Rais kama hutochukua hatua za ziada kwenye mradi wa mabasi yaendayo haraka(DART), basi tujiandae kwa maombolezo

Wasalaam
Ni ukweli usiopingika kuna matatizo makubwa sana tena sana kwenye mradi huu wa mabasi yaendayo haraka na hatua za haraka zisipo chukuliwa ni ukweli ulio wazi taifa litaingia kwenye maafa yanayo weza kuzuilika kabisa!

Mh Rais
Lazima tukubali kuwa matatizo ya mradi huu yamewashinda watu wengi akiwemo waziri mkuu lakini bado matatizo kwenye huu mradi yanaongezeka kila leo.

Mh Rais
Ni ukweli ulio wazi kabisa mradi huu una matatizo mengi na una hatarisha maisha ya watanzania wengi wanao tumia mradi huu na ni kwamba ni mradi hatarishi sana kwa maisha ya watu ni lazima watu wachukue hatua sio kuongea tuuu!

Mh Rais
Mradi huu mabasi yanajaza habaria kupita kiwango

Kupitia Mradi huu umekuwa sehemu ya watu kupoteza vitu vyao vya thamani kutokana na vurugu za kugombania magari

Mh Rais
Kupitia mradi huu watu wamekuwa wakiumizwa na kuvunjwa viungo wakigombea magari...

Kupitia mradi huu imethibitika kabisa waendesha mradi wanafanya makusudi kuchelewesha magari hili watu wajazane kwenye gari moja au mawili ili wasave mafuta maana ni magari machache yatatumika!

Mh Rais

Kupitia mradi huu tumethibitisha kuwa watanzania wenyewe ndio wahujumu namba moja wa miradi yao maana inawezekanaje hakuna kiongozi wa juu au wachini ambaye aoni kama kuna shida kubwa sana....

Kupitia mradi huu watumiaji wa magari haya wameshuhudia magari ya kizidiwa uzito na mengine kupata pancha na hakuna anaye jali kabisa ....kweli hatujui kitakacho fata?


Mh Rais watu wengi wamesema sana tena sana kuhusu mradi huu lakini hakuna linalofanyika kabisa hakuna kiongozi anayechukua hatua lakini ukweli ni kwamba mradii kwa mwendo wake ujiandae kuandika barua ya kutoa pole kwa watanzania kama hatua azito chukuliwa !


Mh Rais mradi huu kila miundombinu yake haifanyi kazi kuanzia kwenye tuketi, speaker na camera na hata vituo mabati yameanza kutoka na hakuna anayefanya lolote............hii ni makusudi kabisa!

Mh Rais
Huhitaji kuwa mtabari kujua kuwa mradi huu kama hatua hazichukuliwi ni lazima utaleta maafa makubwa na tutakuwa wanafiki kutuma salamu za rambi rambi wakati tunaweza tatua matatizo haya!

Ni lazima hatua za haraka zichukuliwe kuzuia maafa kwenye mradi huu

Mkuu unafanya vizuri kuchangia hoja lakini waziri wa usafiri si yupo? Ninachojaribu kusema ni kwamba kila kitu hawezi kufanya rais peke yake la sivyo mtammaliza kwa presha.

Waziri wa usafiri yupo na analipwa na pesa zenu kufanya kazi hizi.
 
Tumeshaandika sana hapa jukwaani kuhusu huduma mbovu za huu mradi watu wakawa wanatukosoa kwa nyimbo na mapambio, ila iko siku watajuta.
 
Kwamba kinachoendelea mwendokasi ni jambo la kawaida?
Sasa hapa hamishia mashaka kwenye akili zako badala ya zangu.

Neno KAWAIDA kama unalielewa maana yake basi hutaogopa kusema 'watu kugombea kuingia kwenye basi ni kawaida'. Labda nikusaidie kitu maana yawezekana umekurupuka kuishambulia akili yangu pasina kutumia ya kwako kuielewa hoja yangu. Hoja yangu ni kubwa SUALA HILI HALIPO KWENYE MWENDO KASI PEKE YAKE NA SI AJABU YA KIASI CHA KUOMBA ATTENTION YA RAIS. Sio kwamba jambo likiwa BAYA basi haliwezi kuwa la kawaida.

Huu mradi ulianzishwa kusolve matatizo ya usafiri, moja wapo likiwa hilo la abiria kujazana vituoni kiasi basi likija wanapanda kwa kugombea, kwa hiyo tuelewane hapa, hili ni TATIZO na lipo tangu zamani. Kilichotokea ni kwamba, mradi umeshindwa kutatua tatizo lililokuwepo.

Jambo fulani kuwa ni TATIZO haimaanishi haliwezi kuwa la kawaida. Ndio maana hata ukienda hospitali na mtoto ana allergy si ajabu daktari akakwambia "ni kawaida watoto kupata mzio" lakini hiyo haimaanishi kuwa kasema sio tatizo...ni tatizo, lakini ni kawaida pia.
 
Tumeshaandika sana hapa jukwaani kuhusu huduma mbovu za huu mradi watu wakawa wanatukosoa kwa nyimbo na mapambio, ila iko siku watajuta.
Huu mradi uliambatanishwa na ushabiki, sasa leo sijui kaamkia wapi ndio kaja kuimba zaburi hapa. Ndio shida ya kutengeneza miundombinu ili ikuletee sifa badala ya kufanikisha huduma.
 
Huu mradi ni mzuri lakini wahujumu wa huu mradi ni watanzania wenyewe!
Watanzania wepi?

1571205201470.png
 
Mdogo wangu rutashobolwa hivi hili nalo ni lazima rais wetu ashughulike nalo??

Kwann siyo wazuri wa uchukuzi kwann siyo mkurugenzi wa mamlaka wa usafiri wa nchi kavu?


Kwan siyo mkuu wa mkoa na wangu wake wa wilaya?

Hebu.tumpe rais muda.wa kupumzika jaman

Kuna Rais ataombwa hadi Kuingilia kati Ndoa za Watu au hata kuwahimiza Wanafamilia Kupiga Miswaki na Kuoga kabisa.
 
Hasa Tibi....
Kuna Siku nilimwaambia msimamizi mmoja kwanini mnawasimamisha watu hivyo ilihali lipo lingine linasubiria.Nikamkumbusha Kuna ugonjwa wa homa ya ini ambao mgusano tu unasababisha maumbukizi.Nilivyomuambia hivyo akashtuka maana ndio mara ya kwanza kusikia homa ya ini.
 
... hadi operations za vimiradi kama DART lazima Rais ahusike? Hana wasaidizi? Kuanzia waziri husika hadi Jijiji na manispaa zake? Tujenge mifumo badala ya watu!
Mbona kama vile amjamuelewa rais. Haya aliyoeleza mleta mada ndiyo rais anapenda na ndiyo anayafanya mara nyingi.

Ikitokea ukajifanyia jukumu kwa mahamuzi yako anakutumbua kisha anakuja kukunanga. Rejea issue ya machinga mwanza, mama wa WHO sijui mwele, nk.

Unless umuulize yeye akwambie haya fanya na akufundishe jinsi ya kueleza mfano anaweza akakwambia kaseme "mh mtukufu rais dokta so-so ameamua 1, 2, 3... kuhusu mradi wa dart. Siyo kujitutumua na kuchukua mahamuzi bila yeye kuhusika na jina lake kutajwa kwa mbwembwe zote kwa regime hii utaumia bure.
 
si ununue gari lako binafsi? mbona unasumbua watu?
Issue siyo gari binafsi wewe acha ujinga wa kujifanya uelewi. Kama IQ yako siyo ndogo basi utakuwa limbukeni wewe. Issue inayoongelewa na mleta mada ni kuwa kuna matatizo katika uendeshaji wa mradi dart. Sasa hiyo inauhusiano gani na gari lake binafsi?
 
Wasalaam
Ni ukweli usiopingika kuna matatizo makubwa sana tena sana kwenye mradi huu wa mabasi yaendayo haraka na hatua za haraka zisipo chukuliwa ni ukweli ulio wazi taifa litaingia kwenye maafa yanayo weza kuzuilika kabisa!

Mh Rais
Lazima tukubali kuwa matatizo ya mradi huu yamewashinda watu wengi akiwemo waziri mkuu lakini bado matatizo kwenye huu mradi yanaongezeka kila leo.

Mh Rais
Ni ukweli ulio wazi kabisa mradi huu una matatizo mengi na una hatarisha maisha ya watanzania wengi wanao tumia mradi huu na ni kwamba ni mradi hatarishi sana kwa maisha ya watu ni lazima watu wachukue hatua sio kuongea tuuu!

Mh Rais
Mradi huu mabasi yanajaza habaria kupita kiwango

Kupitia Mradi huu umekuwa sehemu ya watu kupoteza vitu vyao vya thamani kutokana na vurugu za kugombania magari

Mh Rais
Kupitia mradi huu watu wamekuwa wakiumizwa na kuvunjwa viungo wakigombea magari...

Kupitia mradi huu imethibitika kabisa waendesha mradi wanafanya makusudi kuchelewesha magari hili watu wajazane kwenye gari moja au mawili ili wasave mafuta maana ni magari machache yatatumika!

Mh Rais

Kupitia mradi huu tumethibitisha kuwa watanzania wenyewe ndio wahujumu namba moja wa miradi yao maana inawezekanaje hakuna kiongozi wa juu au wachini ambaye aoni kama kuna shida kubwa sana....

Kupitia mradi huu watumiaji wa magari haya wameshuhudia magari ya kizidiwa uzito na mengine kupata pancha na hakuna anaye jali kabisa ....kweli hatujui kitakacho fata?


Mh Rais watu wengi wamesema sana tena sana kuhusu mradi huu lakini hakuna linalofanyika kabisa hakuna kiongozi anayechukua hatua lakini ukweli ni kwamba mradii kwa mwendo wake ujiandae kuandika barua ya kutoa pole kwa watanzania kama hatua azito chukuliwa !


Mh Rais mradi huu kila miundombinu yake haifanyi kazi kuanzia kwenye tuketi, speaker na camera na hata vituo mabati yameanza kutoka na hakuna anayefanya lolote............hii ni makusudi kabisa!

Mh Rais
Huhitaji kuwa mtabari kujua kuwa mradi huu kama hatua hazichukuliwi ni lazima utaleta maafa makubwa na tutakuwa wanafiki kutuma salamu za rambi rambi wakati tunaweza tatua matatizo haya!

Ni lazima hatua za haraka zichukuliwe kuzuia maafa kwenye mradi huu
Mwenye mkoa wake anasemaje
 
Mdogo wangu rutashobolwa hivi hili nalo ni lazima rais wetu ashughulike nalo??

Kwann siyo wazuri wa uchukuzi kwann siyo mkurugenzi wa mamlaka wa usafiri wa nchi kavu?


Kwan siyo mkuu wa mkoa na wangu wake wa wilaya?

Hebu.tumpe rais muda.wa kupumzika jaman
Mwambie wazi ccm haijawahi kufanikiwa katika huduma za jamii... hivi tulipoandika humu kwamba mradi ule ni mzuri ila siasa itauharibu na hautakuwa tofauti na daladala za mbagala hakusoma au hakutuelewa?
Acha tumalize kampeni kwanza...
 
Nahofia na treni mpya ya SGR isije ikageuka kama huu mradi wa mwendokasi.

Dah! Watanzania bado tuna safari ndefu sana ya kwenda.

Hii nchi tuwarudishie wazungu waje kuiendesha, kwa aina fulani ya makubaliano, kila kitu kitakwenda sawa.
Hoja si wazungu bali siasa za kulindana na kuwapa watu (kampuni) wasio/zisizo na maono wala mwelekeo wenye tija endelevu... hivi CRDB mkurugenzi aliyeifikisha hapo ni mzungu? Nmb ina mkurugenzi mzungu iko wapi?
Tatizo ni CCM... tunajisahaulisha vifo vya viwanda na mashirika kwa majina ya mabeberu na upinzani ili boriti libaki jichoni.
 
Imefikia hatua hata ukiwa na matatizo binafsi na Mfanyakazi wa huu mradi unaweza usiudumiwe. Nakumbuka katika kituo cha Argentina niligomewe uziwa tiketi na moja ya Mdada kisa hana chenji. Hiyo ilikua sababu tulishapishana sehemu. Wapumbavu warudishe Kadi Staff wao wanadharau sana Japo sio wote.
 
Hoja si wazungu bali siasa za kulindana na kuwapa watu (kampuni) wasio/zisizo na maono wala mwelekeo wenye tija endelevu... hivi CRDB mkurugenzi aliyeifikisha hapo ni mzungu? Nmb ina mkurugenzi mzungu iko wapi?
Tatizo ni CCM... tunajisahaulisha vifo vya viwanda na mashirika kwa majina ya mabeberu na upinzani ili boriti libaki jichoni.
Shirika lipi au kiwanda kipi cha umma kilichofanikiwa hadi leo hii?

Licha ya mengineyo.
 
Back
Top Bottom