndio maana kuwazuia wamefikia hatua ya kutaka kupiga kura ya kutokukubaliana na Muungano.

Binafsi naona njia mbadala ya kulinda amani ya nchi yetu ni uwazi katika kujadili mambo yanayotuhusu kwa uhuru. Lakini kutoruhusiwa baadhi ya kero za Muungano hapo moto hauwezi kuzimika, wanachofanya ni kutuliza kwa muda lakini utaibuka tu. Bora kuruhusu yaishe.
 
Binafsi naona njia mbadala ya kulinda amani ya nchi yetu ni uwazi katika kujadili mambo yanayotuhusu kwa uhuru. Lakini kutoruhusiwa baadhi ya kero za Muungano hapo moto hauwezi kuzimika, wanachofanya ni kutuliza kwa muda lakini utaibuka tu. Bora kuruhusu yaishe.

Huu Muungano nini faida kwetu? Huenda unatuongezea gharama za serikali tu.
 
kikwete.jpg


Tukio la amani kuvurugia huko kisiwani Zanzibar na kusababisha mali za watu pamoja na baadhi ya makanisa kuchomwa serikali haiwezi kukwepa lawama kutokana na dalili za wazi watu kutaka mjadala wa Katiba mpya uende sambamba na kujadili Muungano wetu. Hakuna wenye kuchukia Muungano, ila kero mbalimbali zilizofumbiwa macho miaka nenda rudi ndizo zinazofanya watu wafikie hatu ya kuona sasa inatosha, tunataka tujadili Muungano wetu.

Kauli ya Rais Kikwete kabla na alipotangaza kamati ya kuratibu mapendekezo ya marekebisho ya Katiba, alisema Suala la Muungano sisiguswe. Kauli hiyo inaweza kujenga maswali mengi na pengine kufikisha kwenye tukio la Zanzibar ukosekanaji wa amani kama ilivyotoke.

Ulimwengu wa leo utandawazi ndio unaofanya amani ipatikane, na pale wananchi wanaposhinikizwa kutogusa au kuongelea jambo linalowahusu hapo wanachukua njia nyingine ya kudai haki yao.

Busara kwa Rais wetu Kikwete kuruhusu Muungano ujadiliwe na wananchi katika mapendekezo ya mabadiliko ya katiba ya nchi, kwani kwa hali inavyoonekana sasa hivi jambo hilo halikwepeki kwa namna ye yote vinginevyo ni kukaribisha maafa zaidi ya yaliyotokea Zanzibar.


well said candid scope ....
 
Ni ufinyu wa mawazo wa viongozii wetu na ndio matunda ya yanayotokea zanzibar leo hii!shame On.....
 
Au uvunjwe kusiwe na chakujadili

Viongozi wachache hawataki muungano ujadiliwe kwenye katiba inayojadiliwa, wakati huohuo watu wa muungano huo wanataka ujadiliwe...sijui nani atashinda ...yetu masikio na macho ambayo wao hawana
 
Hatuhitaji tena kujadili Muungano; kura imeshapigwa na watawala wetu - Muungano haustahili kuwepo. Sasa ni wakati wa kufikiria tunagawana vipi tulichonacho!
 
Inaelekea bado hayati Mwl. Nyerere anaendesha hii nchi. Tangu alipowaripua baadhi ya wabunge waliotaka serikali tatu na kuhatarisha muungano, marais wetu wa TZ na ZnZ wanaogopa kabisa kuingilia hilo suala utafikiri watapata laana ya huyo mkuu marehemu. Huu uoga ndo unaleta maafa sasa.
 
Binafsi naona njia mbadala ya kulinda amani ya nchi yetu ni uwazi katika kujadili mambo yanayotuhusu kwa uhuru. Lakini kutoruhusiwa baadhi ya kero za Muungano hapo moto hauwezi kuzimika, wanachofanya ni kutuliza kwa muda lakini utaibuka tu. Bora kuruhusu yaishe.

Kiongozi mzuri ni yule anyetatua matatizo wakati wa uongozi wake si kuyaahirisha na kumuachia ajaye. Viongozi wengi wa CCM wana ile dhana ya kwamba 'MUUNGANO USINIFIE MIKONONI MWANGU', hii ndiyo dhana inayowatia woga na hofu, na huo siyo uongozi. waache watu wajadili kila kitu cha kuboresha, kuua, kuhuisha, ila mwisho wa siku unachukua mawazo ya kuboresha na kuhuisha unayaingiza kwenye katiba na kuwaambia wayapigie kura wakikataa maana yake wanaridhika na hali ya sasa.

CCM wanadhani wanaweza ku-dictate kwenye hili, wanatakiwa kujua kuwa Tanzania ya leo ina watu wengi sana waelewa.
 
Viongozi wachache hawataki muungano ujadiliwe kwenye katiba inayojadiliwa, wakati huohuo watu wa muungano huo wanataka ujadiliwe...sijui nani atashinda ...yetu masikio na macho ambayo wao hawana

Hawa viongozi tumeanya nao mkataba wa kutuongoza, wanapotumia nguvu ya dola kushinikiza haki zetu za msingi kujadini mambo muhimu kwa nchi yetu wananchi hawana njia nyingine ila kuunganisha nguvu zao na kudai haki yako kwa njia ambayo wanaona inawalazimisha watawala kulegeza mioyo yao.
 
kikwete.jpg


Tukio la amani kuvurugia huko kisiwani Zanzibar na kusababisha mali za watu pamoja na baadhi ya makanisa kuchomwa serikali haiwezi kukwepa lawama kutokana na dalili za wazi watu kutaka mjadala wa Katiba mpya uende sambamba na kujadili Muungano wetu. Hakuna wenye kuchukia Muungano, ila kero mbalimbali zilizofumbiwa macho miaka nenda rudi ndizo zinazofanya watu wafikie hatu ya kuona sasa inatosha, tunataka tujadili Muungano wetu.

Kauli ya Rais Kikwete kabla na alipotangaza kamati ya kuratibu mapendekezo ya marekebisho ya Katiba, alisema Suala la Muungano sisiguswe. Kauli hiyo inaweza kujenga maswali mengi na pengine kufikisha kwenye tukio la Zanzibar ukosekanaji wa amani kama ilivyotoke.

Ulimwengu wa leo utandawazi ndio unaofanya amani ipatikane, na pale wananchi wanaposhinikizwa kutogusa au kuongelea jambo linalowahusu hapo wanachukua njia nyingine ya kudai haki yao.

Busara kwa Rais wetu Kikwete kuruhusu Muungano ujadiliwe na wananchi katika mapendekezo ya mabadiliko ya katiba ya nchi, kwani kwa hali inavyoonekana sasa hivi jambo hilo halikwepeki kwa namna ye yote vinginevyo ni kukaribisha maafa zaidi ya yaliyotokea Zanzibar.
Off course intakuwa amesurrender kwa huu ugaidi?Na akifanya vibaya atakuwa amewapongeza na kuwazawadia thier wishes.
By the way kwa mwendo huu mazungumzo hayatazaa matunda mkwani wengine hawatasikiliza kitu zaidi ya kutaka taifa lao.Suala ya uhuru ,bado wapo huru kwani muungano ulikuwa wa ridhaa,otherwise wangeitwa mkoa.
 
Mambo yote yanakwenda kwa utaratibu ili kila mtu aepuke lawama mwisho wa siku ;kwa sasa kumeundwa tume ya kuriview katiba. Naomba tuiachie kazi na tuipe ushirikiano ili kutupati akatiba bora.n atuwaachie viongozi wetu wafanye kazi nyengine.hao wazanzibar wanahitaji maelekezo tu ya nini kazi ya tume wakioanisha na malalamiko yao
 
Mambo yote yanakwenda kwa utaratibu ili kila mtu aepuke lawama mwisho wa siku ;kwa sasa kumeundwa tume ya kuriview katiba. Naomba tuiachie kazi na tuipe ushirikiano ili kutupati akatiba bora.n atuwaachie viongozi wetu wafanye kazi nyengine.hao wazanzibar wanahitaji maelekezo tu ya nini kazi ya tume wakioanisha na malalamiko yao

Tume ya kuratibu mapendekezo ya katiba imebanwa kwa agizo lake Rais Kikwete kwamba suala la Muungano lisiguswe, liache lilivo, vinginevyo hawa ndugu zetu wa Zenj wasingefikia hapa kama uhuru wa kujadili ungekuwepo.
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom