Rais Kagame 2019 tu alisafiri nje mara 59. Leo safari 9 tu za nje za Rais Samia kelele kila kona. Je, ni Ushamba?

CM 1774858

JF-Expert Member
May 29, 2021
4,980
4,075
Rais Paul Kagame wa Rwanda mwaka 2019 tu alisafiri nje mara 59 | Rais Samia wa Tanzania Safari 9 tu nje Wazalendo kelele kila kona, Je, Ni ushamba, Uzalendo, Wivu au roho Mbaya Tu.
______

Minong'ona inayoendelea juu ya Safari za Rais Samia nje si za kupuuzwa zinahitaji Ufafanuzi zaidi tena kwa mifano halisia,

Hoja za kubishaniwa ni Mbili tu
1. Ziara za Rais zinafuja pesa ya Umma
2. Ziara za Rais zinafungua nchi

Nimekupa jumla ya ziara za rais wa nchi inayopigiwa mfano kwa maendeleo ya kasi zaidi barani Africa iliyoko Africa Mashariki yaani RWANDA

UWEKEZAJI WA NJE RWANDA (FDI)
______________

Tuangalie uwekezaji wa nje FY2018|19

Mwaka 2017|18 Uwekezaji wa nje wa Rwanda yaani FDI ulifikia $ 0.382BL sawa na Tshs 840.2BL

Tuangazie pia uwekezaji Wa nje FY2018|19
• Mwaka 2018|19 Wakati Rais Kagame anaenda nje X59 nchi ya Rwanda ilipokea uwekezaji toka nje ( Foregh Direct Investment -FDI wa $ 0.91BL karibu sawa na Tshs 2trilioni, hii ni sawa na ongezeko la uwekezaji wa nje kwa Tshs 1.2trilioni ambazo ni sawa na 143%,
Inaitwa the more You go the more You get.

||Kagame Safari 59, faida ya Safari ni uwekezaji wa Tshs 1.2trl ,Je Safari ni faida au hasara?! Jibu waambie na wenzako wanaopinga ziara za Rais nje

• Pamoja na CORONA, Mwaka 2018|19 Wakati wawekezaji wakikimbilia kuwekeza kwenye kanchi kenye watu wasiozidi 12M Sisi Tanzania wenye watu zaidi 60m tuliambulia uwekezaji wa nje yaani FDI ya $1.1BL karibu Tshs 2.2trilioni na hawa niwale waliojilita wenyewe tu,

• Nchi yenye ukubwa kama mkoa wa Tabora inapata uwekezaji karibu sawa na Tanzania,Shida ilikuwa nani awafuate wawekezaji, Mwekezaji akifuatwa na Rais wa nchi anakuwa na assurance kubwa kuliko akifuatwa na Waziri,Kwa Ufafanuzi huu wanaopenda kuelewa mtakuwa mmeelewa umuhimu wa ziara za Rais nje ya nchi

• Nimwenye roho ya kimasikini tu ndio anawaza gharama za rais kusafiri nje badala ya kuwaza uwekezaji wa matrilioni na mabilioni tutakaoupata kama matokeo ya ziara za Rais nje,Ukitaka kula lazima uliwe in JK voice

Yule hakutoka ndio maana tulipata kiduchu | Huyu anatoka kama wenzake mwacheni tutapata chochote kitu



IMG-20210918-WA0036.jpg


VIVA TANZANIA VIVA || VIVA SAMIA VIVA
 
Achana na ukumbwa wa nchi kieneo,

Rwanda inafanya vizuri sana katika areas nyingi kuizidi Tanzania,

Kwenye uwekezaji wanatuzidi mbinu ndio maana leo wao wanatengeneza mpaka magari,

Rais aachwe akatafute wawekezaji nje,

_____________________________________
R
Tanzania kuifananisha na Rwanda kwa vyovyote vile, ni kutuvunjia heshima, na nidharau na kejeli kwa CCM chama tawala toka tupate Uhuru.
 
Kwahiyo PK ndio standard mnayotumia kulinganisha mambo ya uongozi? Tanzania ni nchi tofauti na Rwanda.

Usiwabeze hawa watanzania ambao wanapevuka kila uchao kuhusu mustakabali wa nchi yao, kwa kutoa mifano ambayo ni irerevant.

Rais kusafiri kuna sababu za umuhimu. Ni bora kutoa elimu kwa wanaohoji kuliko kutoa hii mifano mfu
 
Unaelewa maana ya hii,

Hii Rwanda tusiichukulie poa kabisa,
Tuache Rais afungue nchi,


QUOTE="CM 1774858, post: 40269491, member: 635023"]




QUOTE="Tangawizi, post: 40269425, member: 16913"]
Kwahiyo PK ndio standard mnayotumia kulinganisha mambo ya uongozi? Tanzania ni nchi tofauti na Rwanda. Usiwabeze hawa watanzania ambao wanapevuka kila uchao kuhusu mustakabali wa nchi yao, kwa kutoa mifano ambayo ni irerevant.
Rais kusafiri kuna sababu za umuhimu. Ni bora kutoa elimu kwa wanaohoji kuliko kutoa hii mifano mfu
[/QUOTE]
[/QUOTE]
 

Similar Discussions

17 Reactions
Reply
Back
Top Bottom