Rais Kagame ni mfano wa kiongozi kuigwa Africa

PAMBANA

Member
Oct 21, 2010
73
21
Ndugu wanaJF,

Rais Paul Kagame wa Rwanda ni kiongozi anayeheshimika sana ndani na nje ya bara la Afrika na heshima hiyo anaipta kutokana na yale anayofanya kwa nchi yake na watu wake. Ni hivi karibuni kama si kusikia basi tulisoma kwenye vyombo vya habari kuwa Rwanda imefanikiwa kupunguza umaskini kwa kiwango cha 12% yaani kutoka 57% hadi 45%.

Mchumi mmoja wa chuo kikuu cha Oxford bwana Paul Collier aliwahi kusema kuwa Rwanda inafanya vizuri kwa sababu Rais wa nchi hiyo ni mwadilifu na mchapa kazi kweli kweli.

Ni rais ambaye anawapangia mawaziri wake viwango ambavyo wanatakiwa kuvifikia kila mwaka na wanashindwa huwajibika, tofauti na sisi eti waziri anaboronga katika nafasi halafu anaomba kujiuzuru eti rais anakataa.Chukulia suala kashifa ya wizara ya madini kamati ya bunge ilichunguza na kutoa mapendekezo yake lakini mpaka leo bado mawaziri wanakula kuku kwa mrija bila aibu.

Kwa nchi nyingine kitendo tu cha kiongozi kuhusishwa kwenye kashfa kinatosha kiongozi huyo kujiudhuru.siku zote kiongozi anayeteua wasaidizi wabovu naye mbovu pia.
 
kagame yupo smart kichwani alaf anataka kutoa zle fkra za watu kuidharau sana rwanda kwa7b ya background yao..EDIT HYO HEADING HAUJAWEKA KAGAME..
 
download
 
Lakini ana-element za udikteta huyu jamaa japo kuwa unamsifia!Yeyote anayemu-oppose anamdedisha tena anakutumia majasusi huko huko ulipo!!Nimeishi kidogo na wanyarwanda ughaibuni nashangaa hawa niliowaona wanadai hawampendi Kagame kwa sera zake za kibabe so mdau usiangalie upande mmoja tu wa shilingi!!
 
Acheni kusifu mawazo ya wazungu? Rwanda ni nchi ndogo sana? Kwa Tanzania utafananisha na wilaya tu? Hivyo kuitawala ni rahisi sana? Tatu wanyarwanda ni wachapa kazi sio wabongo tunaoshinda kwenye vijiwe vya kahawa na wengine kuinama kutwa nzima kwenye pool tables?
 
Mi chochote wazungu wanachosifia kuhusu africa naonaga magumash tu wanakuwaga na interets zao ,kuna kitu wanavizia tu!!!!
 
sijui kama umefanya utafiti mzuri au umenza na kumpa sifa tu huyu jamaa. Kuna mambo mazuri anayafanya Kagame, lakini maovu mengi pia. Kuna udikiteta mkubwa saana pale Kigali
 
Historia inamhukumu kwa kiasi flani, aliingia madarakani kwa kutumia moja KATI ya machafuko ya kisiasa makubwa zaidi kutokea Afrika yaliyopelekea mauaji ya kimbari. Almost 1 mil. Peoples walikufa....

Vp huwezi jua labda Kama angekuwa mwanadiplomasia zaidi yasingetokea yalotokea 1994 nchini Kwake. Angechelewa kukamata dola lakini pia ile vita ya wenyewe kwa wenyewe ingeweza kuepukika.

Anaweza kuwa mzuri kwa kukuza Uchumi lakini kwa DOA hili in democracy....anamapungufu siwezi kumsifu kwa extent Yako. Kwa ushauri wangu Ni bora angetengeneza njia kwa democracy itawale then aachie madaraka coz elewa kwamba yuko madarakani kwa zaidi ya 15years sasa....

Je, huoni Kama Ni muendelezo wa Yale walio na wanayoendelea kufanya viongozi kama Mugabe, Museveni au Gadafi na wengine Kama hao Africa?
 
Yaani ningekuwa na uwezo ningeomba tubadilishiwe rais maana huyu Janga la Kitaifa tumechoka nae, kama kunakauwezekano tupewe Kagame kwa kipindi cha mwaka mmoja tu watu wanyooke washikishwe adabu kidogo.
 
Mbona mnasahau kwamba ni huyu huyu Kagame anaidhulumu Congo DRC, anaua Wakongomani Mashariki ya nchi, anapora dhahabu, almasi na uranium. Ni huyuhuyu Kagame aliyemuua Rais aliyepita wa Rwanda na kushirikiana na RPF na Museveni. Ni huyuhuyu Kagame anayetia aibu kwa uroho wa mali za Congo mpaka akapigana na Museven katika ardhi ya Congo.
Naomba msaada tunajifunza nini kwake, wizi wa mali za wenzetu? kuwa kibaraka wa Marekani? c'mon guys!
 
Japo ana element ya udikteta huwa nam appreciate Kagame. Alipoingia tu madarakani kitu cha kwanza aliuza magari yote ya kifahari na kuziwekeza zile pesa kwa wananchi. Leo hii Rwanda ni nchi ya 26 kwa maendeleo duniani, wakati Tanzania ni nchi ya 152 pamoja na rasilimali zote lukuki tulizonazo.
 
tafsiri ya demokrasia kwa nchi za afrika ni zaidi ya kupanga foleni kupiga kura na kupishana baada ya miaka kumi au nane. democrasia ionekane katika kulinda na kutetea maslahi ya taifa kwaujuma hata kwa njia za kidkteta! kagame is a man of action. i appreciate him.
 
Japo ana element ya udikteta huwa nam appreciate Kagame. Alipoingia tu madarakani kitu cha kwanza aliuza magari yote ya kifahari na kuziwekeza zile pesa kwa wananchi. Leo hii Rwanda ni nchi ya 26 kwa maendeleo duniani, wakati Tanzania ni nchi ya 152 pamoja na rasilimali zote lukuki tulizonazo.
Mkuu hebu nipe data source ya hiyo ranking yako maana world bank haionyeshi hivyo!
 
Acheni kusifu mawazo ya wazungu? Rwanda ni nchi ndogo sana? Kwa Tanzania utafananisha na wilaya tu? Hivyo kuitawala ni rahisi sana? Tatu wanyarwanda ni wachapa kazi sio wabongo tunaoshinda kwenye vijiwe vya kahawa na wengine kuinama kutwa nzima kwenye pool tables?

Mkuu.Tuko pamoja. "Rwanda ni nchi ndogo sana kama wilaya mojawapo za nchi yetu ndio maana ni rahisi kutawala na kufikia maendeleo waliyonayo. Hatuendelei kwa sababu Watanzania ni wavivu."
 
Yaani ningekuwa na uwezo ningeomba tubadilishiwe rais maana huyu Janga la Kitaifa tumechoka nae, kama kunakauwezekano tupewe Kagame kwa kipindi cha mwaka mmoja tu watu wanyooke washikishwe adabu kidogo.

I once wished the same...but wishes can not be horses.....

Poor Tanzanians.
 
Mkuu, you have correctly identified Kagame in the perspective of desparate cum deplorable people of this Great Tanzanian land, Kagame is ahead of many African presidents all adjectives put together. The size of the Country would not be an issue, if the people are happy with all the non sense attitude he carries around.

Am happy here is a lesson for us all not only JK, he is struggling to eliminate corruption in Rwanda in deed, fruits are very obvious. Am not sure if his legacy wont be tainted with the details put forward by other people, especially his probable linkage to the '94 Rwanda Genocide and the infiltration into DRC.

On the other hand who would have dreamed of the Rwanda we see today some 10 years ago?
at lease He has said, this is his last term, 15Years havent made him and expert in governance like his brother in arms YKM.
Kagame, will become another decent African statesman!
my humble submission
 
Yaani kuna watu mazoba...ukubwa au udogo wa nchi si issue...kwanza ukiangalia rasilimali kuna kuzidiana...Rwanda ni landlocked country na hawana rasilimali kama TZ...swali la msingi hapa ni uwajibikaji HASA kwa tuliowapa dhamana ya kutuongoza.. VIONGOZI TZ WENGI HAMNA KITU WAKIONGOZWA NA MKULU..HUO NDIO UKWELI COZ WAMEPROOVE FAILURE KILA ENEO.
 
Back
Top Bottom