BAK
JF-Expert Member
- Feb 11, 2007
- 124,790
- 288,005
Date::9/5/2008
Rais Kikwete asema siasa basi, sasa tuendeshe nchi kisayansi
Rais Jakaya Kikwete, ametoa tahadhari kuwa kuendesha mambo kisiasa hakuna tija ya kutosha isipokuwa kisayansi.
Na Peter Edson
RAIS Jakaya Kikwete, ameonya kwamba kama nchi ikiendelea kuzalisha wanasiasa kwa wingi itaishia kwenye malumbano na migogoro isiyo na tija, badala yake amewataka Watanzania kuijenga katika misingi ya sayansi na teknolojia.
Akizungumza kwenye mkutano wa sita wa Siku ya Wahandisi nchini uliofanyika jijini Dar es Salaam jana, Rais Kikwete alisema njia pekee ya kuiletea nchi maandeleo ni kuzingatia sayansi na teknoliji badala ya siasa ambayo huishia kwenye porojo na malumbano.
Alisema umefika wakati kwa kutumia wataalam hasa wanasayansi kufanisha utendaji badala ya wanasiasa katika mambo yanatakiwa watu waliobobea kwenye fani hizo.
Rais alisema takwimu zinaonyesha kuwa Tanzania ina wahandisi 8,000 ikimanisha kuwa kila mhandisi mmoja anashughulika na Watanzania 5000, jambo ambalo ni hatari kwa maendeleo ya taifa.
"Wasomi wanaeleza kuwa kama mtu anataka kujua maendeleo ya nchi, anaangalia idadi ya wahandisi na ubora wao, kama sisi tuna wahandisi wasiozidi 8,000 na nchi ina watu karibu milioni 39 hapo mambo yanakuwaje?alihoji Rais Kikwete.
Alisema nchi ya Japan kila mhandisi mmoja anawahudumia wananchi 54, wakati hapa Tanzania mambo uwiano unaonyesha kwamba mhandisi mmoja huwahudumia watu zaidi ya 8,000.
Kiwete alifahamisha kwamba katika kuhakikisha kuwa mabadiliko ya kisayansi yanatokea nchi, serikali imeandaa mpango wa elimu ya sekondari wenye nia ya kuingiza wanafunzi kwa wingi katika masomo ya sayansi ili kupata wataalamu wengi.
"Tukijaza wataalamu wa siasa tutaendele kubishana tu na tukiwajaza wanasheria tutaishia kufungana, kinachotakiwa sasa ni wataalamu wa sayansi na teknolojia, ili nchi yetu iweze kusonga mbele kimaendeleo," alisisitiza Rais.
Alisema wahandisi 500 wanaozalishwa na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam kwa mwaka haiwezi kukidhi mahitaji, hivyo kinachotakiwa kufanyika ni ongezeko la idadi, hadi kufikia wahitimu 1,000.
Rais alisema pamoja na kazi nzuri ya kufundisha wahandisi inayofanywa na UDSM, bado kuna changamoto nyingi za kuboresha fani hiyo, kama vile ubora wa ufundishaji unaoweza kukidhi mahitaji ya sokoni pamoja na upatikanaji wa vitendea kazi vyote muhimu.
Alisema kazi ya uhandisi inahitaji kujiendeleza kimasomo, hivyo aliwataka wahandisi na makandarasi nchini kutotosheka na kiwango cha elimu walicho nacho badala yake watafute nafasi za kujiendeleza kimasomo.
"Heshima ya uhandisi inategemea ubora wa kazi mnayofanya, acheni mambo ya ujanja ujanja," alisonya Rais Kikwete.
Rais Kikwete alitoa wito kwa bodi hiyo kuhakikisha kuwa wanafanya kazi kwa umoja ili kuondoa tofauti dhana iliyojengeka miongoni mwa watu wengi kwamba wazawa hawawezi kufanya vizuri isipokuwa wanaotoka nje ya nchi.
Alisema kama wahandisi na makandarasi wakifuata maadili ya kazi, shughuli nyingi zinazohusiana na fani hiyo zitafanyika kwa ubora unaotakiwa na kuipunguzia hasara taifa kutokana majengo kuporomoka.
Wakati akiyasema hayo, hivi karibuni Mkuu wa Mkoa, Abbas Kandoro na Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, waliunda tume kuchunguza chanzo cha kuporomoka kwa jengo la ghorofa 10, jijini Dar es Salaam Juni 21, mwaka huu ambayo ripoti yake haijatangazwa hadi leo
Si hivyo tu pia kuna tume iliundwa na aliyekuwa Waziri Mkuu, Edward Lowassa kuchunguza chanzo cha kuporomoka jengo la ghorofa tatu, eneo la Chang'ombe Village na nyingine zilizoundwa kuhakiki uhalali wa majengo ya ghorofa katika eneo la Kariakoo na kwingineko nchini, ambazo hazijatolewa ripoti.
Katika hatua nyingine, Rais Kikwete amewashutumu makandarasi wenye tabia ya kuwapa kazi wahandisi ambao hawajasajiliwa na Bodi ya Wakandarasi (ERB), kuwa ndiyo chanzo cha matatizo ya kuporomoka kwa majengo.
Alisema kuna haja ya ERB kuhakikisha kuwa inawapa usajili wahandisi wote nchini, ili kuhakikisha wanafuata misingi, kanuni na sheria katika kutekeleza majukumu yao ya kihandishi.
"Nawaagiza ninyi ERB kuhakikisha kuwa mnawasajili wahandisi wenye sifa zinazotakiwa kimataifa, ili wimbi hili la kuanguka kwa majengo liishe kabisa nchini,"alisisitiza Rais Kikwete.
Naye Mwenyekiti wa ERB, Profesa Ninatubu Lema, alisema ili sekta hiyo iweze kukua inahitaji kuwezeshwa na kupewa fursa mbalimbali zitakazoonyesha ubora wa kazi zao tofauti na sasa ambapo kazi nyingi za uhandisi zimekuwa zikifanywa na wakandarasi kutoka nje ya nchi.
"Ili tuweze kufanyakazi kwa ufanisi tunahitaji kuaminiwa na serikali yetu pamoja na wananchi kwa ujumla, kwa njia hii tutafanya kazi kwa uhuru," alisema Profesa Lema.
Profesa Lema alifahamisha kuwa madoa ndani ya fani hiyo inayosababisha na watu wasio waaminifu na kuahidi kuwa wataedelea kuboresha shughuli zao ili ziwe na viwango vinavyokubalika kimataifa.
Rais Kikwete asema siasa basi, sasa tuendeshe nchi kisayansi
Rais Jakaya Kikwete, ametoa tahadhari kuwa kuendesha mambo kisiasa hakuna tija ya kutosha isipokuwa kisayansi.
Na Peter Edson
RAIS Jakaya Kikwete, ameonya kwamba kama nchi ikiendelea kuzalisha wanasiasa kwa wingi itaishia kwenye malumbano na migogoro isiyo na tija, badala yake amewataka Watanzania kuijenga katika misingi ya sayansi na teknolojia.
Akizungumza kwenye mkutano wa sita wa Siku ya Wahandisi nchini uliofanyika jijini Dar es Salaam jana, Rais Kikwete alisema njia pekee ya kuiletea nchi maandeleo ni kuzingatia sayansi na teknoliji badala ya siasa ambayo huishia kwenye porojo na malumbano.
Alisema umefika wakati kwa kutumia wataalam hasa wanasayansi kufanisha utendaji badala ya wanasiasa katika mambo yanatakiwa watu waliobobea kwenye fani hizo.
Rais alisema takwimu zinaonyesha kuwa Tanzania ina wahandisi 8,000 ikimanisha kuwa kila mhandisi mmoja anashughulika na Watanzania 5000, jambo ambalo ni hatari kwa maendeleo ya taifa.
"Wasomi wanaeleza kuwa kama mtu anataka kujua maendeleo ya nchi, anaangalia idadi ya wahandisi na ubora wao, kama sisi tuna wahandisi wasiozidi 8,000 na nchi ina watu karibu milioni 39 hapo mambo yanakuwaje?alihoji Rais Kikwete.
Alisema nchi ya Japan kila mhandisi mmoja anawahudumia wananchi 54, wakati hapa Tanzania mambo uwiano unaonyesha kwamba mhandisi mmoja huwahudumia watu zaidi ya 8,000.
Kiwete alifahamisha kwamba katika kuhakikisha kuwa mabadiliko ya kisayansi yanatokea nchi, serikali imeandaa mpango wa elimu ya sekondari wenye nia ya kuingiza wanafunzi kwa wingi katika masomo ya sayansi ili kupata wataalamu wengi.
"Tukijaza wataalamu wa siasa tutaendele kubishana tu na tukiwajaza wanasheria tutaishia kufungana, kinachotakiwa sasa ni wataalamu wa sayansi na teknolojia, ili nchi yetu iweze kusonga mbele kimaendeleo," alisisitiza Rais.
Alisema wahandisi 500 wanaozalishwa na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam kwa mwaka haiwezi kukidhi mahitaji, hivyo kinachotakiwa kufanyika ni ongezeko la idadi, hadi kufikia wahitimu 1,000.
Rais alisema pamoja na kazi nzuri ya kufundisha wahandisi inayofanywa na UDSM, bado kuna changamoto nyingi za kuboresha fani hiyo, kama vile ubora wa ufundishaji unaoweza kukidhi mahitaji ya sokoni pamoja na upatikanaji wa vitendea kazi vyote muhimu.
Alisema kazi ya uhandisi inahitaji kujiendeleza kimasomo, hivyo aliwataka wahandisi na makandarasi nchini kutotosheka na kiwango cha elimu walicho nacho badala yake watafute nafasi za kujiendeleza kimasomo.
"Heshima ya uhandisi inategemea ubora wa kazi mnayofanya, acheni mambo ya ujanja ujanja," alisonya Rais Kikwete.
Rais Kikwete alitoa wito kwa bodi hiyo kuhakikisha kuwa wanafanya kazi kwa umoja ili kuondoa tofauti dhana iliyojengeka miongoni mwa watu wengi kwamba wazawa hawawezi kufanya vizuri isipokuwa wanaotoka nje ya nchi.
Alisema kama wahandisi na makandarasi wakifuata maadili ya kazi, shughuli nyingi zinazohusiana na fani hiyo zitafanyika kwa ubora unaotakiwa na kuipunguzia hasara taifa kutokana majengo kuporomoka.
Wakati akiyasema hayo, hivi karibuni Mkuu wa Mkoa, Abbas Kandoro na Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, waliunda tume kuchunguza chanzo cha kuporomoka kwa jengo la ghorofa 10, jijini Dar es Salaam Juni 21, mwaka huu ambayo ripoti yake haijatangazwa hadi leo
Si hivyo tu pia kuna tume iliundwa na aliyekuwa Waziri Mkuu, Edward Lowassa kuchunguza chanzo cha kuporomoka jengo la ghorofa tatu, eneo la Chang'ombe Village na nyingine zilizoundwa kuhakiki uhalali wa majengo ya ghorofa katika eneo la Kariakoo na kwingineko nchini, ambazo hazijatolewa ripoti.
Katika hatua nyingine, Rais Kikwete amewashutumu makandarasi wenye tabia ya kuwapa kazi wahandisi ambao hawajasajiliwa na Bodi ya Wakandarasi (ERB), kuwa ndiyo chanzo cha matatizo ya kuporomoka kwa majengo.
Alisema kuna haja ya ERB kuhakikisha kuwa inawapa usajili wahandisi wote nchini, ili kuhakikisha wanafuata misingi, kanuni na sheria katika kutekeleza majukumu yao ya kihandishi.
"Nawaagiza ninyi ERB kuhakikisha kuwa mnawasajili wahandisi wenye sifa zinazotakiwa kimataifa, ili wimbi hili la kuanguka kwa majengo liishe kabisa nchini,"alisisitiza Rais Kikwete.
Naye Mwenyekiti wa ERB, Profesa Ninatubu Lema, alisema ili sekta hiyo iweze kukua inahitaji kuwezeshwa na kupewa fursa mbalimbali zitakazoonyesha ubora wa kazi zao tofauti na sasa ambapo kazi nyingi za uhandisi zimekuwa zikifanywa na wakandarasi kutoka nje ya nchi.
"Ili tuweze kufanyakazi kwa ufanisi tunahitaji kuaminiwa na serikali yetu pamoja na wananchi kwa ujumla, kwa njia hii tutafanya kazi kwa uhuru," alisema Profesa Lema.
Profesa Lema alifahamisha kuwa madoa ndani ya fani hiyo inayosababisha na watu wasio waaminifu na kuahidi kuwa wataedelea kuboresha shughuli zao ili ziwe na viwango vinavyokubalika kimataifa.