Geza Ulole
JF-Expert Member
- Oct 31, 2009
- 59,062
- 79,089
5th March 10
Rais Kagame aishutumu Tanzania
Mwandishi Wetu
Rais Paul Kagame wa Rwanda ameituhumu Tanzania kwamba inaruhusu watu wanaoipinga Serikali yake kuendeleza harakati za kuhujumu nchi hiyo.
Akizungumza na waandishi wa habari jijini Kigali juzi na taarifa zake kutangazwa na Shirika la Utangazaji la Uingereza (BBC), Kagame alisema atawasiliana na Tanzania ili watu hao wanaoendesha harakati hizo wakamatwe.
Mbali na Tanzania, Kagame pia aliitaja Kenya na Uganda kwamba kuna watu kama hao wanaoendesha harakati dhidi ya serikali yake, lakini akaapa kwamba kamwe hawataweza kuiangusha serikali yake.
Katika mkutano huo, Kagame pia alimshambulia mshirika wake wa zamani wakati wa mapambano ya kuikomboa Rwanda, Luteni Jenerali Kayumba Nyamwasa ambaye alikuwa balozi wa nchi hiyo nchini India kwamba ni miongoni mwa watu wanaoendesha chokochoko dhidi ya serikali yake.
Alisema Kayumba ambaye alivuliwa ubalozi hivi karibuni na sasa amekimbilia Afrika Kusini kuomba ukimbizi wa kisiasa, kuwa wamekuwa na mawasiliano na aliyekuwa mkuu wa mambo ya usalama Luteni Jenerali Patrick Kalegeya katika mipango yao ya kuhujumu Rwanda.
Majenerali hao wote walikuwa washirika wa Kagame lakini sasa wamekimbia nchi kutokana na kutofautiana na Rais huyo huku wakimtuhumu kwa kuendesha nchi kidikteta.
Alimtaja Kayumba kwamba alihusika na mashambulizi ya maroketi jijini Kigali hivi karibuni na kwamba ataiomba Afrika Kusini kumrejesha nyumbani kwa ajili ya kujibu tuhuma zinazomkabili.
Akijibu tuhuma dhidi yake, Jenerali Kayumba alisema kwamba Rwanda inazidi kuzama katika utawala wa kidikteta na kumtaja Rais Kagame kama mtu asiyetaka kukosolewa na yeyote.
Jenerali Kayumba ambaye amekwisha kupata hifadhi ya ukimbizi wa kisiasa Afrika Kusini, alisema Rais huyu anataka watu wa kumlamba miguu kumzunguka lakini si watu wanaoweza kutoa mawazo yao.
Madaraka yasiyokuwa na mipaka huporomoka vivyo hivyo, nchi haiwezi kuendeshwa na mawazo ya mtu mmoja tu huku akipingana na wale wenye mawazo tofauti, alisema Jenerali Kayumba.
Kadhalika, Jenerali Kayumba alikanusha vikali kuhusika na mashambulizi ya Kigali ya hivi karibuni na kusema yalipangwa na serikali ya Kagame mwenyewe kwa nia ya kuwapakazia watu asiowataka.
Rais Kagame alisema Mwendesha Mshitaka Mkuu wa Serikali, Martin Ngoga, hivi karibuni aliwataja Jenerali Kayumba na Jenerali Karegeya kuwa ndio waliopanga mashambulizi hayo.
Wakati Wanyarwanda wakilumbana kuhusu mashambulizi ya Kigali ya hivi karibuni, Nipashe iliwasiliana na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bernard Membe, juu ya Tanzania kutuhumiwa na Rwanda, lakini alisema yuko safarini Cairo, Misri.
Hata hivyo, alisema kwamba bado serikali hajaipata taarifa rasmi za malalamiko ya Rais Kagame ili iyatazame na kuyatolea tamko.
Hata hivyo, Membe alisema Tanzania wakati wote imesema wazi kwamba haifanyi wala kuunga mkono kitendo chochote cha kuhujumu nchi jirani katika ardhi yake.
Membe alisema Tanzania ilikwisha kutoa msimamo wake wakati taarifa za kuhujumiwa kwa Rwanda zilipotolewa na maofisa wa Umoja wa Mataifa na kuitaja serikali kusaidia waasi wa Rwanda na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC), kwa kusisitiza kwamba imejitolea kwa nguvu zake kuhakikisha kwamba amani inarejea katika ukanda wa Maziwa Makuu.
Ni jambo lisiloingia akilini kusema kwamba Serikali ya Tanzania inaweza kupanga mkakati au kutoa msaada kwa kikundi chochote kinachokusudia kuvuruga amani katika ukanda huu, alisema Membe ambaye aliahidi kutoa taarifa zaidi akishawasiliana na ofisi yake.
NIPASHE
Rais Kagame aishutumu Tanzania
Mwandishi Wetu
Rais Paul Kagame wa Rwanda ameituhumu Tanzania kwamba inaruhusu watu wanaoipinga Serikali yake kuendeleza harakati za kuhujumu nchi hiyo.
Akizungumza na waandishi wa habari jijini Kigali juzi na taarifa zake kutangazwa na Shirika la Utangazaji la Uingereza (BBC), Kagame alisema atawasiliana na Tanzania ili watu hao wanaoendesha harakati hizo wakamatwe.
Mbali na Tanzania, Kagame pia aliitaja Kenya na Uganda kwamba kuna watu kama hao wanaoendesha harakati dhidi ya serikali yake, lakini akaapa kwamba kamwe hawataweza kuiangusha serikali yake.
Katika mkutano huo, Kagame pia alimshambulia mshirika wake wa zamani wakati wa mapambano ya kuikomboa Rwanda, Luteni Jenerali Kayumba Nyamwasa ambaye alikuwa balozi wa nchi hiyo nchini India kwamba ni miongoni mwa watu wanaoendesha chokochoko dhidi ya serikali yake.
Alisema Kayumba ambaye alivuliwa ubalozi hivi karibuni na sasa amekimbilia Afrika Kusini kuomba ukimbizi wa kisiasa, kuwa wamekuwa na mawasiliano na aliyekuwa mkuu wa mambo ya usalama Luteni Jenerali Patrick Kalegeya katika mipango yao ya kuhujumu Rwanda.
Majenerali hao wote walikuwa washirika wa Kagame lakini sasa wamekimbia nchi kutokana na kutofautiana na Rais huyo huku wakimtuhumu kwa kuendesha nchi kidikteta.
Alimtaja Kayumba kwamba alihusika na mashambulizi ya maroketi jijini Kigali hivi karibuni na kwamba ataiomba Afrika Kusini kumrejesha nyumbani kwa ajili ya kujibu tuhuma zinazomkabili.
Akijibu tuhuma dhidi yake, Jenerali Kayumba alisema kwamba Rwanda inazidi kuzama katika utawala wa kidikteta na kumtaja Rais Kagame kama mtu asiyetaka kukosolewa na yeyote.
Jenerali Kayumba ambaye amekwisha kupata hifadhi ya ukimbizi wa kisiasa Afrika Kusini, alisema Rais huyu anataka watu wa kumlamba miguu kumzunguka lakini si watu wanaoweza kutoa mawazo yao.
Madaraka yasiyokuwa na mipaka huporomoka vivyo hivyo, nchi haiwezi kuendeshwa na mawazo ya mtu mmoja tu huku akipingana na wale wenye mawazo tofauti, alisema Jenerali Kayumba.
Kadhalika, Jenerali Kayumba alikanusha vikali kuhusika na mashambulizi ya Kigali ya hivi karibuni na kusema yalipangwa na serikali ya Kagame mwenyewe kwa nia ya kuwapakazia watu asiowataka.
Rais Kagame alisema Mwendesha Mshitaka Mkuu wa Serikali, Martin Ngoga, hivi karibuni aliwataja Jenerali Kayumba na Jenerali Karegeya kuwa ndio waliopanga mashambulizi hayo.
Wakati Wanyarwanda wakilumbana kuhusu mashambulizi ya Kigali ya hivi karibuni, Nipashe iliwasiliana na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bernard Membe, juu ya Tanzania kutuhumiwa na Rwanda, lakini alisema yuko safarini Cairo, Misri.
Hata hivyo, alisema kwamba bado serikali hajaipata taarifa rasmi za malalamiko ya Rais Kagame ili iyatazame na kuyatolea tamko.
Hata hivyo, Membe alisema Tanzania wakati wote imesema wazi kwamba haifanyi wala kuunga mkono kitendo chochote cha kuhujumu nchi jirani katika ardhi yake.
Membe alisema Tanzania ilikwisha kutoa msimamo wake wakati taarifa za kuhujumiwa kwa Rwanda zilipotolewa na maofisa wa Umoja wa Mataifa na kuitaja serikali kusaidia waasi wa Rwanda na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC), kwa kusisitiza kwamba imejitolea kwa nguvu zake kuhakikisha kwamba amani inarejea katika ukanda wa Maziwa Makuu.
Ni jambo lisiloingia akilini kusema kwamba Serikali ya Tanzania inaweza kupanga mkakati au kutoa msaada kwa kikundi chochote kinachokusudia kuvuruga amani katika ukanda huu, alisema Membe ambaye aliahidi kutoa taarifa zaidi akishawasiliana na ofisi yake.
NIPASHE