Rais Kikwete (mwenyekiti wa CCM Taifa), umepata pa kuanzia

VUTA-NKUVUTE

JF-Expert Member
Nov 25, 2010
6,135
17,802
Bado nakereketwa na matamshi aliyoyatoa Ndugu Edward Ngoyai Lowassa jana Dodoma. Aliitisha mkutano wa wanahabari na kuzungumza nao mambo mbalimbali. Mawili yanakugusa mwenyekiti wa CCM na rais wa Tanzania, Jakaya Mrisho Kikwete. Moja, Lowassa amedai kuwa amesingiziwa na kuzushiwa kuhusu kashfa ya Richmond. Ni wewe mwenyekiti Kikwete uliyeridhia Lowassa aachie uwaziri mkuu kwa kashfa hii.

Ukiwa kama mwenyekiti wa CCM na rais wa Tanzania, ulikuwa fully informed na kadhia nzima. Uliletewa taarifa za mdomo na nyaraka. Uliletewa ripoti na kuipitia ipasavyo. Ukaridhika nayo na kuridhia Lowassa ajiuzulu. Mwenyekiti Kikwete, naamini ulijiridhisha vya kutosha. Jana, Lowassa anadai alizushiwa na kusingiziwa. Mwenyekiti na Rais atatengwaje na uzushi huu? Yaani Rais aendeshwe na uzushi? Si tu kumchokoza mwenyekiti, bali pia ni dharau na kiburi kwa chama na serikali yake.

Pili, Lowassa ameponda sera ya Kilimo Kwanza. Si hulka ya CCM kupondana hadharani. Ni hulka ya kichama kupongezana kwa ubunifu na utekelezaji wa Ilani. Ndiyo ilivyo. Sera zote huzaliwa na Ilani. Kuponda sera ni kuponda Ilani. Iweje kada, ananyemelea urais na uenyekiti aiponde Ilani waziwazi na abaki salama kichama? Haiwezekani. Lowassa ameonesha dharau na kiburi cha wazi kwa Ilani ya 2010-2015. Si mfano mwema.

Mwenyekiti Kikwete, umepata pa kuanzia. Umeanza kuiona sasa sura halisi ya kauli za Lowassa. Ongoza vyema chama chetu katika haki na wema huk ukizingatia kauli jana za Lowassa pale Dodoma. Kila la kheri Mwenyekiti Kikwete na timu yako.

Mzee Tupatupa wa Lumumba (safarini kwenda Kanda ya Kati)
 
kama Lowasa hajahusika atuambie nani alihusika kwakuwa yeye ndiye alikuwa waziri mkuu kwahiyo bila kutuambia nani mhusika wa richmond basi Lowasa ndiyo anahusika.
 
Bado dakika chache tu kutajana, hapa hatutaelewa mtu kwani Lowasa kachelewa sana miaka nane mpaka tukaamini kuwa Hakika Lowasa amefisadi nchi kupitia Richmond.
 
Lowasa kwa nini alikuwa kimya muda wote watanzania hatuwezi kuamini atakachokiongea kuanzia sasa kuhusu richmond .
VOTE FOR UKAWA
 
Pili, Lowassa ameponda sera ya Kilimo Kwanza. Si hulka ya CCM kupondana hadharani. Ni hulka ya kichama kupongezana kwa ubunifu na utekelezaji wa Ilani. Ndiyo ilivyo. Sera zote huzaliwa na Ilani. Kuponda sera ni kuponda Ilani. Iweje kada, ananyemelea Urais na Uenyekiti aiponde Ilani waziwazi na abaki salama kichama? Haiwezekani. Lowassa ameonesh dharau na kiburi cha wazi kwa Ilani ya 2010-2015. Si mfano mwema
MUSSA ALLAN anasema kupingana hadharani kwa wanaCCM ni kawaida, kuna uhuru wa demokrasia.
Mkuu nadhani wewe ndio hujanielewa!

Demokrasia ndani ya CCM ni pana mno, ndio maana sio ajabu kuona mimi na mwenzangu Lizaboni hatuko pamoja, kwenye masuala fulani fulani, dhana ya kukubaliana kutokukubalina inafanya kazi vyema ndani ya CCM.
I mean, nyie huko CHAGADEMA mtabishania nini wakati mgombea ni mmoja tu, BABU?
 
Lowasa angekuwa amelenga kuwa wa msaada alipaswa kueleza pasipo shaka kwavipi yeye asihusike na kashifa hizo siyo kuongea maneno mepesi kama haya anayozungumza naona anatutia hasira tu.
 
Mzee Tupa Tupa siku zingine zari huwa linakuzidi lipi la Lowssa ambalo sio la KIkwete nyie wana CCM achene utapeli wananchi sasa hivi tumeamka hatuishi kwa propaganda zenu za kipuuzi, Lowassa Kikwete wote ni wale wale mafisadi tu
 
Hakika natumaini hawana wasi wasi juu ya uvunjifu wa kanuni
 
Lowasa kwa nini alikuwa kimya muda wote watanzania hatuwezi kuamini atakachokiongea kuanzia sasa kuhusu richmond .
VOTE FOR UKAWA
Hata kama akiongea na Watanzania wote hakuna Mtanzania atamuamini
 
By MUSSA ALLAN Mkuu nadhani wewe ndio hujanielewa!

Demokrasia ndani ya CCM ni pana mno, ndio maana sio ajabu kuona mimi na mwenzangu Lizaboni hatuko pamoja, kwenye masuala fulani fulani, dhana ya kukubaliana kutokukubalina inafanya kazi vyema ndani ya CCM.
I mean, nyie huko CHAGADEMA mtabishania nini wakati mgombea ni mmoja tu, BABU?
MUSSA ALLAN,

Yaani kufanya kazi za Buku 7 sasa unajiona ni CCM damu...! Sasa kama kweli kuna democracy huko mbona wote mnatumia ID za uongo!? Kweli Pesa mwana haramu!
 
Hadi leo ww Mzee tupa tupa, unajidai uko Lumumba, hujui sio MWENYEKITI WA CCM TU NDIO ANACHAGUA MGOMBEA URAIS...!!? INGEKUWA NI MWENYEKITI NDIO ANACHAGUA MGOMBEA URAIS, wala usingeona makelele, sbb angempoint tu, ila sbb CHAMA HAKIENDESHWI HIVYO...KUNA WANA CHAMA...HAO WANONGOZWA NA VIKAO MBALI MBALI, NDIO VIKAO HiVYO vitatoa mgombea urais...I mean wanachama ndio watamchagaua rais ajaye, ww post yako imeonyesha wazi as if JK ndio final authority ya kumchagua mgombea urais..hilo sio...

Na Mwenyekiti ni mwendesha vikao, na wanachama wakisema wanamtaka Lowassa hana Mwenyekiti jinsi... na ndipo JK anapokwama... sbb wanachama 90% ndani ya CCM NEC ukipiga kura wako na Lowassa...hapo Mwenyekiti anachanganyikiwa kabisa... akija kwa Marais wastafu, na mawaziri wakuu wastafu, wazee wa heshima CCM wako na Lowassa, UVCCM ni Lowassa, UWT ni Lowassa, sasa Mwenyekiti anapata marue rue, sbb anaona kama hana namna, yaani ni Mafuriko, ndipo ugumu haswa unapokuja...!!

Ingekuwa ni Mwenyekiti anachagua tu, aaah mbona mchezo ungeisha muda au ingekuwa nchi ya KIFALME BASI... mwenyekiti anaona yupo against all odds, yaani Lowassa anakubalika sana sana kupita maelezo...

Halafu ww mzee it seems hujui siasa kabisa, UNAJUA KILA MTU ANAANGALIA MBELE, kila mwanachama CCM anajua JK anaondoka zake hatakuwa na effect in the future kabisa, so WATU WALIOKUWA WANAMPENDA JK, WANAMGEUKIA LOWASSA, ssb wanajenga future yao CCM haiko kwa JK tena, bali na Lowassa, SO WENGII WAPENZI WA JK wako kwa Lowassa, sbb ni moja tu, kujitengenezea nafasi zao baada ya October, hili hujui..!!? JK aanondoka zake, kafanya yake, tumwache akapumzike, ni mwana CCM mwenzetu, ila watu wengiii washageukia kwa Lowassa now, sbb hawana future na JK, ndio siasa zilivyo...muda wako UKIISHA KATIKA UONGOZI HATA SIMU UKIMPIGIA MTU anakukatia, au hapokei, na anaweza asikupigie hata kukujulia hali, wakati labda ulimchagua ktk nafasi nyeti Ukiwa RAIS...ndio siasa, mnachekeana ukiwa na nafasi, na MKUU NYINGI NA KUKUSHIKA MIGUU...ngoja siku zako za mwisho zifike unaondoka, hata sms hupati...!!! muulize MKAPA, alisema haya...!!! hutamuona mtu anakuja kwako...ndio uhalisia...watu mafisi...!!!

Sasa upepo wa future ya CCM uko kwa Lowassa, na wanachama wako hivyo, wanaangalia future yao...!!! So Mwenyekiti
anavurugikiwa kabisa..sbb haoni wa wale watu kibaoo wakimsapoti.. hii ndio hali halisi..!!! Siasa ni game..play it well...!!!
 
Hata kama akiongea na Watanzania wote hakuna Mtanzania atamuamini

Jiandae kuwa mkimbizi, Edo ndio huyooo October...fanya fasta, sbb mmasai ni warrior by NATURE...not by training...Maasai are naturally warriors...Lowassa si mchezo...anza kujiandaa kwenda Burundi au cjui wapi..!! utajiju, mdomo ulikuponza..!!!
 
Bado nakereketwa na matamshi aliyoyatoa Ndugu Edward Ngoyai Lowassa jana Dodoma. Aliitisha mkutano wa wanahabari na kuzungumza nao mambo mbalimbali. Mawili yanakugusa mwenyekiti wa CCM na rais wa Tanzania, Jakaya Mrisho Kikwete. Moja, Lowassa amedai kuwa amesingiziwa na kuzushiwa kuhusu kashfa ya Richmond. Ni wewe mwenyekiti Kikwete uliyeridhia Lowassa aachie uwaziri mkuu kwa kashfa hii.

Ukiwa kama mwenyekiti wa CCM na rais wa Tanzania, ulikuwa fully informed na kadhia nzima. Uliletewa taarifa za mdomo na nyaraka. Uliletewa ripoti na kuipitia ipasavyo. Ukaridhika nayo na kuridhia Lowassa ajiuzulu. Mwenyekiti Kikwete, naamini ulijiridhisha vya kutosha. Jana, Lowassa anadai alizushiwa na kusingiziwa. Mwenyekiti na Rais atatengwaje na uzushi huu? Yaani Rais aendeshwe na uzushi? Si tu kumchokoza mwenyekiti, bali pia ni dharau na kiburi kwa chama na serikali yake.

Pili, Lowassa ameponda sera ya Kilimo Kwanza. Si hulka ya CCM kupondana hadharani. Ni hulka ya kichama kupongezana kwa ubunifu na utekelezaji wa Ilani. Ndiyo ilivyo. Sera zote huzaliwa na Ilani. Kuponda sera ni kuponda Ilani. Iweje kada, ananyemelea urais na uenyekiti aiponde Ilani waziwazi na abaki salama kichama? Haiwezekani. Lowassa ameonesha dharau na kiburi cha wazi kwa Ilani ya 2010-2015. Si mfano mwema.

Mwenyekiti Kikwete, umepata pa kuanzia. Umeanza kuiona sasa sura halisi ya kauli za Lowassa. Ongoza vyema chama chetu katika haki na wema huk ukizingatia kauli jana za Lowassa pale Dodoma. Kila la kheri Mwenyekiti Kikwete na timu yako.

Mzee Tupatupa wa Lumumba (safarini kwenda Kanda ya Kati)

sidhani kama ameponda sera ya kilimo kwanza ila tu ametoa mtazamo wake na kipaumbele chake, si lazima uunge kila kitu mkono hata kama sio priority kwako, nadhani ni haki ya kila mmoja kuamua vipaumbele vyake,katiba inaruhusu pia,

+
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom