Rais Donald Trump aliwauliza washauri wake wa usalama iwapo aishambulie Iran kijeshi

RTI

JF-Expert Member
Dec 20, 2018
2,423
7,124
Rais Donald Trump aliwauliza washauri wake iwapo atoe amri ya kushambuliwa kwa vinu vya nyukilia vya Iran akiwa amebakiza miezi 2 aondoke madarakani.

Taarifa hiyo ni kwa mujibu wa jarida la New York Times.

Hata hivyo washauri wake wa usalama walimuonya kutofanya hivyo kwa sababu hatua hiyo ita sababisha mzozo mkubwa kwenye kanda ya mashariki ya kati na kuyaweka na masilahi ya Marekani katika kanda hiyo kwenye hatari kubwa.

Hayo yana kuja baada shirika la atomic dunia kuripoti ya kwamba Iran imeongeza mara 12 kiwango cha urutubishaji wa madini ya uranian ya ile iliyo kubaliwa kwenye mkataba wa nyukilia yaliyo sainiwa na Irani na mataifa yenye nguvu duniani.

Chanzo ( DW Swahili, Aljazera)
 
Trump ni rais wa ajabu kuwahi kutokea😂😂😂

Maskini wale wavaa "majoho" wa TEHRAN wamekuwa SCAPEGOAT wa kila afichae madhaifu yake humo US😂😂

NGOMA IMESHAKUWA NZITO kwa Trump anajaribu kucheza na fikra za wale raia wake wapendao "shari"

When Will Him Concede Biden-Kamala victory?

#APromisedLand Obama's Memoir.
 
Huenda Biden akairejesha Marekani kwenye ule mkataba wa nyuklia na Iran.

Ila pia huenda ataiwekea vigezo Iran vya kusitisha urutubishaji wa uranium ili kuwaondolea vikwazo.
 
"Hayo yana kuja baada shirika la atomic dunia kuripoti ya kwamba Iran imeongeza mara 12 kiwango cha urutubishaji wa madini ya uranian ya ile iliyo kubaliwa kwenye mkataba wa nyukilia yaliyo sainiwa na Irani na mataifa yenye nguvu duniani."

Haya ndiyo mafanikio makubwa ya Trump.Trump hana tofauti na lile zezeta la Tanzania.
 
Mkataba si alishindwa kuheshimu Trump mwenyewe. Basi hauna maana maana alisaini mkataba asiwekewe vikwazo lakii Trump akaendelea kumwekea so mkataba haukuwa na maana.
 
Huenda Biden akairejesha Marekani kwenye ule mkataba wa nyuklia na Iran.

Ila pia huenda ataiwekea vigezo Iran vya kusitisha urutubishaji wa uranium ili kuwaondolea vikwazo.
Ila mkuu Trump saa nyingine hazimtoshi sasa kakaa madarakani miaka nne alikuwa ana subili nn kuchukua hatua? Au ali taka kumuachia Baiden kizaazaa?

Duuh maana washauri wake wasinge muwahi na akafanikiwa kutimiza alichokuwa amekusudia mashariki ya kati pangewaka moto sio wa dunia hii aise.

Na ukijaribu kuona maadui wa Marekani wameimarika zaidi chini ya uongozi wa Trump.
 
Lakini kuna tetesi kuwa huenda Israel ikavishambulia vinu hivyo kama matokeo ya uchaguzi wa US yatampa ushindi Biden.Inapanga kuivishambulia kabla ya Biden kuchukua ofisi ya White House 20 jan 2021.
 
Lakini kuna tetesi kuwa huenda Israel ikavishambulia vinu hivyo kama matokeo ya uchaguzi wa US yatampa ushindi Biden.Inapanga kuivishambulia kabla ya Biden kuchukua ofisi ya White House 20 jan 2021.
...Not likely to happen.
 
Ushaambiwa shida ni interests za Marekani hapo Middle East, Iran hana ubavu kwa Marekani.
Kwa hiyo interests hizo una ziona ndogo sio?

Hivi unadhani USA akiishambuli Iran washirika wa Marekani katika eneo hilo watabaki salama kweli?
 
Back
Top Bottom