Rais Jammeh wa Gambia awafuta kazi mabalozi wake 12

shige2

JF-Expert Member
Oct 11, 2016
8,106
3,967
Kweli msemo unaosema Siku zikikaribia za nyani kufa kila mti HUTELEZA. Inasemekana kuwa rais Jammeh wa Gambia amewafukuza kazi mabalozi wake 12 waliokuwa wakiwakilisha nchi za nje.

Inasemekana walimwandikia barua ya kumwambia AMWACHIE madaraka MPINZANI wake Adama Barrow aliyemshinda katika uchaguzi ulifanyika hivi karibuni.

Pia inasemekana walimpongeza mpinzani wake jambo ambalo lilimkasirisha rais Jammeh.
Pamoja na pigo jingine, kesi aliyokuwa amepeleka mahakamani kupinga uchaguzi majaji wawili kutoka Nigeria na Siera Leoni HAWAKUHUDHURIA.

Na tayari Mkuu wa sheria Emmanuel F. ameiahirisha kesi hii mpaka kati ya Mwezi wa 5 na wa11 mwaka huu. Na hivyo kumpa rais Jammeh PIGO KUBWA kisiasa!

Sijui Jammeh atang'ang'ania madaraka ama majes
hi ya jumuia ya ECOWAS watamtoa kwa nguvu ama ATAACHIA kwa HIARI?
Chanzo: Gambia Daily Mail
 
Hivi haka ka nchi kana ubavu wowote kijeshi ....kweli
 
Hivi haka ka nchi kana ubavu wowote kijeshi ....kweli
Hakana nchi yenyewe jumla ya watu wote ni chini ya milioni mbili. Jeshi lao dogo, mfano hawana Jeshi la anga. Ndio maana ECOWAS wameipa senegal tu kumuadabisha huyo Yahya. Khaaaaaa
 
Bro. Dont undermine the power of any sovereign state in this world.......
Sawa kaka lakini sio Gambia bhana! An embryo inside the womb of Senegal; a naval blockade of the sea front and the capital Banjul is enough for Jameh to flee and the army to surrender!
 
Sawa kaka lakini sio Gambia bhana! An embryo inside the womb of Senegal; a naval blockade of the sea front and the capital Banjul is enough for Jameh to flee and the army to surrender!
As simple as you have just put it.
And the guy anakimbia yeye mwenyewe!!
 
  • Thanks
Reactions: MTK
Asipokabidhi madaraka tar 19 basi ataondolewa na Jeshi la Gambia. Ndivyo nionavyo mimi!
 
Back
Top Bottom