Rais kapewa ushauri mzuri sana pengine kuliko mwana CCM yoyote yule

Salary Slip

JF-Expert Member
Apr 3, 2012
46,987
144,319
Huyu dada kila siku mnamponda kwa kumkosoa Mkulu lakini ushauri alioutoa leo kwa Mkulu nahakika hakuna mwana-CCM hata mmoja aliewahi kuutoa.

Kwakweli yote aliyoshauri ni mambo ya msingi sana ila nimeguswa zaidi na tahadhari aliompa Mkulu baada ya yeye kuondoka ofisini kwani hata mimi nimewahi kuwaza hivyo mara nyingi sana.

Kwenye maisha kwakeli ni bora wanaokukosoa kuliko wanaokupigia makofi kwa kila jambo.

Mkuu, umepewa ushauri mzuri na wa bure sasa kazi kwako.


===
Najua hawezi kunisikiliza mimi sana sana atafanya opposite kama siku zote ila najua atasoma, hiyo inatosha.

Rais Magufuli, It’s not too late to change! Unaweza kutubu na ukabadilika ukarudi kuwa yule Magufuli tuliempigia kura. Mtu asie na dharau, anaeongea na wnanchi wake kwa unyenyekevu na upendo na sio kwa ukali na matusi, rais asie na double standards.

Unaweza kubadilika, naamini umeshaona watanzania hawampendi huyu Magufuli wa sasa. Ndio umaskini unachangia watu kutokukupenda lakini kinachochangia zaidi ni hali ya hofu wanayoishi nayo wananchi.

Kama wewe ni mzalendo wa kweli Tafadhali badilika. Achana na wapinzani.waache waongeee, Maneno yao hayakuzuiii kufanya lolote. Tunaokuchamba mitandaoni acha tukuchambe, ukibadilika tutakosa la kukuchamba tutaacha wenyewe bila kuambiwa na mtu.Achia demokrasia ya nchi irudi kama zamani. Hii issue ya demokrasia inakimbiza mpaka wawekezaji! .

Watanzania wanachokihutaji kwako ni maendeleo tu sio kuona ubabe wako!

Watanzania ni watu waelewa sana unaweza kusimama ukawaambia ukweli kuwa serikali inapitia muda mgumu huwezi kutoa ajira au kupandisha mishahara na inabidi uwapunguze wafanyakazi wengine. That’s is better than kuwaondoa watu kwa kuwasingizia mambo kama vyeti feki etc. Ni bora ukawaambia ukweli . Itauma lakini tukiona unaonyesha utu tutakuelewa. Au hizo nyumba unazobomoa kweli serikali imeshindwa kabisa kutafuta option ya kibinadamu kuliko kuwaacha wananchi homeless? .

Bashite anakujengea chuki na wananchi hakuna kura hata moja anayokuongezea Bashite.ila ndo umemfanya muwakilishi wa serikali yako.Why?? Unafaidika nini na Bashite zaidi ya kumtuma kufanya uhalifu? Uhalifu ambao huitaji kuufanya, wewe ulishapendwa na watanzania bila kumtuma Bashite akafanye uhalifu so why now? .

Kingine acha visasi, kweli kila rais anaeingia madarakani akianza kulipiza visasi itakuwaje? Kumbuka na wewe kuna siku utaondoka Ikulu, unadhani watakuacha salama?? Ukiendelea hivi nakuhakikishia wewe ndo utakuwa rais wa kwanza Tanzania kufanyiziwa baada ya kutoka Ikulu na haitojalisha rais atakaefuata atakuwa ccm au upinzani wananchi watamlilia akufanyizie. Mark my words!
 
Salary Slip nadhani ni kamanda mwenye medani kubwa ya uwoga ufipa. Hata screenshot umeogopa kuweka, sasa umeandika nn hapa hata mange hatumjui wengine

a4e4de33d61722a68cac68027b1e1c55.jpg
1d615af95e3cd58498dd4a51799c4fd1.jpg
4b38c7124638b3a4152e7a418433b292.jpg
4f2b703a8e49dedb47270abfa0440d64.jpg


Hiyo hapo
 
Huyu dada kila siku mnamponda kwa kumkosoa Mkulu lakini ushauri alioutoa leo kwa Mkulu nahakika hakuna mwana-CCM hata mmoja aliewahi kuutoa.

Kwakweli yote aliyoshauri ni mambo ya msingi sana ila nimeguswa zaidi na tahadhari aliompa Mkulu baada ya yeye kuondoka ofisini kwani hata mimi nimewahi kuwaza hivyo mara nyingi sana.

Kwenye maisha kwakeli ni bora wanaokukosoa kuliko wanaokupigia makofi kwa kila jambo.

Mkuu, umepewa ushauri mzuri na wa bure sasa kazi kwako.

Siku zote hata Kuku akijua kuwa leo anaenda ' Kuchinjwa ' huwa anakuwa na busara zake zote.
 
Salary Slip huo ujinga upeleke kwenye blog za chadema..

Najua mnataman sana mange awe msemaji ya chama chenu lakn mmeshindwa kwakuwa ameshakuwa most wanted,
Hivyo nyinyi manyumbu ambao mlimtukana kikwete lakn leo mmemsifia, mlimtukana lowasa lakn Leo amekuwa ndio mkombozi wenu , mlimtukana nyalandu lakn Leo amekuwa ndio dume lenu la mbegu mpaka amekuja kiwapandikizia mbegu bora nyinyi ndio muuchukue huo ushauri maana mpaka sasa mmekuwa wafu msio na uhai
 
Aliyoyaandika hayo analenga yale yale anayotaka yatokee tangu mwanzo kwa chuki zake alizozijaza rohoni pake..

Hakuna jipya.. na hajatumia akili kabisa na kuandika mgazeti wote huo hana ujanja.. angemezea mengine.. ila hawezi sababu hana lingine zaidi ya chuki za wivu.. ameona njia za kumtukana Mkulu na viongozi wengine hazimpi kiki.. wafuasi wake walianza kumdharau.. zimeshindikana sasa anafikiri akili hiyo ya kuandika hayo itapenya.. ni kama anaomba msamaha kwa Mkulu kwa kutumia ulimi ila rohoni kajaa majanga matupu ya chuki za kibinafsi juu ya maisha yake yalivyompiga chini.

Maisha yake aliyokuwa nayo miaka miwili mitatu iliyopita kamwe hakutegemea kuwa alipo leo.. bora tu alie aondoe uchungu la sivyo atazidi kuwashwa washwa.. na ajipige vibao vya usoni..

Mwambieni ujanja wake aliotumia kuandika hayo yote haupenyi ng'ooo

Pole kwa upinzani kwa kuzidi kuonyesha hamna jipya bali mnaweweseka sana sana kwa kuisoma namba.. na kuwa na wasemaji wenu anyau kabisa

Kawa karibu na wafuasi wa Chadema wa USA wamepiga pesa mnazochangia za matibabu jata kuwalipia wengine likizo kwenda Tanzania na kuchungulia Nairobi kwa masaa kupiga picha za kuwaonyesha... nyuma ya pazia wanawacheka.. endeleeni kuwapa pesa watanue bora mngetuma michango kwa mkewe moja kwa koja hata ndugu wengine..
 
Huyu dada kila siku mnamponda kwa kumkosoa Mkulu lakini ushauri alioutoa leo kwa Mkulu nahakika hakuna mwana-CCM hata mmoja aliewahi kuutoa.

Kwakweli yote aliyoshauri ni mambo ya msingi sana ila nimeguswa zaidi na tahadhari aliompa Mkulu baada ya yeye kuondoka ofisini kwani hata mimi nimewahi kuwaza hivyo mara nyingi sana.

Kwenye maisha kwakeli ni bora wanaokukosoa kuliko wanaokupigia makofi kwa kila jambo.

Mkuu, umepewa ushauri mzuri na wa bure sasa kazi kwako.
Huo ushauri uko wapi hapa?,au mpaka twende instagram iwe DA MANGE kasema?,uweke hapa buana,wengine hatuna hiyo app ya instagram
 
Back
Top Bottom