Rais Kenyatta aelezea kuridhika chini ya utawala wake na kudai kuwa amewatimizia wakenya ahadi zote

Ghazwat

JF-Expert Member
Oct 4, 2015
23,718
66,262
2f9c92abf6143208c592e46ff7f0a170.jpg
Rais Uhuru Kenyatta ameelezea kuridhika kwake na kile alichotaja kuwa ufanisi mkubwa chini ya utawala wake, akisema historia itamkumbuka kwa kuleta mageuzi muhimu nchini, hasa ugatuzi

Kwenye taarifa ya kuadhimisha miaka minne ya utawala wake, alisema kumekuwa na mafanikio mengi kuliko yaliyofanywa tangu Kenya ipate uhuru.

"Ninajivunia kuwa ugatuzi sasa umetekelezwa kikamilifu. Ninaamini historia itamkumbuka wajibu wa utawala katika kipindi hiki cha mageuzi kwa nchi yetu", alisema huku akikumbuka Aprili 9 kama siku muhimu kwake alipoapishwa kama Rais.

"Juhudi zetu ziliongozwa na utekelezaji wa kiapo changu kuheshimu, kulinda na kutetea Katiba yetu na pia kwasababu ninaamini ugatuzi kama muundo bora wa uongozi".

Hata hivyo viongozi wa upinzani walipuuzilia mbali mafanikio yaliyotajwa wakisema wananchi wamezidi kutaabika chini ya utawala wake. Naibu Kiongozi wa Wachache Bungeni Bw. Jokoyo Midiwo alisema utawala huu utakumbukwa tu kwa ufisadi na ubaguzi wa kikabila katika utoaji wa vyeo Serikalini.


"Kuanzia masuala unyakuzi wa ardhi hadi sakata kubwa la kiuchumi, na jinsi Rais mwenyewe alivyokiri hajui la kufanya kukabiliana na ufisadi, hii Serikali imefeli kabisa", alisema Midiwo

Chanzo: TaifaLeo
 
Amefanikiwa kidemokrasia na kuleta amani na maridhiano kisiasa, zaidi ya wote wale waliomtangulia, ila asijaribu kutuhadaa. Kazi bado ipo, akifanikiwa kutokomeza ufisadi ndio tutamkumbuka. Kama tunavomkumbuka Emilio Mwai Kibaki kwa kuboresha na kujenga miundo mbinu kote nchini Kenya na kuweka misingi bora ya mazingira mema ya kibiashara. Kampuni za Kenya zilifanikiwa kutanua misuli ndani na nje ya ukanda huu kwa sababu ya sera za Mwai Kibaki. God bless the old man.
 
Back
Top Bottom