Rais John Magufuli ndiye sampuli ya Mtanzania mwenye maadili mema

May 3, 2019
53
144
KOMREDI JOHN MAGUFULI, NDIYE SAMPULI YA MTANZANIA MWENYE MAADILI MEMA

Leo 15:15pm,15/09/2019.

Komredi Rais John Magufuli ndiye muungwana na mstaarabu anayefuata mambo mema yaliyokubaliwa katika jamii, naamini ndiye Kiongozi mwenye kuita koleo ni koleo na kijiko ni kijiko, ndiye mwenye kutoa elimu ya mema na mabaya.

Maadili mema yanayooneshwa na Komredi, Rais John Magufuli vinatoa elimu kubwa kwa uzao ujao wa Uongozi na Uzao wa kizalendo utakaolinda heshima ya Taifa la Tanzania kimaadili na kulifanya Taifa kubwa.

Mwenendo mwema wa Rais John Magufuli umepigiwa mfano bora kulingana na kanuni na taratibu zetu Watanzania katika jamii zetu, katika sekta mbalimbali na taasisi binafsi na Serikali, Komredi John Magufuli amekuwa kipimo sawia cha yeyote atakaye kufanya jambo ili kupata matokeo chanya.

Katika nguzo kuu ya Utamaduni wa Mtanzania, katika mila, desturi, sanaa, lugha, Elimu, Michezo, tiba, ulinzi, ujuzi, mavazi, Ngoma, utani, imani, na itikadi katika taasisi mbalimbali za kiasili na kisiasa,hivi vyote vinasimama katika mhimili wa maadili na nguzo ya kifalsafa ya uadilifu.

Komredi Rais John Magufuli ameonyesha uadilifu mkubwa katika kulitumikia Taifa la Tanzania, ameweza kuchagua lipi ni jema na kuwafanyia Watanzania hata kama likiwa halionekani katika macho ya wengi. Komredi John Magufuli ndiye kiongozi pekee mwenye kuchagua yaliyo mema kwa manufaa ya Taifa zima la Tanzania.

-Falsafa ya imani,nguvu na hamasa.

Maadili hujengwa kwa mtu kupitia hatua mbalimbali,hatua ya kwanza ya msingi ni malezi ya utotoni kutoka kwa Wazazi na jamii inayokuzunguka, baadae shuleni na kuendelea hadi uzeeni. Familia bora zinatoa Watanzania wenye malezi bora kabisa na ya kizalendo kwa nchi yao, watanzania wataozaliwa katika familia yenye malezi bora, utupatia ujumbe mzuri wa malezi bora na ya kizalendo kupitia hotuba zao pindi wahutubiapo hadhara mbalimbali.

Raia mwema wa Tanzania ni yule aliyelelewa vyema na wazazi na jamii inayomzunguka na kuwa na nidhamu,tabia njema,kuwa mkweli,mwenye utii na kufuata taratibu za utamaduni wa Mtanzania.

Raia wa Tanzania tunategemea awe mwaminifu na mwenye kufanya mambo kwa haki,kwa maana ya kutopendelea au kukiuka sheria, kanuni na taratibu zilizowekwa. Daima, Mtanzania ni mwenye kufanya kazi za halali, kwa bidii, kwa haki, bila unyanyasaji au upendeleo, kushiriki kazi za kujenga taifa, kuhimiza upendo,mshikamano na amani ambayo hutokana na kutoelewana.

Daima Mtanzania anapaswa kuwa mvumilivu na mwenye hulka ya kuheshimiana, Mtanzania ni yule aliyelelewa kutobagua wengine kwa misingi ya kabila, dini, jinsi, au rangi mambo ambayo Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Nyerere na Komredi John Magufuli wanayasisitiza na kuyaishi.

-Maadili ya Mtanzania yanaendelezwa vyema na Komredi John Magufuli.

Kama nilivyoitaja misingi ya maadili ya Mtanzania ambayo inapaswa kulindwa,kuendelezwa na kuenziwa,ni lazima kutambua na kuendeleza,mila na desturi yetu sisi Watanzania kama ilivyosisitizwa na Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Nyerere. Kuthamini elimu na mafunzo, wakati wa Mwalimu tulipata mafunzo toka Jkt,Vyuo vya Uongozi kama hombolo,na mashamba darasa katika kilimo.

Tunapaswa Kuthamini tunu zetu za asili kama tamaduni zetu ambazo hazina mambo ya kutweza utu wa mtu au kumkufuru Mwenyezi Mungu.Uzalendo ukawe wa kwanza katika maisha yako, kuilinda nchi yako na kutimiza itikadi ya Afrika ni moja na Waafrika wote ni ndugu zangu.

Kuthamini na kutunza rasilimali za taifa, kukataa kutoa na kupokea rushwa, kutii sheria, kanuni, na taratibu zilizowekwa, kuthamini utu na kulinda maisha ya binadamu wengine.

Uvaaji wa mavazi ya heshima yenye kusitiri miili yetu, lugha safi, kuwa na heshima kwa wakubwa na wadogo, kusaidia watu wenye mahitaji, kuthamini na kutunza mazingira yanayoizunguka Tanzania, haya yote ni maadili ya Mtanzania.

-Maadili ya Mtanzania huonekana katika mambo ya kijamii

Mavazi, lugha, kufanya kazi kwa bidii na ushirikiano, kudumisha mila na desturi, ukarimu, upendo, heshima, na nidhamu, haya ni mambo yanaweza kuonyesha wewe ni mwenye maadili ya Kitanzania.

Mila na desturi ni pamoja na kusalimia wakubwa kwa adabu na heshima,haya ni mazoea katika jamii,lakini yana maana kubwa sana kwa maana aliyeanza kuona jua basi ameona mengi ambayo kwa mdogo yanapaswa kuwa darasa tosha.

Mila na desturi zimebeba hazina kubwa ya maadili ya Mtanzania, utandawazi,kasumba ya kuiga si maadili ya Mtanzania, Maadili ya Mtanzania ni kupendana kama ndugu, kuheshimiana, kukirimiana ili kuondoa chuki zilizosababishwa na ukoloni, hivyo basi kwa kumbukumbu nzuri ya maadili ya Mtanzania, na kwa kumpata Rais John Magufuli ambaye amekuwa mfano bora wa Mtanzania mwenye maadili mema, basi na turudi kwenye mstari wa maadili ya Mtanzania ili tuweze kulipeleka mbele taifa letu la Tanzania.

Nimalizie kwa kusema Utanzania ni alama ya maadili mema yaliyokubaliwa katika jamii,Tunamshukuru Mungu kwa kutupatia Komredi, Ndugu, Daktari John Magufuli kama Rais wetu ambaye anaenenda na kutenda sawa sawa na utanzania yaani maadili ya Mtanzania yaliyokubaliwa katika jamii yetu sisi Watanzania, Ahsante Mungu kwa kuibariki Tanzania, Ahsante Mwenyezi Mungu kwa kumbariki Rais John Magufuli.

Nikiishia hapa, Mimi ni,
Msemakweli Chakubanga.
Dar es Salaam.
0755078854.
 
Mstari wa mwisho ndo lilikuwa lengo lako, wamekuona subiri kupigiwa usizime Simu.

Maadili ya kitanzania yanayonyanyasa familia hadi wakosoaji wa kisiasa na kijamii ndo maadili mapya haya. Ongea yote lakini usihusishe maadili mema ya Kitanzania na mambo ya kijinga.
 
SGR, Ndege, Barabara, Mafisadi, Uchumi Wa Kati, 50 Millions, Tembeeni Kifua Mbele,
Hakika Tulichelewa Kumpata Rais Wa Jamhuri Ya Muungano Wa Tanzania
 
Kwa msisitizo 0755078854. Ni mwendo wa kuchomoa tu betri awamu hii! Hakuna namna, unaweza ukashangaa mtu anakumbukwa hivi hivi kwenye hizi teuzi na tumbua tumbua zisizoisha!
 
Nyuzi za watu wenye njaa na mbumbumbu kama hawa ndo zinanipotezea stimu ya JK. Acha niendee jukwaa la love connect kuliko kusoma upuuzi wa vibaraka njaa wa mzee meko
 
Unaweka namba zako ili nini!? acha tabia za kishoga na kujipendekeza wewe kwa wenye madaraka..utaolewa wewe na familia yako
 
Yaani watu kupotea, kutekwa, kuuawa, kupotezwa, kuminya demokrasia, kuzuia uhuru wa habari, mikutano ya kisiasa, kubana vyombo vya habari, kuteka wakosoaji wa serikali, kuua uchumi, biashara, uwekezaji, mahusiano ya kidiplomasia ya kimataifa, kushindwa kuajiri, kuongeza mshahara, kupandisha madaraja, kuharibu mzunguko wa fedha ndio maaadili mema?
 
Comment yako inaendana kabisa na akili yako
nyuz za watu wenye njaa na mbumbumbu kama hawa ndo zinanipotezea stimu ya jf..acha niendee jukwaa la love connect kuliko kusoma upuuzi wa vibaraka njaa wa mzee meko
 
UPUUZI MTUPU! Tangu lini mzinzi, mwizi, fisadi, anayekiuka taratibu mbali mbali, mtekaji, mtesaji na MUUAJI akawa ana MAADILI MEMA!?
 
Back
Top Bottom