Rais Jakaya Kikwete apigwa picha upya kwa matumizi ya kiserikali

Mtu wa Pwani

JF-Expert Member
Dec 26, 2006
4,184
671
Rais Jakaya Kikwete apigwa picha upya kwa matumizi ya kiserikali Na Mwandishi Wetu

SERIKALI imebadilisha picha ya Rais Jakaya Kikwete iliyokuwa ikitumika katia shughuli za kiserikali (Official Portrait)


Akizungumza na waandishi wa habari jijini jana, Mkurugenzi wa Idara ya Habari (Maelezo), Kassim Mpenda alisema serikali imeamua kubadilisha picha hiyo baada ya kupata ushauri kutoka kwa wataalam mbalimbali wa masuala ya picha.


Mpenda alisema wataalam hao walishauri kuwa picha iliyopigwa baada ya kumalizika kwa Uchaguzi Mkuu wa Rais mwaka 2005, haifai kwa matumizi kwa kuwa wakati huo, rais alikuwa anakabiliwa na uchovu na mawazo ya kuanza kazi hiyo mpya.


Alifafanua kuwa picha hiyo, ilikuwa haionyeshi sura halisi ya sura ya Rais kwa kuwa ilionyesha msongo wa mambo mbalimbali.


''Picha hiyo ilipiga mwaka 2005 mara tu baada ya Tume ya Uchaguzi kumtangaza kuwa ndiye mshindi wa urais; Hivyo kipindi hicho bado alikuwa na msongo na mavune (stress & strain) ya kampeni za uchaguzi wa mwaka huo,'' alifafanua Mpenda.


Mpenda alisema Rais Kikwete alilazimika kupiga picha katika kipindi hicho kwa kuwa ilikuwa inahitajika haraka kwa ajili ya matumizi mbalimbali ya ofisi, ikiwemo mahakama ambayo haziwezi kufanya kazi bila kuwepo kwa picha ya rais.


''Ofisi mbalimbali za serikali na hasa mahakama zinapofanya kazi zake ni lazima iwepo picha ya rais na picha ya Baba wa Taifa mbele. Tunamshukru sana aliyeipiga picha hiyo, lakini sasa tumeamua kuibadilisha,'' alisema Mpenda.


Mpenda alisema picha ya sasa ambayo imepigwa na mpiga picha, Zahur Ramji ni bora kwa kuwa inaonyesha sura halisi ya Rais Kikwete.


Alisema picha hiyo itaanza kuuzwa na Idara ya Habari Maelezo kwa wizara, wakala na mashirika ya serikali kuanzia juma la kwanza la Julai, mwaka huu kwa Sh15,000 na kwamba watu binafsi wataanza kuuziwa baadaye kuwa sababu, kwa sasa wamechapisha nakala chache.

source: mwananchi
 
Mpenda alisema Rais Kikwete alilazimika kupiga picha katika kipindi hicho kwa kuwa ilikuwa inahitajika haraka kwa ajili ya matumizi mbalimbali ya ofisi, ikiwemo mahakama ambayo haziwezi kufanya kazi bila kuwepo kwa picha ya rais.

Ninashauri tubadilishe utaratibu huu. Mahakama kama bunge ni mhimili mwingine wa serikali unaotakiwa kujitegemea. Ni muhimu vyombo vya mahakama na bunge viwe vinatumia coat of arms (ngao ya adam na eva) na bendera ya taifa tu, siyo sura ya rais; Vile vile kila kimoja kinatakiwa kuwa na nembo yake. Picha ya raisi iwe inatumika katika ofisi za serikali zinazonfaya kazi chini ya executive branch tu.
 
Kweli hii kali!

Option 1.....

Yani anataka kujifanya anazaliwa UPYA?

ANAWAPA ISHARA WANAMTANDAO KUWA ANA WACHENJIA?

AMA NA YEYE NI MWANAMTANDAO NA WANATUZUGA!

SURA YA FISADI NI YA FISADI TU!

Haya mambo yanayoendelea ni kama hints wanapeana hapa!
Kuna watu wake ana wabeep kuwa he is gonna change his face!?

Option 2....Mbinu ya kuanza kujikita kwenye mazungumzo ya wananchi kwani kila mtu anaimba...KIKWETE FISADI...KIKWETE FISADI!

NB:KIKWETE ACHANA NA MAMBO YA KUPIGA PICHA!
KAMATA MAFISADI MARA MOJA!
 
Au Ana Wabeep Wanamtandao Waliompiga Hiyo Picha?
Eti Uchovu!
Uchovu Toka 2005 Aliposhinda Uraisi KWA MSAADA WA WANAMTANDAO NA EPA?
 
Watuletee Habari Za Kina Slaa,mwakyembe Bana Wasilete Habari Za Picha Za Kikwete!

Jamaa Kamiss Safari Nini?
Maana Kama Ni Picha Keshapigwa Nyingi Tu!

Kila Pahala!
Marekani, KENYA, japani,china, scandnavia, uk, Everywhere You Name It.

Waache Utani Bana Bunge Lina Muda Hadi Ijumaa Na Baada Ya Hapo..changa La Macho!
 
Rais Jakaya Kikwete apigwa picha upya kwa matumizi ya kiserikali Na Mwandishi Wetu

SERIKALI imebadilisha picha ya Rais Jakaya Kikwete iliyokuwa ikitumika katia shughuli za kiserikali (Official Portrait)


Akizungumza na waandishi wa habari jijini jana, Mkurugenzi wa Idara ya Habari (Maelezo), Kassim Mpenda alisema serikali imeamua kubadilisha picha hiyo baada ya kupata ushauri kutoka kwa wataalam mbalimbali wa masuala ya picha.


Mpenda alisema wataalam hao walishauri kuwa picha iliyopigwa baada ya kumalizika kwa Uchaguzi Mkuu wa Rais mwaka 2005, haifai kwa matumizi kwa kuwa wakati huo, rais alikuwa anakabiliwa na uchovu na mawazo ya kuanza kazi hiyo mpya.

Wakamtengeneze awe kama Michael Jackson, miaka miwili na nusu sasa tangu aingie madarakani, muda wote huu hao 'wataalamu' walikuwa hawajaona kwamba anaonekana mchovu katika hizo picha hadi hivi sasa!!!! Ni gharama nyingine za kifisadi!!!
 
Uharaka wa kupiga picha ulitoka wapi wakati walijua watashinda hata kabla ya kupigwa kura?
 
mambo mengine yamepitwa na wakati na ni uharibifu wa pesa za walipa kodi tuu.
 
Mnakumbuka huyu jamaa hapa chini?...je manajua toafauti za picha hizo mbili?


doe_lg1.jpg
180px-HD-SC-98-07558_Ausschnitt_fcm.jpg
 
Well... you change the picture, you change the man.. wangapi hapa mmewahi kupiga picha mkono mmoja uko kiunoni na mwingine umeonesha bonge la gumba? Sasa picha kama ile kweli utaiweka ofisini..?
 
well... You Change The Picture, You Change The Man.. Wangapi Hapa Mmewahi Kupiga Picha Mkono Mmoja Uko Kiunoni Na Mwingine Umeonesha Bonge La Gumba? Sasa Picha Kama Ile Kweli Utaiweka Ofisini..?

Makubwa!
Yani Kama Wananchi Waki Conclude Kikwete Ni Fisadi...picha Will Change The Man Kuwa Mtakatifu?
 
Masuala ya picha ya rais umepitwa na wakati. Nimeshangaa sana kuona Tanzania mpaka maofisi ya makampuni binafsi wanatundika picha ya rais, eti wanasema ni sheria. Nikauliza sheria ipi, wanashindwa kujibu, this personal cult ended with Nyerere, lakini utakuta makampuni binfasi, mabenki etc wanatundika picha ya rais! It's really disturbing. lazima mbunge yeyote achallenge hii. Sisi hatumtukuzi mtu yoyote, tunamtukuza Mungu tu!
 
Masuala ya picha ya rais umepitwa na wakati. Nimeshangaa sana kuona Tanzania mpaka maofisi ya makampuni binafsi wanatundika picha ya rais, eti wanasema ni sheria. Nikauliza sheria ipi, wanashindwa kujibu, this personal cult ended with Nyerere, lakini utakuta makampuni binfasi, mabenki etc wanatundika picha ya rais! It's really disturbing. lazima mbunge yeyote achallenge hii. Sisi hatumtukuzi mtu yoyote, tunamtukuza Mungu tu!

eti kesi mahakamani haisikilizwi bila kuwepo picha ya rais, hapo kweli tunayo kazi nchi hii
 
wakati ukifika na kuonekana ni suala ambalo linahitaji mabadiliko ni juu ya wabunge kulijadili.

ila kwa sasa hio ni sheria na ni wajibu kuitumikia unaipenda huipendi
 
kikwete_front1.gif


Frankly speaking,

Hii picha ya sasa ya rais iliyopigwa na Freddy Maro kweli haijatulia. Ukiangalia vizuri kama vile Rais wetu hakunyoa hizo mustach zake, akaziacha kidogo pembeni. Alafu kama vile ni refu kwa kenda chini. Hii ni kwa maoni yangu. Sijui hiyo iliyopigwa sasa itakuwaje.

kikwete.gif


kikwete.gif
 
Tender ilitangazwa lini katika gazeti la serikali?
Je ilikuwa ni National Competetive Tender au?
Je malipo ya gharama ni kiasi gani,sababu kupiga picha nyingi za Rais inaweza ikawa imegharimu pesa nyingi nailibidi watumie PPRA katika hili.


Hayo maneno ya Msongo,atakuwa aliyasema Muungwana Mwenyewe,Si mnamfahamu ?

Yaani sababu ya kijinga sana
 
Back
Top Bottom