Rais kikwete bora uahidi vyumba vya madarasa kwanza kabla ya kompyuta

Magezi

JF-Expert Member
Oct 26, 2008
3,359
692
Hali halisi ya elimu ktk sehemu nyingi za nchi ni kama inavyoonekana ktk picha hii hapa chini. Nakumbuka Rais Kikwete alisema na kuahidi kwamba ktk miaka 5 ijayo kila mwanafunzi wa sekondari atakuwa na kompyuta yake. Je kama vyumba vya madarasa ni tatizo, hizo kompyuta zitawekwa chini au??? Tafakari
tarime.jpg
Wanafunzi wa shule ya sekondari Rebu katika wilaya ya Tarime mkoani Mara wakifanya mtihani wao wa kumaliza muhula chini ya miti kutokana na shule kukabiliwa na uhaba wa vyumba vya madarasa kama walivyokutwa mwishoni mwa wiki. (Picha na Shadrack Sagati - Habari Leo).
 
nakumbuka kipindi niko primary enzi za mzee ruksa awamu yake ya kwanza tulikua darasa la la kwanza na pili, tunaandika chini(ardhini) ili kusave madaftari na kalamu kwa madarasa ya kuanzia la tatu! tumetoka mbali!
 
kuku na yai kipi kilitangulia?maana anataka wawe na computer wakati 89%ya wanafunzi wanakaa sakafuni.vyumba havitoshi hata vyoo hakuna.why asiache usanii na kulaghai watu wakati huu wa kampeni
 
jana tar 15/09/10 akiwa katika mkutano wake wa kampeni huko tarakea rombo, mgombea urais wa ccm mhe jakaya kikwete alitoa ahadi kuwa serikali yake itahakiksha kuwa inafikisha teknolioia ya habari katika kila sekondari hapa nchini zikiwemo zile za kata, akirejea ahadi yake ya awali ya waalimu kutumia teknolojia hiyo kufundishia na kila mwanafunzi kuwa laptop yake mwenyewe.

Kwa kuwa najua na yeye anajua kuwa hadi sasa ni asilimia 10% tu ya watanzania wanafikiwa na nishati ya umeme ambayo ni ya lazima kwa teknolojia hii kufanya kazi. Ni wazi kuwa ahadi hii ni hewa, kwa hakuna uwezekano wa kutekelezwa kwake.

Najua akina tandale one, yaya, matejoo n.k watakuja hapa kudai kuwa seriklali itatumia umeme wa nguvu za jua yaani (solar) kufikisha teknolojia hiyo katika sekondari za kata. Lakini ni serikali hiyo hiyo ya ccm ambayo kwa miaka 20 imejaribu bila mafanikio yoyote ya kuridhisha kusambaza teknolojia ya umeme wa solar na friji za mafuta ya taa kwa ajili ya kuhifadhi chanjo katika zahanati na vituo vya afya visivyokuwa na nuishati ya umeme katika sehemu mbali mbali hapa nchini.

Kwa kuwa watanzania wengi hasa wa vijijini hawajawahi kumshuhudia kiongozi wa kitaifa kama vile rais akisema uongo hadharani wanaweza kumwamini na kumpatia kura zao.

Hii ni kwa sababu ya wananchi kunyimwa fursa huru ya kuuliza maswali kuhusu utekelezaji wa ahadi zilizopita n.k. Na uwezekano wa ahadi mpya kutekelezwa. Sababu ingine inayoweza kufanya wananchi kuingia mkenge ni ccm kukataa kushiriki midahalo ambapo wagombea wake wangehojiwa na wagombea wenzaop kuhusa ahadui wanozotoa.

Kwa hali hiyo ni vyema wagombea wa chadema na vyama vingine vya upinzania kuwaeleza wananchi kinagaubaga kuwa ahadi kama hiyo haiwezi kutekelezwa hata kwa miaka 20 ijayo.

Wapinzani watumie ushahidi wa kukosekana kwa umeme kuwafafanulia wananchi kuwa ahadi hizi hazitekelezeki hata kidogo.

Tunaomba pia mwenye data kuhusu waalimu kama alivyoahidi kikwete jana atumwagie humu kwa ajili ya kutumiwa na wagombea wa upinzania kupinga hoja za chama tawala, hiyo ndio demokrasia.
 
Jakaya na chama chake tulishasema ni wasanii; AHADI ZA 2005 KEDE KEDE HAWAJATIMIZA KAMA VILE KUIMALISHA SHIRIKA LA NDEGE LA ATCL na bado wanatoa ahadi hewa!! Hawaoni hata aibu waziri wa miundombinu kulidanganya Taifa kupitia bunge kuwa majadiliano na muwekezaji yalikuwayanakamilika huo ukiwa mwaka 2009 na mpaka leo wafanyakazi wanalipwa kutokana na kodi zetu bila kufanya kazi!! Hii ni dhahili kuwa kazi imewashinda achieni ngazi.
 
jana tar 15/09/10 akiwa katika mkutano wake wa kampeni huko tarakea rombo, mgombea urais wa ccm mhe jakaya kikwete alitoa ahadi kuwa serikali yake itahakiksha kuwa inafikisha teknolioia ya habari katika kila sekondari hapa nchini zikiwemo zile za kata, akirejea ahadi yake ya awali ya waalimu kutumia teknolojia hiyo kufundishia na kila mwanafunzi kuwa laptop yake mwenyewe.

Kwa kuwa najua na yeye anajua kuwa hadi sasa ni asilimia 10% tu ya watanzania wanafikiwa na nishati ya umeme ambayo ni ya lazima kwa teknolojia hii kufanya kazi. Ni wazi kuwa ahadi hii ni hewa, kwa hakuna uwezekano wa kutekelezwa kwake.

Najua akina tandale one, yaya, matejoo n.k watakuja hapa kudai kuwa seriklali itatumia umeme wa nguvu za jua yaani (solar) kufikisha teknolojia hiyo katika sekondari za kata. Lakini ni serikali hiyo hiyo ya ccm ambayo kwa miaka 20 imejaribu bila mafanikio yoyote ya kuridhisha kusambaza teknolojia ya umeme wa solar na friji za mafuta ya taa kwa ajili ya kuhifadhi chanjo katika zahanati na vituo vya afya visivyokuwa na nuishati ya umeme katika sehemu mbali mbali hapa nchini.

Kwa kuwa watanzania wengi hasa wa vijijini hawajawahi kumshuhudia kiongozi wa kitaifa kama vile rais akisema uongo hadharani wanaweza kumwamini na kumpatia kura zao.

Hii ni kwa sababu ya wananchi kunyimwa fursa huru ya kuuliza maswali kuhusu utekelezaji wa ahadi zilizopita n.k. Na uwezekano wa ahadi mpya kutekelezwa. Sababu ingine inayoweza kufanya wananchi kuingia mkenge ni ccm kukataa kushiriki midahalo ambapo wagombea wake wangehojiwa na wagombea wenzaop kuhusa ahadui wanozotoa.

Kwa hali hiyo ni vyema wagombea wa chadema na vyama vingine vya upinzania kuwaeleza wananchi kinagaubaga kuwa ahadi kama hiyo haiwezi kutekelezwa hata kwa miaka 20 ijayo.

Wapinzani watumie ushahidi wa kukosekana kwa umeme kuwafafanulia wananchi kuwa ahadi hizi hazitekelezeki hata kidogo.

Tunaomba pia mwenye data kuhusu waalimu kama alivyoahidi kikwete jana atumwagie humu kwa ajili ya kutumiwa na wagombea wa upinzania kupinga hoja za chama tawala, hiyo ndio demokrasia.

Magufuli amekata na kubandika. Watanzania tuwe makini na hizi ahadi zisizokuwa na kichwa wala miguu. Nafikiri Magufuli ni JK 2.0 (version 2)
 
Hali halisi ya elimu ktk sehemu nyingi za nchi ni kama inavyoonekana ktk picha hii hapa chini. Nakumbuka Rais Kikwete alisema na kuahidi kwamba ktk miaka 5 ijayo kila mwanafunzi wa sekondari atakuwa na kompyuta yake. Je kama vyumba vya madarasa ni tatizo, hizo kompyuta zitawekwa chini au??? Tafakari
View attachment 10945
Wanafunzi wa shule ya sekondari Rebu katika wilaya ya Tarime mkoani Mara wakifanya mtihani wao wa kumaliza muhula chini ya miti kutokana na shule kukabiliwa na uhaba wa vyumba vya madarasa kama walivyokutwa mwishoni mwa wiki. (Picha na Shadrack Sagati - Habari Leo).
Point.yule shetani FaixaFOXY WAPI? Bora hatete hii point kuliko kujikomba na Bakwata.
 
Back
Top Bottom