Rais hapaswi kufanya kazi za kawaida za Rais akiwa nje ya nchi

Pulchra Animo

JF-Expert Member
Jun 16, 2016
3,398
2,990
Nimeona Chifu Hangaya (akiwa Glasgow, Scotland) amefanya uteuzi wa Mkurugenzi Mkuu wa NDC. Huu ni ukiukaji wa Katiba yetu.

Kwa mujibu wa Ibara ya 47(1)(c) ya Katiba yetu, Makamu wa Rais atafanya kazi zote za Rais kama Rais hayuko kazini au yuko nje ya nchi. Na kwa mujibu wa Ibara ya 37(6)(b) ya Katiba hiyo hiyo, ili Rais ahesabike kuwa yuko nje ya nchi, lazima awe nje ya nchi kwa muda unaozidi saa ishirini na nne.

Ingawa Ofisi ya Rais wa JMT yaweza kuwa mahali popote ndani ya mipaka ya JMT, katu haiwezi kuwa mahali popote tu duniani, kama Chifu Hangaya anavyotaka kuifanya. Ni lazima iwe ndani ya mipaka ya nchi yetu.

Vilevile, nchi haiwezi kuwa na Rais zaidi ya mmoja kwa wakati mmoja. Rais awapo nje ya nchi kwa muda unaozidi saa ishirini na nne, Makamu wa Rais (au Waziri Mkuu, endapo Makamu wa Rais naye hayupo) ndiye Rais wa nchi kwa kipindi hicho (Kaimu Rais)! Period.
 
A good president does with executive power what Pablo Picasso did with paint. He takes bills into new and slightly discomfiting territory. He puts extra eyes on policies. He moves the mouth of the Supreme Court from where it should be to where it must be.
 
Kikwete aliwahi kutumbua mawaziri kadhaa akiwa Marekani miongoni mwao ni Dr Nchimbi na Dr Mathayo kwenye ile Operesheni Tokomeza!
 
Nimeona Chifu Hangaya (akiwa Glasgow, Scotland) amefanya uteuzi wa Mkurugenzi Mkuu wa NDC. Huu ni ukiukaji wa Katiba yetu.

Kwa mujibu wa Ibara ya 47(1)(c) ya Katiba yetu, Makamu wa Rais atafanya kazi zote za Rais kama Rais hayuko kazini au yuko nje ya nchi. Na kwa mujibu wa Ibara ya 37(6)(b) ya Katiba hiyo hiyo, ili Rais ahesabike kuwa yuko nje ya nchi, lazima awe nje ya nchi kwa muda unaozidi saa ishirini na nne.

Ingawa Ofisi ya Rais wa JMT yaweza kuwa mahali popote ndani ya mipaka ya JMT, katu haiwezi kuwa mahali popote tu duniani, kama Chifu Hangaya anavyotaka kuifanya. Ni lazima iwe ndani ya mipaka ya nchi yetu. Vilevile, nchi haiwezi kuwa na Rais zaidi ya mmoja kwa wakati mmoja. Rais awapo nje ya nchi kwa muda unaozidi saa ishirini na nne, Makamu wa Rais (au Waziri Mkuu, endapo Makamu wa Rais naye hayupo) ndiye Rais wa nchi kwa kipindi hicho (Kaimu Rais)! Period.

Umesema mambo yafuatayo:-

1. Taifa haliwezi kuwa na maRais wawili kwa wakati mmoja.

2. Majukumu "yote" ya Urais yatafanywa na Makamu wa Rais endapo Rais atakua nje ya nchi kwa zaidi ya saa 24.

Kwa maelezo yako hayo hapo juu, maana yake kwa sasa Rais wa Tanzania ni Dr. Mpango (maana Mh. Samia hayupo nchini kwa zaidi ya saa 24).
Je, Mh. Samia yuko kule kama nani ? Jibu lako likiwa yupo kule kama Rais wa Tanzania, swali linalofuata ni je, kwa sasa Tanzania ina maRais wawili ?
 
Umesema mambo yafuatayo:-

1. Taifa haliwezi kuwa na maRais wawili kwa wakati mmoja.

2. Majukumu "yote" ya Urais yatafanywa na Makamu wa Rais endapo Rais atakua nje ya nchi kwa zaidi ya saa 24.

Kwa maelezo yako hayo hapo juu, maana yake kwa sasa Rais wa Tanzania ni Dr. Mpango (maana Mh. Samia hayupo nchini kwa zaidi ya saa 24).
Je, Mh. Samia yuko kule kama nani ? Jibu lako likiwa yupo kule kama Rais wa Tanzania, swali linalofuata ni je, kwa sasa Tanzania ina maRais wawili ?
Akikujibu naomba nitag mkuuu nipate maarifa

Sent from my SM-G955F using JamiiForums mobile app
 
Mwambieni Hangaya atulie nchini,hizi safari za kuzungumzia tabia nchi awaachie mataifa makubwa.
Kati ya matatizo lukuki ya nchi hilo wala halitusumbui
PS; Dar es Salam kuna mgao wa maji huku tunaambiwa tunawe na maji tiririka
Mabadiliko ya tabia ya nchi ni tatizo la wote, ni suala mtambuka. Ni changamoto isiyozingatia mipaka mkuu.

Tena athari zake ni kubwa zaidi kwa sisi tusiojiweza kuliko wale wenzetu.
 
Umesema mambo yafuatayo:-

1. Taifa haliwezi kuwa na maRais wawili kwa wakati mmoja.

2. Majukumu "yote" ya Urais yatafanywa na Makamu wa Rais endapo Rais atakua nje ya nchi kwa zaidi ya saa 24.

Kwa maelezo yako hayo hapo juu, maana yake kwa sasa Rais wa Tanzania ni Dr. Mpango (maana Mh. Samia hayupo nchini kwa zaidi ya saa 24).
Je, Mh. Samia yuko kule kama nani ? Jibu lako likiwa yupo kule kama Rais wa Tanzania, swali linalofuata ni je, kwa sasa Tanzania ina maRais wawili ?
Uelewa wako ni mdogo..

nakusihi kuwa ni vema kukaa kimya kama hauna cha ku-comment

Sent from my Infinix X683 using JamiiForums mobile app
 
Mabadiliko ya tabia ya nchi ni tatizo la wote, ni suala mtambuka. Ni changamoto isiyozingatia mipaka mkuu.

Tena athari zake ni kubwa zaidi kwa sisi tusiojiweza kuliko wale wenzetu.
Ukikuta kikundi Cha watu 10 waulize ,Tania nchi Ni nini?
Hutapatata jibu wengi watakuwa wanafikili labda Serikali imewaletea mbegu mpya za korosho, Tumbaku ,Alizeti,pamba au Aina mpya ya bodaboda au bajaji.

Sisi tupambane na vyumba vya madalasa,vyoo umeme na maji,Tania nchi haituhusu zaidi ya Nchi zenye viwanda.
 
Kikwete aliwahi kutumbua mawaziri kadhaa akiwa Marekani miongoni mwao ni Dr Nchimbi na Dr Mathayo kwenye ile Operesheni Tokomeza!
Kikwete hakuwahi tumbua mawaziri hawa, baada ya mambo kuwa magumu Bungeni,na mawaziri hawa waligoma katu kujiuzuru,ndipo kikwete akiwa huko ulikotaja,akawashauri wajiuzuru
 
Kikwete hakuwahi tumbua mawaziri hawa, baada ya mambo kuwa magumu Bungeni,na mawaziri hawa waligoma katu kujiuzuru,ndipo kikwete akiwa huko ulikotaja,akawashauri wajiuzuru
Nakumbuka Zitto Kabwe alihoji kwa Spika kwanini Dr Mathayo anaondolewa ilhali ripoti haijamtaja popote?

Mama Makinda akasema " na yeye Rais amemuondoa"
 
Nimeona Chifu Hangaya (akiwa Glasgow, Scotland) amefanya uteuzi wa Mkurugenzi Mkuu wa NDC. Huu ni ukiukaji wa Katiba yetu.

Kwa mujibu wa Ibara ya 47(1)(c) ya Katiba yetu, Makamu wa Rais atafanya kazi zote za Rais kama Rais hayuko kazini au yuko nje ya nchi. Na kwa mujibu wa Ibara ya 37(6)(b) ya Katiba hiyo hiyo, ili Rais ahesabike kuwa yuko nje ya nchi, lazima awe nje ya nchi kwa muda unaozidi saa ishirini na nne.

Ingawa Ofisi ya Rais wa JMT yaweza kuwa mahali popote ndani ya mipaka ya JMT, katu haiwezi kuwa mahali popote tu duniani, kama Chifu Hangaya anavyotaka kuifanya. Ni lazima iwe ndani ya mipaka ya nchi yetu. Vilevile, nchi haiwezi kuwa na Rais zaidi ya mmoja kwa wakati mmoja. Rais awapo nje ya nchi kwa muda unaozidi saa ishirini na nne, Makamu wa Rais (au Waziri Mkuu, endapo Makamu wa Rais naye hayupo) ndiye Rais wa nchi kwa kipindi hicho (Kaimu Rais)! Period.
Kama uteuzi huo umeanza tarehe 29 Oktoba 2021 na Rais Samia ameondoka nchini kwenda Scotland tarehe 30 Oktoba 2021 na kuwasili tarehe 31 Oktoba 2021, kwa akili za kawaida Rais Samia alifanya uteuzi huo akiwa wapi mkuu?
 
Nimeona Chifu Hangaya (akiwa Glasgow, Scotland) amefanya uteuzi wa Mkurugenzi Mkuu wa NDC. Huu ni ukiukaji wa Katiba yetu.

Kwa mujibu wa Ibara ya 47(1)(c) ya Katiba yetu, Makamu wa Rais atafanya kazi zote za Rais kama Rais hayuko kazini au yuko nje ya nchi. Na kwa mujibu wa Ibara ya 37(6)(b) ya Katiba hiyo hiyo, ili Rais ahesabike kuwa yuko nje ya nchi, lazima awe nje ya nchi kwa muda unaozidi saa ishirini na nne.

Ingawa Ofisi ya Rais wa JMT yaweza kuwa mahali popote ndani ya mipaka ya JMT, katu haiwezi kuwa mahali popote tu duniani, kama Chifu Hangaya anavyotaka kuifanya. Ni lazima iwe ndani ya mipaka ya nchi yetu.

Vilevile, nchi haiwezi kuwa na Rais zaidi ya mmoja kwa wakati mmoja. Rais awapo nje ya nchi kwa muda unaozidi saa ishirini na nne, Makamu wa Rais (au Waziri Mkuu, endapo Makamu wa Rais naye hayupo) ndiye Rais wa nchi kwa kipindi hicho (Kaimu Rais)! Period.
Unajua unawaza kana vile uko msalani unakata kimba

Sent from my SM-N960F using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom