Rais Dr. Magufuli anaungana rasmi na Mwl. Nyerere na Mzee Mugabe

kavulata

JF-Expert Member
Aug 2, 2012
12,233
12,506
Rais Magufuli ni mzalendo kwelikweli wa taifa hili anayeipenda nchi yake sawa na walivyo Baba wa Taifa Mwl Nyerere na Robert Mugabe.

Bahati yao mbaya ni kuwa wanazipenda sana nchi zao lakini hawana uwezo wala namna ya kuyatatua matatizo ya kiuchumi ya wananchi wao kwa kuorodhesha tu ubaya wa wakoloni mamboleo. Ukoloni ulikuwepo, upo, na utakuwepo. Mzee Nyerere, Gadafi, na Mzee Mugabe hawakufua dafu kiuchumi pamoja na kuthubutu kuuorodhesha ubaya wa wanyonyaji.

Wakoloni ndio wenye mitaji, teknolojia na masoko ya kuchimba na kununua madini yoooote duniani. Bahati mbaya viongozi wetu wanaoingia mikataba na wakoloni hawa hawana tofauti na akina Mangungo wa enzi zile. Maana bila kuyachimba na kuyauza madini hayatakuwa na maana yoyote kwetu na sisi uwezo wa kuyachimba wenyewe bado uko mbali sana. Tunachohitaji ni win-win kwenye kuchimba.

Taifa liketi chini bila kubaguana, tushirikishwe kujadili nini chakufanya juu ya maliasili zetu na taifa letu. Rais peke yake hana na hatakuwa na majibu ya tatizo hili la kimfumo na kihitoria. Sanasana bila kujali dini wala vyama atuunganishe kupata katiba na Sheria safi zitakazoweza kulinda rasilimali zetu kikamilifu, hata ikibidi kutoa adhabu za vifo kwa walafi.
 
Nilishasema,Ngosha kacheza na elimu za Wabongo wengi wao hata f4 hawajafika......wanashangilia ujinga kama huu....let's wait n see kama tutaendelea kuskia kuhusu ACACIA baada ya hii wiki kuisha
 
Wengine tuliamini magufuli akishika nchi atarekebisha mauozo ya waliomtagulia kwa kuangalia maslahi ya taifa

Binafsi jinsi alivyokuwa anafanya kazi huko nyuma kama waziri ilinipa imani kubwa sana kwa huyu jamaa kwamba akiwa raisi wa nchi atatusaidia sana

Mungu akulinde magufuli. Angalau na sisi waafrika tuonekane tuna viongozi wasio vikaragosi
 
Angalau tuna rais kwa Mara ingine anayejua kuwa ni Rais wa nchi ya Tanzania na si mamluki wa wazungu
 
Nilishasema,Ngosha kacheza na elimu za Wabongo wengi wao hata f4 hawajafika......wanashangilia ujinga kama huu....let's wait n see kama tutaendelea kuskia kuhusu ACACIA baada ya hii wiki kuisha
Mjinga ni mjinga tu haijalishi ana elimu ipi!
Mikataba mibovu kama hiyo imetengenezwa na watu wenye elimu,
Ndo maana kuna watu wenye maisha duni sana ingawa wana elimu kubwa.
Kitu cha mhimu ni kuwa na nia, kuamua, kufanya na kutenda!
 
Rais Magufuli ni mzalendo kwelikweli wa taifa hili anayeipenda nchi yake sawa na walivyo Baba wa Taifa Mwl Nyerere na Robert Mugabe. Bahati yao mbaya ni kuwa wanazipenda sana nchi zao lakini hawana uwezo wala namna ya kuyatatua matatizo ya kiuchumi ya wananchi wao kwa kuorodhesha tu ubaya wa wakoloni mamboleo. Ukoloni ulikuwepo, upo, na utakuwepo. Mzee Nyerere, Gadafi, na Mzee Mugabe hawakufua dafu kiuchumi pamoja na kuthubutu kuuorodhesha ubaya wa wanyonyaji. Wakoloni ndio wenye mitaji, teknolojia na masoko ya kuchimba na kununua madini yoooote duniani. Bahati mbaya viongozi wetu wanaoingia mikataba na wakoloni hawa hawana tofauti na akina Mangungo wa enzi zile. Maana bila kuyachimba na kuyauza madini hayatakuwa na maana yoyote kwetu. Tunachohitaji ni win-win.

Taifa liketi chini bila kubaguana tushirikishwe kujadili nini chakufanya juu ya maliasili zetu na taifa letu.
Acha mambo ya ndioooooooooooooooo, nyumba za serikali ziko wapi? acha ujinga wa kuwa swayed na vitu vidogo!
 
Rais Magufuli ni mzalendo kwelikweli wa taifa hili anayeipenda nchi yake sawa na walivyo Baba wa Taifa Mwl Nyerere na Robert Mugabe. Bahati yao mbaya ni kuwa wanazipenda sana nchi zao lakini hawana uwezo wala namna ya kuyatatua matatizo ya kiuchumi ya wananchi wao kwa kuorodhesha tu ubaya wa wakoloni mamboleo. Ukoloni ulikuwepo, upo, na utakuwepo. Mzee Nyerere, Gadafi, na Mzee Mugabe hawakufua dafu kiuchumi pamoja na kuthubutu kuuorodhesha ubaya wa wanyonyaji. Wakoloni ndio wenye mitaji, teknolojia na masoko ya kuchimba na kununua madini yoooote duniani. Bahati mbaya viongozi wetu wanaoingia mikataba na wakoloni hawa hawana tofauti na akina Mangungo wa enzi zile. Maana bila kuyachimba na kuyauza madini hayatakuwa na maana yoyote kwetu. Tunachohitaji ni win-win.

Taifa liketi chini bila kubaguana tushirikishwe kujadili nini chakufanya juu ya maliasili zetu na taifa letu.

Hivi uyu sialipitisha sheria zote hizi za madini? Tena alikua anaongoza kwa kupiga vigelel na meza pale wapinzani walivyokua wanafukuzwa bungeni.
 
Mugabe si mtu wa kufananishwa naye kabisa aisee.

Kibabu kile kingekuwa kinaipenda Zimbabwe kisingeiharibu vile kilivyoiharibu.
Kibabu Mugabe kaiharibu Zimbabwe kwa mgongo wa kupigania wazimbabwe wanyonge wasiyo na ardhi. Lkn kama afanyavyo Magifuli leo ktk madini na Mugabe alipambania haki hiyo bila akili. Ndiyo maana leo taifa là Zimbabwe limehujumiwa kiuchumi na mabeberu. Magufuli vita aliyo ianzisha ni nzuri lkn alipaswa kwenda kisheria. Badala ya kutoa visingizio uchwara eti kampuni haijasajiriwa ili hali kamapuni inapata stahiki zote na kulipa kodi zote.
 
Mikataba Ya Ujenzi Wa Airport Chato Na Ujenzi Wa Reli Ya SGR Itapelekwa Bungeni au Tusubiri Mpaka Aondoke Madarakani Ndo Tuongee?
 
bora alieko madarakani kuliko wale wakipewa ukuu wa mkoa hata tarafa tu wapo radhi kusaliti chama ni wazi hata nchi watauza kwa buku na watanzania tutasalitiwa.


GO GO GI GO GO UNCLE!!!!!!!!!!
 
Nilishasema,Ngosha kacheza na elimu za Wabongo wengi wao hata f4 hawajafika......wanashangilia ujinga kama huu....let's wait n see kama tutaendelea kuskia kuhusu ACACIA baada ya hii wiki kuisha
stupidity is not a crime!, you are free to bluff!!..
 
4 Reactions
Reply
Back
Top Bottom