#COVID19 Rais Duterte wa Ufilipino asema raia wote wasiochanjwa dhidi ya COVID-19 hawataruhusiwa kutoka majumbani mwao, yupo tayari wafe

Cannabis

JF-Expert Member
Jan 20, 2014
8,938
25,281

Rais wa Ufilipino Rodrigo Duterte anaonya kuwa Wafilipino ambao wanakataa kupata chanjo dhidi ya coronavirus hawataruhusiwa kuondoka nyumbani kwao kama kinga dhidi ya aina ya kirusi cha delta kinachoenea zaidi.

Duterte alisema kwa njia ya televisheni Jumatano usiku kwamba hakuna sheria inayoamuru kizuizi kama hicho lakini akaongeza yuko tayari kukabiliwa na mashtaka ili kuwaweka watu ambao "wanasambaza virusi kushoto na kulia" barabarani. Amesisitiza iwapo raia hao waliokataa kuchanjwa watatoka nje ya nyumba zao, atalazimika kuagiza polisi kuwarudisha majumbani mwao.

Rais huyo akizungumza kwa ukali aliongeza kuwa kwa watu ambao hawataki kupatiwa chanjo, wanaweza kufa muda wowote.

Hata hivyo, licha ya kusita kwa umma kupokea chanjo dhidi ya COVID-19, nchi hiyo yenye raia ya zaidi ya milioni 108 imekuwa ikikabiliwa na upungufu wa chanjo.

Karibu Wafilipino milioni 7 wamepewa chanjo kamili na wengine zaidi ya milioni 11 wamepokea dozi ya kwanza. Hiyo ni asilimia ndogo ya lengo la serikali la kichanja kati ya watu milioni 60 hadi 70.
 
666 loading... Satan is on control of the world as it was being prophesied by John's revelation
 
Ufilipino


Rais wa Ufilipino Rodrigo Duterte amewaonya raia wan chi hiyo wasiotaka kuchanjwa dhidi ya Corona kusalia majumbani mwao .

Amesema nchi yake imechukua hatua ya kuwachanja wanaotaka kupokea chanjo hiyo huku akiongeza kwamba wasiotaka kuchanjwa wakifa basi yeye hajali .

Amesema raia wanaokataa chanjo ni tisho kwa nchi kwa sababu watakuwa wasambazaji wanaotembea wa virusi hivyo . Katika hotuba kwa nchi yake Duterte amesema;

‘ Kwa wale watu ambao hamtaki kuchanjwa nawaambia msitoke nyumbani kwenu.Ukitoka nyumbani kwako ,nitawaambia polisi wakurejeshe ndani.

Utasindikizwa kurejea kwako kwa sababu wewe ni msambazaji anayetembea wa virusi hivi …Iwapo hutaki kuchanjwa basi usitoke kwako..tuwape chanjo wanaozitaka… na wasiotaka kuchanjwa basi mnaweza kufa wakati wowote,mimi sijali’
 
hata hapa tutachanja tu ni suala la muda mabeberu wakiamua yao hawapingwi sisi tunapiga porojo tu hapa kukataa.
 
Na huku ikifikia critical watu wakaanza kutondoka tutaanza kuulizana vitambulisho vya chanjo kabla ya kutembeleana..., hatutahitaji polisi wala serikali ni self policing

Usicheze na maisha hizi hiyari zipo sababu hali sio critical....
 
Back
Top Bottom