nzagambadume
JF-Expert Member
- Apr 9, 2018
- 2,430
- 5,769
Inaonekana anatumiwa na mabeberu kukushushia credibillity kwa wanyonge.
Wewe ushafanya utafiti kabla ya maamuzi kwamba tunaweza KULIPA, KUSAFIRISHA AU KUBANGUA KOROSHO WENYEWE
Ulisema, hela tayari zipo benki ya wakulima, zishaingizwa.
Ulisema ikibidi wanjeshi hata kwa meno watabangua. Nchi hiii tayari kwa miaka 3 imejenga viwanda 3,000, tani 295,000 sio kitu kwetu
Ulikagua magari ya jeshi ukachungulia hadi uvunguni, ukatoa speech ya kishujaa kabisa, ukawatuma vijana kwenda mtwara na lindi KUPIGANA VITA YA KIUCHUMI.
Mheshimiwa Rais, ukikubali hili la huyu waziri anayetumiwa na mabeberu ina maana Kangomba watarudi tena, heshima yako itashuka sana na mabeberu watakuwa wanajua kumbe unatikisika kwa issue ndogo. Mbaya zaidi kwa mara ya kwanza JWTZ itakuwa imeshindwa vita katika historia yake na heshima ya CDF Mabeyo itashuka vibaya mnoooo maana ni juzi tu alitoa meli ikapigane vita hiyo ya kiuchumi kwa kubeba mzigo wa korosho.
Usikubali baba, endelea kukandamiza wanyonge wa kusini mtwara na lindi wanakukubali sana hadi walipiga magoti kwa yule mkuu wa mkoa.
Wewe ushafanya utafiti kabla ya maamuzi kwamba tunaweza KULIPA, KUSAFIRISHA AU KUBANGUA KOROSHO WENYEWE
Ulisema, hela tayari zipo benki ya wakulima, zishaingizwa.
Ulisema ikibidi wanjeshi hata kwa meno watabangua. Nchi hiii tayari kwa miaka 3 imejenga viwanda 3,000, tani 295,000 sio kitu kwetu
Ulikagua magari ya jeshi ukachungulia hadi uvunguni, ukatoa speech ya kishujaa kabisa, ukawatuma vijana kwenda mtwara na lindi KUPIGANA VITA YA KIUCHUMI.
Mheshimiwa Rais, ukikubali hili la huyu waziri anayetumiwa na mabeberu ina maana Kangomba watarudi tena, heshima yako itashuka sana na mabeberu watakuwa wanajua kumbe unatikisika kwa issue ndogo. Mbaya zaidi kwa mara ya kwanza JWTZ itakuwa imeshindwa vita katika historia yake na heshima ya CDF Mabeyo itashuka vibaya mnoooo maana ni juzi tu alitoa meli ikapigane vita hiyo ya kiuchumi kwa kubeba mzigo wa korosho.
Usikubali baba, endelea kukandamiza wanyonge wa kusini mtwara na lindi wanakukubali sana hadi walipiga magoti kwa yule mkuu wa mkoa.