Mkuu unaweza kutufafanulia kuhusu huo upendeleo....nani amependelewa?
Swali zuri sana hilli Mkuu, naungana nawe, maana najua tayari watu wanaangalia majina.Sisi wana asili na jadi hatotulalaamika, tunajali zaidi huduma, ufanisi na umoja wa kitaifa, maana hata watu wetu wakijazaana katika posts kama hizo, kama hakuna ufanisi haina maana na hatutojisikia sifa kwamba watu wetu wamejaa kule bali tutaangalia zaidi huduma tutakayoipata hata ikitokaa upande upi ili mradi tu, kigezo cha kuchaguliwa ama kuteuliwa ni sifa na weledi wa mhusika na si dini! Nadhani imefikia wakati tusahau vigezo vinavyotutenganisha kama taifa, na tutoe nafasi kwa hao wanaofanya teuzi wazifanye bila kuogopa lawama za vigezo ambavyo si muhimu sana kwa nyakati hizi, after all hawaendi kutangaza dini bali kuhudumia watu kwa nafasi hizo.