sammosses
JF-Expert Member
- Jan 24, 2011
- 1,682
- 1,110
Ama kweli zimwi likujualo halikuli likakwisha.Ahadi kubwa kuliko zote alizowahi kuahidi JK(Baba Mwanaasha) ni serikali yake kuhakikisha ina nunua mitambo ya IPTL na kuahidi tatizo la umeme litakuwa ndoto, lakini mpaka leo hatuoni hatua za serikali ya chama cha mapinduzi kuhakikisha suala hili linashughulikiwa.
Tuna kila sababu kuhoji juu ya nchi yetu na ahadi tunazoahidiwa wakati wagombea nafasi mbalimbali wanapojinadi kuomba ridhaa ya wananchi.
Wengi tulijua ili kuwa changa la macho kufunika kombe mwanaharamu apite.Suala hili JK hawezi kulikwepa japokuwa mara nyingi amekuwa akilikanusha kuhusika na mkataba kandamizi wakati akiwa waziri wa nishati na madini kuhusiana na IPTL.
Hata kama lengo ni kufunika scandal ya IPTL na ameshindwa kuitekeleza basi atueleze watanzania amefikia wapi,kwani jinamizi hili litamtesa bila kutoa ufafanuzi wake kamwe hatutamwelewa,vinginevyo nawe upime uone.
Tuna kila sababu kuhoji juu ya nchi yetu na ahadi tunazoahidiwa wakati wagombea nafasi mbalimbali wanapojinadi kuomba ridhaa ya wananchi.
Wengi tulijua ili kuwa changa la macho kufunika kombe mwanaharamu apite.Suala hili JK hawezi kulikwepa japokuwa mara nyingi amekuwa akilikanusha kuhusika na mkataba kandamizi wakati akiwa waziri wa nishati na madini kuhusiana na IPTL.
Hata kama lengo ni kufunika scandal ya IPTL na ameshindwa kuitekeleza basi atueleze watanzania amefikia wapi,kwani jinamizi hili litamtesa bila kutoa ufafanuzi wake kamwe hatutamwelewa,vinginevyo nawe upime uone.