Fred Katulanda
JF-Expert Member
- Apr 1, 2011
- 374
- 509
RAIS Jakaya Kikwete kesho ataanza ziara ya siku tatu mkoani Mwanza hii ikiwa ni ziara yake ya kwanza baada ya kumalizika kwa uchaguzi mkuu uliofanyika Oktoba mwaka 2010 na chama chake kupoteza majimbo ya Nyamagana na Ilemela.
Katika ziara hiyo mara baada ya kuwasili Rais Kikwete atahudhuria Ibada ya misa takatifu ya kuwekwa wakfu kwa Askofu Mteule Albert Randa wa kanisa la Mennonite Mwanza.
Rais Kikwete ambaye atawasili kwa njia ya ndege atapokelewa na viongozi mbalimbali ya wa mkoa wa Mwanza, ikiwa ni pamoja na wajumbe wa kamati ya ulinzi na usalama huku mwenyeki wake akiwa ni mkuu wa mkoa wa Mwanza Abbasi kandoro na Meya wa Jiji la Mwanza ambaye ni kutoka chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) Josephat Manyerere ndiye takaye mpokea kama mwenyeki wake.
Kwa mujibu wa ratiba yake iliyotolewa na ofisi ya mkuu wa mkoa wa Mwanza chini ya Abbas Kandoro, baada ya ibada hiyo ya kuwekwa wakfu kwa Askofu huyo atapumzika mpaka Jumatatu ambako atashiriki sherehe za uzinduzi wa ujenzi wa barabara ya Usagara- Geita ambayo imejengwa kwa kiwango cha lami.
Baada ya kumaliza uzinduzi huo Rais Kikwete atatembelea kukagua ujenzi wa chuo cha mafunzo ya Polisi Marine ambacho kinajengwa Nyegezi jijini Mwanza kwa uhisani wa serikali ya Marekani.
Serikali ya Marekani ilifadhili kiasi cha Dola za kimarekani 3 milioni baada ya kuliana saini mkataba wa kujenga chuo hicho kwa lengo la kusaidia kukomesha uhalifu ziwani Victoria.
Mkataba huo wa ujenzi wa chuo hicho ulisainiwa na Balozi wa Marekani nchini, Alfonso Lenhardt na Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi wakati huo, Lawrence Masha katika ofisi ya mkuu wa Mkoa wa Mwanza Februari 18 mwaka 2010.
Mbali na kufadhili ujenzi huo pia serikali ya Marekani ililizia kutoa msaada wa boti 10 zitakazokuwa zikifanya operesheni katika visiwa vilivyomo ndani ya Ziwa Victoria, msaada ambao utatekelezwa kwa kipindi cha miaka miwili kuanzia mwaka jana hadi mwaka huu.
Katika ziara hiyo mara baada ya kuwasili Rais Kikwete atahudhuria Ibada ya misa takatifu ya kuwekwa wakfu kwa Askofu Mteule Albert Randa wa kanisa la Mennonite Mwanza.
Rais Kikwete ambaye atawasili kwa njia ya ndege atapokelewa na viongozi mbalimbali ya wa mkoa wa Mwanza, ikiwa ni pamoja na wajumbe wa kamati ya ulinzi na usalama huku mwenyeki wake akiwa ni mkuu wa mkoa wa Mwanza Abbasi kandoro na Meya wa Jiji la Mwanza ambaye ni kutoka chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) Josephat Manyerere ndiye takaye mpokea kama mwenyeki wake.
Kwa mujibu wa ratiba yake iliyotolewa na ofisi ya mkuu wa mkoa wa Mwanza chini ya Abbas Kandoro, baada ya ibada hiyo ya kuwekwa wakfu kwa Askofu huyo atapumzika mpaka Jumatatu ambako atashiriki sherehe za uzinduzi wa ujenzi wa barabara ya Usagara- Geita ambayo imejengwa kwa kiwango cha lami.
Baada ya kumaliza uzinduzi huo Rais Kikwete atatembelea kukagua ujenzi wa chuo cha mafunzo ya Polisi Marine ambacho kinajengwa Nyegezi jijini Mwanza kwa uhisani wa serikali ya Marekani.
Serikali ya Marekani ilifadhili kiasi cha Dola za kimarekani 3 milioni baada ya kuliana saini mkataba wa kujenga chuo hicho kwa lengo la kusaidia kukomesha uhalifu ziwani Victoria.
Mkataba huo wa ujenzi wa chuo hicho ulisainiwa na Balozi wa Marekani nchini, Alfonso Lenhardt na Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi wakati huo, Lawrence Masha katika ofisi ya mkuu wa Mkoa wa Mwanza Februari 18 mwaka 2010.
Mbali na kufadhili ujenzi huo pia serikali ya Marekani ililizia kutoa msaada wa boti 10 zitakazokuwa zikifanya operesheni katika visiwa vilivyomo ndani ya Ziwa Victoria, msaada ambao utatekelezwa kwa kipindi cha miaka miwili kuanzia mwaka jana hadi mwaka huu.