Rais Kikwete anamhujumu waziri Magufuli?

Wakubwa,

Tuliangalie suala hili tofauti kidogo. Hakuna hujuma hapo. Hii ni mara ya kwanza kukamatwa kwa wavuvi Maharamia katika pwani na Tanzania. Kumuhusisha Rais katika suala hili ni kutokuelewa taratibu za ki-Mahakama zinavyofanya kazi. Katika utawala wa Kisheria kama ilivyo hapa kwetu Tanzania, suala likiwa Mahakamani haliingiliwi na yeyote isipokuwa Mahakama yenyewe.

Kwa Maana hiyo Rais hakuwa na mamlaka ya kulizungumza au kulichelewesha aua hata kulifuta mpaka pale Mahakama itakapokuwa imemaliza kazi yake. Jambo la msingi hapa kuepusha tatizo kama hili na mengine kama hayo siku za usoni ni kuangalia na kuzipa uwezo Mahakama zetu na ofisi ya DPP (Mkurugenzi wa Mashitaka) kuweza kusimamia kesi zake kwa haraka na kuweza kuzimaliza kwa wakati ha hapo tutakuwa tumeepuka kumtupia lawama yeyote na pia kuepuka kuwaweka Rais na Mawaziri wake kwenye mapambano ambayo ni ya kufikirika na kusadikika tu.

Hoja hapa ni uwezo wa Mahakama zetu kuendesha kesi kwa haraka na ufanisi ili kuweza kusimamia na kutoa haki katika jamii husika. Lakini si Mahakama pekee na jeshi la Polisi na Mwanasheria Mkuu na DPP wote wanahitaji kuwa na Raslimali watu na vifaa vya kuwawezesha kufanya kazi zao kwa wakati na kuweza kusimamia haki pale inapokuwa inastahili.

Unaweza usiione hujuma kwa macho ya kawaida lakini ikawepo vile vile unaweza kusingizia Mahakama na DPP kuchelewesha kesi kumbe ndipo hujuma inapoanzia mara ngapi DPP anakalia kesi zilizowazi kabisa kesi za EPA,BOT nk ni wangapi wamefikishwa mahakamani kwa hiyo hujuma si lazima rais mwenyewe aende kuzuia kitu inaweza kutekelezwa kwa mbinu mbalimbali halafu umeongelea zaidi hawa samaki wa juzi umeshindwa kuoanisha mtiririko mzima wa matukio toka Magufuli yuko wizara ya miundombinu
 
Nakubaliana na wewe lakini si kwa tiketi ya CCM.
As longer as atashika nchi kwa tiketi ya chama hiki mambo ya Longolongo yataendelea kama kawa.
Nakubali mkuu hapo umenena lkn kwa ticket ipi sasa?au ajiunge na CCJ maana vyama vingine ndo kuna longolongo sana
 
ninachoshangaa ni kwa nini Budget iliyotumika ilikuwa ni ile ya idara ndani ya wizara hiyo, kweli hapo aliachwa pekee. Lakini pia haiingii akilini kwa nini Mheshimiwa rais ampige vita waziri aliyemteua mwenyewe. Kama hamtaki asingemchagua toka day one, hana sababu ya kufanya hivyo leo. chunguzeni zaidi leteni hoja, hiyo hapo is not water tight.
 
ninachoshangaa ni kwa nini Budget iliyotumika ilikuwa ni ile ya idara ndani ya wizara hiyo, kweli hapo aliachwa pekee. Lakini pia haiingii akilini kwa nini Mheshimiwa rais ampige vita waziri aliyemteua mwenyewe. Kama hamtaki asingemchagua toka day one, hana sababu ya kufanya hivyo leo. chunguzeni zaidi leteni hoja, hiyo hapo is not water tight.

Jamaa alitaka asimpange kwenye baraza la mawaziri akaogopa makelele ya watanzania, akaamua ampe wizara isiyo na jina, matokeo yake kwa kuwa Magufuli ni Kichwa, sasa hivi wizara yake ndiyo kati ya wizara tatu bora kwenye serikali ya JK. Ukiondoa wizara hizi tatu.....nyingine zilizobaki ni upupu tu.

JK anatakiwa agundue kuwa wachapakazi kama magufuli hata uwape wizara ya vitumbua na kalmati, watavuma tu.

Lakini problem kwa watu kama magufuli na wenye msuli na damu ya kazi kama yeye ni hii hapa chini kwenye signature.......hapa chini hapa........
 
acheni porojo, kwani nani kati yenu aliepiga kura ya kumchagua magufuli kwenye uwaziri, mnge juaje utendaji wake kwenye hiyo wizara kama sio busara ya Rais kuunda wizara hiyo? kama suala la kutumia bajeti yake kuhudumia hao samaki kwani tatizo liko wapi, hakuna pesa iliyokuwa inazagagaa. Mema ya Waziri mnayatenganisha na Rais, bt Mabaya ya waziri lazima muunganishe na Rais?? jifunzeni kufikiri kabla ya kusema.Kikwete ni Tishio ukibisha rejea 2005 au subiri Octoba2010 then unikumbushe kama utakuwa na ujasiri wa kukumbuka kunikumbusha!!!!!!!!!!
 
acheni porojo, kwani nani kati yenu aliepiga kura ya kumchagua magufuli kwenye uwaziri, mnge juaje utendaji wake kwenye hiyo wizara kama sio busara ya Rais kuunda wizara hiyo? kama suala la kutumia bajeti yake kuhudumia hao samaki kwani tatizo liko wapi, hakuna pesa iliyokuwa inazagagaa. Mema ya Waziri mnayatenganisha na Rais, bt Mabaya ya waziri lazima muunganishe na Rais?? jifunzeni kufikiri kabla ya kusema.Kikwete ni Tishio ukibisha rejea 2005 au subiri Octoba2010 then unikumbushe kama utakuwa na ujasiri wa kukumbuka kunikumbusha!!!!!!!!!!

Kama mfu anayeongea akiwa kaburini. Inaonekana hujafufuka sawasawa, kwa sababu unajifufua mwenyewe, subiri ufufuliwe wewe.................ebo!!!
 
lakini wote mnafahamu kuwa mbinu za kikwete zote huwa zinashinda kwa nguvu na watu wanazijua kabla hata hajafika mbali sijui ana balaa gani au ni washauri? ebu ona akaanza zoezi la kuzungumza na wananchi kwa simu, watu wakasema sisi sio wajinga hizo simu hazikupatikana wala nini na kilwa swali alijibu utadhani ni katibu mkuu wa wizara husika. watu walivoona kamchezo hako, akaacha, akaona noma hii tena. na sasa anawatumia waandishi, shehe yahya, akina mrema. mbinu zooote anatumia na wale ambao anaona wana nguvu na community anawa frustrate akina baregu, kilaini n.k. sihangai kwa hilo la magufuli na ungekuwepo uwaziri wa kupumzika na kutokusema kitu angesha mchagua huko.
 
Luteni,

Kama huwezi kuiona inakuwaje unasema Rais anamhujumu Waziri Magufuli au ni kupiga porojo na mbwembwe?

Sun Tzu sijakuelewa nilichosema inawezekana kabisa Magufuli akawa anahujumiwa ila kwa macho ya kawaida unaweza usijue sasa kutokuona kwa macho si kwamba hakuna hujuma au unasemaje
 
Sun Tzu sijakuelewa nilichosema inawezekana kabisa Magufuli akawa anahujumiwa ila kwa macho ya kawaida unaweza usijue sasa kutokuona kwa macho si kwamba hakuna hujuma au unasemaje

Luteni,

Hoja ya msingi ni kwamba huyu Mheshimiwa anahujumiwa na Rais Kikwete, mimi nasema lahasha, tuboreshe na kukuza ufanisi na uwezo wa Mahakama, ofisi ya Mkurugenzi wa Mashitaka na uwezo wa kipolisi wa kuchunguza na kuhitimisha uchunguzi kwa haraka na kuzipeleka kwa Mkurugenzi wa Mashitaka na AG zikiwa zimekamilika na hapo ndiyo haki itakuwa imetendeka bila ya mtu kudhulumiwa au kuwekwa ndani pasipo ushahidi wa kutosha. Lakini tukikimbilia kusema kuwa Rais anamhujumu Magufuli wakati hatuna ushahidi na ukiulizwa unasema ushahidi unaweza kuwepo lakini hauonekani hapo unakuwa hujitendei haki katika fikra zako na hata sisi wengine tunaosoma unachokiandika kwani zinakuwa hazitofautiani sana na porojo.
 
Luteni,

Hoja ya msingi ni kwamba huyu Mheshimiwa anahujumiwa na Rais Kikwete, mimi nasema lahasha, tuboreshe na kukuza ufanisi na uwezo wa Mahakama, ofisi ya Mkurugenzi wa Mashitaka na uwezo wa kipolisi wa kuchunguza na kuhitimisha uchunguzi kwa haraka na kuzipeleka kwa Mkurugenzi wa Mashitaka na AG zikiwa zimekamilika na hapo ndiyo haki itakuwa imetendeka bila ya mtu kudhulumiwa au kuwekwa ndani pasipo ushahidi wa kutosha. Lakini tukikimbilia kusema kuwa Rais anamhujumu Magufuli wakati hatuna ushahidi na ukiulizwa unasema ushahidi unaweza kuwepo lakini hauonekani hapo unakuwa hujitendei haki katika fikra zako na hata sisi wengine tunaosoma unachokiandika kwani zinakuwa hazitofautiani sana na porojo.

Mfano DPP kuwa na faili kwa zaidi ya miaka miwili wakati ameshalifanyia kazi wewe bado unaona ni sawa wengine tunaona ni hujuma fulani
 
nakubaliana na wewe lakini si kwa tiketi ya ccm.
As longer as atashika nchi kwa tiketi ya chama hiki mambo ya longolongo yataendelea kama kawa.

mfano mzuri ni mh pinda, alivyochukuwa nafasi ya lowasa ilidhaniwa na watanzania kwamba nuru mpya imeangaza na kiama cha mafisadi kimewadia. Tatizo hatukuwazia kwamba bado yupo ndani ya ccm. System imembana vilivyo na sasa hivi amageuka kuwa mpambe wa kina rostam tena kwa gharama ya kulitukana benge kwa kuwaaminisha wananchi kwamba mijadala ya bungeni ni porojo.
 
mfano mzuri ni mh pinda, alivyochukuwa nafasi ya lowasa ilidhaniwa na watanzania kwamba nuru mpya imeangaza na kiama cha mafisadi kimewadia. Tatizo hatukuwazia kwamba bado yupo ndani ya ccm. System imembana vilivyo na sasa hivi amageuka kuwa mpambe wa kina rostam tena kwa gharama ya kulitukana benge kwa kuwaaminisha wananchi kwamba mijadala ya bungeni ni porojo.

umepotea mkuu!

unachosema ni kweli, Magufuli anajihujumu mwenyewe! akiwa CCM hadithi zitakuwa zina recycle zile zile. one simple test, if he cares for people aondoke CCM.
 
..kuna madai kwamba, Magufuli alilazimisha ujenzi wa barabara jimboni kwake kwa kutumia madaraka yake ya Uwaziri wa Ujenzi na Miundo mbinu.

..Magufuli tena akatumia ubabe na kukiuka ushauri wa wataalamu wake na kuvunja kituo cha mafuta kule Mwanza. Mahakama Kuu imetoa hukumu kwamba serikali ilipe fidia ya shilingi bilioni 15.

..Magufuli tena amehusika na kashfa ya viongozi kujiuzia nyumba za serikali kwa bei ya kutupa. katika kashfa hiyohiyo Magufuli anatuhumiwa kuwauzia ndugu na rafiki zake nyumba za serikali.

..KAMA KWELI MAGUFULI NI MSAFI NA ANA NIA NJEMA NA TAIFA HILI BASI ARUDISHE NYUMBA YA SERIKALI ALIYOJITWALIA.

..WATANZANIA TUNALILIA MAPESA NA MALI ZILIZOFICHWA NJE[SWISS,DUBAI] YA NCHI ZIWE-RECOVERED WAKATI TUNA MALI/NYUMBA ZETU HAPAHAPA NCHINI KWANINI ZISIREJESHWE?
 
umepotea mkuu!

Unachosema ni kweli, magufuli anajihujumu mwenyewe! Akiwa ccm hadithi zitakuwa zina recycle zile zile. One simple test, if he cares for people aondoke ccm.

ni kweli mkuu nilipotea kidogo nilikuwa nimetingwa na shughuli nyingi, ila kwa sasa niko jamvini kikamilifu. Heshima yako mkuu na wana jf wote.
 
..kuna madai kwamba, Magufuli alilazimisha ujenzi wa barabara jimboni kwake kwa kutumia madaraka yake ya Uwaziri wa Ujenzi na Miundo mbinu.

..Magufuli tena akatumia ubabe na kukiuka ushauri wa wataalamu wake na kuvunja kituo cha mafuta kule Mwanza. Mahakama Kuu imetoa hukumu kwamba serikali ilipe fidia ya shilingi bilioni 15.

..Magufuli tena amehusika na kashfa ya viongozi kujiuzia nyumba za serikali kwa bei ya kutupa. katika kashfa hiyohiyo Magufuli anatuhumiwa kuwauzia ndugu na rafiki zake nyumba za serikali.

..KAMA KWELI MAGUFULI NI MSAFI NA ANA NIA NJEMA NA TAIFA HILI BASI ARUDISHE NYUMBA YA SERIKALI ALIYOJITWALIA.

..WATANZANIA TUNALILIA MAPESA NA MALI ZILIZOFICHWA NJE[SWISS,DUBAI] YA NCHI ZIWE-RECOVERED WAKATI TUNA MALI/NYUMBA ZETU HAPAHAPA NCHINI KWANINI ZISIREJESHWE?
mwenda wazimu hutambulika kwa matendo yake, unachojaribu kupenyeza, hakiwezi kufanikiwa labda kwa maamuma
 
Sina hakika kwamba Rais Kikwete anaweza kumuonea wivu Waziri wake be it Magufuli au yeyote mwingine maana yeye mwenyewe ndiye mamlaka kuu ya uteuzi. Ni dhahiri kuwa kama anaona mtu fulani anamfunika kiaina bila shaka anaweza kumbadili pasipo kutoa sababu za kufanya hivyo. Ni kweli kwamba Waziri Magufuli amekuwa na mn'gao wa kutosha machoni mwa Watanzania wengi, nami nikiwa mmoja wao, kwa umakini, weledi, ujasiri wa kuyasimamia yale anayoamini ni sahihi na kujitoa muhanga. How I wish ifike siku moja tuwe na people like Magufuli 6 katika Serikali. Nadhani, mambo mengi yatanyooka. Big up Magufuli. 2015 inasogea, jipange mzee.!
 
3 Reactions
Reply
Back
Top Bottom