sweetlady
JF-Expert Member
- Dec 24, 2010
- 16,947
- 8,409
Tumepata kuandika na leo tunaandika tena tukimsisitiza Rais Jakaya Kikwete na washauri wake kupunguza safari za nje ya nchi kikazi wakati taifa likiwa kwenye hali tete.
Licha ya misafara yake kulalamikiwa ndani na nje ya nchi kwa sababu ya kuongozana na msururu wa watendaji ambao wengine hawana umuhimu, safari hizo hazizingatii utulivu wa nchi.
Ni mara kadhaa wananchi wamewahi kuhoji majukumu ya rais na wasaidizi wake kwa sababu sio lazima kila safari nje ya nchi anatakiwa aende, ndiyo maana wapo wasaidizi wake katika ngazi mbalimbali ambao wanaweza kumwakilisha. Pamoja na ushauri tunaompa rais kupitia vyombo vya habari hususani magazeti, watendaji wake huibuka na kumjibia kwamba safari hizo zina tija hivyo lazima asafiri, wanasahau kwamba wasaidizi wanaweza kwenda ili rais abaki nchini kumaliza kero za waliomwajiri kupitia sanduku la kura.
Tunafahamu kwamba nyingi ya safari hizo ni kutembeza bakuli kuomba msaada ambao hana muda wa kufuatilia matumizi ya fedha hizo kwa sababu anakuwa nje ya nchi. Kwetu tutaendelea kulisema tukiamini ipo siku rais Kikwete ataona umuhimu wetu japo atakuwa amechelewa.
Wataalamu wanasema msafara wa watu 20 ambayo ni idadi ya kawaida kwa msafara wa rais Kikwete hasa anapokwenda nje ya nchi wastani wa matumizi kwa siku huweza kufikia dola 15'000 za maarekani ambazo ni zaidi ya sh milioni 20.
Sasa gharama hiyo ni kwa siku, wakati mwingine ziara zake huchukua hadi siku 10 au zaidi na idadi ya wasindikizaji huweza kuongezeka hadi kufikia 40; tutafakari ni kiasi gani taifa linapoteza fedha nyingi pasi na sababu za lazima? Takwimu zinaonyesha mpaka sasa rais na wapambe wake wamesafiri zaidi ya mara 320 tangu aingie madarakani Desemba mwaka 2005 tukisema kila safari amekaa huko kwa siku tano, tunaona jinsi Taifa letu linavyotiwa umaskini na wachache wanaozunguka meza ya rais.
Tunaamini kwamba matatizo yanayotokea hivi sasa kama mauaji ya raia kule Songea, migogoro kwenye Bodi ya Pamba, mfumko wa bei unaosababisha kuyumba kwa uchumi wetu, migomo ya walimu wanaodai marupurupu, madaktari na mengine mengi angeweza kuyasimamia kwa karibu zaidi na kuyamaliza.
Alipata kunena aliyekuwa Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT) Hayati Daudi Balalli akiishauri serikali kuacha kuwa omba omba badala yake tutangulize uzalendo kwa kulinda maliasili.
Source: Tanzania Daima - Jumanne julai 17,2012
Licha ya misafara yake kulalamikiwa ndani na nje ya nchi kwa sababu ya kuongozana na msururu wa watendaji ambao wengine hawana umuhimu, safari hizo hazizingatii utulivu wa nchi.
Ni mara kadhaa wananchi wamewahi kuhoji majukumu ya rais na wasaidizi wake kwa sababu sio lazima kila safari nje ya nchi anatakiwa aende, ndiyo maana wapo wasaidizi wake katika ngazi mbalimbali ambao wanaweza kumwakilisha. Pamoja na ushauri tunaompa rais kupitia vyombo vya habari hususani magazeti, watendaji wake huibuka na kumjibia kwamba safari hizo zina tija hivyo lazima asafiri, wanasahau kwamba wasaidizi wanaweza kwenda ili rais abaki nchini kumaliza kero za waliomwajiri kupitia sanduku la kura.
Tunafahamu kwamba nyingi ya safari hizo ni kutembeza bakuli kuomba msaada ambao hana muda wa kufuatilia matumizi ya fedha hizo kwa sababu anakuwa nje ya nchi. Kwetu tutaendelea kulisema tukiamini ipo siku rais Kikwete ataona umuhimu wetu japo atakuwa amechelewa.
Wataalamu wanasema msafara wa watu 20 ambayo ni idadi ya kawaida kwa msafara wa rais Kikwete hasa anapokwenda nje ya nchi wastani wa matumizi kwa siku huweza kufikia dola 15'000 za maarekani ambazo ni zaidi ya sh milioni 20.
Sasa gharama hiyo ni kwa siku, wakati mwingine ziara zake huchukua hadi siku 10 au zaidi na idadi ya wasindikizaji huweza kuongezeka hadi kufikia 40; tutafakari ni kiasi gani taifa linapoteza fedha nyingi pasi na sababu za lazima? Takwimu zinaonyesha mpaka sasa rais na wapambe wake wamesafiri zaidi ya mara 320 tangu aingie madarakani Desemba mwaka 2005 tukisema kila safari amekaa huko kwa siku tano, tunaona jinsi Taifa letu linavyotiwa umaskini na wachache wanaozunguka meza ya rais.
Tunaamini kwamba matatizo yanayotokea hivi sasa kama mauaji ya raia kule Songea, migogoro kwenye Bodi ya Pamba, mfumko wa bei unaosababisha kuyumba kwa uchumi wetu, migomo ya walimu wanaodai marupurupu, madaktari na mengine mengi angeweza kuyasimamia kwa karibu zaidi na kuyamaliza.
Alipata kunena aliyekuwa Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT) Hayati Daudi Balalli akiishauri serikali kuacha kuwa omba omba badala yake tutangulize uzalendo kwa kulinda maliasili.
Source: Tanzania Daima - Jumanne julai 17,2012