Rais Kikwete amwagiwa sifa toka Cameroon

Mtu wa Pwani

JF-Expert Member
Dec 26, 2006
4,184
671
Rais Kikwete amwagiwa sifa toka Cameroon

Mwandishi Wetu na Mashirika ya Habari

RAIS Jakaya Kikwete amemwagiwa sifa na kutajwa kuwa miongoni mwa viongozi wa daraja la kwanza duniani, ambaye ni mfano wa pekee katika Afrika, kutokana na utendaji wake unaoonyesha kujali watu wa tabaka zote bila ubaguzi.

Katika waraka wake uliochapishwa kwenye gazeti la The Post la Cameroon hivi karibuni, Mwanasheria wa kimataifa, Mwandishi na mwana-umajumui wa Afrika, (Pan-Africanist) Chief Charle Taku alisema Rais Kikwete alianza kuonyesha kitu cha pekee tangu alipoingia madarakani, kwa kuleta sura mpya baada ya kuamua kuteua wanawake kushika nafasi nyeti za uongozi ukiwemo uwaziri.

Alisema hatua hiyo iliyotoa nafasi kwa Tanzania kupata Naibu Katibu Mkuu wa kwanza mwanamke kwenye Umoja wa Mataifa.

Taku ambaye pia ni Kiongozi wa Baraza la mashauri la Mahakama ya Kimataifa ya Rwanda (ICTR) na Mahakama maalum ya Sierra Leone, pia kwenye Baraza la Mahakama ya Kimataifa ya Uhalifu wa Kivita (ICC) alisema Rais Kikwete ameonyesha njia na kuwafanya wanawake kupata upenyo kwenye siasa za kimataifa.

"Kikwete aneonekana kuwa hana mchezo katika kupambana na rushwa, umaskini na maradhi, tofauti na viongozi wengine wengi wa Afrika ambao wameshindwa kabisa kuyapa kipaumbele. Lakini pia ziara yake kwenye magereza, hospitali, kwenye masoko na maeneo mengine inaonyesha nia yake ya dhati katika kuwajenga wananchi wake kuwa watu wanaojitambua na kushiriki kikamilifu katika kujiletea maendeleo yao," alisema.


Aliongeza kuwa umaarufu wa Rais Kikwete unaonekana kukua kwa kasi duniani, hasa kutokana na namna alivyotumia nafasi yake kupitia hotuba yake ya Umoja wa Mataifa, akiyataka mataifa duniani kuhakikisha yanapambana na kumaliza vita, umaskini na maradhi, kwa kutoa wito wa kuanzishwa kwa mtizamo wa Jamiii mpya yenye amani ya kutosha duniani, ili kuchochea maendeleo na kudumisha heshima miongoni mwa wanajamii.

Taku alisema wa mara ya kwanza kiongozi huyo wa Afrika aliweza kuzungumza na kuleta mwamko mpya wa kifikra kwa Afrika na dunia akiwa na mtizamo mpya, huku matumaini mapya ya kujali utu, pia kuwasilisha ujumbe maalum wenye maana kubwa kusisitiza amani, matumaini na heshima kwa kila binadamu bila kujali rangi, dini wala asili ya watu.

"Huyu ni miongoni mwa viongozi wa awali katika Afrika, ambaye kwa asil yake, anaonekana kutokuwa na makuu na kuleta mtizamo mpya unaobadilisha mtizamo na kuleta tumaini jipya la viongozi wanaotakuwa kuwepo Afrika, baada ya kizazi cha viongozi wazee waliopo kumalizika, sula ambali ninaamini halina muda mrefu," alisema Chief Taku katika makala hiyo.

Alisistiza kuwa kutokana na mtizamo huo, Rais Kikwete anaonekana kufuata nyayo za baba wa Taifa, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere ambaye alikuwa ni kipenzi cha watu na mpenda amani, kiasi cha kuufanya hata mji wa Arusha kuwa kituo cha kimataifa, kwa kutoa nafasi kwa masuala mengi yahusuyo mikakati ya kidunia kufanyika hapo.

source mwananchi
 
"Kikwete aneonekana kuwa hana mchezo katika kupambana na rushwa, umaskini na maradhi, tofauti na viongozi wengine wengi wa Afrika ambao wameshindwa kabisa kuyapa kipaumbele. Lakini pia ziara yake kwenye magereza, hospitali, kwenye masoko na maeneo mengine inaonyesha nia yake ya dhati katika kuwajenga wananchi wake kuwa watu wanaojitambua na kushiriki kikamilifu katika kujiletea maendeleo yao," alisema.

Nimeipenda hii... Wapo wanaomjua zaidi yetu! I see...!
 
Si huyo tu, hata humu JF tunao ona kazi njema anazofanya, katika kipindi kifupi cha uongozi wake amefanya mengi mazuri ambayo kwa wenye chuki za kibinafsi hawayaoni.

Hata Mengi (Reginald) kamsifu sana jana (ITV Habari).

Mwenye macho haambiwi tazama mwenye masikio haambiwi sikia.
 
Ukiitazama shilingi upande wa mbele utafurahishwa na picha ya mwalimu,lakini igeuze nyuma basi,utakutana na mwenge ambao unachoma.Wacha wamsifie wao sisi ndio tunaofahamu upande huo wa pili.
 
Si huyo tu, hata humu JF tunao ona kazi njema anazofanya, katika kipindi kifupi cha uongozi wake amefanya mengi mazuri ambayo kwa wenye chuki za kibinafsi hawayaoni.

Hata Mengi (Reginald) kamsifu sana jana (ITV Habari).

Mwenye macho haambiwi tazama mwenye masikio haambiwi sikia.

Yaani we ushamuona Mengi ndiye mtu wa integrity kiasi cha kuwa yardstick siyo?

Huyo jamaa aliyeandika hiyo article kaweka vitu shallow kama kutembelea masoko na magereza yaani hata kupiga propaganda za upambe hajui, anaonekana kabisa anaandikia ushabiki.Yaani kaweka mambo ya cheap popularity, hamna economic data wala policy issues.Si ajabu anajikomba "aonwe" au kashaonwa tayari analipa fadhila.

Kikwete anavyotuchefua mijitu iliyomjua jana inajifanya kuleta upambe hapa?
 
Mh. Dar Es Salaam i like you men.
Let me ask you few questions. Can you name five good things ambazo JK amefanya hapo Tanzania ambazo zina effect direct kwa watanzania wa kawaida. Then can you name three ways ambazo JK amefanya kucrack corruption down in his cabinet? Then can you defend about his government overspending habit?

Then let get into juice part, since Tanzania are suffering for years because poor economic policy of his political party, what ways Hon.Jakaya Kikwete took to reduce: first, inflation rate which runs in double digit, second, reduction of Current Account defecit, third, goverment spending, fourth, independence from international aides? Please help me on those few things so i can be proud of Mr. President, other than that i dont care who said what.

Ukinisaidia hayo tuu, then i will come ask you other questions concern yeye kuweka his old bodies kwenye nyeti zote za uchumi, kuanzia centeral bank, mpaka kwenye Board of External Trade.
 
Yaani we ushamuona Mengi ndiye mtu wa integrity kiasi cha kuwa yardstick siyo?

Huyo jamaa aliyeandika hiyo article kaweka vitu shallow kama kutembelea masoko na magereza yaani hata kupiga propaganda za upambe hajui, anaonekana kabisa anaandikia ushabiki.Yaani kaweka mambo ya cheap popularity, hamna economic data wala policy issues.Si ajabu anajikomba "aonwe" au kashaonwa tayari analipa fadhila.

Kikwete anavyotuchefua mijitu iliyomjua jana inajifanya kuleta upambe hapa?

Wengine anawachafua wengine anatukosha huo ndio muono wa kila binadam lakini ukweli tuseme na waswahili hunena "mnyonge mnyongeni haki yake mpeni".

Jee hamuoni mema afanyayo JK? ni Rais gani katika awamu zilizopita kaibua mambo mazito ambayo yanaweka historia katika siasa za Tanzania?

Kwa uchache:

-Tunayaona ya BoT, hayana mjadala kazi inafanyika na chini ya uongozi wa nani?

-Tunayaona ya kina Lowassa, kazi inafanyika na chini ya uongozi wa nani?

-Tunayaona ya Buzwagi, kazi inafanyika na chini ya uongozi wa nani?

_ Tumeona ya magogo maliasili, kazi inafanyika na chini ya uongozi wa nani?

-Tumeona ya Zombe, kazi inafanyika na chini ya uongozi wa nani?

-Tumeona ya Balozi wa Italy, kazi inafanyika na chini ya uongozi wa nani?

-Tumeona ya ujio wa bwana Bushi, kazi inafanyika na chini ya uongozi wa nani?

-Tumeona ya Osullivan, kazi inafanyika na chini ya uongozi wa nani?

-Tumeona ya mashule ya sekondari kazi inafanyika na chini ya uongozi wa nani?

-Tumeona ya Chuo kikuu cha Dodoma, kazi inafanyika na chini ya uongozi wa nani

Kwa hayo machache na mengine mengi anafaa kila sifa tunazompa na nina kuhakikishia na wewe unajua ya kuwa madudu mengi anayo ya safisha kayakuta, kama haya ya BoT, Buzwagi, Matatizo ya Umeme, Matatizo ya njaa, kukosa mashule ya sekondaro, kukosa vyuo vikuu vya kutosha. aaah mengi tuu.

Na sasa tunangoja madudu ya Ufisadi ya Mkapa, Sumae na wengine, yapo jikoni yanapikwa, kaaeni mkao wa kula.
 
Mh. Dar Es Salaam i like you men.
Let me ask you few questions. Can you name five good things ambazo JK amefanya hapo Tanzania ambazo zina effect direct kwa watanzania wa kawaida. Then can you name three ways ambazo JK amefanya kucrack corruption down in his cabinet? Then can you defend about his government overspending habit?

Then let get into juice part, since Tanzania are suffering for years because poor economic policy of his political party, what ways Hon.Jakaya Kikwete took to reduce: first, inflation rate which runs in double digit, second, reduction of Current Account defecit, third, goverment spending, fourth, independence from international aides? Please help me on those few things so i can be proud of Mr. President, other than that i dont care who said what.

Ukinisaidia hayo tuu, then i will come ask you other questions concern yeye kuweka his old bodies kwenye nyeti zote za uchumi, kuanzia centeral bank, mpaka kwenye Board of External Trade.

Naona hapo juu nimetaja machache, sasa wewe unaweza kunieleza awamu ipi ya kabla yake iliofanya kama hayo?
 
Tunayaona ya BoT, hayana mjadala kazi inafanyika na chini ya uongozi wa nani?
Mbona kafara ni ya Balali tuu,na wadogo wadogo wengine

-Tunayaona ya kina Lowassa, kazi inafanyika na chini ya uongozi wa nani?
Infact ni shinikizo la Kamati ya Mwakyembe na Bunge otherwise ilibidi awe proactive enough kuact sio mpaka asukumwe/shinikizo

-Tunayaona ya Buzwagi, kazi inafanyika na chini ya uongozi wa nani?
No comment

_ Tumeona ya magogo maliasili, kazi inafanyika na chini ya uongozi wa nani?
No comment

-Tumeona ya Zombe, kazi inafanyika na chini ya uongozi wa nani?
No comment

-Tumeona ya Balozi wa Italy, kazi inafanyika na chini ya uongozi wa nani?
-Others can comment

-Tumeona ya ujio wa bwana Bushi, kazi inafanyika na chini ya uongozi wa nani?
Yule mzee yuko na interest zake behind the scene tunaliwa na tutaendelea kuliwa.Bepali ni bepari ni mwendo wa kuuma na kupuliza.Be open minded tafadhali.

-Tumeona ya Osullivan, kazi inafanyika na chini ya uongozi wa nani?
No comment

-Tumeona ya mashule ya sekondari kazi inafanyika na chini ya uongozi wa nani?

Apo nimechefuka just last week nimetoka tozwa elfu ishirini kuchangia ujenzi wa shule ya kata.Jan tuu kuna watu wamefunguliwa mashitatka kisa hawana 20,000 za ujenzi wa zahanati na as aresult ni mahabusu au fine 75,000

-Tumeona ya Chuo kikuu cha Dodoma, kazi inafanyika na chini ya uongozi wa nani
No comment.
JK ana mazuri yake ila na mabaya anayo mengi,anyway lets give him sometime.
Kama all arround the country ni maandamanao kwa kiongozi hii inaleta picha mbaya na hasa unapochukua maamuzi ya kiswahi swahiba uku wananchi wakiteseka.
 
Back
Top Bottom