Rais Dkt. Hussein Mwinyi kumuwakilisha Rais Samia Suluhu kwenye mkutano wa Wakuu wa nchi SADC

Rais wa Zanzibar hatakiwi kumwakilisha rais kwa mambo ya muungano ndio maana kwenye katiba wameweka wazi rais akitoka upande mmoja makamu wake anatoka upande mwingine na hata rais tuliyenaye tumempata kwa utaratibu huo
Mbona unasema uongo? Hamna mahali kwenye Katiba panapo mkataza Rais kuchagua mtu yeyote kumwakilisha? Zanzibar ni sehemu ya Jamhuri ya Muungano na raia wake ni watanzania kama tulivyo wengine watanganyika. Kwa sababu hiyo Rais ana haki ya kumchagua kutoka sehemu yeyote ya JMT kumwakilisha katika shughuli yoyote. Hata akitaka anaweza kumuomba Lissu amuwakilishe katika kikao kitakachofanyika The Hague na hamna atakayeweza kumzuia.

Kama hampendezwi na hili, badilisheni Katiba na muongeze kipengele kuwa Rais wa Zanzibar haruhusiwi kumuwakilisha rais wa JMT katika masuala ya kimataifa. Sitashangaa kama wazanzibari hawatakuja na hoja ya kutaka Rais wao awe makamu wa Kwanza wa Rais kama ilivyokuwa zamani.

Huu ni uwakilishi tu na sio kuwa amemkabidhi urais Mwinyi. Kuna mambo ya msingi ya kujadili kuliko hili.

Amandla...
 
Usiwe mchoyo wa maarifa mkuu, kama unayo lakini.
Mkuu kujua kwanini fulani kamtuma fulani KWA KWELI SIJUI kama ambayo hakuna aneyejua kwa nini umlimuoa/kuolewa na unaendelea kuishi na huyo aliyemuoa/kuolewa naye
 
Mbona haukuuliza alivyoingia kwenye kikao cha baraza la mawaziri? Je unajuaje ndio alichopangiwa kufanya kwenye kile kikao?
 
Haina neno kabisa katumwa na AMIRI JESHI MKUU yeye na timu yake wanaandaa mkeka wa Wakuu wa Mikoa na Wilaya pia MADED...MDA MCHACHE
 
9 April 2021
Maputo, Mozambique

Mkutano wa Usalama na Ulinzi wa SADC "Double Troika" kuhusu Cabo Delgado
Rais Dr. Hussein Mwinyi akiwa mkutanoni ameongozana na Dr. Liberata Mulamula waziri wa mambo ya nje. Katibu mtendaji wa SADC Bi. Stergomena Lawrence Tax azungumzia maazimio yaliyofikiwa baada ya kikao hicho maalum cha wakuu wa nchi za SADC.

 
I

Limekaa vizuri tu, tena Lima afya na linaleta taswira nzuri mno kwenye JAMII ya kimataifa.
Kimsimgi, Rais Wa Jamhuri ya Tanzania amaweza kumtuma raia yeyote ndani ya mipaka ya Jamhuri ya muungano Wa Tanzania!! Hapo ni credit kwa mama!!
Ndiyo maana ya MUUNGANO Mkuu. Halafu hivi hawaoni jinsi Mwinyi alivyo na credibility? Yaani hakika hata Wazanzibari wanafurahia. Kifupi Mwinyi ataibadilisha sana Zanzibar kiuchumi, kisiasa na kijamii. Na dada yake huku tunaamini mambo mengi yataboreka sana.

MATHA = Make Tanzania Happy Again
 
Ndugu zangu!

Ni huyu mtoto wangu mdogo kaniuliza hilo swali.

Kwamba kwenye mkutano wa SADC inasemekana Rais wetu atawakilishwa na Rais wa Zanzibar, Dr Hussein Mwinyi.

Hii ikoje kiitifaki?

Rais wa Mwinyi anawajibika kuripoti kwa Samia?

Huko SADC Zanzibar ni nchi mwanachama?

Maswali ni mengi, karibuni tujadili.
Rais wa Zanzibar ni sehemu ya Baraza la Mawaziri la Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania. Rejea ibara ya 54(1) ya Katiba ya JMT.
 
Back
Top Bottom