Rais Kenyatta aitisha mkutano wa kikanda kujadili usalama DR-Congo

The Supreme Conqueror

JF-Expert Member
Feb 13, 2017
320
899
Rais wa Kenya, Uhuru Kenyatta ameitisha mkutano wa Wakuu wa Nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki siku ya Jumatatu kujadili amani na usalama katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, kulingana na taarifa ya serikali.

Uhuru ambaye pia ni Mwenyekiti wa Jumuiya ya Afrika Mashariki Jumatano alitoa wito wa kupelekwa kwa Kikosi cha Kudumu cha Afrika Mashariki ili kukomesha ghasia katika eneo la Mashariki mwa nchi hiyo.

DRC hata hivyo inapinga Rwanda kuwa sehemu ya jeshi lililopendekezwa la kikanda na imesitisha uhusiano wa pande mbili na Kigali.

Nchi hiyo inaishutumu Rwanda kwa kuwaunga mkono waasi wa M23 ambao hivi majuzi waliuteka mji wa mpakani Bunagana.

Rwanda inakanusha madai hayo.

Rais Felix Tshisekedi katika taarifa yake aliishutumu Rwanda kwa kutaka kuikalia kimabavu nchi yake ili kutumia madini yake na kuitaka Uingereza kuishinikiza Kigali kukomesha uchokozi wake.

Mvutano kati ya nchi hizo mbili umeongezeka katika wiki za hivi karibuni huku maandamano ya kuipinga Rwanda yakiripotiwa mjini Kinshasa na mashariki mwa Congo.

Siku mbili zilizopita, mwanajeshi wa Congo aliwafyatulia risasi walinda usalama wa Rwanda katika kituo cha mpakani mjini Bukavu na kuwajeruhi maafisa wawili wa polisi.

Kenya ndiyo mwenyeji wa mazungumzo ya moja kwa moja ya amani kati ya serikali ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo na makundi tofauti vya waasi.

Mazungumzo hayo bado hayajazaa matokeo yoyote.
 
DRC hata hivyo inapinga Rwanda kuwa sehemu ya jeshi lililopendekezwa la kikanda na imesitisha uhusiano wa pande mbili na Kigali.
Hili jeshi la kikanda litaongeza jipya lipi tofauti na majeshi ya Monusco au kile kikosi maalum cha UN (FIB) ?...Nani atachangia gharama za hicho kikosi cha kikanda ?..

Majukumu ya hicho kikosi yatakuwa kusaidia jeshi la Drc au kushirikiana na Monusco ?...

Kama Monusco chenye askari kutoka mataifa mengi tena kina bajeti kubwa ya mamilioni ya dola wanashindwa kumaliza uasi huko Kivu, hicho kikosi kipya kitaweza kutafuna huo mfupa ?

mtu chake zitto junior Moronight walker Count Capone
 
Hili jeshi la kikanda litaongeza jipya lipi tofauti na majeshi ya Monusco au kile kikosi maalum cha UN (FIB) ?...Nani atachangia gharama za hicho kikosi cha kikanda ?..

Majukumu ya hicho kikosi yatakuwa kusaidia jeshi la Drc au kushirikiana na Monusco ?...

Kama Monusco chenye askari kutoka mataifa mengi tena kina bajeti kubwa ya mamilioni ya dola wanashindwa kumaliza uasi huko Kivu, hicho kikosi kipya kitaweza kutafuna huo mfupa ?

mtu chake zitto junior Moronight walker Count Capone
Kuna mtu anafaidika na hawa jamaa huko Kivu
Haiwezekan nchi Zaid ya 3 mshindwe
Kuthibit Waas walio mkoa mmoja
 
Rais wa Kenya, Uhuru Kenyatta ameitisha mkutano wa Wakuu wa Nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki siku ya Jumatatu kujadili amani na usalama katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, kulingana na taarifa ya serikali.

Uhuru ambaye pia ni Mwenyekiti wa Jumuiya ya Afrika Mashariki Jumatano alitoa wito wa kupelekwa kwa Kikosi cha Kudumu cha Afrika Mashariki ili kukomesha ghasia katika eneo la Mashariki mwa nchi hiyo.

DRC hata hivyo inapinga Rwanda kuwa sehemu ya jeshi lililopendekezwa la kikanda na imesitisha uhusiano wa pande mbili na Kigali.

Nchi hiyo inaishutumu Rwanda kwa kuwaunga mkono waasi wa M23 ambao hivi majuzi waliuteka mji wa mpakani Bunagana.

Rwanda inakanusha madai hayo.

Rais Felix Tshisekedi katika taarifa yake aliishutumu Rwanda kwa kutaka kuikalia kimabavu nchi yake ili kutumia madini yake na kuitaka Uingereza kuishinikiza Kigali kukomesha uchokozi wake.

Mvutano kati ya nchi hizo mbili umeongezeka katika wiki za hivi karibuni huku maandamano ya kuipinga Rwanda yakiripotiwa mjini Kinshasa na mashariki mwa Congo.

Siku mbili zilizopita, mwanajeshi wa Congo aliwafyatulia risasi walinda usalama wa Rwanda katika kituo cha mpakani mjini Bukavu na kuwajeruhi maafisa wawili wa polisi.

Kenya ndiyo mwenyeji wa mazungumzo ya moja kwa moja ya amani kati ya serikali ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo na makundi tofauti vya waasi.

Mazungumzo hayo bado hayajazaa matokeo yoyote.
Haya madai yanakuja kwa kasi ni baada CHOGM kufanyila wiki hii kigali au.wasiwaharbie Rwanda wanaugeni mkubwa sana wiki hii.
 
DRC waache kuwa mazuzu. Hivi ki-nchi cha Rwanda kinawanyanyasaje wakati mna rasilimali kuliko hako Ka nchi mpaka kuwapigia kelele Uingereza walioko huko mbali?
Ni kukosa tuu kuwajibika katika wanajeshi wao, na kuwekeza zaidi ktk usalama , naona serikari yao bado hawajaweka nguvu zaidi kule
 
Hili jeshi la kikanda litaongeza jipya lipi tofauti na majeshi ya Monusco au kile kikosi maalum cha UN (FIB) ?...Nani atachangia gharama za hicho kikosi cha kikanda ?..

Majukumu ya hicho kikosi yatakuwa kusaidia jeshi la Drc au kushirikiana na Monusco ?...

Kama Monusco chenye askari kutoka mataifa mengi tena kina bajeti kubwa ya mamilioni ya dola wanashindwa kumaliza uasi huko Kivu, hicho kikosi kipya kitaweza kutafuna huo mfupa ?

mtu chake zitto junior Moronight walker Count Capone
Ila mkuu ninavyojua mimi Munisco kazi yao ni walinda amani hawaruhusiwi kupigana sehemu,
Nakumbuka ishu ya mali kule walinda amani walikuwa wanaondoka kwa sababu ya mashambulizi ni mengi.
Ila kipo cha FIB cha nchi za sadc ni cha kujibu mashamburizi ni kama kusaidiwa jeshi la congo.
Sasa shida kama wenyewe wacongo Hawana moyo wa kupigana wageni watawasaidiaje, pia na mazingira ya congo sio rafiki sana. Coz ya misitu ni mingi.
 
Rais wa Kenya, Uhuru Kenyatta ameitisha mkutano wa Wakuu wa Nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki siku ya Jumatatu kujadili amani na usalama katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, kulingana na taarifa ya serikali.

Uhuru ambaye pia ni Mwenyekiti wa Jumuiya ya Afrika Mashariki Jumatano alitoa wito wa kupelekwa kwa Kikosi cha Kudumu cha Afrika Mashariki ili kukomesha ghasia katika eneo la Mashariki mwa nchi hiyo.

DRC hata hivyo inapinga Rwanda kuwa sehemu ya jeshi lililopendekezwa la kikanda na imesitisha uhusiano wa pande mbili na Kigali.

Nchi hiyo inaishutumu Rwanda kwa kuwaunga mkono waasi wa M23 ambao hivi majuzi waliuteka mji wa mpakani Bunagana.

Rwanda inakanusha madai hayo.

Rais Felix Tshisekedi katika taarifa yake aliishutumu Rwanda kwa kutaka kuikalia kimabavu nchi yake ili kutumia madini yake na kuitaka Uingereza kuishinikiza Kigali kukomesha uchokozi wake.

Mvutano kati ya nchi hizo mbili umeongezeka katika wiki za hivi karibuni huku maandamano ya kuipinga Rwanda yakiripotiwa mjini Kinshasa na mashariki mwa Congo.

Siku mbili zilizopita, mwanajeshi wa Congo aliwafyatulia risasi walinda usalama wa Rwanda katika kituo cha mpakani mjini Bukavu na kuwajeruhi maafisa wawili wa polisi.

Kenya ndiyo mwenyeji wa mazungumzo ya moja kwa moja ya amani kati ya serikali ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo na makundi tofauti vya waasi.

Mazungumzo hayo bado hayajazaa matokeo yoyote.
Hakuna haja ya mazungumzo na waasi ikiwa lengo lao ni kutaka haki kuliko raia wengine wa congo. Wanataka mbari yao ya kitutsi kupewa madaraka makubwa kisiasa na kijeshi huku hawana utiifu na uzalendo kwa taifa la congo. Wao wana uzalendo wa kimbari tu na ni watiifu kwa utawala wa rwanda unaoongozwa na watutsi.
Huko nyuma congo ilifanya makosa makubwa kuwaingiza waasi wa kitutsi kwa wingi kwenye jeshi lao la taifa na kuwapa vyeo vikubwa. Tatizo ni kua na jeshi linalosalitiwa kwa rwanda saa zote.
 
Hili jeshi la kikanda litaongeza jipya lipi tofauti na majeshi ya Monusco au kile kikosi maalum cha UN (FIB) ?...Nani atachangia gharama za hicho kikosi cha kikanda ?..

Majukumu ya hicho kikosi yatakuwa kusaidia jeshi la Drc au kushirikiana na Monusco ?...

Kama Monusco chenye askari kutoka mataifa mengi tena kina bajeti kubwa ya mamilioni ya dola wanashindwa kumaliza uasi huko Kivu, hicho kikosi kipya kitaweza kutafuna huo mfupa ?

mtu chake zitto junior Moronight walker Count Capone
Inshu iko hivi, robo 3 ya jeshi la kongo lina watusi hadi ngazi za juu Ivo mipango yote m23 wanakua wanapenyezewa, jeshi halisi la lisilo na mamluki ni mayi mayi na ndio mahana Jana wameiomba sirikali ya Kinshasa indoe majeshi yake yote toka eneo la Kivu hadi beni halafu wao waende kufanya kazi yakupiga hao wanyarwanda na hadi sasa hao mayi mayi ndio wanatoa msaada mkubwa sana Kwa jeshi la kongo bila hivo Kagame angeshaichukua Kongo siku nyingi sana
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom