Ndugu wanaJF,
Rais Paul Kagame wa Rwanda ni kiongozi anayeheshimika sana ndani na nje ya bara la Afrika na heshima hiyo anaipta kutokana na yale anayofanya kwa nchi yake na watu wake. Ni hivi karibuni kama si kusikia basi tulisoma kwenye vyombo vya habari kuwa Rwanda imefanikiwa kupunguza umaskini kwa kiwango cha 12% yaani kutoka 57% hadi 45%.
Mchumi mmoja wa chuo kikuu cha Oxford bwana Paul Collier aliwahi kusema kuwa Rwanda inafanya vizuri kwa sababu Rais wa nchi hiyo ni mwadilifu na mchapa kazi kweli kweli.
Ni rais ambaye anawapangia mawaziri wake viwango ambavyo wanatakiwa kuvifikia kila mwaka na wanashindwa huwajibika, tofauti na sisi eti waziri anaboronga katika nafasi halafu anaomba kujiuzuru eti rais anakataa.Chukulia suala kashifa ya wizara ya madini kamati ya bunge ilichunguza na kutoa mapendekezo yake lakini mpaka leo bado mawaziri wanakula kuku kwa mrija bila aibu.
Kwa nchi nyingine kitendo tu cha kiongozi kuhusishwa kwenye kashfa kinatosha kiongozi huyo kujiudhuru.siku zote kiongozi anayeteua wasaidizi wabovu naye mbovu pia.
Rais Paul Kagame wa Rwanda ni kiongozi anayeheshimika sana ndani na nje ya bara la Afrika na heshima hiyo anaipta kutokana na yale anayofanya kwa nchi yake na watu wake. Ni hivi karibuni kama si kusikia basi tulisoma kwenye vyombo vya habari kuwa Rwanda imefanikiwa kupunguza umaskini kwa kiwango cha 12% yaani kutoka 57% hadi 45%.
Mchumi mmoja wa chuo kikuu cha Oxford bwana Paul Collier aliwahi kusema kuwa Rwanda inafanya vizuri kwa sababu Rais wa nchi hiyo ni mwadilifu na mchapa kazi kweli kweli.
Ni rais ambaye anawapangia mawaziri wake viwango ambavyo wanatakiwa kuvifikia kila mwaka na wanashindwa huwajibika, tofauti na sisi eti waziri anaboronga katika nafasi halafu anaomba kujiuzuru eti rais anakataa.Chukulia suala kashifa ya wizara ya madini kamati ya bunge ilichunguza na kutoa mapendekezo yake lakini mpaka leo bado mawaziri wanakula kuku kwa mrija bila aibu.
Kwa nchi nyingine kitendo tu cha kiongozi kuhusishwa kwenye kashfa kinatosha kiongozi huyo kujiudhuru.siku zote kiongozi anayeteua wasaidizi wabovu naye mbovu pia.