Rais Dkt.Magufuli Atoa Maagizo Viwango Vipya Vya Kodi Ya Nyumba

Trump2

JF-Expert Member
May 28, 2017
1,553
2,608
Rais Dkt. John Pombe Magufuli ameziagiza Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) na Wizara ya Fedha kutoza Kodi ya nyumba 10,000/= kwa nyumba ya kawaida, 20,000/= kwa Gorofa zilizopo Wilayani na vijijini na 50,000/= Kwa nyumba kubwa. Rais amesema viwango hivyo vizingatie Hati ya nyumba na siyo idadi ya nyumba katika kiwanja.
Screenshot_20181211-050549.png
 
Rais Dkt. John Pombe Magufuli ameziagiza Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) na Wizara ya Fedha kutoza Kodi ya nyumba 10,000/= kwa nyumba ya kawaida, 20,000/= kwa Gorofa zilizopo Wilayani na vijijini na 50,000/= Kwa nyumba kubwa. Rais amesema viwango hivyo vizingatie Hati ya nyumba na siyo idadi ya nyumba katika kiwanja.
View attachment 963854
Nao hao walizidi kukomoa watu! Eti, kuna nyumba ya zilizokuwa NHC, imejengwa ya familia tatu kiwanja kimoja, ikiwa na vyumba viwili ,sebule, jiko choo na bafu, wanatoza 38,800/= kila familia!
 
Hivi nyumba ya kawaida ina sifa zipi na nyumba kubwa ina sifa zipi?

Kuna nyumba maeneo mengine hazina hata hati.

Ni jambo jema ila vigezio na mashart viwekwe wazi kwa wapangaji na wenye nyumba
 
Kodi ya nyumba haikutakiwa kuwepo kabisa ilitakiwa ifutwe kwani ni mojawapo ya kodi kandamizi, kitu kimoja unalipia zaidi ya kodi 3 wakati wa kununua vifaa vya kujengea vifaa vyote unalipia kodi wakati wa kununua, kiwanja unalipia kodi, kama ni nyumba ya wapangaji unalipa kodi ndiyo na jengo nalo kama jengo nalo unalipia kodi.

Hapo ndipo inapoonekana kuwa kwa sasa hakuna kitu cha bure, hata elimu ya bure nayo hakuna, kinachofanyika ni kuchezewa shele kitu kinasamehewa huku hichohicho ulichotangaziwa kusamehewa unakilipia kwa upande mwingine.
 
Rais Dkt. John Pombe Magufuli ameziagiza Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) na Wizara ya Fedha kutoza Kodi ya nyumba 10,000/= kwa nyumba ya kawaida, 20,000/= kwa Gorofa zilizopo Wilayani na vijijini na 50,000/= Kwa nyumba kubwa. Rais amesema viwango hivyo vizingatie Hati ya nyumba na siyo idadi ya nyumba katika kiwanja.
View attachment 963854
Sheria inamruhusu kufanya hivyo?
 
Huu Uzi ulitakiwa uwekwe Kama stick thread ila wahusika TRA watakapokuja kukurupuka Tena wakifungua Jamiiforums wanaona tamko la mkuu we nchi.
 
Nyumba kubwa ni ya vipi? Mpaka kodi anaweka viwango yeye?
 
Jujaelewa soma kiswahili..... rais hana mamlaka ya kufanya haya mabo, anapeleka bungeni kupitia kwa waziri. Bunge haliwezi on its motion kufanya haya!


Utaratibu wa kutunga sheria kuhusu mambo ya fedha Sheria ya 1984 Na.15 ib.14 (hii ni side note ya ibara hiyo chini:

99.-(1) Bunge halitashughulikia jambo lolote kati ya mambo yanayohusika na ibara hii isipokuwa kama Rais amependekeza kwamba jambo hilo lishughulikiwe na Bunge na pendekezo hilo la Rais liwe limewasilishwa kwenye Bunge na Waziri.

(2) Mambo yanayohusika na ibara hii ni haya yafuatayo:-
(a) Muswada wa Sheria kwa ajili ya lolote kati ya mambo yafuatayo:- (i) kutoza kodi au kubadilisha kodi kwa namna nyingine yoyote isipokuwa kupunguza; (ii) kuangiza kwamba malipo au matumizi ya fedha yafanywe kutokana na Mfuko Mkuu wa Hazina ya Serikali au mfuko wa Serikali mwingine wowote au kubadilisha kiwango hicho na namna nyingine yoyte isipokuwa kupunguza; Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

71 (iii) kuagiza kwamba malipo au matumizi ya fedha yafanywe kutokana na Mfuko Mkuu wa Hazina ya Serikali au mfuko wa Serikali mwingine wowote wakati ikifahamika kwamba fedha iliyomo katika mifuko hiyo haikupangiwa itolewe kwa ajili ya malipo au matumizi hayo, au kuagiza kwamba malipo au matumizi yanayofanywa kutokana na mifuko hiyo yaongezwe; (iv) kufuta au kusamehe deni lolote linalotakiwa lilipwe kwa Serikali ya Jamhuri ya Muungano;
(b) hoja au mabadiliko yoyote ya Hoja kwa ajili ya lolote kati ya mambo yaliyoelezwa katika aya ya (a) ya ibara hii ndogo.
(3) Masharti ya ibara hii yatatumika kwa muswada wowote uliowasilishwa kwenye Bunge au Hoja yoyote iliyotolewa katika Bunge na Waziri au Naibu Waziri. Madaraka na Hak(iv) kufuta au kusamehe deni lolote linalotakiwa lilipwe kwa Serikali ya Jamhuri ya Muungano; (b) hoja au mabadiliko yoyote ya Hoja kwa ajili ya lolote kati ya mambo yaliyoelezwa katika aya ya (a) ya ibara hii ndogo.
 
Rais Dkt. John Pombe Magufuli ameziagiza Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) na Wizara ya Fedha kutoza Kodi ya nyumba 10,000/= kwa nyumba ya kawaida, 20,000/= kwa Gorofa zilizopo Wilayani na vijijini na 50,000/= Kwa nyumba kubwa. Rais amesema viwango hivyo vizingatie Hati ya nyumba na siyo idadi ya nyumba katika kiwanja.
View attachment 963854

Dah! Tanzania imekuwa kama familia ya bwana mmoja!!! Hivyo 2015 tulikosea wapi!
 
Rais Dkt. John Pombe Magufuli ameziagiza Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) na Wizara ya Fedha kutoza Kodi ya nyumba 10,000/= kwa nyumba ya kawaida, 20,000/= kwa Gorofa zilizopo Wilayani na vijijini na 50,000/= Kwa nyumba kubwa. Rais amesema viwango hivyo vizingatie Hati ya nyumba na siyo idadi ya nyumba katika kiwanja.
View attachment 963854
JPM ana pointi hapo tatizo huenda ni sheria ya kodi ambayo TRA wanapaswa kuifuta. Kwenye hati ya makadirio, TRA wanauliza maswali ambayo ndio hupelekea makadirio, mfano aina ya paa, ni bati au kigae, kama ni bati; ni la aina gani? Aina ya sakafu na kuta zake.

Ingawa nakubaliana na JPM, nina mashaka huenda kodi anayoipendekeza ikawa haileti usawa.

Vv
 
Back
Top Bottom