Jidu La Mabambasi
JF-Expert Member
- Oct 20, 2014
- 15,314
- 24,177
Rais Mwinyi kajazwa upepo.Kwa akili ya kawaida floor 4 zinajengwa miezi 6??
Na haku act proffessionally.
Rais Mwinyi kajazwa upepo.Kwa akili ya kawaida floor 4 zinajengwa miezi 6??
Kakamilisha %ngapi? Maana yake hana uwezo wa kifedha. Ukipewa mradi uwe na fedha siyo kila hatua ulipwe ndo ufanyekazi.Mbona mkandarasi kachukua kias kidogo Cha pesa
Jinga wewe kwani wakati wanampa kadarasi alikuwa mzanzibar, baada ya kuboronga kawa mtanganyika.Kisa contractor ni mtanzania bara..
#MaendeleoHayanaChama
Sent from my SM-A207F using JamiiForums mobile app
Huyu nae Kazi yake ni kukurupuka na kulalamika kila siku 👇View attachment 2294959
Rais wa Zanzibar, Dk Hussein Mwinyi ameifukuza Kampuni ya Ujenzi ya Associated Investment Service Ltd ya Dar es Salaam kufanya kazi Zanzibar kwa kile alichodai haina uwezo.
Pia, alisitisha mkataba wa mkandarasi huyo wa ujenzi wa Shule ya Mtopepo katika Shehia ya Monduli Wilaya ya Magharibi A, Mkoa wa Mjini.
Rais Mwinyi alichukua hatua hiyo jana, baada ya kutembelea ujenzi wa shule hiyo yenye ghorofa tatu.
Kwa mujibu wa mkataba huo ulioanza Februari mwaka huu, ujenzi unatakiwa kukamilika Agosti mwaka huu, lakini bado upo asilimia 35.
“Nimesikitishwa sana, kazi ya miezi sita na sasa inaelekea kwisha lakini hakuna kilichofanyika, huyu mkandarasi hafai, haya sio makubaliano yetu, nasitisha mkataba na aondoke asipewe kazi nyingine Zanzibar,” alisema Dk Mwinyi.
Mbali na mkandarasi huyo, pia Rais Mwinyi alionyesha kuchukizwa na mkandarasi mshauri Kampuni ya Edge Consultancy, akisema ameshindwa kutoa ushauri wake wa kitaalamu, hivyo na yeye hana uwezo kiutendaji.
Pia, aliiagiza Wizara ya Elimu kuwa wakali na iwapo wakiendelea kuwakumbatia na kuwaonea muhali watu wasiokuwa na uwezo mambo yatazidi kuharibika.
Mradi wa ujenzi wa shule hiyo yenye vyumba 41, matundu ya vyoo 44, unagharimu Sh4.5 bilioni na ikikamilika itakuwa na uwezo wa kubeba wanafunzi 3,690, tayari mkandarasi alikuwa amelipwa Sh1.08 bilioni.
Mkandarasi wa mradi huo, Theodory Zani alisema eneo linapojengwa shule hiyo mazingira hayakuwa mazuri.
Katika hatua nyingine, Rais Mwinyi amewataka viongozi na watendaji wa Serikali kuwa wabunifu na kutafuta njia mbadala kutatua kero zinazowakabili wananchi.
Rais Mwinyi alitoa kauli hiyo kwa nyakati tofauti jana, wakati akikagua na kuweka mawe ya msingi katika miradi ya elimu, afya na maji Wilaya ya Kaskazini Magharibi A Mkoa wa Mjini Magharibi.
“Changamoto nyingi zipo ndani ya Serikali, viongozi wetu sio wabunifu kutatua changamoto za wananchi haraka, ukiangalia changamoto nyingi zipo ndani ya serikali, lazima tuwe wepesi,” alisema Rais Mwinyi.
Alisema Serikali inafanya jitihada kubwa kuhakikisha huduma za jamii ambazo zimekosekana na kusababisha kero kwa muda mrefu zinatatulika na kupata majibu.
Chanzo: Mwananchi
Mkandarasi anakopeshwa pesa mwanzo wa mradi tu. Pesa ambayo inarejeshwa kupitia malipo atakayolipwa kwa kazi atakayofanya. Na huu mkopo hapewi mpaka atoe Bond ya benki itakayomhakikishia mwenye mradi kuwa huo mkopo utalipwa.Kakamilisha %ngapi? Maana yake hana uwezo wa kifedha. Ukipewa mradi uwe na fedha siyo kila hatua ulipwe ndo ufanyekazi.
Makandarasi wengi hawajui kutayarisha programu ya kazi. Wanafuata tu maelekezo ya client ili kumridhisha. Unaweza kukuta kuwa huu mradi usingeweza kumalizika ndani ya miezi sita lakini mkandarasi akaahidi kufanya hivyo kwa kuhofia kuukosa mradi.
Aidha, makandarasi hawakagui eneo la mradi ili kujua changamoto zake. Changamoto hizi ni pamoja na upatikanaji wa vifaa na vibarua. Sidhani kama unaweza kupata vibarua kirahisi wa kumwaga zege Zanzibar wakati wa mwezi wa Ramadhani.
Makandarasi hawatoi tahadhari mapema za ucheleweshwaji kutokana na mapungufu ya mshauri ( kuchelewa kupitisha kazi, mapungufu katika michoro, kuchelewesha uandikaji wa certificate ya malipo n.k.), client(kuchelewa kukabidhi eneo la mradi, kuchelewa kupata mkandarasi msaidizi hasa wa umeme, kuchelewesha malipo, kuchelewa kutoa uamuzi wa mambo ya kimkataba n.k).
Matokeo ya haya yote ni mkandarasi kubebeshwa lawama zote, anazostahili na asizostahili.
Amandla...
Mkuu nina uhakika hapo ulipo Hujui mikataba ya Ujenzi.Unamfukuza bila kusikiliza the other side of the story? Pathetic
Hiyo ndio akili ndogo ya watu wengi.Kakamilisha %ngapi? Maana yake hana uwezo wa kifedha. Ukipewa mradi uwe na fedha siyo kila hatua ulipwe ndo ufanyekazi.
Na imani nyingine potofu ni kufikiri unaweza kumfukuza mkandarasi utakavyo. Pamoja na kuwa Rais ametoa agizo lakini mkataba hautasitishwa mpaka pale mwenye mradi ( aliyetajwa kwenye mkataba) amuandikie mkandarasi yq kuvunja mkataba akitoa pia sababu za kuuvunja. Mkandarasi asiporidhishwa na hizo sababu anaweza kuomba arbitration. Kama akiona isiwe shida, atawasilisha madai ya kazi aliyoifanya na gharama nyingine kama zipo ( za kuvunja kambi na kuondoa vifaa vyake vya kufanyia kazi). Hii nayo itakuwa na matatizo kwa sababu anayepaswa kuhakiki hilo deni ni mshauri ambae nae ametimuliwa! Kwa hali hiyo mkandarasi anaweza kwenda Mahakamani na kuweka zuio mpaka atakapolipwa pesa zake.Hiyo ndio akili ndogo ya watu wengi.
Mradi ni wa mwenye Mradi na ndiye anatakiwa kuwa na fedha ya kutosha na kwa wakati kutekeleza fedha.
Ni wale wajinga tu wanaofikiri unaweza kumlipa mkandarasi wakati uupendao, tena kwa kuchelewa , halafu kazi iende mwa kasi aipendayo!
Mkuu umelidadavua vyema ili vilaza na wanasiasa waweze kuelewa kile wanachokifanya na madhara yake.Na imani nyingine potofu ni kufikiri unaweza kumfukuza mkandarasi utakavyo. Pamoja na kuwa Rais ametoa agizo lakini mkataba hautasitishwa mpaka pale mwenye mradi ( aliyetajwa kwenye mkataba) amuandikie mkandarasi yq kuvunja mkataba akitoa pia sababu za kuuvunja. Mkandarasi asiporidhishwa na hizo sababu anaweza kuomba arbitration. Kama akiona isiwe shida, atawasilisha madai ya kazi aliyoifanya na gharama nyingine kama zipo ( za kuvunja kambi na kuondoa vifaa vyake vya kufanyia kazi). Hii nayo itakuwa na matatizo kwa sababu anayepaswa kuhakiki hilo deni ni mshauri ambae nae ametimuliwa! Kwa hali hiyo mkandarasi anaweza kwenda Mahakamani na kuweka zuio mpaka atakapolipwa pesa zake.
Aidha, kama mshauri ndie aliyetarisha michoro inabidi kibali chake ili michoro yake iendelee kutumiwa na huyo mshauri mpya unless mkataba wake na mwenye mradi umetoa haki miliki ya michoro kwa mshitiri.
Baada ya kuweka yote haya sawa inatakiwa apatikane mkandarasi mwingine wa kuimalizia kazi. Huyu mkandarasi mpua nae anaweza kudai pesa za kuanza mradi. Aidha, quotation yake inaweza kuwa kubwa kuliko huyo aliyefukuzwa kutokana na vitu kupanda bei na hivyo gharama ya mradi kuongezeka.
Aidha, inaweza kubidi kutafuta ma sub contractor wapya, ambayo nayo itachelewesha mradi.
Kwa kawaida, hatua ya kuvunja mkataba inatakiwa kuwa ya mwisho baada ya juhudi zote za kunusuru mradi kushindikana. Mkandarasi anapochelewesha mradi bila sababu inayoridhishwa anakatwa pesa katika malipo yake mpaka kiwango kilichowekwa katika mkataba kinapofikiwa. Ikifika hapo anafukuzwa.
Haya mambo ya kufanya maamuzi jukwaani yana gharama zake. Uzuri tu ni kuwa makandarasi wengi wazawa wanaogopa kuchukua hatua wanapoonewa kwa kuhofia kuwa watanyimwa kazi nyingine.
Haya mambo ya mikataba yafanywe kwa ueledi na sio siasa.
Amandla...