Rais JK ajiandikisha kwenye daftari la wapiga kura Msoga

Lucchese DeCavalcante

JF-Expert Member
Jan 10, 2009
5,471
734
8D6U7669.JPG


Rais Jakaya Kikwete akijiandikisha kupiga kura kwenye kituo kipya cha kupigia kura kijijini kwake Msoga,wilayani Bagamoyo. Pembeni akiangalia ni msimamizi wa kituo cha kuandikisha wapiga kura cha Msoga Bi.Diana Fredrick. Kituo cha zamani cha Rais Kikwete kilikuwa Bwilingu, Kata ya Chalinze, wilayani Bagamoyo. Mama Salma Kikwete pia alijiandikisha kupiga kura kwenye daftari hilo la kudumu la wapiga kura kijijini hapo.

8D6U7737.JPG


Rais Jakaya Kikwete na Mama Salma Kikwete wakikagua kwa makini vitambulisho vyao vipya vya kupiga kura walipojiandikisha katika daftari la kudumu la wapiga kura na kupatiwa vitambulisho vipya huko kijijini Msoga wilayani Bagamoyo.Kushoto ni msimamizi wa kituo hicho cha wapiga kura Msoga Bi.Diana Fredrick.


Source: MichuziJr Blog.
 
Ni haki yake kikatiba...... ila nina wasiwasi km Bi.Diana Fredrick jinsi anavyoonekana kama kweli aweza simamia haki hata kama matokeo ya kura kituo hicho yanaonyesha ushindi mkubwa upande wa upizani???
 
Kazi nzuri Rais wetu na pia itakuwa vizuri sana kama uchaguzi ukiwa huru na haki kwa vyama vyote vya siasa Tanzania
 
Rais Jakaya Kikwete (pichani) na mkewe, Salma, wamejiandikisha kama wapiga kura katika kijiji cha kwao cha Msoga, Wilaya ya Bagamoyo, Mkoa wa Pwani.
Rais Kikwete na Mama Salma Kikwete waliwasili kwenye kituo cha kuandikisha wapiga kura cha Shule ya Msingi Msoga, kijiji cha Msoga, juzi asubuhi na kupokelewa na msimamizi wa kituo hicho, Diana Frederick.
Kwenye uchaguzi mkuu uliopita, Rais Kikwete na Mama Salma walipiga kura kwenye mji mdogo wa Chalinze wilayani Bagamoyo.
Rais Kikwete na Mama Salma walijiandikisha katika kituo kipya kufuatia kuanza kwa zoezi la uboreshaji wa Daftari la Wapiga Kura kwa Kanda ya Mashariki.
Uboreshaji wa Daftari la Wapigaji Kura kwa Kanda ya Mashariki ulianza Jumatatu, na umepangwa kumalizika kesho. Rais Kikwete alirudia tena wito wake kwa wananchi wenye sifa za kupiga kura kutumia nafasi ya uboreshaji wa daftari la wapiga kura kwa kujiandikisha kwa mara ya kwanza kama wapigaji kura, na kwa wale waliopoteza shahada zao kujiandikisha upya, ili wapate sifa za kutumia haki yao ya kupiga kura katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka huu.

CHANZO: NIPASHE
 
Mh Rais alishajiandikisha kwenye kituo cha Bunge Primary school! Sasa anapojiandikisha tena huko Msoga inakaaje hii! Hivi si kosa kujiandisha mara mbili?
 
Mh Rais alishajiandikisha kwenye kituo cha Bunge Primary school! Sasa anapojiandikisha tena huko Msoga inakaaje hii! Hivi si kosa kujiandisha mara mbili?
Wakati ule alijiandikisha kwa ajili ya uchaguzi wa serikali za mitaa, ni tofauti na uchaguzi mkuu
 
Back
Top Bottom