Rais Kikwete na mazungumzo na ujumbe wa CHADEMA

Nimefurahi sana kuona hii movement.CCM na CDM vinaunganika pamoja kuitengeneza tanzania tuitakayo.
Mwanzoni hili waliliweza CUF na sasa naona CDM wameingia. Kwa mantiki hii upinzani Tanzania sasa basi.
Mara nyingi CDM wamekuwa hawazingatii nini wanataka na kwa njia gani mbadala, maana busara chache nguvu nyingi katika kukabili masuala nyeti. Sasa wametumia busara wanasikilizwa. Nadhani wataendelea kujifunza busara zaidi. PEACE!
 
Politics is the art of looking for trouble, finding it whether it exists or not, diagnosing it incorrectly , and applying the wrong remedy.

things always are valueless except we give them, in this particular thing i.e politics, you are confusing yourself.
 
Hawa viongozi wa CHADEMA wamenihuzunisha sana leo. Yaani wanapiga picha na Rais wasiyemtambua huku wanacheeeeeeka meno yote 32 nje. Hapo unategemea nini zaidi ya kushuhudia ndoa nyingine ya mke wa pili wa CCM mwaka 2015. Kweli siasa za Tz ni vichekesho tupu.
Anayeoa ndiye humfuata anayeolewa kwa maana hiyo Unamtusi Mkuu Wa Kaya maana ndiye aliyefuatwa hapo Ikulu.
 
Moll.1981.kamwe CDM hawawez kujiunga na C.C.M, wana akili sn hawa cdm wanataka kumzuia kikwete asisain muswada wa kijinga ule.funguka man
 
Wacheni kupotosha wananchi elezeni walicho ongea sio kutengeneza stori Chadema hawawezi kufunga safari kusifia katiba mbovu hiliyopo.
 
Hivi hiyo kurugenzi ya habari ya ikulu haiwezi kutoa habari bila spinning????
 
Nadhani tutafika pale tunapopataka sasa, JK awe msikivu sasa
Hiyo haiwezekani, tatizo sio JK kama yeye, bali akisema afanye haki na kusimamia katiba bora ni lazima itakula chama chake na washirika wake waliotuibia kwa miaka nenda rudi, sio kwamba ccm hawajui katiba ina matatizo wanajua, ndio mianya wanayotumia katika kulitafuna taifa.

Sasa leo hii kwa CHADEMA kwenda kuongea na JK hapo IKULU inaweza kumfanya abadilishe msimamo wake kusaini hiyo sheria ya kutengeneza katiba mpya?

Maana hiyo ndio msingi wa katiba yenyewe na hiyo sheria imeshapitishwa bungeni bado kusainiwa na raisi tu, kama chadema walishindwa kuwashawishi wabunge wa ccm wasipitishe hiyo sheria inayompa raisi mamlaka makubwa zidi ya utengenezaje wa katiba mpya wanaweza je kumshawishi mwenyekiti wa chama chao ambaye hana nguvu ndani ya chama chake hasisaini huo mswada wa sheria? na kama hoja ya CHADEMA sio mabadiliko kwenye huo mswada wa sheria basi wametuhuza na wanatafuta masilahi yao kama chama sio nchi kwa ujumla wake.

Ninacho ona mimi ni kwamba chadema wanashiriki kudanganya umma kwa makusudi au bila kujua maana kilichowapeleka IKULU wanajua fika hakiwezi kutekelezeka wangefanya hivyo kabla ya bunge kupitisha. Lakini pia wanapotosha au kupingana na kauli mbiu ya PEOPLE POWER, ni lini people power walinyoosha mikono na kwenda kunywa kahawa kwenye makasili ya watawala? Sio ongelea BODY LANGUAGE yao maana hapo napo wamechafua kabisa it was totally wrong.

Wanakwenda kumshawishi Kikwete kufanya nini? maana ninavyojua mimi ni kwamba kilichobaki ni kukusanya maoni ya wananchi kuhusu katiba mpya, ambapo hapo ndipo penye tatizo maana mchakato mzima umejaa wateule wa raisi na unaishia kwa raisi hivyo kutoa nafasi kubwa kwa uchakachuaji kufanyika, au wamekwenda kuomba kupewa nafasi kwenye hizo tume na kamati.

Kama wanataka nafasi kwenye hizo kamati wawe wazi sio kutudanganya kama watoto, haya maongezi haya tija tena yamepitwa na wakati na CCM kwa sasa wameshikiria mpini wakati CHADEMA wanafanya wrong move badala kwenye kwa wananchi wanakwenda MAGOGONI
nini wananchi tulichowafanya CHADEMA mpaka sasa hawana imani ana sisi tena?

Kukosekana kwa DR SLAA mtendaji mkuu wa chama kuna maswali mengi

je dr slaa akwenda IKULU kwa sababu aligomea kwenda kwenye kuapiswa kwa raisi ?

Je Dr Slaa hakubaliani na wanachofanya wenzake yaani kuomba kumuona raisi na kupewa mwaliko?

Je Dr Slaa bado ana amini nguvu ya umma yaani PEOPLE POWER na falisafa ya mahakama ya mwisho kuwa ya wananchi?
 
Kikwete hakurupuki, bado hujamjuwa tu?
Today i will sticky with you for a while, CHADEMA wamechagua kujidhalilisha, yote waliyokwisha sema kuhusu kikwete, wananchi kuwa mahakama ya mwisho na kutoka bungeni kaaa.

Leo hana hoja ya kusema wananchi ni mahakama ya mwisho wamekwenda kupiga magoti kwa KIKWETE, sidhani kama kikwete anaitaji support ya chadema kupitisha mswada huo ulishapita wasasa wanaongea naye nini? Kabla ya kutoka bungeni hawakujua kama kikwete ni raisi?
 
Mawazo yako kama yangu, kama katiba ni nzuri na imetuletea maendeleo kwa nini tupoteze muda na pesa kuibadilisha? Wajumbe wa cdm watueleze wazi kama ni kweli walikubaliana hivyo, kama si kweli tafadhali wakanushe mara moja kwa sababu huu ni upotoshaji wa hali ya juu. Kwa nini taarifa hiyo inazungumzia ubora wa katiba tu bila mapungufu yake, in actual fact, hivi kuna mtanzania sasa hivi ana interest ya kujua kama katiba ya sasa ni nzuri au la? Kuna umuhimu gani wa taarifa hiyo kutuambia kuwa wamekualiana kwamba katiba ya sasa ni nzuri. Kwa nini watanzania tunafanywa misukule? narudia tena, katiba ingekuwa nzuri kungkuwa na haja ya cdm kufanya mkutano na jk leo na kuendelea kesho????????? Chadema watch your step.

Watu makini huwa wakimaliza mashauriano wote wanakwenda mbele ya umma yaani waandishi wa habari kuwaeleza walichokubaliana ili kutokutoa mwanya wa spinning kama inavyofanywa sasa na kina Salva. Ni wajibu wa ujumbe wa CDM kutoka mbele ya umma na kukubali au kukataa huu ujumbe wa akina Salva. Kama kweli haya ndiyo yaliyowapeleka Ikulu ni ajabu sana, sitaki kuamini natumaini Tundu au Mnyika wataweka mambo sawa.
 
.....Aidha, pande zote mbili zimekubaliana kuwa mchakato huo uendeshwe kwa kuzingatia misingi ya mambo mengine muhimu kwa taifa la Tanzania kama vile kujiepusha na vitendo vya uvunjifu wa amani, kuligawa Taifa kwa misingi ya udini na ukabila ama kutugawa kwa misingi ya maeneo.

Imetolewa na:Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais,Ikulu,DAR ES SALAAM.27 Novemba, 2011

Amani ni kitu muhimu lakini hakipaswi kuwa sababu ya kuzuia mambo mhimu yasijadiliwe
 
Kikwete hakurupuki, bado hujamjuwa tu?
umesahau alivyokurupuka na falsafa ya kujivua gamba na ilivyomuumbua juzi dodoma!?

Umesahau watu waliposema anayoyaongea Nape ni yake JK alivyokurupuka na kusema Nape anachokisema ni msimamo wa chama na juzi akamkana dodoma!?

Kimsingi sio tu ni mkurupukaji bali hajui anachokifanya pia!
 
Jana wajumbe 8 wa CDM, walienda ikulu kuongea na rais juu ya sakata la katiba, wamweleze kwa niaba ya wananchi nini wananchi wanataka katika mbio za kupata katiba mpya.

Watu wengi wameponda picha zilizopigwa, na kusema ndo maandalizi ya kuwa na CCM C yaani CCM+CDM. Inaweza kuwa kweli hasa ukizingatia tabasam waliyokuwa nayo.

Mimi Bado nina imani na CDM kwa maana hii.



Wameenda Ikulu ili kuweka kumbukumbu sahihi. Iwapo Kikwwete atakubali mswaada urudi bungeni na kutoa maelekezo yatakayowapa nguvu wananchi namna gani ya kuunda katiba, nani wawe wajumbe na idadi gani nani awachague, basi mgogoro kati ya CCM. CDM, NCCR na makundi mbalimbali ya wanaharakati utakuwa umekwisha.

Lakini iwapo rais atawapokea, wapeane mikono kama walivyofanya, apewe mapendekezo kama walivyofanya CDM, halafu Rais, kwa utashi wake wa kisiasa, ayaweke kwenye masaburi yake, ayakalie mapendekezo yale, na aamue kusaini mswaada huo kanadamizi utakotumia hela nyingi kurudisha katiba iliyopo, basi CDM, NCCR na wanaharakati, watakapoanzisha nguvu ya umma kudai umma kuwa na nguvu kwa wanasiasa na makundi mengine watakuwa na kinga kwamba tulishauri hatukusikilizwa.

Hiki ndicho ninachokiona kwa hawa CDM na wanaharakati wengine waliotangaza maandamano nchi nzima, lakini mkwara wa baba ritz1 alipoongea na CCM DSM umewaogopesha, mpaka sasa hakuna aliyeandamana na hakuna aliyeafanya mdaharo tena.

Ni mawazo yangu, tujadili kwa hoja
.
 
Jana wajumbe 8 wa CDM, walienda ikulu kuongea na rais juu ya sakata la katiba, wamweleze kwa niaba ya wananchi nini wananchi wanataka katika mbio za kupata katiba mpya.

Watu wengi wameponda picha zilizopigwa, na kusema ndo maandalizi ya kuwa na CCM C yaani CCM+CDM. Inaweza kuwa kweli hasa ukizingatia tabasam waliyokuwa nayo.

Mimi Bado nina imani na CDM kwa maana hii.



Wameenda Ikulu ili kuweka kumbukumbu sahihi. Iwapo Kikwwete atakubali mswaada urudi bungeni na kutoa maelekezo yatakayowapa nguvu wananchi namna gani ya kuunda katiba, nani wawe wajumbe na idadi gani nani awachague, basi mgogoro kati ya CCM. CDM, NCCR na makundi mbalimbali ya wanaharakati utakuwa umekwisha.

Lakini iwapo rais atawapokea, wapeane mikono kama walivyofanya, apewe mapendekezo kama walivyofanya CDM, halafu Rais, kwa utashi wake wa kisiasa, ayaweke kwenye masaburi yake, ayakalie mapendekezo yale, na aamue kusaini mswaada huo kanadamizi utakotumia hela nyingi kurudisha katiba iliyopo, basi CDM, NCCR na wanaharakati, watakapoanzisha nguvu ya umma kudai umma kuwa na nguvu kwa wanasiasa na makundi mengine watakuwa na kinga kwamba tulishauri hatukusikilizwa.

Hiki ndicho ninachokiona kwa hawa CDM na wanaharakati wengine waliotangaza maandamano nchi nzima, lakini mkwara wa baba ritz1 alipoongea na CCM DSM umewaogopesha, mpaka sasa hakuna aliyeandamana na hakuna aliyeafanya mdaharo tena.

Ni mawazo yangu, tujadili kwa hoja
.

wakuu samahani, kwa uchungu nilionao, na ubantu wangu NCCR imesomeka NSSR, kama vipi modes warekebishe isomeke NCCR.
 
hapa hakuna ligi, nani mshindi au nani kaogopeshwa , tunachotaka ni mabadiliko

hata CDM wakilamba soksi na madiliko yakapatikana ni vizuri pia

naona upo kiubishi ubishi na mashindano zaidi
 
Back
Top Bottom